Kwa waziri wa kilimo

Ahead

JF-Expert Member
Jan 11, 2013
2,205
2,431
Kwa niaba ya wakulima wenzangu tulio wilaya sumbawanga vijijini,naomba kuleta malalamiko yetu juu ya unyanyasaji wa kodi ya mazao i.e mpunga,mwaka jana tulilipa gunia la debe kumi sh 2000,ndani ya mwaka huohuo tukaambiwa tunatakiwa kulipa gunia la debe saba 2000 leo hii tar 11/06/2017 tukaambiwa gunia la debe sita 2000,na ikiwa ni siku mbili tu toka bajeti ya serikali imesomwa naomba sana utusaidie kuhusu swala hili hasa ukizingatia sisi ni wakulima ambao tunakumbana na changamoto nyingi ikiwemo tabia nchi na bei kubwa ya pembejeo,tumezuiliwa hapa Sumbawanga kwenye geti la myangalua na mtoza ushuru anaeitwa Bitu Sadi,najua nimefikisha kilio cha wanyonge mahali sahihi
 
Msiwe wapole sana ndugu. Mfuatilie kama wanachokifanya ni Sawa kisheria au ni makubaliano ya huko mashambani ambayo ni ya kionevu. Kama sio Sawa msitoe. Ingia website yabunge utakutana na namba za wakuu hao waelezee.
 
maishamewewe post: 21567913 said:
Tafadhari usilete mzaha kwenye mambo ya msingi,hivi vitu visikie kwa jirani.
Mzaha gani sasa wewe unanijuwa Mimi ni NANI? Nimekuambia nafatilia hili swala lako
 
Back
Top Bottom