Kwahali hii TFF ijitazame sana la sivyo ligi kuu ya Tanzania haina hadhi ya kuitwa ligi bali ni kichekesho tu na kuibua malalamiko yasiyo na tija.

Mromboo

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
2,923
6,406
Wasalaam!
Kwa wapenda michezo wote wa Tanzania. Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) ndilo limepewa dhamana ya kusimamia mpira wa miguu Tanzania kwa usawa na haki. Lakini kwa hali halisi na nikichukulia mfano hii ligi yetu bado TFF na wadau wa mpira (bodi ya ligi) wana kazi kubwa sana.

Ligi yetu inaonekana kutokuwa na maana hasa pale ushindani unapoonekana dhahiri kuzibeba baadhi ya timu na kuonea timu nyingine. Leo nimeamua kufuatilia mwenendo wa ligi nikashangaa sana kuona timu moja ina viboro 11. Tangu nizaliwe sijawahi kuona ligi ya namna hiyo.
Kwa mantiki hii sioni haja ya kuiita ligi maana kuna timu zinachoka wakati nyingine zinarelax tu. Ajabu nyingine ni kuona kuna timu moja imepangiwa mechi mfululizo 11 katika uwanja mmoja jambo ambalo linaondoa hadhi ya ligi. Kwa mantiki hii kuna haja gani ya kuwa na bodi ya ligi au shirikisho la mpira wa miguu kama.mambo yanaachwa yaende hivi?
Inakuwaje timu moja inasafiri mikoa karibia sita ndani ya wiki moja kucheza mechi tofauti ukichukulia hali halisi ya barabara zetu na ligi kukosa mdhamini?
Inakuwaje viongizi wa mpira wa miguu hawaoni haja ya kutengeneza uwiano sawa wa ushindani kwenye ligi ilihali wanajua kuwa ni kosa kisheria kwani inaleta malalamiko na kukatisha tamaa baadhi ya timu?
Nawaomba TFF waache siasa waangalie mpira wa Tanzania.
Al ahly ya Misri ilicheza na Simba jumamosi lakini jana imecheza mechi ya ligi. Ni kitu gani kinazuia Simba kucheza game zake? Na kwanini iwe mwaka huu tu wakati simba inashiriki kimataifa?
Je kama timu zikilalamikia yatakayotokea kwenye mechi za viporo ikifikia kuleta tuhuma za rushwa TFF watakwepaje huo mtego?
Naomba sana wadau wa mpira wa miguu waliangalie hili jambo kwa jicho la tatu la sivyo mpira wetu utakuwa wa hovyo hovyo mpaka mwisho.
Sioni haja ya kuwa na chama cha mpira wa miguu wala bodi ya ligi bali kilichopo ni ubabaishaji na uonevu kwa baadhi ya timu.
Shame on you TFF
 
Yanga waliomba wasicheze game zao away kwasababu walikua hawana pesa, mfano yanga ilibidi aanze na mtibwa morogoro yanga wakaomba ipigwe Dar, hivyo hivyo kwa mwadui na Coastal Union sasa ratiba zinawabana mbeleni mnaanza kulalamika.

Simba tumecheza na Js saoura jumamosi na jumapili tukacheza fainali tukapoteza na hatujalalamika. Hakuna masuala ya bodi hapa vyura hamjui mpira shame on you!!!
 
Yanga waliomba wasicheze game zao away kwasababu walikua hawana pesa, mfano yanga ilibidi yanga aanze na mtibwa morogoro yanga wakaomba ipigwe Dar, hivyo hivyo kwa mwadui na Coastal Union sasa ratiba zinawabana mbeleni mnaanza kulalamika.

