Kwako bwana Silinde, siyo kweli kwamba dawa zinaibiwa kwenye Hospitali za Umma

Kinoamiguu

JF-Expert Member
Nov 29, 2018
10,526
13,013
Bwana David Silinde popote ulipo.

Hongera kwa kuula. Umeula uwaziri. Mpe Salaam ndugu waitara. Mwambie wanawaukonga na wapenda mabadiliko wote wanakumbuka michango na kujitolea kwai hata akawa mbunge. Kumbe leo amerejea nyumbani nae sasa ni Waziri ameulamba.

Bwana silinde asubuhi nilikusikia ukidanganya bungeni. Sijui kwa faida ya nani? Uliulizwa swali juu ya upungufu wa wataalamu wa afya na dawa. Hilo ni tatizo sugu kwenye hospitali za umma. Ukajibu kwa mbwembwe kwamba "Luna watumishi wasio waaminifu wanaiba dawa" sijui kwamba huwa mnafanya Tafiti au majibu ya kisiasa tu.

Ukweli ni kwamba hakuna dawa zinaibiwa ila dawa hazipelekwi za kutosha huo ndio ukweli. Serikali ya ccm imeshindwa kutenga bajeti ya kutosha ya kununulia dawa na vitendanishi badala yake wanajisifia kujenga Majengo wanayoyaita Vito vya " afya" kituo cha afya bila dawa. Katika kukabiliana na wizi huu wa dawa kama upo. Walikuja na mpango wa kuzipiga nembo za MSD dawa zote za serikali!

Je ile nembo haisaidii kuendelea kuwaita?
 
inategemea na aina ya dawa, kuna vidonge vinapigwa nembo tokea kiwandani zinapo zalishwa, nyingine ni kwa nje inawekwa lebo, alama au rangi fulani
Wacha kudanganya bwana!

Kutokana na jina lako inawezekana ukwa unatokea huko kwenye madawa, lakini hii habari ya "vidonge kupigwa nembo tokea kiwandani", ni uongo mtupu.

Hao watengenezaji wa dawa hizo utawalipa kiasi gani wakuwekee nembo yako kwenye hizo dawa? Ni wewe pekee utakuwa unanunua hizo dawa kwao, na kwa muda gani?

Zamani kulikuwa na vidonge, kwa mfano vina nembo juu yake ya 'MSD', Merk Sharp Dohm - hiyo ilikuwa zamani, na nembo hiyo ilikuwa ni ya kampuni, siyo ya muuziwa hizo dawa.

Wanachoweza kufanya MSD ni kuweka alama tu kwenye maboksi au hata kwenye vichupa vya dawa za sindano (wakitaka), lakini zoezi hilo litawaongezea gharama kubwa sana.

Inashangaza na kusikitisha kwamba, enzi hizi za teknologia bado serikali inahangashwa na wizi wa kijinga wa aina hii huko mahospitalini kwake.
Kwa nini wasipeleke tu watu wao wakajifunze kwenye hospitali binafasi wanavyodhibiti madawa na vifaa vyao visiibiwe?

Waende tu pale Shree Hindu Mandal waone jinsi wanavyobana matumizi ya hovyo ya dawa zao.
 
Kama kuna ushahidi kwamba wanaiba msiwalaumu.
Mtu wa afya alipwe 500,000 kwa mwezi.
Mbunge hiyo anapata kwa siku halafu bado anadai hazitoshi wakati kazi yake nikupiga meza tu.
 
Wacha kudanganya bwana!

Kutokana na jina lako inawezekana ukwa unatokea huko kwenye madawa, lakini hii habari ya "vidonge kupigwa nembo tokea kiwandani", ni uongo mtupu.

Hao watengenezaji wa dawa hizo utawalipa kiasi gani wakuwekee nembo yako kwenye hizo dawa? Ni wewe pekee utakuwa unanunua hizo dawa kwao, na kwa muda gani?

Zamani kulikuwa na vidonge, kwa mfano vina nembo juu yake ya 'MSD', Merk Sharp Dohm - hiyo ilikuwa zamani, na nembo hiyo ilikuwa ni ya kampuni, siyo ya muuziwa hizo dawa.

