Kwako Rais Mwinyi; Bandari ya Zanzibar unaiua kwa haya mambo unayoyafanya

silent lion

JF-Expert Member
Feb 28, 2012
1,161
1,535
Mheshimiwa wakati unaingia madarakani , wazanzibari wengi nyoyo zetu zilifarijika kwa jinsi ulivoanza kuchapa kazi.

Ziara yako ya bandarini iliibua matumaini kwamba yajayo ni neema tupu.

Mwaka mmoja sasa tokea ushike madaraka , hakuna kilichobadilika zaidi ya kuongezeka kwa usumbufu wa utitiri wa vitengo bandarini. Yaani kila kitengo sasa hivi kiko bandari ya Zanzibar.

Mheshimiwa nikukumbushe tu Zanzibar ni visiwa vyenye idadi chache ya wakaazi, ambao wengi wao wanaishi katika lundo la umasikini. Hivyo mizigo mingi inayoshushwa hapa Zanźibar huwa kama inapita njia tu kuelekea Tanzania bara.

Kitendo cha kuiwekea vikwazo cha sijui mizigo ikaguliwe na majeshi ya ulinzi au ZAECA (takukuru Ya Znz) ni suicidal move na si tu kitafukuza Wafanya biashara, bali kitaua biashara ambayo tayari iko hoi. Ikumbukwe pia gharama za kuleta mizigo Zanzibar (freight charges) ni kubwa mno kulinganisha na bandari ya Dar, na mizigo hua inachelewa mno kuwasili tofauti na bara.

Mheshimiwa kitendo cha kudharau watendaji wa bandari na TRA na kuwaona kama hawafanyi kazi si cha busara.

Its never too late to mend, you can still save Zanzibar,
 
Combination ya JPM na Mwinyi ingeleta maajabu Afrika.

Sasa hivi wakwepa kodi wa Zanzibar wamekimbilia kushusha mizigo yao bara.
usiongee kitu ulichokua hukijui, sasa huko Bara umeona ndo shamba la bibi na hio mizigo kwani inafunguliwa kama sanduku la harusini?
 
Alichofeli watu ni wale wale waliokua kwenye mfumo hivyo wanafanya mgomo baridi kwani vitengo vilivyoletwa ni kusimamia uharamia wa kodi ila alichofeli kuwaweka wale wale ilibidi apige chini wote
 
Kiukweli Dr. ana mambo mengi sana Zanzibar yaani mipango yake ni kama ile ya Late Pombe, buluu economy ndiyo janga kwa wazanzibari, na kama waznz wasipokuwa makini utashangaa mniongezee mi5 nimalizie niliyokusudia kufanya!.

Issue ya bandari iko wazi, wafanyabishara kadhaa wa unguja wanalia na hali iliyopo ilihali wengine kama mimi nawasemea "mlizoea kutoa bure mizigo, tena kwa sababu ya kufahamiana" ila anapaswa kuangalia upya kabla maji hayaja mwagika.
 
Kiukweli Dr. ana mambo mengi sana Zanzibar yaani mipango yake ni kama ile ya Late Pombe, buluu economy ndiyo janga kwa wazanzibari, na kama waznz wasipokuwa makini utashangaa mniongezee mi5 nimalizie niliyokusudia kufanya!.

Issue ya bandari iko wazi, wafanyabishara kadhaa wa unguja wanalia na hali iliyopo ilihali wengine kama mimi nawasemea "mlizoea kutoa bure mizigo, tena kwa sababu ya kufahamiana" ila anapaswa kuangalia upya kabla maji hayaja mwagika.

moja ya tatizo kubwa la mwinyi ni kushindwa kuwa na vipaumbele vinavyoweza kutatua matatizo ya kiuchumi, si kwenye biashara wala utalii.
 
moja ya tatizo kubwa la mwinyi ni kushindwa kuwa na vipaumbele vinavyoweza kutatua matatizo ya kiuchumi, si kwenye biashara wala utalii.
Ombwe la wafanyabishara kuwa viongozi kwenye nafasi ya juu kabisa unaweza kuona anafanya biashara ya 10per.
 
Kutawala Tanzania bara na visiwani kunahitaji umafia, bila umafia lazima uvune mabua...wapumbavu lazima wafe maendeleo yaje..
visiwa vyote duniani vinakua ni tax haven ndugu yangu kama hujui, ata visiwa vya Zanzibar kwa muda mrefu vimekua vikipatiwa unafuu fulani wa kodi ili kuvutia uwekezaji na kuimarisha biashara, na Marais wote waliopita hili walilijua si kama walikua wajinga.

Sasa Mheshimiwa Mwinyi yeye amekuja kufanya kinyume chake, kapandisha kodi pamoja na tozo mbali mbali pamoja na usumbufu wa ufanyaji kazi, haiwezekani mzigo ukaguliwe na TRA , USALAMA WA TAIFA, JESHI, TAKUKURU, SIJUI KUNA ZBS KUNA WAKEMIA KUNA MPAKA WATU KILIMO BANDARINI.

Kinachosikitisha zaidi pesa zinapotea huko huko Serikalini na hii ni kwa mujibu wa CAG lakini hakuna hatua yoyote inayochukuliwa ni kama kuna kuogopana. Mabilioni kwa mabilioni yanapotea bure bure halafu unakuja kumkamua mfanyabiashara mnyonge. Time will tell.
 
Kitendo cha kuiwekea vikwazo cha sijui mizigo ikaguliwe na majeshi ya ulinzi au ZAECA (takukuru Ya Znz) ni suicidal move na si tu kitafukuza Wafanya biashara, bali kitaua biashara ambayo tayari iko hoi. Ikumbukwe pia gharama za kuleta mizigo Zanzibar (freight charges) ni kubwa mno kulinganisha na bandari ya Dar, na mizigo hua inachelewa mno kuwasili tofauti na bara.


Ila banDARI Ya Zanzibar ni shamba la bibi
 
Kwahiyo hamtaki ukaguzi
Mheshimiwa Mwinyi yeye amekuja kufanya kinyume chake, kapandisha kodi pamoja na tozo mbali mbali pamoja na usumbufu wa ufanyaji kazi, haiwezekani mzigo ukaguliwe na TRA , USALAMA WA TAIFA, JESHI, TAKUKURU, SIJUI KUNA ZBS KUNA WAKEMIA KUNA MPAKA WATU KILIMO BANDARINI
 
Kiukweli Dr. ana mambo mengi sana Zanzibar yaani mipango yake ni kama ile ya Late Pombe, buluu economy ndiyo janga kwa wazanzibari, na kama waznz wasipokuwa makini utashangaa mniongezee mi5 nimalizie niliyokusudia kufanya!.

Issue ya bandari iko wazi, wafanyabishara kadhaa wa unguja wanalia na hali iliyopo ilihali wengine kama mimi nawasemea "mlizoea kutoa bure mizigo, tena kwa sababu ya kufahamiana" ila anapaswa kuangalia upya kabla maji hayaja mwagika.
Kuna point umeigusia hapo na hiyo ndio inayosababisha wapiga deal walielie.

Sent from my TECNO CD7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom