Kwako Ndg. Pasco: Maandamano Yamefanyika Bila Idhini ya Katibu wa Chama!

wananchi wako wakikuambia kua wako tayari kukupa kura lakini hawaitaki ccm kwa hiyo uhamie chadema..utakua tayari kwa hilo au ni bora usiwe mbunge lakini ubakie ccm?
wapiga kura hawawezi kuwa na locus ya kuamua kunitaka mimi bila chama changu. hizo ni hadithi za baniani mbaya kiatu chake dawa...na kwa nini wanichagulie chama?
Mind you Ubunge is not everything that there is...kuna maisha mazuri tu nje ya Ubunge
 
Itategemeana na uamuzi nitakaochukua muda huo ukifika. kwamba nigombee tena ama la? Mimi nina fani ya kazi, nina nguvu na ujuzi wa kutosha, pia nina shughuli nyingi na halali za kunipatia kipato changu cha riziki ya kila siku. sitegemei siasa pekee kama ajira yangu, nikionekana sifai basi nitapumzika, hata hivyo wenye uamuzi wa mwisho ni wananchi wenyewe na wala siyo mtu mwenye lengo la kulipiza kisasi. hivyo kama nitaamua kugombea nitawaomba ridhaa wananchi wenzangu wa Nzega, wakisema natosha nitagombea wakisema hapana umechemsha na haujafanya kitu nitaacha! Huwezi kufanya kazi huku ukihofia kufukuzwa chama, ama kuacha kuteuliwa na chama uchaguzi ujao --- sasa utaishije? Zaidi ya hapo una ahadi gani na Mungu kwamba utafika hiyo 2015? Ishi kama vile utakufa leo na utakuwa huru

Nilidhani ina PhD kumbe ni MD ? Wenzako wa fani zako Ulaya hawaitwi na Dr.Hata kama ni MD hadi wawe na PhD wewe kaka vipi ?
 
Hongera Dr Kigwa, I just hope something good will come out of this maandamano. Bado nashauri uunganishe nguvu na wabunge wengine toka Tabora. Vingenevyo itakuwa ngumu sana kupata mabadiliko ya kweli.
 
Hongera Mh. Dr. H kwa kuthubutu ingawa wanywa maji ya bendera hawajafurahia hilo, naomba unijuze outcome ya hayo maandamano
 
Katika post fulani last week mdau maarufu wa hapa JF, ndg PASCO, alitaahadharisha kwamba MB wa CCM ndg Hamisi Kigwangalla (Nzega) hawezi kufanya maandamano akiambatana na wananchi kwa kuwa tayari chama chake wilayani hakimuungi mkono. Kilichotokea ni kwamba maandamano yamefanyika na viongozi wa chama na serikali (inayotokana na chma tawala) waliridhia maandamano hayo na tunashukuru yalifanikiwa na yalikuwa na amani tele. Anayeweza kuzuia maandamano ni polisi (kwa sababu za kiusalama) na si katibu wa chama ambaye alikurupuka kuandika barua bila kujua kanuni na taratibu za kisheria zinazohusiana na maandamano na mikutano ya hadhara. Chama cha mapinduzi hakikatai maandamano, in fact kimetufundisha kuandamana kupinga baadhi ya mambo na hata kuunga mkono baadhi ya mambo na maamuzi yanayofanyika. Mimi ni mwanafunzi mzuri wa siasa za CCM na ninaelewa misingi ya uongozi kama inavyowekwa wazi na CCM kwenye maandiko yake, labda kama mtu aniambie leo hii kwamba Katiba, Kanuni na maandiko mbalimbali ya miongozo ya CCM hayafuatwi tena hapo nitaelewa na pengine nitafikiria sasa kama nina ulazima wa kuendelea kufuata itikadi ya chama hiki ama la!
Mkuu Dr. Kigwa,
Kwanza natanguliza hongera za awali, nikishasoma taarifa rasmi za maandamano hayo from independent source, nitakupatia hongera zako stahiki kwa kusimama na kuhesabiwa!. Naamini waandishi walikuwepo na yamekuwa reported!.
 
DR Hamis. Unaposema "mabadiriko ya kweli yataletwa na sisi ...!" unamaanisha nini?

Hivi wewe ni mtu wa wapi? hebu soma alivyoandika Mbunge na ulivyoandika wewe. Usituchafulie lugha yetu tamu.
 
Hongera Sana Dr.

Nimeisoma hii mahali.

Mbunge CCM aongoza maandamano kumpinga mwekezaji Atiwa Misukosuko Send to a friend

Sunday, 17 June 2012 09:26
0digg

Patricia Kimelemeta, Dar na Shija Felician, Nzega
WANACHAMA wa CCM na Chadema wilayani Nzega mkoani Tabora jana waliweka pembeni tofauti zao za kisiasa na kuandamana kwa pamoja kuushinikiza uongozi wa Mgodi wa Resolute kutekeleza ahadi walizoahidi wakati wakikabidhiwa mgodi huo miaka mitatu iliyopita.

Maandamano hayo yaliyoanzia Nzega mjini hadi Kijiji cha Nata kilichopo nje kidogo ya mji huo yaliandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Nzega, Dk Hamis Kigwangallah.

Yalifanyika baada ya wamiliki wa migodi hiyo kushindwa kutekeleza ahadi za ujenzi wa shule, Zahanati pamoja na kutoa ajira kwa wakazi wa eneo hilo.

Wanachama wa Chadema walionekana wakiwa na bendera za chama hicho huku wakionyesha ishara ya vidole viwili ambayo hutumiwa na chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Pamoja na polisi kutanda kila kona waandamanaji hao waliokuwa na bendera huku wamkitembea kwa miguu na baadhi wakiwa katika magari, waliingia katikati ya kundi la wanachama wa CCM na kuanza kutembea kuelekea katika katika Kijiji cha Mwabangu ambapo ulifanyika mkutano huo.

Waandamani hao walikuwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali unaoleza jinsi wasivyotendewa haki na wawekezaji kampuni za uchimbaji madini hasa Kampuni ya Golden Pride ya Nzega.

Akizungumza katika mkutano huo, Dk Kigwangallah aliwapongeza viongozi wa Chadema waliomuunga mkono katika maandamano hayo na kuwataka wananchi waendelee kumuunga mkono huku akiahidi kuwaletea mabadiliko makubwa.

Alisema kuwa wananchi wanatakiwa kudai haki zao kwa njia ya amani na kuongeza kuwa kilio chao tayari serikali imeshakisia na inakifanyia kazi.

"Tumieni njia ya amani kudai haki zetu na sio kudai haki kwa kuvunja sheria, niko pamoja na nyinyi nitahakikisha haki zetu zinapatikana," alisema Dk Kigwangallah.

Maandamano hayo yalifanyika chini ya ulinzi mkali baada ya awali Jeshi la polisi kuyazuia, lakini baadaye lilitoa kibali kwa masharti kwamba mkutano ukimalizika wananchi watawanyike mara moja.

Awali Dk Kigwangallah wakati akizungumza kwa njia ya simu alisema mpaka sasa wananchi wa eneo hilo wanaishi katika mazingira magumu kutokana na wawekezaji kuchukua mgodi huo,jambo ambalo limesababisha kushindwa kumudu hali ngumu ya maisha.

Alisema kutokana na hali hiyo wananchi hao wameandamana ili kushinikiza kutekeleza ahadi walizoahidi ili wananchi waweze kunufaika nayo.

Aliongeza, mbali na ahadi hiyo, wawekezaji hao pia waliahidi kusimamia miradi ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na kuwapa wananchi maji safi na salama lakini mpaka sasa wameshindwa.

Alisema kutokanaa na hali hiyo mgodi huo umezalisha zaidi ya Sh1 trilioni,ambapo jumla ya fedha walizoahidi kutoa kwa wananchi ni Sh3bilioni, ambazo kati ya hizo Sh1.9bilioni kwa ajili ya miradi ya maji, lakini mpaka sasa hawalipi bili ya maji, jambo ambalo linaonyesha wazi kuwa wanatumia kwa ajili ya kulipa fidia ya fedha zao.

Kigwangwalah alisema kuwa kutokana na hali hiyo wananchi wanaendelea kutaabika na hali ngumu ya maisha huku wawekezaji hao wakivuna mali bila ya kuwatumia wananchi, jambo ambalo ni kinyume na makubaliano.
Sasa nakupongeza rasmi na kukupa pole kwa misukosuko hii, ila pongezi rasmi za dhati na hongera kwa ku invest on your people.
IMG-20200408-WA0069.jpg
 
hahahaaa usituchonganishe na PASCO bana. hatukufanya maandamano ili kumkomesha PASCO ama mtu yeyote yule. tulifanya maandamano haya ili kuonyesha mshkamano wetu na machungu tuliyonayo. nimemuweka pasco hapa ili kutia chachu ya mjadala wa hoja ya MB anawajibika kwa wananchi waliomchagua ama Chama kilichompa tiketi! nadhani huu ni mjadala muhimu kwa demokrasia ya nchi yetu na haswa ukizingatia tumo kwenye mchakato wa kuandika katiba mpya!
Kuna mambo kama ya mgombea binafsi, hapa yanapata nafasi ya kujadiliwa sasa na umuhimu wake kuonekana


Hapa Mh ndo penye kiini cha tatizo. Wabunge wengi including wewe inapofika wakati wa issue muhimu za taifa hili, huwa mnaamua kutetea chama na serikali na kuwatosa wale waliowaweka madarakani. Kumbuka utetezi wako kwenye hoja ya zitto. Tunataka katiba mpya itupe mamlaka ya kuwawajibisha mkienda kinyume na yale tulowatuma ili at the end iwe ni taifa kwanza, vyama baadaye.
 
hamisi acha kuwadanganya wenzako kwani hao wenye mgodi wapo hapo kwa ajili ya kutengeneza faida na siyo kuwaletea maendeleo wananchi wa nzega ukweli ndio huo. unaleta propaganda zako za kisiasa kutaka kuwadanganya wananchi ili wakuone kuwa ni mtetezi wao kumbe unatetea maslahi yako binafsi. kama kuna mkataba ulisainiwa wa mwenyekezaji kufanya jambo lolote kwa nzega mpeleke mahakamani kwa kuvunja mkataba na kuwaambia wananchi waandamane ili ujipatie umaarufu chini ya migongo ya maskini wa nzega wasiojuwa nini kinachoendelea. mahakama zipo uende huko ndiko haki zinazopatikana.
 
Nilidhani ina PhD kumbe ni MD ? Wenzako wa fani zako Ulaya hawaitwi na Dr.Hata kama ni MD hadi wawe na PhD wewe kaka vipi ?
Mkuu kama hauelewi basi bora uulize kulikokupotosha umma! Kuna aina tatu za ma Dr na wote wanastahiki kuitwa Dr.1 ni mtu yoyote ambae amesoma na kupata Shahada ya Uzamivu yaani PhD yeye anastahiki kuitwa Dr mfano Dr Festus Limbu.2 mtu yoyote ambae amesoma na Shahada ya kwanza ya Utabibu wa Binadamu kama alivyo Dr Kigwa ama Tabibu wa mifugo kama alivyokuwa Hayati Dr Omary Ali Juma wote wanastahiki kuitwa Dr.Aina ya 3 na ya mwisho ni mtu yoyote ambae ametunikiwa Shahada ya Heshima kutoka Chuo kikuu chochote kwa mchango wake mkubwa kwa jamii kama alivyo Dr Jakaya Mrisho Kikwete na wengine wengi tu nao wanastahiki kuitwa Dr. Ni hali tu ya watu wengine kupenda kuwabeza wenzao kitu ambacho si sahihi tujifunze kuwa wavumilivu pindi yule tusiye mpenda anapotoa mawazo yake. Hoja ilikuwa si kumjadili Dr Hamisi bali ni maandamano aliyoyaongoza naomba wakuu tujifunze kujibu hoja kwa hoja na tukianza kumjadili mtu badala ya hoja aliyoileta basi tutaonekana ni dhaifu na tuna nia ya kumchafua mtu tu!
 
Katika post fulani last week mdau maarufu wa hapa JF, ndg PASCO, alitaahadharisha kwamba MB wa CCM ndg Hamisi Kigwangalla (Nzega) hawezi kufanya maandamano akiambatana na wananchi kwa kuwa tayari chama chake wilayani hakimuungi mkono. Kilichotokea ni kwamba maandamano yamefanyika na viongozi wa chama na serikali (inayotokana na chma tawala) waliridhia maandamano hayo na tunashukuru yalifanikiwa na yalikuwa na amani tele. Anayeweza kuzuia maandamano ni polisi (kwa sababu za kiusalama) na si katibu wa chama ambaye alikurupuka kuandika barua bila kujua kanuni na taratibu za kisheria zinazohusiana na maandamano na mikutano ya hadhara. Chama cha mapinduzi hakikatai maandamano, in fact kimetufundisha kuandamana kupinga baadhi ya mambo na hata kuunga mkono baadhi ya mambo na maamuzi yanayofanyika. Mimi ni mwanafunzi mzuri wa siasa za CCM na ninaelewa misingi ya uongozi kama inavyowekwa wazi na CCM kwenye maandiko yake, labda kama mtu aniambie leo hii kwamba Katiba, Kanuni na maandiko mbalimbali ya miongozo ya CCM hayafuatwi tena hapo nitaelewa na pengine nitafikiria sasa kama nina ulazima wa kuendelea kufuata itikadi ya chama hiki ama la!

Hebu twambie tangu mwaka 1992, ni lini CCM imeandamana kupinga jambo lolote!
Acha kutwambia theory
 
Wanachadema basi hata kumpongeza mtu hamjui?Hizi siasa za maji taka mtaacha lini kama mh. Kigwangalla amesimama kidete kutetea maslahi ya wananchi wa Nzega mnapaswa kumpongeza na si vinginevyo; au kwenu kutetea maslahi ya Taifa hili ni anaposimama mh. Zitto tu? Mh. Kigwangalla endeleza mapambano ya kweli ni aibu kuona dhahabu inachimbwa na wananchi hawana hata huduma muhimu; mwanzo mzuri usikate tamaa.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Itategemeana na uamuzi nitakaochukua muda huo ukifika. kwamba nigombee tena ama la? Mimi nina fani ya kazi, nina nguvu na ujuzi wa kutosha, pia nina shughuli nyingi na halali za kunipatia kipato changu cha riziki ya kila siku. sitegemei siasa pekee kama ajira yangu, nikionekana sifai basi nitapumzika, hata hivyo wenye uamuzi wa mwisho ni wananchi wenyewe na wala siyo mtu mwenye lengo la kulipiza kisasi. hivyo kama nitaamua kugombea nitawaomba ridhaa wananchi wenzangu wa Nzega, wakisema natosha nitagombea wakisema hapana umechemsha na haujafanya kitu nitaacha! Huwezi kufanya kazi huku ukihofia kufukuzwa chama, ama kuacha kuteuliwa na chama uchaguzi ujao --- sasa utaishije? Zaidi ya hapo una ahadi gani na Mungu kwamba utafika hiyo 2015? Ishi kama vile utakufa leo na utakuwa huru

HK,
Nilikuona jana kwenye ITV ukiwa unaandamana 'kwenye barabara ya lami iliyowekwa na CCM'(Magufuli, J.P. 2012).
Kama hayo uliyoyaandika yanatoka moyoni mwako, basi utakuwa umejikomboa sana kifikra na kiakili.Maana umetuhumiwa kwa tabia zako za kupenda madaraka
1. Ulikuwa mstari wa mbele kuwatetea madaktari wenzako, lakini ulivyopigwa Mkwara na akina Hawa, ukanywea kabisa na huku JF ukapakimbia, ukawa unaonekana tu kule FB kwenye mijadala ya kidini na kejeli na maneno ya kuudhi
2. Lilipokuja suala la kusaka saini 70 kwa wabunge, ulijotokeza humu na kuandika waraka mzio sana ukimshambulia Zito(nilitegemea na Lugola na Haule pia ungewashambulia, laini la).
3. Mabadiliko ya baraza la mawaziri katika Wizara 5 hivi, yakaganyika.Ukawa standby ukisubiria uwaziri au unaibu.Kumrithi Nkya au mzee wa IHI.Haikutokea.
4. Ukaona sasa hauna cha kupoteza; ukajilipua na kutokelezea tena kwenye sura za jamii.; na kuja na kauli kama wananchi wakisema HAPANA, wewe utakuwa sawa na utaendelea na shughuli zako na kuendeleza fani yako.

Swali la msingi hapa ni kuwa, ulikuwa wapi wakati wa kusaka saini 70 katika kuwaaminisha wapiga kura na wananchi wako wa Nzega kuwa unasimamia maslahi ya Taifa na si ya Chama na leo umeibuka 'baada ya habari kuenea kuwa umefanya hivo kwa kuwa tu umeukosa uwaziri?'


NGUVU YA UMMA
 
tatizo la kina hamis wenzake kama mgulu yule jamaa anayejifunga matambara shingoni unafiki,mtu anasimama analalamika serikal haijatekeleza kitu fulani mwisho wa siku naunga mkono hoja mia kwa mia,tutawaamin vp?
 
Itategemeana na uamuzi nitakaochukua muda huo ukifika. kwamba nigombee tena ama la? Mimi nina fani ya kazi, nina nguvu na ujuzi wa kutosha, pia nina shughuli nyingi na halali za kunipatia kipato changu cha riziki ya kila siku. sitegemei siasa pekee kama ajira yangu, nikionekana sifai basi nitapumzika, hata hivyo wenye uamuzi wa mwisho ni wananchi wenyewe na wala siyo mtu mwenye lengo la kulipiza kisasi. hivyo kama nitaamua kugombea nitawaomba ridhaa wananchi wenzangu wa Nzega, wakisema natosha nitagombea wakisema hapana umechemsha na haujafanya kitu nitaacha! Huwezi kufanya kazi huku ukihofia kufukuzwa chama, ama kuacha kuteuliwa na chama uchaguzi ujao --- sasa utaishije? Zaidi ya hapo una ahadi gani na Mungu kwamba utafika hiyo 2015? Ishi kama vile utakufa leo na utakuwa huru


utawaomba ridhaa wananchi au vingozi wa CCM waliokubeba?. wananchi si unajua kuwa hawakupendi ndo maana ukashika nafasi ya 3 kwenye kura za maoni lakini mfumo wa kubebana wa CCM ukakuteua ww ugombee. Kweli nimeamini kwa utaratibu uliotumika kukupa wewe nafasi ya kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM ikitumika siku ya mwisho ya hukumu, shetani anaweza kuingia peponi na malaika akatupwa motoni.
 
Back
Top Bottom