Gily Gru

JF-Expert Member
Jul 4, 2016
7,766
20,556
Kitanda changu ni nne kwa sita, mke wangu aisee ana staha sana. Kinachofurahisha Zaidi ukimshika mgongo nywele zinasisimka, ukimshika paja linatelezaa tu, ukimnong’oneza mpaka nywele za kichwani zinasimama, ukimbinya hata sauti inabadilika “mm m-mm-e wangu” Ukimaliza anashukuru na siku hazifanani siku ‘ukiwaza kodi na kununua kiwanja madale’ haujamfikisha hata halalamiki yani moyo mweupe tena na mabusu mengi na anashukuru sana “asante mume wangu” basi mie walahi moyo wangu una rahaaa. Pale ninapomuita mke wangu anavyonijibu “abeeeeee mume wangu” mie mpaka machozi yanatoka yani unajikuta naridhika sana sio kunenepa huku kwa kula manyama hapana basi tu mapenzi yake yananinenepesha. Nikimkumbuka ex hata ukimwita anaitika "nini", hata hajui unamwitia nini. Kuna siku nilikuja na chakula kwenye kifungasho nikamwambia fungua begi langu kuna ndizi za kuchoma nimekuwekea, alinijibu "sili mandizi mimi" kumbe nilikuwa nimemletea nyama ya mbuzi, mapenzi yalikuwa mabovu mno..

Yule ex kwenye nne kwa sita, yani kwanza lazima ujiandae kama unakwenda kushiriki ndondi. Usipojiandaa lazima ufeli, maana unaumiza kichwa sana na unatumia nguvu nyingi kumridhisha. Mana hata kumuandaa unakuta unashika chuchu anakuangaliza, unanyonya yeye ndo kwanza asubuhi, sasa basi shika wewe wapi, shika ziwa shika tako shika nywele wapi yani kwa kipindi kile mwisho nikajikuta nimemshikisha MIMBA. Vingine wala hashikiki. Siku umechoka na mawazo mengi “Man U imefungwa’ na mie mechi lazima nipoteze. Nakumbuka siku nachomeka wazungu hao, nikambembeleza kipindi cha pili nachomeka dakika kumi tu wajapani hao, akanuna nikabembeleza sasa kipindi cha dakika ya nyongeza nachomeka dakika moja tu ile wabongo haooo nakwambia nilikula makofi aisee siwezi sahau. Yule ex anapiga makofi kama nyani vile, kupenda huku kuna gharama, kesho yake nikaenda chukua vumbi ya Kongo nikanunua mechi hapo yakaisha ila hisia hazikuwepo, lile vumbi noma mechi ilichezwa mpaka majeruhi ndo mpira ukaisha...

Wakati wa kula mke wangu huwa ananinawisha mikono na hali chakula kwanza mpaka nitie mkono mie. Tena labda chai huwa ndo anakunywa yeye kwanza na ananikaribisha. Nikichelewa kazini usiku labda saa tano si unajua kazi zetu za uhasibu hizi, basi atanisubiria mpaka nirudi na kama kala basi anakula vijiko viwili anasubiri tuje tule wote. Yule ex alikuwa anakula nikirudi nijipakulie yani hatakia amshwe namuharibia ndoto zake nzuri. Kwa ex hata mikono nilikuwa sinawishi unanawa mwenyewe, sahani hatoi mezani mnaweza kaa mnatazamana tu unajikuta unatoa. Kuna siku tumekula samaki na wale samaki walikuwa na mifupa kweli kweli, basi ile sijui anaona namaliza kwenye sahani basi zile papara papara si akala mwiba bhana. Ule mwiba ulimtesa nikasema naenda kuzika maana alimeza tonge saba za ugali ndo mwiba ukatoka. Na nikajua wale waliobaki hatokula mweee si akaanza kugonga wale samaki mie moyoni najisemea nilikosea wapi huyu mwanamke. Simsingizii kwa kweli alikuwa mroho sana, maana kama akila nyama ya mfupa basi anaona unamchelewesha anauweka pembeni anagonga nyama nyingine chakula kikiisha alikuwa anarudia ile mifupa basi anainyonya kwa kweli nikikumbuka sijui alikuwa fisii….

Basi siku moja tumeenda kula mgahawani na ex, ile tunaagiza chakula, mie nikaagiza ndizi nyama mwenzangu kaagiza wali njegere. Basi tunakula mie nikawa napiga matonge nashangaa mwenzangu katenga njegere pembeni kagonga wali kamaliza kanywa soda kamaliza, sasa akawa anakula njegere moja moja kama karanga vile nilichukia. Alafu kula yake anakula kama anafukuzwa akila na mkono mie simwelewi mara akate ugali tonge kubwa alafu mkononi analigawa mara mbili anameza lile la kwanza huku anafinyanga la pili kama chakula kitaisha mapema, ulaji wake ulikuwa hauvutii hata kidogo. Lakini mke wangu hagusi chakula bila kuomba maana usikute tunakula chakula kimoja na shetani tukashindwa shiba. Lazima akibariki chakula ‘eh mola kibariki chakula hiki kitupe nguvu ya kuweza kukutumikia milele Amina...

Baada ya kula ex hanawi mikono kwanza unamkuta anakaa pembeni ananyonya madole yake sijui utamu wa chakula uishe. Unaweza kuona sawa ila wageni wakija inakuwa kero mtu kakaaa chini kazi kunyonya madole tuuuu. Yule ex unakuta umenunua kuku umeenda kazini ile umerudi kazini unajua umeacha kuku nyumbani unakuta kala paja zote ameacha sijui vimbavu na kichwa. Mke wangu yani tabia za kula jikoni hana Zaidi tu ya kuonja chumvi kama imekolea. Kuna siku tulipika nyama basi sasa yani mie sijala hata moja nakula tonge la ugali yeye kala nne, mie nikajisemea moyoni ngoja nione atakula ngapi, alivyokuwa boya alikula nyama zote, ile anajiuliza kama nimekula nyama maana kwake alipokaa kulikuwa na mifupa mingi wakati kwangu hakukuwa na mfupa hata mmoja, eti anajiuliza kwani umekula nyama, huku anameza ile nyama ya mwisho. Siku hiyo nilimuona kama mchawi….

Tuko kwenye daladala tumesimama huyu mke wangu kama kuna siti moja huwa lazima aniite “mume wangu, njoo ukae”. Ila kwa upendo na kwa kuwa mie ni gentleman huwa namwambia “kaa mke wangu” au nikiwa nina hamu ya kumpakata basi nakaa nampakata mapenzi mubashara. Ila yule ex yani tulivyokuwa kwenye daladala mtu kasimama basi unakuta ile siti tunaigombania wakati mie nilikuwa nataka nikae ili nimpakate. Mke wangu tukiwa barabarani ananishika mkono basi tunakuwa kama vipepeo, watu wanatuoneaje wivu. Yule ex kuna siku tuko njiani tukakutana na watu niliowahi soma nao basi si akajisahau akajamba. Baada ya kuvunga mana nilikuwa napotezea kwa wale jamaa niliosoma nao, si akaropoka ‘Gilly najisikia kuharisha’. Nilisikia aibu sana na sio mara ya kwanza kuniabisha. Kuna siku weekend niko kijiweni na masela eti katuma mtoto wa jirani aje kuniomba hela ya unga robo, nikamjibu ‘mwambie nakuja’. Naye akamtuma yule mtoto nenda usubirie pale pale mpaka akupe Yani wale vijana niliwaza watanifikiria kwamba situnzi familia yangu mana mie mtu na heshima zangu; wakti siku zote naacha hela mezani…

Kwa mke wangu ananipikia mapocho pocho sana tena kwa jinsi navyopenda kula. Usiku huwa anapika chapati na mchuzi na juisi kama navyopenda, tena wali wa nazi na kismvu. Ila pale anapopika kisamvu cha karanga jamani kwa kweli ni kitamu sana mtu asikwambia. Katika mapishi yote hakuna chakula kitamu kama wali na kisamvu cha karanga weeeeeee. Nikikumbuka yule ex chakula kila siku kilikuwa na kasoro, ukimuliza kwa nini maharage yameungua “eti aliinjika sufuria ya maharage jikoni bila maji” sijui alikuwa anataka kukaanga. Ushawahi ona wapi mtu anatia ndimu kwenye wali, au samaki anampika bila kumpaa kwa kweli hakuna siku nayoijutia kama kula samaki ambae hajatolewa magamba. Yani wale samaki kila nikila ilikuwa kama nakula ndala vile ulimi ulikatika sana damu zilitoka nyingi, siwezi sahau nakumbuka machungu mie…

