Kwaherini wana_Forum

Ngida1

JF-Expert Member
Aug 25, 2009
586
206
Ndugu Wana_Forum,

Hapo nyuma kuna mwana-Forum mmoja ambae alisema kuwa anataka kuihama nchi kutokana na kero za siasa zetu za CCM zisizo na mipango ambazo zinamdhalilisha mwananchi kuwa maskini kila siku. Mimi kwa mchezo nilikuwa wa mwanzo kumcheka kwenye hio thread yake. Leo, nami ninataka kuihama sio nchi bali hii Forum kwasabau naona afya yangu itaathrika kutokana na siasa mbovu za hii nchi yetu chini ya CCM.

Leo kwa mara ya mwanzo niliona ile picha ya wanafunzi wa Mbagala wakisoma shule nje kwenye mchanga bila ya madeski na machozi yalinioka - yalinitoka machozi nikukumba 540,000 Sterling Pounds alizokutwa nazo Chenge na mabilioni ambayo akina Rostam wanazo. Baada ya kuiona hii picha nikaona bora nitoke kwenye hii Forum, kwani kila siku naona habari ninazozipata zinanitia uchungu kiasi ambacho afya yangu inaathirika, kutokana na pressure yangu bure bure kupanda. Kwahivyo, nimeamua bora kutoka kwenye hii Forum kabla sijapata heart attack kutokana na stress ninyoipata kutokana na news ninazozisoma hapa kwenye hii Forum. Sitaki tena kusoma habari zozote zile za hii nchi yangu kwani kila mara ninaposoma naona maisha yangu yanakuwa hatarini.

Kwahivyo, kwa wale marafiki zangu wa hapa kwenye hii Forum na wale watani wangu akina Lampart na wengine ninawaeleze kuwa mimi hawatoniona tena na yule ambae atataka kuniona basi awasiliane na mimi kwenye hii private email address yangu:
<ngida1@hotmail.com>

Nimeona bora nitokane na hii Forum kwasababu kila siku presssure yangu inapanda. Kwa yoyote atakaewasiliana na mimi kwenye private address yangu basi tafadhali asinieleze chochote kuhusu maendeleo ya siasa ya hii nchi. Labda mtu ataweza kunielezea bei mpya ya bia, massage parlours mpya zilizofunguliwa, etc etc etc

Kuhusu siasa sitaki kusikia chochote kutoka mtu yoyote yule. Sitaki kusikia kabisa habari kama vile watu wametembelea shamba la mifugo la Raisi huko Bagamoyo, kwasababu sifahamu kwanini Rais atakuwa kwenye Miradi kama hio. Kama 5 million kwa mwezi hazimtoshi basi ni kusema mtu na State itamuengezea. Kila mtu anafahamu kuwa ukiwa mwenye Miradi basi ni lazima upoteze 60% ya time yako huko kwenye Miradi yako japokuwa unao wafanyakazi 1000. Sijui kama Raisi mwenye Miradi anapata wakati wa kushughulikia kero za wananchi. Labada pengine hata hajui kama wanafunzi kule Mbagala wanakaa chini bila ya madeski!

Anyway, wale niliowakera hapa kwenye hii Forum kama akina ndugu yangu Mzee Bubu Ataka Kusema na akina Nd. Lampart ninawaomba samahani sana na wale tutakaoendelea kuwasilian basi wajue kuwa there will be no politics in our discussions. Sitaki kupata heart attack at this young age.

Kila la kheri / Ngida1
 
Kwa vile huyu Ngida anawaogopa mafisadi,anataka kutoka Jamii Forums. Mafisadi watamuharibia afya yake. Kuanzia sasa,anataka ''safe'',yaani kunywa pombe na kufanya massage.

Ina maana hawa mafisadi ni very dangerous,ikiwa mtu anadhani kulewa chakari kila siku,itakuwa much safer kuliko kubishana na mafisadi. Ukishaanza tu kusema,mafisadi ni dangerous,''the syndicate will kill someone'',,then all these people gravitate towards these carnal matters.That is the way it seems to me.
 
I say, Ndugu Ngida1, huwezi kabisa kutuacha mimi na Ndugu Bubu Ataka Kusema peke yetu hapa kwenye hii Forum. Tunajua news za hapa zinakutia pressure, lakini tutafanya nini hii ndio nchi yetu jamani?. Yule ndugu mwengine kakimbilia Botswana na wewe unataka kutoka kwenye hii Forum, sasa jamani nchi hii ataiendeleza nani? Hao akina Waungwana, akina Chenge na akina Rostam wewe usiwe na wasiwasi nao. Wao wanakuja na kupotea kama walivyopotea wengine, lakini we cannot afford to miss you.

Mimi pamoja na Nd. Bubu Ataka Kusema tunakuangukia chini ya miguu yako ili ubakie hapa kwenye hii Forum. Kila mtu akihama kutokana na mambo ya Muungwana na rafikize basi jamani nchi itakuwa ishatushinda na hapo Muungwana na wenziwe watafurahi sana!

Tafadhali Nd. Ngida ninajumuika na Wana_Forum wote wa hii Forum ili ubadilishe mawazo yako.
Ni kweli kuwa hata mimi niliwahi kukosa kazi kwasababu kwenye interview nilisema kuwa ninakazi zangu nyengine. Interviewer akanifelisha kwa kusema kuwa kama ninakazi zangu nyengine basi kazi zao sitozishukulikia kama ipasavyo. Kwavile Muungwana ni mwenye Miradi yake binafsi pembeni huko Bagamoyo ya ufugaji, ni kweli kabisa kuwa atapoteza muda wake mwingi huko Bagamoyo (mentally though not necessarily physically) kuliko kwenye kero zetu. Hatuna la kufanya kwasababu Watanzania tumemsaliti the very person who liberated us!

Hii naona ndio adhabu yetu kutoka kwa Mola kutokana na kumsaliti Baba yetu wa Taifa!
Please, Nd, Ngida usituhame hapa kwenye Forum. Bado tunataka kusikia fikra zako kila siku!

Kila la kheri / Mtaani Wako Lamaprt.
 
Kwa vile huyu Ngida anawaogopa mafisadi,anataka kutoka Jamii Forums. Mafisadi watamuharibia afya yake. Kuanzia sasa,anataka ''safe'',yaani kunywa pombe na kufanya massage.

Ina maana hawa mafisadi ni very dangerous,ikiwa mtu anadhani kulewa chakari kila siku,itakuwa much safer kuliko kubishana na mafisadi. Ukishaanza tu kusema,mafisadi ni dangerous,''the syndicate will kill someone'',,then all these people gravitate towards these carnal matters.That is the way it seems to me.

Dear Nd. Ganesh,

Hio ni sawa kabisa!

Ndugu Ngida fikiria tena juu ya uamuzi wako!

We still need you. No amount of beer guzzling will set you free!
 
Shujaa kamili huwa hakimbii vita, hupigana hadi tone la mwisho la damu yake.
 
Mwacheni aende na tumtakie safari na maisha mema. Kama kuna mtu ambaye anaogopa kufa kwa presure kisa zogo hapa jukwaani basi huyo hapa hapamfai. Maana watanzania wenzetu wasiojua JF wala kupata habari ya yanayoendelea nchini mwetu ndio wanaishi maisha anayoyataka huyu mwenzetu kitu ambacho ni kinyume cha wazo zima la kulipeleka taifa letu mbele.

Wengi tu walishaaga kwa sababu tofauti lakini maisha yameendelea tu hapa kijiweni, kwahiyo braza/ dada safari njema
 
Ngida1 ndugu yangu mimi sikumbuki ni lini uliwahi kunikera au labda wewe uliona umenikera na mimi sikuona hivyo. Kama kweli una pressure na inapanda baada ya kuona/kusoma mambo mbali mbali yanayoudhi yanayofanywa au kutofanywa na viongozi wetu basi kwa afya yako hata mimi nakushauri upumzike labda kwa muda. Ni kweli haya mambo yanaudhi mno maana ni mwaka nenda mwaka rudi habari ni ile ile tu. Kama utaamua kuondoka basi nakutakia kila la heri katika maisha yako na hiyo pressure ipungue au kuondoka kabisa. Kila la heri Mkuu Ngida1
 
Huyu Ngida inaonekana ni mayai sana au ana sababu zake zingine? Kama "shell" yake inashuka baada ya kuona picha tena ya watoto wanaosoma kwenye mazingira magumu sasa akiwaona live wenye shida zaidi ya hizo itakuwaje? Namtakia maisha mema kwenye "safe" place!
 
hii thread yako imeniacha katika hamasa .