Wanachoweza kufanya MSD ni kuweka alama tu kwenye maboksi au hata kwenye vichupa vya dawa za sindano (wakitaka), lakini zoezi hilo litawaongezea gharama kubwa sana.

Inashangaza na kusikitisha kwamba, enzi hizi za teknologia bado serikali inahangashwa na wizi wa kijinga wa aina hii huko mahospitalini kwake.
Kwa nini wasipeleke tu watu wao wakajifunze kwenye hospitali binafasi wanavyodhibiti madawa na vifaa vyao visiibiwe?

Waende tu pale Shree Hindu Mandal waone jinsi wanavyobana matumizi ya hovyo ya dawa zao.

Mkuu umepuyanga hapo kwenye lebo za MSD, na kwa mbwembwe mno unamkemea mdau eti muongo!

Jiruhusu kujifunza.
 
Mkuu umepuyanga hapo kwenye lebo za MSD, na kwa mbwembwe mno unamkemea mdau eti muongo!

Jiruhusu kujifunza.
EeenHeee,
Hivi nyinyi watu mmekuwaje wapuuzi kiasi hiki? Hii nchi mnaipeleka wapi na watu wa aina hii!

Mimi ninakueleza, nikiwa na asili mia ya uhakika ninachokizungumzia. Wewe unapinga, hata kueleza tu unachojuwa huweki, bali unaacha mipasho tu! Ni kipi umeweka hapa ambacho unanihimiza "nijiruhusu kujifunza"? Kuna kipi alichoeleza niliyemjibu ambacho unaona sikijui, na unataka nijifunze?

Kwa hiyo, kama mimi ni mwongo, mwite huyo unayemwamini na nyote kwa pamoja tujadili ukweli wa jambo hili. SAWA!

Mwite aje hapa na wewe mueleze MSD wanawezaje kuweka nembo yao kwenye vidonge na 'capsules' na dawa za maji maji za kunywa kwa mdomo na zile za sindano; waweke nembo yao, sijui wataanzia wapi kwa vile wao siyo watengenezaji wa dawa hizo! Haya siyo mashuka ya kuwekewa alama kama yale unayoyaona kwenye mashuka hospitalini.

Wewe hapa hujui hizo dawa zinatengenezwa vipi, lakini unajitia kimbelembele uonekane ni mjuwaji!

Na mtu kama wewe unaweza kabisa ukawa upo huko serikalini ukiongoza idara fulani, kwa ujinga namna hii, halafu tutegemee taifa hili litasonga mbele!

Ni hatari kubwa sana kwetu.
 
Bwana David Silinde popote ulipo.

Hongera kwa kuula. Umeula uwaziri. Mpe Salaam ndugu waitara. Mwambie wanawaukonga na wapenda mabadiliko wote wanakumbuka michango na kujitolea kwai hata akawa mbunge. Kumbe leo amerejea nyumbani nae sasa ni Waziri ameulamba.

Bwana silinde asubuhi nilikusikia ukidanganya bungeni. Sijui kwa faida ya nani? Uliulizwa swali juu ya upungufu wa wataalamu wa afya na dawa. Hilo ni tatizo sugu kwenye hospitali za umma. Ukajibu kwa mbwembwe kwamba "Luna watumishi wasio waaminifu wanaiba dawa" sijui kwamba huwa mnafanya Tafiti au majibu ya kisiasa tu.

Ukweli ni kwamba hakuna dawa zinaibiwa ila dawa hazipelekwi za kutosha huo ndio ukweli. Serikali ya ccm imeshindwa kutenga bajeti ya kutosha ya kununulia dawa na vitendanishi badala yake wanajisifia kujenga Majengo wanayoyaita Vito vya " afya" kituo cha afya bila dawa. Katika kukabiliana na wizi huu wa dawa kama upo. Walikuja na mpango wa kuzipiga nembo za MSD dawa zote za serikali!

Je ile nembo haisaidii kuendelea kuwaita?
Kwani ww unaushahidi gani kuwa dawa hazibwi?
 
Kalamu1
Heshima mbele.

Hoja haikuwa kuweka lebo kwenye kila kidonge au capsule, hiyo ni wewe ulitoa kama mfano ukijaribu kufafanua hoja yako uliyoijenga kuwa haiwezekani kufanya hivyo ….kwa maana itaongeza gharama na serikali haina uwezo wa kumudu hilo.

Nilikuelewa hapo?

Hivyo basi, mimi niliingilia hapo… lengo ikiwa ni kupinga hoja yako haiko sahihi.

Ni kweli kuwa dawa haziwekwi lebo kwenye kila kidonge, bali kila pakiti (wewe uliita boksi).

Pia ni kweli kuwa lebo hizo huwekwa tangu huko huko kiwandani.

Lakini si kweli kwamba uwekaji wa lebo huongeza gharama, kama ni hivyo basi gharama hizo huwa zimejumuishwa kwenye makubaliano.

Kabla sijaendelea, naomba nikuulize swali moja la msingi:

Je, unajua utaratibu unaotumika na serikali kuagiza dawa kupitia?

Karibu.
 
Kalamu1
Heshima mbele.

Hoja haikuwa kuweka lebo kwenye kila kidonge au capsule, hiyo ni wewe ulitoa kama mfano ukijaribu kufafanua hoja yako uliyoijenga kuwa haiwezekani kufanya hivyo ….kwa maana itaongeza gharama na serikali haina uwezo wa kumudu hilo.

Nilikuelewa hapo?

Hivyo basi, mimi niliingilia hapo… lengo ikiwa ni kupinga hoja yako haiko sahihi.

Ni kweli kuwa dawa haziwekwi lebo kwenye kila kidonge, bali kila pakiti (wewe uliita boksi).

Pia ni kweli kuwa lebo hizo huwekwa tangu huko huko kiwandani.

Lakini si kweli kwamba uwekaji wa lebo huongeza gharama, kama ni hivyo basi gharama hizo huwa zimejumuishwa kwenye makubaliano.

Kabla sijaendelea, naomba nikuulize swali moja la msingi:

Je, unajua utaratibu unaotumika na serikali kuagiza dawa kupitia?

Karibu.
Ahsante kwa kunikaribisha.

Nieleweshe vizuri kwanza.
1. Unasema ulielewa kuhusu ugumu wa kuweka nembo (siyo lebo) kwenye kidonge , n.k.; halafu unaeleza "uliingilia hapo, kupinga hoja yangu". Sasa sielewi ulielewa kipi na kwa vipi unapinga ulichokielewa. Hapa unachanganya kidogo.

Ukweli ni kwamba MSD itawawiya vigumu sana kuingia mkataba wa kuweka nembo yao kwa vitu hivyo na kampuni zinazotengeneza dawa hizo, gharama zake zitakuwa kubwa na pengine hata mikataba hiyo italazimu iwe ya muda mrefu.

Unasema kuwa "Sikweli kwamba uwekaji wa "lebo", 'NEMBO' huonheza gharama. Sijui una maana gani na hili, maanake sioni jinsi gani itazuia kuongeza gharama, kwa sababu ni kazi ya ziada, na mahitaji ya kuziandaa hizo nembo ni lazima zitakuwa na gharama, hakuna kitu cha bure viwandani, tokea wafanya kazi na mali ghafi, na muda. Kwa hiyo katika hili pia hupo sahihi kabisa, gharama ni lazima iongezeke, na hii lazima imfikie mlaji wa mali hiyo.

Sawa, gharama zinaweza kuwekwa kwenye "makubaliano", ambayo ni lazima gharama zilipiwe humo humo kwenye makubaliano hayo.
Kwa hiyo ujue kwamba dawa za MSD zitakuwa ni za ghali zaidi kutokana na gharama hizi zinazoongezeka kwa kuweka nembo.

Umeniuliza swali, unalosema kwamba ni la msingi: Kama ninajuwa "utaratibu unaotumika na serikali kuagiza dawa kupitia?"

Hapa sijui unataka nieleze utaratibu wa 'tender' au nitaje tu kwamba serikali hukaribisha 'tender' na wanaoshinda hiyo tenda hupewa jukumu la kuiuzia serikali kwa makubaliano ya tenda hizo.

Waomba tender hao yanaweza kuwa makampuni yanayotengeneza dawa au kampuni zinazojihusisha na ununuzi na uuzaji wa mali hizo; wao wanaweza kujuwa watakapozipata mradi zikidhi matakwa.

Sasa sijui hapa unataka nieleze utaratibu vipi zaidi ya hivyo.

Nilipoelezea uwekaji wa 'nembo' kwenye 'unit dose' kama kidonge, huu huwa ni utaratibu wa kawaida unaotumika na makampuni yanayotengeneza madawa. Kwao inawawia rahisi kufanya hivyo kwa sababu vifaa wanavyovitumia kutengeneza dawa hizo zinatumika kuzalisha kwa kiasi kikubwa sana, na siyo kwa mteja mmoja mmoja. Nilitoa mfano wa Merk Sharpe & Dohme (MSD) na vidonge vyake vya Aldomet wakati ule. Gharama za kuchonga 'punch' mpya za kutengenezea nembo za "Medical Stores Department" (MSD) ya Tanzania kwa Kampuni iliyoshinda Zabuni kuleta dawa zake Tanzania ni lazima itakuwa ni kubwa, kwa sababu, kwanza ni limited supply, tena kwa muda maalum. Na elewa kwamba, siyo swala la kuweka nembo tu kwenye hizo 'punches' (vyuma vya kutengenezea hizo dawa), ni lazima kuvfanya utafiti wa utengenezaji kwa kutumia vyuma hivyo vyenye nembo mpya, kama havitaathiri ubora wa 'formulation' iliyokwishatengenezwa na kuonekana inafaa.

Hata kuweka maandishi kwenye 'vials, na 'ampules', elewa kwamba kazi hizo ni 'automation'. Mabadiliko yoyote yanapofanyika ni lazima mfumo mzima urekebishwe.

Sasa basi, kama wewe unazungumzia kuweka mhuri wa 'MSD' juu ya viboksi vya nje, hiyo ni kazi rahisi inayoweza kufanyika hata hapo hapo MSD penyewe, lakini haitazuia wizi, kwa sababu chupa zitafunguliwa na dawa kumiminwa kwenye chupa zingine.

Nimekwishaeleza, swala la wizi wa madawa katika hospitali za serikali dawa yake ni rahisi sana. Ni swala la kutokuwa na utashi tu wa kulimaliza tatizo hilo. Teknologia iliyopo sasa inaziba kabisa mianya ya wizi wa dawa mahospitalini.
 
Ahsante kwa kunikaribisha.

Nieleweshe vizuri kwanza.
1. Unasema ulielewa kuhusu ugumu wa kuweka nembo (siyo lebo) kwenye kidonge , n.k.; halafu unaeleza "uliingilia hapo, kupinga hoja yangu". Sasa sielewi ulielewa kipi na kwa vipi unapinga ulichokielewa. Hapa unachanganya kidogo.

Ukweli ni kwamba MSD itawawiya vigumu sana kuingia mkataba wa kuweka nembo yao kwa vitu hivyo na kampuni zinazotengeneza dawa hizo, gharama zake zitakuwa kubwa na pengine hata mikataba hiyo italazimu iwe ya muda mrefu.

Unasema kuwa "Sikweli kwamba uwekaji wa "lebo", 'NEMBO' huonheza gharama. Sijui una maana gani na hili, maanake sioni jinsi gani itazuia kuongeza gharama, kwa sababu ni kazi ya ziada, na mahitaji ya kuziandaa hizo nembo ni lazima zitakuwa na gharama, hakuna kitu cha bure viwandani, tokea wafanya kazi na mali ghafi, na muda. Kwa hiyo katika hili pia hupo sahihi kabisa, gharama ni lazima iongezeke, na hii lazima imfikie mlaji wa mali hiyo.

Sawa, gharama zinaweza kuwekwa kwenye "makubaliano", ambayo ni lazima gharama zilipiwe humo humo kwenye makubaliano hayo.
Kwa hiyo ujue kwamba dawa za MSD zitakuwa ni za ghali zaidi kutokana na gharama hizi zinazoongezeka kwa kuweka nembo.

Umeniuliza swali, unalosema kwamba ni la msingi: Kama ninajuwa "utaratibu unaotumika na serikali kuagiza dawa kupitia?"

Hapa sijui unataka nieleze utaratibu wa 'tender' au nitaje tu kwamba serikali hukaribisha 'tender' na wanaoshinda hiyo tenda hupewa jukumu la kuiuzia serikali kwa makubaliano ya tenda hizo.

Waomba tender hao yanaweza kuwa makampuni yanayotengeneza dawa au kampuni zinazojihusisha na ununuzi na uuzaji wa mali hizo; wao wanaweza kujuwa watakapozipata mradi zikidhi matakwa.

Sasa sijui hapa unataka nieleze utaratibu vipi zaidi ya hivyo.

Nilipoelezea uwekaji wa 'nembo' kwenye 'unit dose' kama kidonge, huu huwa ni utaratibu wa kawaida unaotumika na makampuni yanayotengeneza madawa. Kwao inawawia rahisi kufanya hivyo kwa sababu vifaa wanavyovitumia kutengeneza dawa hizo zinatumika kuzalisha kwa kiasi kikubwa sana, na siyo kwa mteja mmoja mmoja. Nilitoa mfano wa Merk Sharpe & Dohme (MSD) na vidonge vyake vya Aldomet wakati ule. Gharama za kuchonga 'punch' mpya za kutengenezea nembo za "Medical Stores Department" (MSD) ya Tanzania kwa Kampuni iliyoshinda Zabuni kuleta dawa zake Tanzania ni lazima itakuwa ni kubwa, kwa sababu, kwanza ni limited supply, tena kwa muda maalum. Na elewa kwamba, siyo swala la kuweka nembo tu kwenye hizo 'punches' (vyuma vya kutengenezea hizo dawa), ni lazima kuvfanya utafiti wa utengenezaji kwa kutumia vyuma hivyo vyenye nembo mpya, kama havitaathiri ubora wa 'formulation' iliyokwishatengenezwa na kuonekana inafaa.

Hata kuweka maandishi kwenye 'vials, na 'ampules', elewa kwamba kazi hizo ni 'automation'. Mabadiliko yoyote yanapofanyika ni lazima mfumo mzima urekebishwe.

Sasa basi, kama wewe unazungumzia kuweka mhuri wa 'MSD' juu ya viboksi vya nje, hiyo ni kazi rahisi inayoweza kufanyika hata hapo hapo MSD penyewe, lakini haitazuia wizi, kwa sababu chupa zitafunguliwa na dawa kumiminwa kwenye chupa zingine.

Nimekwishaeleza, swala la wizi wa madawa katika hospitali za serikali dawa yake ni rahisi sana. Ni swala la kutokuwa na utashi tu wa kulimaliza tatizo hilo. Teknologia iliyopo sasa inaziba kabisa mianya ya wizi wa dawa mahospitalini.
Mimi nashughulika na mifumo ya ulinzi(security systems), Serikali haiku serious kulinda Mali Zale.
 
Mimi nashughulika na mifumo ya ulinzi(security systems), Serikali haiku serious kulinda Mali Zale.
Mkuu, ninakubaliana na wewe kwa asili mia moja.

Na kwa bahati mbaya sana mkuu, siyo mambo ya ulinzi tu, sijui ni wapi ambako tunaweza kusema kwamba serikali inafanya vizuri. Mi nadhani tunaelekea kwenye mgongano mkubwa sana utakaokuja kulitikisa taifa hili.
 
Huo ndiyo ukweli dawa hazitoshi...

Alafu zilizopo zinaharibika tu huko kwenye mabohari yao kwa uzembe wa ucheleweshawji...
 
Bahati mbaya kila mtu anajua kila kitu.
Dawa zinaibwa sana tena sio kidogo hasa za misaada. Pia uagizaji wa dawa, kuna wakati wazalishaji hupokea oda kisha wakazalisha.
Gharama za kuweka label kwenye vidonge sio kubwa hivyo.
Pamoja na mtu kuwa katibu wa afya eneo lako, tambua kwako unafahamu kiasi kidogo tu juu ya kinachoendelea nchini.
 
Back
Top Bottom