Kwa yale tuliyoyaona katika ziara ya Rais kule Rukwa na Waziri Mkuu kule Morogoro, Tanzania tuna ombwe la uongozi

Mathanzua

JF-Expert Member
Jan 4, 2017
15,810
20,654
Sio siri kwamba Rais na Waziri Mkuu wanafanya kazi nzuri sana ya kuwatumikia wananchi,na wote hatuna budi kuwapa pongezi.Kote walipokwenda tumeona wakitatua matatizo ya wananchi on the spot,kukemea watejdaji wabovu na wakati mwingine kuwasimamisha kazi.

Watendaji wengi wa serikali kuu na halimashauri ni kama wapo wapo,tu hawana kabisa nia ya kweli ya kuwatumikia wananchi.Nia yao kubwa ni kujineemesha binafsi,familia zao na ndugu zao.Tatizo ni kubwa katika kila Mkoa na Wilaya.Hii inawapa shida sana Rais na Waziri Mkuu katika kutekeleza maono yao ya kuwaletea Watanzania maendeleo.

Ni hivi karibuni tu Waziri mkuu alitembelea Wilaya za Ifakara,Kilombero na Malinyi.Wote tulishuhudia madudu Waziri Mkuu aliyokutana nayo kule,hata ikabidi viongozi mbali mbali wa Wilaya hizo waondolewa katika nafasi zao.Ni hivi majuzi tu tumeshuhudia pia utendaji mbovu kabisa wa viongozi kule Rukwa,hata ikabidi Rais aingilie kati kisa cha mama mmoja aliyenyang'anywa mifugo yake kwa hila na viongozi waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi,huku viongozi wa Wilaya na Mkoa wakishindwa kabisa kumsaidia mama yule.

Jambo linalo onekana dhahiri katika matukio ya Morogoro na Rukwa ni kwamba viongozi ni sehemu ya matatizo ya wananchi.Je mpaka Rais au Waziri Mkuu aje ndio matatizo ya wananchi yapate ufumbuzi?Je Rais na Waziri Mkuu wataweza kweli kutembelea kila Mkoa na Wilaya ili kutatua matatizo ya wananchi?Jibu ni kwamba haiwezekani.Ni nini hasa kinasababisha viongozi wetu wengi kutopenda kuwahudumia wananchi inavyopaswa kiasi hiki,ni kukosa weledi
,mgomo baridi,ni nini hasa.Jambo moja ni dhahiri,nalo ni kwamba lipo tatizo kubwa la kiuongozi,ambalo kama halikutatuliwa Watanzania kupata "maendeleo ya kweli" itakuwa vigumu sana.

Napenda nimalizie kwa kusema kwamba tunao viongozi Tanzania,lakini bado tuna ombwe la uongozi.Mungu isaidie nchi yetu.
 
Tatizo aina machaguo ya uteuzi, wengi wametoka eneo mmoja la kijiografia hususani kabila! Dhahiri hakuna mchanganyiko unaokidhi wa jamii za Kitanzania.Na hiyo ndio changamoto.Wengi si wazoefu kazini(Mwanzo uteuzi ulilenga wakuu wa idara na watumishi makada wenye uzoefu),Wana tabia,maono,uzoefu,utendaji na mtazamo uinaofanana kulingana na mazingira wanayotoka kufanana.

Hivyo changamoto ndogo inaweza kuwa kikwazo kwao.
 
Tatizo moja viongozi wengi wanaoteuliwa hawana dhamira ya kweli ya kuhakikisha nchi inaendelea. Viongozi wengi kuanzia ngazi ya chini hadi juu ni wabinafsi sana na hawajitambui.

Ndio maana unaweza kusikia Serikali imetoa ela ya kujenga kituo cha afya Ila kituo husika kinaweza kisijengwe kwa hata zaidi ya mwaka kisa kuna mvutano au ugomvi wa viongozi flani.

Viongozi husika hawawazi ni namna gani watu wanateseka kwa kukosa kituo cha afya kisa wao wanauwezo wa kutibiwa hata India.

Fikiria watu wanadhubutu kula fedha za miradi ya maji safi na kuwaacha wananchi wakitumia maji machafu. Watu hawana huruma.
 
Tatizo watumishi wengi wako kimaslahi zaidi kuliko kua kikazi zaidi ,yaani unaweza fika office ya Umma ukaomba uoneshwe office ya mkuu Wa Idara na bado hapo hapo ukazungushwa hadi unyooshe mkono ndiyo watakuonyesha iko wapi!!
Mkuu shida ni kubwa sana.Huwa nawaza, hivi ni lazima Rais na Waziri Mkuu wapite kila sehemu watishie watumishi na kuwatumbua ndio watumishi wakae mkao wa angalao kutumikia wananchi?Inasikitisha sana.Kule Malinyi baada ya Waziri Mkuu kutumbua na kuondoka,jamaa bado wakapiga maboksi hamsini ya dawa.Nafika mahali nasema labda hii tumbua tumbua haitoshi.May be and just may be,we need to go farther than that.Wewe una mawazo gani mkuu?
 
