Kwa wazazi na walezi: Mada maalum ya watoto

Ni kweli mshana jr na hata sasahv bado makabila mengine (likiwepo letu) yanatahiri vijana porini wakiwa mostly 14-18 ages,na pia huko wanafunzwa ujasiri,adabu na heshima kwa kila mtu.

Phylosophy yangu naamini vibamia vinasababishwa na watoto kuvaa chupi na haya mapampasi tangu wadogo. Enzi zetu tulikuwa tunaanza kuvaa chupi darasa la saba, hivyo hiyo kitu kwa kuning'inia muda mrefu hurefuka. Si unaona ndugu zetu wa marubega ingawa siku hizi nao wanaiga umagharibi walivyo na mutulinga ya uhakika ( kwa jinsi nilivyokuwa nawaona siku hizo wakiwa na marubega)
 
Wadada mkiwa na watoto wachanga mambo ya makeup,perfume na mawigi myaache mnawaumiza watoto.
 
kwa watoto wanaosumbua kula kuna dawa inaitwa pharmactin
hii dawa huwa inasaidia sana kumuongezea mtoto hamu ya kula ila kwa experiency nilo nayo ukiandikiwa dozi ukaanza kumpa akianza kuchanganya kula usiendelee na dozi maana atakuwa msumbufu wa kuhitaji kula


Ushauri wa pili kama unasimu na unamuachia mtoto kuangalia video iweke kwenye flight mode

muwekee mtoto wako education videos za shule za chekechea kuliko kumuwekea nyimbo za bongofleva au video za ajabu ajabu. hili ninaushuda nalo kwa mwanangu niliye naye kwa sasa ana miaka miwili lkn anajua namba hadi 20 na anafahamu ABC...Z kutamka akiziona na kuziandika

mkaririshe mwanao namba moja wapo ya mzazi hii itakusaidia sana
mlishe mwanao samaki kwa wingi hasa sato au sangara inasaidia ukuaji wa ubongo na akili kwa mtoto

tenga muda wa kucheza na watoto wako hii inasaidia kumjengea mtoto mapenzi ya wazazi na kujiamini na kutokuwa na nidhamu ya woga

mjengee mwanao mazoea ya kuhoji na kuweza kutoa sababu ya anachohoji

hata kama uwe busy vipi jitahidi kuwatoa wanao out mkiwa wazazi wote wawili baba na mama. Jitahidi walau kula pamoja na watoto wako hata chakula cha jioni.

usigombane na mkeo au mumeo huku watoto wanashuhudia.
usimuongelee mabaya mkeo au mumeo mbele ya watoto.
Jitahidini kila mara watoto wawaone wazazi mna furaha.
Salini pamoja na watoto wenu kwa wakristo waweza teua mtoto aongoze sala
kwa waislamu kama wasalia nyumbani baba ongoza sala ila ukimaliza mwambie mtoto aombe dua.

mpongeze mpe zawadi mtoto pindi afanyapo jambo lolote zuri.
Afya ya mwanao ni muhimu fuatilia afya ya mwanao na tabia za mwanao mueleze wajibu wake ni nini kama mtoto na wewe kama mzazi wajibu wako nini
Mueleze mali ulizonazo ni zenu ninyi wazazi anatakiwa yeye baadae atafute mali zake atapokuwa mkubwa.

unapofikiria kuchepuka au kumfanyia vitimbi mwenzio kwenye ndoa ujue mwisho wa siku mtaachana na hakika nakiri Hakuna Mama kama mama na hakuna baba kama baba. hivyo mwanao hatopata malezi bora kama kutoka kwa baba halisi au kwa mama halisi, kwakuwa hakuna mzazi halisi apendae mwanae kuwa na mwisho mbaya.

Usimueleze mwanao matatizo ya baba yake au mamaake akiwa bado mdogo badala yake tatue matatizo na tofauti zenu kabla hamjapanda kitandani kulala. maana penye maudhi shetani hutawala mwaweza fanya tendo la ndoa mkazaa shetani badala ya binadamu Mshana Jr anaweza tolea ufafanuzi hili.

Ikumbukwe mtoto ni wako anapokuwa mdogo lkn akikua huwa ni wa jamii inayomzunguko lea mwanao kwa maadili mazuri ili tuwe na jamii Bora

Kumbuka hakuna mtu yeyote atayekulelea mwanao kama wewe mwenyewe mzazi.

Kumbukeni kuna maisha baada ya watoto wasisitize wanao kuheshimu kila binadamu duniani


Kama hakuna ulizima usimpeleke mwanao boarding school akiwa vidudu na shule ya msingi, hii inaweza sababisha mtoto akakosa mapenzi na mzazi.
msikilize mwanao usipende kumkatisha anapokuambia jambo hata kama nila kitoto au kipuuzi msikilize then shauri au onya au pongeza kutegemeana na jambo lenyewe. usipofanya hivyo utasababisha asijekukuambia lolote na akajenga nidhamu ya woga kwako.

Mwambie mwanao akuheshimu ila asikuogope
Thank you Mshana....hii elimu moja muhimu sanaa
 
Makuzi ya mtoto kiakili
Makuzi ya mtoto kimwili
Makuzi mtoto kimaadili

Naamini tuna wataalam wengi kwenye hizo nyanja ambao watakuja na mada zenye kujenga na kuelimishana.


*MRC Tanzania*

Je! Una tatizo la utumiaji wa pombe au mihadarati

Je! mtoto au mwenza wako ana tatizo la ulevi na utumiaji wa mihadarati

Kwa huduma ya usaidizi wa kuachana na utumiaji wa pombe na dawa nyingine za kulevya unaweza kujaza form ya maombi kupitia link hapa chini

*KIGAMBONI SOBER HOUSE* Tuko kwa ajili ya kukusaidia wewe, Mwenza wako, Mtoto au ndugu yako

Piga simu *+255 742 550 551*

au *+255 655 056 382*
*Bofya hapa*👇🏽

KIGAMBONI SOBER HOUSE
 
*MRC Tanzania*

Je! Una tatizo la utumiaji wa pombe au mihadarati

Je! mtoto au mwenza wako ana tatizo la ulevi na utumiaji wa mihadarati

Kwa huduma ya usaidizi wa kuachana na utumiaji wa pombe na dawa nyingine za kulevya unaweza kujaza form ya maombi kupitia link hapa chini

*KIGAMBONI SOBER HOUSE* Tuko kwa ajili ya kukusaidia wewe, Mwenza wako, Mtoto au ndugu yako

Piga simu *+255 742 550 551*

au *+255 655 056 382*
*Bofya hapa*

KIGAMBONI SOBER HOUSE


Jr
 
Habari za jioni.. Ninamtoto wa kike miez 11, tatizo mtoto huyu anakula sana nguo.. Yaani akiona nguo umeivaa au ipo mahali popote anaitafuna .. Hii husababishwa na nini? Au ni hali ya ukuaji kwa mtoto
 
Habari za jioni.. Ninamtoto wa kike miez 11, tatizo mtoto huyu anakula sana nguo.. Yaani akiona nguo umeivaa au ipo mahali popote anaitafuna .. Hii husababishwa na nini? Au ni hali ya ukuaji kwa mtoto
Ni tatizo la kisaikolojia.. Wengine hula udongo vipande vya sigara njiti za kibiriti nknk... Ni tatizo lenye mahusiano makubwa tangu kutungwa kwa mimba na vitamin alizokosa mama. Tafuta daktari bingwa kwakuwa wengine hufikia hatua ya kula kinyesi
 
Back
Top Bottom