Mimi binafsi kuvaa shati la kitenge kwa kweli na mwanamke awe mke au nani sipendi huku mwanamke kashona kagauni. Nikiwaonaga watu barabarani wamevaaa ivyo siwaelewagi ila kwa mapenzi anayonipa mke wangu basi nahakikisha mwaka huu tukienda kanisani basi lazima nivae shati la kitenge huku yeye anavaa gauni la kitenge. Ila kwa yule ex hapana kwa kweli nisingeweza kufikiria hivyo, simsemi vibaya au kumjungua namshukuru sana kuna mabaya mengi aliniepushia mfano sikuwa mtu wa kuhangaika na wanawake ovyo. Ila kwa kweli hakunifanya niwaze maendeleo hata kidogo. Kwa mke nimefanya makubwa mengi sana tena kwa mda mfupi. Nawashauri vijana wenzangu bora ukosee kunyoa kuliko kukosea kuoa. Fanyeni fikra za busara na Mungu awabariki wote mnaosoma ujumbe huu mpate mwanamke bora na kama ni mwanamke wapate wanaume sahii. .

Nasisitiza: Heshima haiuzwi dukani tuheshimiane, nafurahi sana kwamba JF imetukutanisha na kunazungumza na kucheka pamoja ni jambo la Kheri. Wako watu wengi huko Libya au Syria hawana nafasi kama zetu, tusitoleane maneno ya kashfa au kubezana. Kwenye huu uzi tucheke pamoja na kufurahi pamoja. .

Kissing na mke unakuwa na hamu tu ya kumkiss. .
1582123732582.png


1582123766368.png



Ex alikuwa anakisi kama anakula muwa vilee alafu michezo ya kukisiana asubuhi kabla hatujapiga miswaki dah. .
1582124851157.png


1582125140908.png
 
Piga nyagi mpaka jamaa aliyeweka mikono juu kwa chupa ashushe mikono chini. Labda atakuozesha mwanae, ile mikono atakuwa amechoka kuiweka kichwani mana ameiweka kitambo......
I am on to the next one
 
Nadhan ex wako ndo nimemuoa mimi...duh!

Sent using Jamii Forums mobile app

Mwanangu, kuna jamaa anaendesha bajaji juzi alikuwa ananiambia siku akikosa hela mkewe anayefanya kazi akitoa hata elfu mbili, kesho yake anaporudi kazini jamaa lazima alipe. Yule dada ana gubu sana aisee, kuna mda kabla hujaoa unamuona anafaa sana ile ukimuoa anatoa makucha yake. Pole sana ndugu ndo maisha hayo wewe jitahidi tu kumuelimisha, ukielimisha mwanamke mmoja wanadai kuwa unaelimisha jamii. Watoto tu wasije kuwa kama mama yao. .
 
Kitanda changu ni nne kwa sita, mke wangu aisee ana staha sana. Kinachofurahisha Zaidi ukimshika mgongo nywele zinasisimka, ukimshika paja linatelezaa tu, ukimnong’oneza mpaka nywele za kichwani zinasimama, ukimbinya hata sauti inabadilika “mm m-mm-e wangu” Ukimaliza anashukuru na siku hazifanani siku ‘ukiwaza kodi na kununua kiwanja


Ex alikuwa anakisi kama anakula muwa vilee alafu michezo ya kukisiana asubuhi kabla hatujapiga miswaki dah. .
View attachment 1363001

View attachment 1363012
Kama hujawahi kuona watu wanaojinyonga na kujiua kisa mapenzi ni mtu kama ww, mwanamke anaweza kukwambia kesho tu kwamba tuachane. utalia sana kama mambo ya hamida. ni vizuri kutumia akili kuishi nao
 
kama hujawahi kuona watu wanaojinyonga na kujiua kisa mapenzi ni mtu kama ww, mwanamke anaweza kukwambia kesho tu kwamba tuachane. utalia sana kama mambo ya hamida. ni vizuri kutumia akili kuishi nao

Hahaha kwa sababu nimependa sana au? To love is not a crime, if someone leaves me for loving them definitely shame on them. .

Ina maana google helper wewe hujawahi kupenda????? Ila ulichosema ni sahihi hutakiwi kumpenda mtu ambaye hakupendi. Hawezi na haiwezi tokea mtu akaamka asubuhi akakutamkia hakupendi, lazima kutakuwa na jambo tu, unless hakukupenda toka mwanzo. .
 

Similar Discussions

10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom