Superb2014
JF-Expert Member
- Jul 29, 2017
- 8,444
- 6,480
Poleni na majukumu wana JF!
Naombeni msaada wa ushauri.
Iko hivi, mimi ni mwanamke ni mkristo ninafanya kazi katika kampuni moja. Kuna mwanaume mmoja ambaye ni mume wa mtu imani yake inaruhusu kuwa na mke zaidi ya mmoja.
Tulikuwa tunafanya kazi katika kampuni moja baadaye aliacha kazi katika kampuni tuliyokuwa tunafanya kazi wote na kupata kazi katika kampuni nyingine.
Miezi michache baada ya kuacha kazi alinipigia simu tukasalimiana vizuri.
Baada ya kusalimiana akaniambia kuwa amenipigia simu kwa lengo kuwa alitokea kunipenda sana sana kipindi tukiwa tunafanya kazi pamoja, lakini alishindwa kunieleza kutokana na mazingira ya kazi hivyo basi kwa vile hatuko pamoja kikazi anamshukuru Mungu anaomba niwe mpenzi wake.
Ni miezi minne sasa ananiambia ananipenda sana, mara nyingi huwa ananiambia imani yake inamruhusu kuwa na mke zaidi ya mmoja.
Siijui kesho yangu, huenda nikawa mke wake wa pili. Pia anasisitiza kuwa yuko tayari kupima afya kabla ya kufanya chochote.
Swali langu ni hili: Je nitakuwa sahihi kuwa na mahusiano na huyu mwanaume?
Naombeni msaada wa ushauri kwa watu wa imani zote.
Nawakilisha kwa niaba ya rafiki yangu.
Naombeni msaada wa ushauri.
Iko hivi, mimi ni mwanamke ni mkristo ninafanya kazi katika kampuni moja. Kuna mwanaume mmoja ambaye ni mume wa mtu imani yake inaruhusu kuwa na mke zaidi ya mmoja.
Tulikuwa tunafanya kazi katika kampuni moja baadaye aliacha kazi katika kampuni tuliyokuwa tunafanya kazi wote na kupata kazi katika kampuni nyingine.
Miezi michache baada ya kuacha kazi alinipigia simu tukasalimiana vizuri.
Baada ya kusalimiana akaniambia kuwa amenipigia simu kwa lengo kuwa alitokea kunipenda sana sana kipindi tukiwa tunafanya kazi pamoja, lakini alishindwa kunieleza kutokana na mazingira ya kazi hivyo basi kwa vile hatuko pamoja kikazi anamshukuru Mungu anaomba niwe mpenzi wake.
Ni miezi minne sasa ananiambia ananipenda sana, mara nyingi huwa ananiambia imani yake inamruhusu kuwa na mke zaidi ya mmoja.
Siijui kesho yangu, huenda nikawa mke wake wa pili. Pia anasisitiza kuwa yuko tayari kupima afya kabla ya kufanya chochote.
Swali langu ni hili: Je nitakuwa sahihi kuwa na mahusiano na huyu mwanaume?
Naombeni msaada wa ushauri kwa watu wa imani zote.
Nawakilisha kwa niaba ya rafiki yangu.