Simba tumecheza na Js saoura jumamosi na jumapili tukacheza fainali tukapoteza na hatujalalamika. Hakuna masuala ya bodi hapa vyura hamjui mpira shame on you!!!
Hilo ni miongoni mwa malalamiko yangu. Ila pia kuna hoja ya viporo 11. Kama simba ilihitaji muda kujianda na hiyo michezo ya kimataifa na kuamua kutelekeza ligi, ilikuwaje wakacheza sportpesa na mapinduzi?
Bado TFF na ligi yao ni wababaishaji tu na hakuna mpira hapo bali maigizo tu.
Kuhusu hiyo michezo 11 katika uwanja mmoja, tatizo ni TFF na bodi ya ligi. Kinachotakiwa kufuatwa ni kanuni za ligi na sio matakwa ya timu
 
mlitakiwa muanze kulalamika wakati mnacheze mfululizo mechi 10 dar.
Kwani ni nani anapanga ratiba? Angalia huko nyuma malalamiko yalikuwepo. Kinachotakiwa ni kanuni za ligi na sio matakwa ya timu.
 
Hilo ni miongoni mwa malalamiko yangu. Ila pia kuna hoja ya viporo 11. Kama simba ilihitaji muda kujianda na hiyo michezo ya kimataifa na kuamua kutelekeza ligi, ilikuwaje wakacheza sportpesa na mapinduzi?
Bado TFF na ligi yao ni wababaishaji tu na hakuna mpira hapo bali maigizo tu.
Kuhusu hiyo michezo 11 katika uwanja mmoja, tatizo ni TFF na bodi ya ligi. Kinachotakiwa kufuatwa ni kanuni za ligi na sio matakwa ya timu
Mkuu hapa una hoja!
 
Yanga waliomba wasicheze game zao away kwasababu walikua hawana pesa, mfano yanga ilibidi aanze na mtibwa morogoro yanga wakaomba ipigwe Dar, hivyo hivyo kwa mwadui na Coastal Union sasa ratiba zinawabana mbeleni mnaanza kulalamika.

Simba tumecheza na Js saoura jumamosi na jumapili tukacheza fainali tukapoteza na hatujalalamika. Hakuna masuala ya bodi hapa vyura hamjui mpira shame on you!!!
Mikia aka mbumbumbu fc,

Sent from my SM-T355Y using Tapatalk
 
kausha mkuu, ninyi yanga mlitangulia na gari la mabox limeanza kunyeshewa mvua sasa linatepeta.
Simba atacheza kila baada ya siku tatu tafuta ratiba yake ndipo uanze kulalamika.
Hii ratiba inambeba azam zaidi
 
kausha mkuu, ninyi yanga mlitangulia na gari la mabox limeanza kunyeshewa mvua sasa linatepeta.
Simba atacheza kila baada ya siku tatu tafuta ratiba yake ndipo uanze kulalamika.
Hii ratiba inambeba azam zaidi
Ila tuweke akiba ya maneno. Uzuri tunaomba Azam TV wawe fare kwenye kurusha matangazo. Ila naona dalili za baadhi ya Timu na TFF yao kupelekwa Takukuru.
 
Wasalaam!
Kwa wapenda michezo wote wa Tanzania. Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) ndilo limepewa dhamana ya kusimamia mpira wa miguu Tanzania kwa usawa na haki. Lakini kwa hali halisi na nikichukulia mfano hii ligi yetu bado TFF na wadau wa mpira (bodi ya ligi) wana kazi kubwa sana.

Ligi yetu inaonekana kutokuwa na maana hasa pale ushindani unapoonekana dhahiri kuzibeba baadhi ya timu na kuonea timu nyingine. Leo nimeamua kufuatilia mwenendo wa ligi nikashangaa sana kuona timu moja ina viboro 11. Tangu nizaliwe sijawahi kuona ligi ya namna hiyo.
Kwa mantiki hii sioni haja ya kuiita ligi maana kuna timu zinachoka wakati nyingine zinarelax tu. Ajabu nyingine ni kuona kuna timu moja imepangiwa mechi mfululizo 11 katika uwanja mmoja jambo ambalo linaondoa hadhi ya ligi. Kwa mantiki hii kuna haja gani ya kuwa na bodi ya ligi au shirikisho la mpira wa miguu kama.mambo yanaachwa yaende hivi?
Inakuwaje timu moja inasafiri mikoa karibia sita ndani ya wiki moja kucheza mechi tofauti ukichukulia hali halisi ya barabara zetu na ligi kukosa mdhamini?
Inakuwaje viongizi wa mpira wa miguu hawaoni haja ya kutengeneza uwiano sawa wa ushindani kwenye ligi ilihali wanajua kuwa ni kosa kisheria kwani inaleta malalamiko na kukatisha tamaa baadhi ya timu?
Nawaomba TFF waache siasa waangalie mpira wa Tanzania.
Al ahly ya Misri ilicheza na Simba jumamosi lakini jana imecheza mechi ya ligi. Ni kitu gani kinazuia Simba kucheza game zake? Na kwanini iwe mwaka huu tu wakati simba inashiriki kimataifa?
Je kama timu zikilalamikia yatakayotokea kwenye mechi za viporo ikifikia kuleta tuhuma za rushwa TFF watakwepaje huo mtego?
Naomba sana wadau wa mpira wa miguu waliangalie hili jambo kwa jicho la tatu la sivyo mpira wetu utakuwa wa hovyo hovyo mpaka mwisho.
Sioni haja ya kuwa na chama cha mpira wa miguu wala bodi ya ligi bali kilichopo ni ubabaishaji na uonevu kwa baadhi ya timu.
Shame on you TFF
Kweli Yanga ndo mana ni ombaomba Fc, sasa sababu Yanga ameanza kupata matokeo mabovu ndo mana mmeanza kulalamika, mlikua wapi kusema haya kipindi timu yenu inashinda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli Yanga ndo mana ni ombaomba Fc, sasa sababu Yanga ameanza kupata matokeo mabovu ndo mana mmeanza kulalamika, mlikua wapi kusema haya kipindi timu yenu inashinda

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio kwamba mm ni mshabiki wa yanga wala nini. Nataka tuweke mambo sawa ili ligi yetu iwe na hadhi. Sijui ni kwanini TFF na bodi ya ligi wanakubali upuuzi kama huu. Huwezi kuwa na ligi timu moja ina viporo 11. Wapi uliona hili ndugu yangu?
 
Sio kwamba mm ni mshabiki wa yanga wala nini. Nataka tuweke mambo sawa ili ligi yetu iwe na hadhi. Sijui ni kwanini TFF na bodi ya ligi wanakubali upuuzi kama huu. Huwezi kuwa na ligi timu moja ina viporo 11. Wapi uliona hili ndugu yangu?
Ka si mpenzi wa Yanga subiri ligi imalizike tupeleke malalamiko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
unazungumzia Al ahily kucheza jana hivi unasahau kuwa walikuwa nyumbani na simba walikuwa ugenini naona matokeo mnayopata sasa yanawachanganya wakati ule mnacheza mfululizo dar hamkulalamika ila mmeanza kutoka nje ya Dar na kutopata matokeo mnapiga kelele
 
Yanga waliomba wasicheze game zao away kwasababu walikua hawana pesa, mfano yanga ilibidi aanze na mtibwa morogoro yanga wakaomba ipigwe Dar, hivyo hivyo kwa mwadui na Coastal Union sasa ratiba zinawabana mbeleni mnaanza kulalamika.

Simba tumecheza na Js saoura jumamosi na jumapili tukacheza fainali tukapoteza na hatujalalamika. Hakuna masuala ya bodi hapa vyura hamjui mpira shame on you!!!
Si kweli ratiba ilikuwa Yanga aanzie kanda ya ziwa..Amunike akawaita wachezaji stars
 
Hili unalolisema sio kwamba tu wewe ni yanga laah!, upo sahihi kabisa, ligi yetu haina viongozi.
Tatizo watanzania tunaonekana wakati wa matokeo mabovu tu ndio tunatoa malalamiko.. Kama tunaipenda ligi yetu tusiwe nyuma ya timu zetu... Hata wakati wa malinzi kuna maujinga mengi tuliyaona, sijui hawa watu hawana uchungu na soka letu?
We viporo 11, mechi 10+ Uwanja mmoja sio sawa... ligi haina mdhamini kweli?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom