Tamati
JF-Expert Member
- May 15, 2017
- 1,085
- 1,956
Hiyo simu ni aina gani napenda kuifahamu kwa jina au pichaOk Mkuu, nadhani ninakuelewa,. Hapa kazini kwangu nina mtu alipata shida ya masikio ukubwani. Anaweza kuongea, naye hivyo hivyo ukitaka muongee lazima muangaliane usoni wakati mnazungumza.
Pia anasimu yake maalumu,ni simu ya kazini na nyumbani anayo ya hivyo. Anaweza kupiga yeye kwenye simu yoyote, inavyofanya kazi ni kwamba ukiongea inaandika maneno kwenye screen na yeye anakuwa anasoma unachoongea kwenye screen na kukujibu kwa kuongea.
Audiologist wanatofautiana pia hivyo sikatai ukisema hapa Nyumbani hukupata msaada zaidi ya kukupa hearing aid zenye sauti kubwa labda pia hawakuelewa tatizo lako walidhani husikii tu, kumbe unahitaji kusoma lips pia ili uelewe. Basi sina msaada zaidi, nilidhani ungesaidika kwa namna nilivyoshauri.