Umasikini ni tatizo kubwa kuliko tunavyofikiria. Unapokua na viongozi wenye NJAA usitegemee kuna lolote la maana litakalofanyika. Kila mtu yupo kwenye uongozi kutetea tumbo lake tu hakuna anaewaza lingine.
Tatizo watumishi wengi wako kimaslahi zaidi kuliko kua kikazi zaidi ,yaani unaweza fika office ya Umma ukaomba uoneshwe office ya mkuu Wa Idara na bado hapo hapo ukazungushwa hadi unyooshe mkono ndiyo watakuonyesha iko wapi!!
 
Ukiona mambo kama hayo hayafanyiki au kujulikana na/ au yanajulikana ila anasubiriwa Rais au waziri mkuu aje kuchukua hatua ujue mfumo wa uongozi ni mbovu na wa hovyo kabisa.
Dawa ni kuuweka pembeni tuu
 
Tatizo pia hapa ni namna ya upataji viongozi Tz . Umelenga zaidi ukada na watoto wa mwenzetu ndani ya chama na si ueledi na uwezo binafsi .

Pili taasisi zetu eg Takukuru , Tiss, Nec, police, mahakama nk kukosa meno kwa wanasiasa (viongozi ) lakini vinginevyo kwa wananchi !!

Ni kweli kabisa mkuu. Tanzania watu wanaopewa nafasi za uongozi ni ama makada, watoto/ndugu wa watu fulani, waropokaji wasio na dira wala mwelekeo nk. Nadhani kuna assumption huwa inafanyika kwamba mtu akishapewa uongozi "automatikale" ataanza kua na akili na kujua anachokifanya..! Haya yanayotokea ni matokeo ya mfumo mbovu wa upatikanaji wa viongozi.
 
Tatizo aina machaguo ya uteuzi, wengi wametoka eneo mmoja la kijiografia hususani kabila! Dhahiri hakuna mchanganyiko unaokidhi wa jamii za Kitanzania.Na hiyo ndio changamoto.Wengi si wazoefu kazini(Mwanzo uteuzi ulilenga wakuu wa idara na watumishi makada wenye uzoefu),Wana tabia,maono,uzoefu,utendaji na mtazamo uinaofanana kulingana na mazingira wanayotoka kufanana.

Hivyo changamoto ndogo inaweza kuwa kikwazo kwao.
Hujaeleweka vizuri sana,ila naona kwa mtizamo wako unadhani uteuzi wa watumishi kutoka kwenye kabila moja unachangia kwenye tatizo,ingawa sioni hata kama hiyo ingekuwa kweli hilo linawezaji kuchangia kwenye utendaji mbovu.Labda wale wasiotoka kwenye kabila lile wanasema liwalo na liwe na sisi tutavuruga mambo?Sijui.Hata hivyo nadhani si kweli kwamba kuna undugu wa kiwango hicho unacho ongelea,anyway tusubiri michango ya wengine.

Hili la kukosa uzoefu kazini nalikubali 100% na tumeliongelea sana hata hapa JF.Ni vema vijana wanaonekana "wanafaa" wakapikwa vizuri kwenye vyuo vyetu vya utumishi na baada ya hapo waachwe wapate uzoefu kazini.Wakishaonekana wanafaa ndio wapewe uongozi.Even though thankyou for sharing.
 
Tatizo moja viongozi wengi wanaoteuliwa hawana dhamira ya kweli ya kuhakikisha nchi inaendelea. Viongozi wengi kuanzia ngazi ya chini hadi juu ni wabinafsi sana na hawajitambui. Ndio maana unaweza kusikia Serikali imetoa ela ya kujenga kituo cha afya Ila kituo husika kinaweza kisijengwe kwa hata zaidi ya mwaka kisa kuna mvutano au ugomvi wa viongozi flani. Viongozi husika hawawazi ni namna gani watu wanateseka kwa kukosa kituo cha afya kisa wao wanauwezo wa kutibiwa hata India.
Fikiria watu wanadhubutu kula fedha za miradi ya maji safi na kuwaacha wananchi wakitumia maji machafu. Watu hawana huruma.
Inasikitisha sana.Nini kifanyike sasa?
 
Mkuu shida ni kubwa sana.Huwa nawaza, hivi ni lazima Rais na Waziri Mkuu wapite kila sehemu watishie watumishi na kuwatumbua ndio watumishi wakae mkao wa angalao kutumikia wananchi?Inasikitisha sana.Kule Malinyi baada ya Waziri Mkuu kutumbua na kuondoka,jamaa bado wakapiga maboksi hamsini ya dawa.Nafika mahali nasema labda hii tumbua tumbua haitoshi.May be and just may be,we need to go farther than that.Wewe una mawazo gani mkuu?
Mkuu, ifike mahala tutazame wenzetu ni dawa gani hutumika katika majambo kama haya, nasikia kule china ukipatikana na vitendo vya uhujumu au rushwa adhabu yake ni kufungwa jela au kunyongwa kabisa, nasi bora tufike huko.
Hawa wazee watazunguka mpaka wapi wakati wateule wapo kwenyemaeneo yao ya kazi lakini wamekalia uvivu rushwa ubinafsi uonevu chuki binafsi na uzembe, ifike mahala tubadili gia.
Zitungwe sheria kali zaidi kuwabana hawa wahalifu.
 
Ni kweli kabisa mkuu. Tanzania watu wanaopewa nafasi za uongozi ni ama makada, watoto/ndugu wa watu fulani, waropokaji wasio na dira wala mwelekeo nk. Nadhani kuna assumption huwa inafanyika kwamba mtu akishapewa uongozi "automatikale" ataanza kua na akili na kujua anachokifanya..! Haya yanayotokea ni matokeo ya mfumo mbovu wa upatikanaji wa viongozi.
Kwa mawazo yako ni kwamba vetting kwa sasa ni kama haipo,kwa hiyo kama viongozi wa juu wanataka mambo yaende kama wanavyotaka,ni lazima upendeleo ukomeshwe na nafasi za ajira katika ngazi zote zijazwe na watu waliohakikishwa kwamba wana weledi unaotakiwa na wana uchungu na nchi yao,vinginevyo maendeleo ya kweli hayawezi kupatikana,ni kudanganyana.
 
Umasikini ni tatizo kubwa kuliko tunavyofikiria. Unapokua na viongozi wenye NJAA usitegemee kuna lolote la maana litakalofanyika. Kila mtu yupo kwenye uongozi kutetea tumbo lake tu hakuna anaewaza lingine.
Kweli njaa, lakini pia hatuna huruma hatuna woga wa haki za watu na mali za serikali?
 
Inasikitisha sana.Nini kifanyike sasa?
Swala sio kuweka na kutumbua....ndo maana wajuvi wanasisitiza kua na katiba inayojitosheleza hv ushawaza raisin.a. waziri mkuu wakiumwa hali itakuaje......kaulize Nigeria buhari alipolazwa nje
 
Umasikini ni tatizo kubwa kuliko tunavyofikiria. Unapokua na viongozi wenye NJAA usitegemee kuna lolote la maana litakalofanyika. Kila mtu yupo kwenye uongozi kutetea tumbo lake tu hakuna anaewaza lingine.
Hili jambo watu wengi wanaliongelea,lakini sidhani kama ni kweli,ni kisingizio tu.Mbona hata baada ya kuiba na kutajirika kishenzi bado watumishi bado wanaendelea kuiba?Tatizo nadhani ni tabia.Ni kwamba Upendo wa wengi umepoa,tamaa na tabia ya kupenda fedha kupindukia imetawala sana.Kama ingekuwa tatizo ni umaskini,Mwalimu Nyerere angekuwa mwizi au watu wote wangekuwa wezi mkuu.
 
Mkuu, ifike mahala tutazame wenzetu ni dawa gani hutumika katika majambo kama haya, nasikia kule china ukipatikana na vitendo vya uhujumu au rushwa adhabu yake ni kufungwa jela au kunyongwa kabisa, nasi bora tufike huko.
Hawa wazee watazunguka mpaka wapi wakati wateule wapo kwenyemaeneo yao ya kazi lakini wamekalia uvivu rushwa ubinafsi uonevu chuki binafsi na uzembe, ifike mahala tubadili gia.
Zitungwe sheria kali zaidi kuwabana hawa wahalifu.
Asante sana mkuu,tuko pamoja.Ni kweli kabisa kwamba kwa haya tunayoyashuhudia,sheria tulizo nazo hazitoshi tunahitaji sheria kali zaidi,labda sawa na China.Umengusa mkuu,thankyou.Ila katika hili nadhani tunahitaji Katiba mpya ili liwezekane.
 
Swala sio kuweka na kutumbua....ndo maana wajuvi wanasisitiza kua na katiba inayojitosheleza hv ushawaza raisin.a. waziri mkuu wakiumwa hali itakuaje......kaulize Nigeria buhari alipolazwa nje
Nakubaliana na wewe mkuu.Kwa kuwa hata kuingiza vipengele vya adhabu ya kifo au indefinite detention without trial kwa economic saboteurs katika sheria zetu kunahitaji mabadiliko ya Katiba!May be we need to go the China way,kwa kuwa ni wazi sasa kwamba sheria zetu haziwezi kutusaidia.Yes tunahitaji katiba mpya au vipengele vipya vya katiba.Lakini tutaweka viraka mpaka lini?
 
Back
Top Bottom