carmel
JF-Expert Member
- Aug 24, 2009
- 2,836
- 262
Sijui ni mimi peke yangu ndo naliona hili au kuna wengi pia mmeligundua. Kuna ongezeko kubwa sana la domestic violence (kwa maana ya wanandoa na walio kwenye mahusiano)kwa vijana wa umri wa kati, wasomi, wenye kazi nzuri (professionals), Nasema hivi kutokana na experience ya watu wangu wa karibu, ndugu, marafiki na hata wafanyakazi wenzangu. Mimi nilidhani watu wakipata elimu na kupata kazi nzuri wanakuwa na uwezo mkubwa wa kutatua matatizo yao ya kimahusiano bila kutumia nguvu, kupigana, kutishana, kuumizana nk.
Hivi kwaa nini inakuwa hivi? Inakuwaje watu wanaopendana wanapigana? Japo kuna kesi za wanawake wanaopiga waume zao, lakini ile ya waume kupiga wake zao ndo zaidi niliyoiona, tena wanapenda kupiga sehemu za usoni, unashangaa mtu kaja ofisini kavimba uso au ana bruises mwilini, kisa kapigwa. Ningependa tupeane experience kwa kudiscuss waziwazi tukitilia mkazo vipengele vilivyopo hapo chini ili tujue picha halisi ya mahusiano yetu na jinsi ya kuyaboresha ili kuepusha ndoa kuvunjika na kujazana kwa watoto wa mitaani. Guiding questions ni:
Umewahi kupigwa au kumpiga, kumkashifu na kumtisha mwenza wako?
unadhani ni vema kufanya hivyo?
Ulitoa taarifa police? Kama hapana kwa nini?
Athari zake je kwa muhusika ni zipi?
Domestic violence ina athari zozote kwenye career yako? Toa experience yako.
Ukiacha kupigana na kutishiana, ni njia gani zingine zaweza kutumika kuresolve issues za mahusiano?
Ukijikuta uko kwenye uhusiano au ndoa yenye domestic violence utachukua hatua gani?
Je unaweza kuongea na kushare na marafiki zako au jamaa zako masahibu yanayokukuta?
Ni jinsi gani tunaweza kuzuia domestic violence?
Hivi kwaa nini inakuwa hivi? Inakuwaje watu wanaopendana wanapigana? Japo kuna kesi za wanawake wanaopiga waume zao, lakini ile ya waume kupiga wake zao ndo zaidi niliyoiona, tena wanapenda kupiga sehemu za usoni, unashangaa mtu kaja ofisini kavimba uso au ana bruises mwilini, kisa kapigwa. Ningependa tupeane experience kwa kudiscuss waziwazi tukitilia mkazo vipengele vilivyopo hapo chini ili tujue picha halisi ya mahusiano yetu na jinsi ya kuyaboresha ili kuepusha ndoa kuvunjika na kujazana kwa watoto wa mitaani. Guiding questions ni:
Umewahi kupigwa au kumpiga, kumkashifu na kumtisha mwenza wako?
unadhani ni vema kufanya hivyo?
Ulitoa taarifa police? Kama hapana kwa nini?
Athari zake je kwa muhusika ni zipi?
Domestic violence ina athari zozote kwenye career yako? Toa experience yako.
Ukiacha kupigana na kutishiana, ni njia gani zingine zaweza kutumika kuresolve issues za mahusiano?
Ukijikuta uko kwenye uhusiano au ndoa yenye domestic violence utachukua hatua gani?
Je unaweza kuongea na kushare na marafiki zako au jamaa zako masahibu yanayokukuta?
Ni jinsi gani tunaweza kuzuia domestic violence?