8691jakigili
Senior Member
- Mar 30, 2012
- 179
- 67
Habari za ajali nimezipata kutoka kwa vyanzo sahihi. Dereva (Ibra ambaye ni mtoto wa dada yake Diana) aliyenusurika na ajali hiyo anasema: Mbele yao kulikuwa na magari makubwa mawili yaliyoharibika njiani upande wa kulia eneo la kona lenye mwinuko Machimboni Igawa. Hao madereva w magari yaliyoharibika hawakuchukua tahadhari yoyote. Wahanga walikuwa upande sahihi, lakini katikati ya magari mawili hayo yaliyoharibika Fuso ilikuwa inakuja kwa kasi upande wao. Ibra alijaribu kuingia kwa Ghafla katikati ya Magari mawili kulikwepa Fuso lililokuwa liwagonge uso kwa uso; lakini alichelewa na kubamizwa upande wa nyuma ambao ndio walikaa wahanga.