Mromboo
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 2,923
- 6,406
Wasalaam!
Kwa wapenda michezo wote wa Tanzania. Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) ndilo limepewa dhamana ya kusimamia mpira wa miguu Tanzania kwa usawa na haki. Lakini kwa hali halisi na nikichukulia mfano hii ligi yetu bado TFF na wadau wa mpira (bodi ya ligi) wana kazi kubwa sana.
Ligi yetu inaonekana kutokuwa na maana hasa pale ushindani unapoonekana dhahiri kuzibeba baadhi ya timu na kuonea timu nyingine. Leo nimeamua kufuatilia mwenendo wa ligi nikashangaa sana kuona timu moja ina viboro 11. Tangu nizaliwe sijawahi kuona ligi ya namna hiyo.
Kwa mantiki hii sioni haja ya kuiita ligi maana kuna timu zinachoka wakati nyingine zinarelax tu. Ajabu nyingine ni kuona kuna timu moja imepangiwa mechi mfululizo 11 katika uwanja mmoja jambo ambalo linaondoa hadhi ya ligi. Kwa mantiki hii kuna haja gani ya kuwa na bodi ya ligi au shirikisho la mpira wa miguu kama.mambo yanaachwa yaende hivi?
Inakuwaje timu moja inasafiri mikoa karibia sita ndani ya wiki moja kucheza mechi tofauti ukichukulia hali halisi ya barabara zetu na ligi kukosa mdhamini?
Inakuwaje viongizi wa mpira wa miguu hawaoni haja ya kutengeneza uwiano sawa wa ushindani kwenye ligi ilihali wanajua kuwa ni kosa kisheria kwani inaleta malalamiko na kukatisha tamaa baadhi ya timu?
Nawaomba TFF waache siasa waangalie mpira wa Tanzania.
Al ahly ya Misri ilicheza na Simba jumamosi lakini jana imecheza mechi ya ligi. Ni kitu gani kinazuia Simba kucheza game zake? Na kwanini iwe mwaka huu tu wakati simba inashiriki kimataifa?
Je kama timu zikilalamikia yatakayotokea kwenye mechi za viporo ikifikia kuleta tuhuma za rushwa TFF watakwepaje huo mtego?
Naomba sana wadau wa mpira wa miguu waliangalie hili jambo kwa jicho la tatu la sivyo mpira wetu utakuwa wa hovyo hovyo mpaka mwisho.
Sioni haja ya kuwa na chama cha mpira wa miguu wala bodi ya ligi bali kilichopo ni ubabaishaji na uonevu kwa baadhi ya timu.
Shame on you TFF
Kwa wapenda michezo wote wa Tanzania. Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) ndilo limepewa dhamana ya kusimamia mpira wa miguu Tanzania kwa usawa na haki. Lakini kwa hali halisi na nikichukulia mfano hii ligi yetu bado TFF na wadau wa mpira (bodi ya ligi) wana kazi kubwa sana.
Ligi yetu inaonekana kutokuwa na maana hasa pale ushindani unapoonekana dhahiri kuzibeba baadhi ya timu na kuonea timu nyingine. Leo nimeamua kufuatilia mwenendo wa ligi nikashangaa sana kuona timu moja ina viboro 11. Tangu nizaliwe sijawahi kuona ligi ya namna hiyo.
Kwa mantiki hii sioni haja ya kuiita ligi maana kuna timu zinachoka wakati nyingine zinarelax tu. Ajabu nyingine ni kuona kuna timu moja imepangiwa mechi mfululizo 11 katika uwanja mmoja jambo ambalo linaondoa hadhi ya ligi. Kwa mantiki hii kuna haja gani ya kuwa na bodi ya ligi au shirikisho la mpira wa miguu kama.mambo yanaachwa yaende hivi?
Inakuwaje timu moja inasafiri mikoa karibia sita ndani ya wiki moja kucheza mechi tofauti ukichukulia hali halisi ya barabara zetu na ligi kukosa mdhamini?
Inakuwaje viongizi wa mpira wa miguu hawaoni haja ya kutengeneza uwiano sawa wa ushindani kwenye ligi ilihali wanajua kuwa ni kosa kisheria kwani inaleta malalamiko na kukatisha tamaa baadhi ya timu?
Nawaomba TFF waache siasa waangalie mpira wa Tanzania.
Al ahly ya Misri ilicheza na Simba jumamosi lakini jana imecheza mechi ya ligi. Ni kitu gani kinazuia Simba kucheza game zake? Na kwanini iwe mwaka huu tu wakati simba inashiriki kimataifa?
Je kama timu zikilalamikia yatakayotokea kwenye mechi za viporo ikifikia kuleta tuhuma za rushwa TFF watakwepaje huo mtego?
Naomba sana wadau wa mpira wa miguu waliangalie hili jambo kwa jicho la tatu la sivyo mpira wetu utakuwa wa hovyo hovyo mpaka mwisho.
Sioni haja ya kuwa na chama cha mpira wa miguu wala bodi ya ligi bali kilichopo ni ubabaishaji na uonevu kwa baadhi ya timu.
Shame on you TFF