Nimepigwa butwaa na mshangao sana ..lakini kwa nini hutaki kusikia mambo yanayoendelea kufanyika KATIKA NCHII HII wewe ni mmojawapo kumake changes
Pamoja tutashinda
 
Mkuu

1. Hujawahi kupitia shida wewe kbs haya yasingekupa presha
2. Kukimbia tatizo ni njia ya kusolve?
3. Wewe bana ukiona mambo huku yamekushinda kimya kimya ondoka usikatishe wenzio tamaa.
4. Kwani huku JF kuna SIASA tu?
5. Kama bia ndio the best kwako ikiwa excessesive hio presha na kisukari utakikwepa?
6. Matatizo kwenye familia yako yakizidi unakimbilia kwa wakwe au baba yako ili usiyakabili?
8.............................
9.................................
 
Ngida utakuwa una lako jambo lingine kabisa ,itabidi uwe muwazi.kama siasa ndo tatizo si unaipotezea tu usiingie kwenye hicho chumba?hapa kuna vitu vingine vingi vya msingi kama mahusiano,JF dokta, entertainment n.k
Kujitenga sio jambo zuri kiafya na hapa unaweza kupata marafiki wengi mkafurahi pamoja na kusahau hayo matatizo ya nchi kama kweli hupendi kuyasikia.
Dont go yet,we still love you!
 
Wanaoondoka JF hawaagi, wanaoaga hawaondoki.

Ahh mkuu, haya mambo hata hayaelezeki; ukweli ni kwamba kuna wakati mtu unashinda hata kulala kutokana na taarifa tunazopata humu ndani. Tangu niwe memba nimeijua zaidi hii nchi.... unfortunately, ukimchambua kuku huwezi kumla; ndio maana wengine tunaishia kule kwenye mahaba na kwenda kulala

...hakyanani kuna siku nilimuona mkapa njia ya tanga [ilikuwa mara tu baada ya kusoma issue ya meremeta, nilitamani afe tu; dhambi tupu nilichuma

Ombi kwa mhusika, usiondoke ila ona dakitari akuandalie special regimen ya kupunguza hasira usije ukaua bure!!!
 
Nyie wote mnaonyesha jinsi gani mlivyo wadhaifu wa kukubali kushindwa kirahisi na kukata tamaa harakka kama hivi, Lazima uwe imara siku zote na pia kama huyu jamaa anamua kuondoka hapa basi afanye hivyo haraka sana, ila watakuja watu wengine walio bora.. Huwezi kujitoa kwa hali kama hii maana sisi ndio tulizembea kwa kuwaweka watu wabaya katika siasa zetu na siasa ni nzuri ila watu ndio wabaya.
 
Nyie wote mnaonyesha jinsi gani mlivyo wadhaifu wa kukubali kushindwa kirahisi na kukata tamaa harakka kama hivi, Lazima uwe imara siku zote na pia kama huyu jamaa anamua kuondoka hapa basi afanye hivyo haraka sana, ila watakuja watu wengine walio bora.. Huwezi kujitoa kwa hali kama hii maana sisi ndio tulizembea kwa kuwaweka watu wabaya katika siasa zetu na siasa ni nzuri ila watu ndio wabaya.


Okay...Unaweza kunipa impact ya JF katika siasi bongo?

We need to change kwa kusudi la kuwa na impact ya uhakika.
 
Wanaoondoka JF hawaagi, wanaoaga hawaondoki.

Sure man! Huyu anataka kutupima akili zetu. Kila la kheri Ngida1. Salamu zao. Sisi tunaendelea kuipigania nchi yetu. Hatukati wala kukatishwa tamaa mpaka kieleweke. Ukitaka kurudi, milango iko wazi.
 
Ndugu yangu Ngida1 utakuja kumkimbia mwanamke uliyemuoa kwa mambo madogo!PAMBANA BWANA
 
Back
Top Bottom