Kwa yanayojili Zanzibar kuna haja ya kuomba uraia wa visiwa hivyo. Naomba mnipe utaratibu wa kupata uraia

Sexless

JF-Expert Member
Mar 11, 2017
21,518
50,254
Kwanza, mafuta bei yake iko chini huko Zanzibar. Pia maisha ya Wazanzibari ni nafuu mno kwasababu hakuna mfumuko wa bei.

Pili, ukitupia jicho kwenye umeme bei iko chini na ni karibu na bure. Mwaka huu rais wa visiwa hivyo alitangaza kuwa nguzo za umeme itakuwa bure

Tatu, mwaka wa mwisho wa awamu 7, mzee Mohammed Shein aliongeza mishahara ya watumishi wa umma kima cha chini kwa 100%.
Screenshot_20220508-223325_1.jpg



Nne, hivi leo 8/5/2022, rais wa sasa (awamu ya 8) wa visiwa hivyo Dr. Hussein Mwinyi ametangaza nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma kwa15%.

Zanzibar kuna neema kubwa kubwa na neema ndogo ndogo, tuombe uraia tukaishi huko. Kuishi Tanganyika ni mateso ya kujitakia.
 
Tafsida unaijua ndugu?
Sijui , nakushangaa unaweka lawama la ongezeko la mshahara liliongezwa na Maraisi wa Zanzibar kwa wazanzibar lawama unazipeleka kwa Mwigulu as if Mwigulu ameshawai Kua raisi comment ukiwa haujalewa banana
 
Sijui , nakushangaa unaweka lawama la ongezeko la mshahara liliongezwa na Maraisi wa Zanzibar kwa wazanzibar lawama unazipeleka kwa Mwigulu as if Mwigulu ameshawai Kua raisi comment ukiwa haujalewa banana
Mwigulu nani yako mbona unateseka Sana?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom