Kwa yaliyotokea kwa Kangi Lugola kuna funzo kubwa

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,874
Viongozi walioko madarakani na kwa sisi vijana pia kuna la kujifunza.Kuna kitu kinaitwa misingi (values) au principles ,sheria na taratibu.Katika maisha yako unapopata nafasi yeyote ya kutumikia usijiaribu kumfurahisha aliyekuteuwa ukasahau kushikamana na misingi,taratibu na sheria.

Ukishikilia misingi , taratibu,kanuni na Sheria utaishi kwa kujiamini na kwa amani mara zote ,utapendwa na kila mtu sababu una simamia misingi kama ya haki ,usawa,upendo, uwajibikaji, heshima n.k. Misingi na taratibu hizi huishi milele .

Hata aliyekuteuwa akikuona unasimamia misingi , principles,Sheria ,na taratibu atakuogopa na kukuheshimu sana.Utapendwa sana na jamii hata siku akikuondoa katika nafasi yako utakuwa na amani moyoni na jamii itaendelea kukuheshimu mfano mkubwa ni CAG aliyeondolewa Prof.Mussa Assad anaheshimika hata na waliomteuwa katika mioyo yao wanamuheshimu , wananchi na jamii nzima tunamuheshimu sababu alisimamia misingi,Sheria,kanuni na taratibu wala hakufanya kazi zake kumfurahisha mtu.

Ila ukiacha misingi ,ukataka kumfurahisha aliyekuteuwa ukadhani ndio muarubani ,basi umepotea .Misingi huwa haibadiliki Ila viongozi unaowasifu na kuwafurahisha wanabadilika na hawatabiriki sababu wote wewe na yeye ni wanasiasa kila mtu mbele ya macho yake hutazamia kupata fursa ya sifa za kisiasa kwa maslahi binafsi hivyo anaweza kukugeuka muda wowote .

Ukajikuta upo pekeako ,uliitenga misingi na Sheria na taratibu ,ukatenga wananchi na watu ukatumia muda kumfurahisha aliyekuteuwa.Hatimaye aliyekuteuwa amekugeuka kwa kudharau na kuvunja misingi.Wewe ulidhani kuvunja misingi ndio mbadala wa kumfurahisha aliyekuteuwa.Sasa misingi imekutenga , wananchi wamekutenga na uliyekuwa ukimsifia amekutenga.

Huu ni ugonjwa ambao unatafuna viongozi wengi wa serikali ya awamu ya tano kwa kudhani ndio usalama wao ,mtu akisima jina Mh.Rais Magufuli linatajwa kwa marudio yasio hesabika,sifa hujaa pipa ,akidhani ndio njia yeye kupendwa badala ya kuishi na misingi ,kanuni , taratibu na Sheria .

Mjirekebishe ,heshimuni misingi ,kanuni , taratibu na sheria zitawaheshimu na kuwalinda pia .Mh Kangi alikwama hapo tuu alijisahau akidhani kumsifia na kumtukuza aliyemteuwa ndio mbadala wa kufuata misingi ya kazi na cheo chake leo hii anataka kufunguliwa mashtaka ya uhujumu uchumi.

Huu ugonjwa upo pia kwa Mh. Makonda ,@baba_keagan na viongozi wengine pia,kama hawatojitathimin na kubadilika watakumbuka maneno yangu.

Abdul Nondo.
0683494398

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeandika ujinga na mambo ya kusadikika, Binadamu huyo mwenye hizo sifa ulizoziongelea hayupo hapa Duniani, kila mtu anatetea mkate wake, hata Asadi hayuko hivyo unavyomdhania, maadamu Bosi wako ndo anayekuweka mjini na kuhakikisha familia yako inapata mlo, hauna ujanja, ni lazima u bow down kwake.

Sasa kuna watu ambao wana options au plan B, hao wanaweza kuwa wabishi, lkn haina uhusiano na hiyo misingi ulioiongelea, labda unachanganya hapo, kuna watu wana options lkn siyo misingi, hakuna kitu kinaitwa msingi mbele ya njaa.
 
Kwel wajinga hamtoisha nchi hii
Umeandika ujinga na mambo ya kusadikika, Binadamu huyo mwenye hizo sifa ulizoziongelea hayupo hapa Duniani, kila mtu anatetea mkate wake, hata Asadi hayuko hivyo unavyomdhania, maadamu Bosi wako ndo anayekuweka mjini na kuhakikisha familia yako inapata mlo, hauna ujanja, ni lazima u bow down kwake.

Sasa kuna watu ambao wana options au plan B, sasa hao wanaweza kuwa wabishi, lkn haina uhusiano na hiyo misingi ulioiongelea, labda unachanganya hapo, kuna watu wana options lkn siyo misingi, hakuna kitu kinaitwa msingi mbele ya njaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeandika ujinga na mambo ya kusadikika, Binadamu huyo mwenye hizo sifa ulizoziongelea hayupo hapa Duniani, kila mtu anatetea mkate wake, hata Asadi hayuko hivyo unavyomdhania, maadamu Bosi wako ndo anayekuweka mjini na kuhakikisha familia yako inapata mlo, hauna ujanja, ni lazima u bow down kwake.

Sasa kuna watu ambao wana options au plan B, hao wanaweza kuwa wabishi, lkn haina uhusiano na hiyo misingi ulioiongelea, labda unachanganya hapo, kuna watu wana options lkn siyo misingi, hakuna kitu kinaitwa msingi mbele ya njaa.
Nimefurahishwa na hitimisho lako "hakuna kitu kinaitwa misingi mbele ya njaa" huu ndo ukweli,ingawa ni ukweli mchungu.
 
Tatizo we Abdul unadhani una akili kupita watu wote, hata rafiki zako wengi wameshalalamika sana husikilizi mawazo ya yoyote unaona ya kwako ndio bora, hapo ACT unamuheshimu Zito tu wengine wote unawadharau, hufai kuwa kiongozi
 
Hakuna kesi itakayo mkabili mh Kangi Lugola, hawa watu wanajuana kabisa....siku zote Tanzania ukihisiwa umeiba kuku unawekwa ndani kisha uchunguzi unaendelea lakini kwa akina Mh Kangi uchunguzi unaanza kufanyika kwanza kisha waje wafikishwe mahakamani. A Nondo, umenena vyema na ndivyo inavyopaswa kuwa lakini haiwezekani sisi ngozi nyeusi tuna laana ya asili njaa tu inatuondoa kwenye reli tunavunja misimamo yetu...muda si mrefu hata wewe ukianza kuimarika kisiasa kama mpinzani ghafla unaunga juhudi za Mh Rais uliyokuwa unayapinga sasa unaanza kuyaona yanafaa. Rejea swaga za Potrobasi Katambi kabla hajaonjeshwa mkate mkavu na nyama ya shua kwa pamoja....na wengine walivyokuwa wanajaribu kuinanga serikali ya Magufuli...leo wako wapi?
 
Umeandika ujinga na mambo ya kusadikika, Binadamu huyo mwenye hizo sifa ulizoziongelea hayupo hapa Duniani, kila mtu anatetea mkate wake, hata Asadi hayuko hivyo unavyomdhania, maadamu Bosi wako ndo anayekuweka mjini na kuhakikisha familia yako inapata mlo, hauna ujanja, ni lazima u bow down kwake.

Sasa kuna watu ambao wana options au plan B, hao wanaweza kuwa wabishi, lkn haina uhusiano na hiyo misingi ulioiongelea, labda unachanganya hapo, kuna watu wana options lkn siyo misingi, hakuna kitu kinaitwa msingi mbele ya njaa.
Usidhani Watanzania wote bootlickers- speak for yourself.
 
Viongozi walioko madarakani na kwa sisi vijana pia kuna la kujifunza.Kuna kitu kinaitwa misingi (values) au principles ,sheria na taratibu.Katika maisha yako unapopata nafasi yeyote ya kutumikia usijiaribu kumfurahisha aliyekuteuwa ukasahau kushikamana na misingi,taratibu na sheria.

Ukishikilia misingi , taratibu,kanuni na Sheria utaishi kwa kujiamini na kwa amani mara zote ,utapendwa na kila mtu sababu una simamia misingi kama ya haki ,usawa,upendo, uwajibikaji, heshima n.k. Misingi na taratibu hizi huishi milele .

Hata aliyekuteuwa akikuona unasimamia misingi , principles,Sheria ,na taratibu atakuogopa na kukuheshimu sana.Utapendwa sana na jamii hata siku akikuondoa katika nafasi yako utakuwa na amani moyoni na jamii itaendelea kukuheshimu mfano mkubwa ni CAG aliyeondolewa Prof.Mussa Assad anaheshimika hata na waliomteuwa katika mioyo yao wanamuheshimu , wananchi na jamii nzima tunamuheshimu sababu alisimamia misingi,Sheria,kanuni na taratibu wala hakufanya kazi zake kumfurahisha mtu.

Ila ukiacha misingi ,ukataka kumfurahisha aliyekuteuwa ukadhani ndio muarubani ,basi umepotea .Misingi huwa haibadiliki Ila viongozi unaowasifu na kuwafurahisha wanabadilika na hawatabiriki sababu wote wewe na yeye ni wanasiasa kila mtu mbele ya macho yake hutazamia kupata fursa ya sifa za kisiasa kwa maslahi binafsi hivyo anaweza kukugeuka muda wowote .

Ukajikuta upo pekeako ,uliitenga misingi na Sheria na taratibu ,ukatenga wananchi na watu ukatumia muda kumfurahisha aliyekuteuwa.Hatimaye aliyekuteuwa amekugeuka kwa kudharau na kuvunja misingi.Wewe ulidhani kuvunja misingi ndio mbadala wa kumfurahisha aliyekuteuwa.Sasa misingi imekutenga , wananchi wamekutenga na uliyekuwa ukimsifia amekutenga.

Huu ni ugonjwa ambao unatafuna viongozi wengi wa serikali ya awamu ya tano kwa kudhani ndio usalama wao ,mtu akisima jina Mh.Rais Magufuli linatajwa kwa marudio yasio hesabika,sifa hujaa pipa ,akidhani ndio njia yeye kupendwa badala ya kuishi na misingi ,kanuni , taratibu na Sheria .

Mjirekebishe ,heshimuni misingi ,kanuni , taratibu na sheria zitawaheshimu na kuwalinda pia .Mh Kangi alikwama hapo tuu alijisahau akidhani kumsifia na kumtukuza aliyemteuwa ndio mbadala wa kufuata misingi ya kazi na cheo chake leo hii anataka kufunguliwa mashtaka ya uhujumu uchumi.

Huu ugonjwa upo pia kwa Mh. Makonda ,@baba_keagan na viongozi wengine pia,kama hawatojitathimin na kubadilika watakumbuka maneno yangu.

Abdul Nondo.
0683494398

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani wewe pia upo kama uliowataja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo we Abdul unadhani una akili kupita watu wote, hata rafiki zako wengi wameshalalamika sana husikilizi mawazo ya yoyote unaona ya kwako ndio bora, hapo ACT unamuheshimu Zito tu wengine wote unawadharau, hufai kuwa kiongozi
Laki Si Pesa, hii ndiyo hulka ya Waha
 
Mkandarasi wa Romania kachomoa hadai kitu.Serikali haitapata hasara yoyote.Kange na wenzake hawana kesi ya kujibu.Adhabu waliopewa ya kufukuzwa kazi inatosha.
 
Back
Top Bottom