Kwahiyo wana Yanga SC duniani kote tumekubali hii ' Kashfa ' isiyovumilika kutoka kwa Injinia Hersi Said wa GSM dhidi yetu?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,542
108,852
" Tumeitoa Yanga SC Uswahilini pale Manzese wakiwa na hali mbaya, Njaa wakila Maharage na Ugali wa Kugombania na Wanang'atwa na Mbu na sasa tumewaweka pale Avic Town Kigamboni wanakula vizuri sana "

Yaani wana Yanga SC wote kama kuanzia Usiku huu na mpaka Kesho hatujamfukuza Injinia Hersi Said na GSM yake Yanga basi Mimi GENTAMYCINE nahamia rasmi Simba SC kwa Mo Dewji ambako kuna Raha, Utamu, Heshima na Mafanikio.

Injinia Hersi katutukana vjbaya sana tu.
 
" Tumeitoa Yanga SC Uswahilini pale Manzese wakiwa na hali mbaya, Njaa wakila Maharage na Ugali wa Kugombania na Wanang'atwa na Mbu na sasa tumewaweka pale Avic Town Kigamboni wanakula vizuri sana "

Yaani wana Yanga SC wote kama kuanzia Usiku huu na mpaka Kesho hatujamfukuza Injinia Hersi Said na GSM yake Yanga basi Mimi GENTAMYCINE nahamia rasmi Simba SC kwa Mo Dewji ambako kuna Raha, Utamu, Heshima na Mafanikio.

Injinia Hersi katutukana vjbaya sana tu.
Hakuna kashfa yoyote hersi aliyofanya,ila wewe ndio una ajenda yako ya kutaka kuleta chokochoko yanga,hitafanikiwa
 
Wewe inakuuma nini?mbona Muddy aliitoa Mbumbumbu SC mikononi mwa Kaduguda mkila mahindi ya kuchemsha na kutumia koni zake za mazoezi na hatujatangaza mpaka ikafikia akadai hela zake za chai na mihogo ya kukaanga

Sent using Jamii Forums mobile app
Tena Kaduguda anadai pesa za matikiti maji alizotumia kuwanunulia wachezaji wale wasife njaa.

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu, unafikiri hii ni " kashfa" basi!

Huu ni ukweli mtupu, japo kaongeza chumvi kiasi chake.

Nini maana ya kashfa?

-Ni namna ya kutumia maneno au vitendo visivyo vya kweli kwa nia ya kumfua mtu au watu fulani.

Ila kusema kweli, Yanga wanachezewa sana na viongozi wao, Sponsor wao hadi msemaji wao.

Utopolo
 
Back
Top Bottom