Kwa Watani Wa Jadi Kenya: Moment of Truth

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,695
1,696
Wadau;

Nimekuwa ni kija mara kwa mara hapa kwa watani wa jadi na in particular Nairobi kwa shughuli za kikazi siku za hivi karibuni. Hivyo nina makazi DSM na NRB. Haya ndiyo niliyoyaona na kuyashuhudia:

1. City Centre mji ni msafi sana, bustani za kupendeza na majengo mazuri

2. Ujenzi wa majengo makubwa na ya kuvutia unaendelea sehemu mbali mbali na kwa kasi ya ajabu

3. Kenyatta Airport iko busy sana. wastani wa ndege kuruka au kutua ni kila baada ya dakika 15. Counter za uhamiaji ni nyingi na average unagongewa passport yako si zaidi ya dakika 5.

4. Dereva wa ofisi anapaki gari kwangu na kuacha funguo kwangu, anafika nusu saa kabla ya muda asubuhi na kufanya usafi wa gari mwenyewe. Anaongea kiingereza kizuri tu. Hii ni kwa madereva wote.

5. Daladala (Matatu) hazisimamishi watu. Kama unapenda Lupango au faini au kunyang'anywa leseni jaribu kusimamisha.

6. Fly-Overs si suala la kisiasa. Nimeona baadhi ya sehemu wanazijenga.

7. Ofisini watu wanafanya kazi, hakuna vigenge vya story za Simba na yanga, wala uchaguzi wala bongo fleva wala stories zozote. Ni kazi tu, moto juu moto chini.

8. Vijana wadogo sana wanashikilia position nyingi sana za juu level ya managers na wakurugenzi. Na wanajua wanachofanya inside out.

9. Kuna magari mengi kuliko DSM, lakini kila mahali traffic light zilipo zinafanya kazi, ambako hakuna pana traffic full time yuko kazini na si pembeni. So, que inatembea pamoja na kuwa magari ni mengi.

10. Maji ni mengi sana na hajawahi kukatika wala sijaona mgao na same kwa umeme.

12. Supermarket kubwa ziko kwenye vitongoji vingi.

13. Bei ya nyumba si ghali kama DSM: Mfano ninalipa $ 400 kwa apartment ya 1 bedroom, Dining Room, Sitting Room; Kitechen; Choo na bafu ikiwa full furnished including TV yenye 100 Channels, Internet na Simu. Serviced Apartment.

14. Watu wanaheshimu utawala wa sheria. Siku za hivi karibuni mawaziri walijiuzulu ili kupisha uchunguzi.

15. Wana moyo wa Utaifa kuliko kawaida.

16. Wamachinga wa Barabarani wapo wa kike na wa kiume

17. Huduma zao katika Mahoteli ni nzuri sana na wana uchangamfu wa hali ya juu.

18. Wanaofanya baishara, kazi ni kazi tu, hakuna kuchanganya biashara na mambo mengine.

19. Makampuni ya biashara na huduma yako serious kutoa huduma bora

20. Wako so strict kuhusu miadi au appointments

Hata hivyo, watani wa jadi bado wana kasumba ya ukabila kwa mbali na hata kupenda ukubwa na kujionyesha wao ni nani. Kura ya maoni hivi karibuni juu ya katiba inaonyesha kuwa Wakikuyu ambao ndiyo wengi wana-own land kubwa walipiga kura ya NO where as makabila mengine kura ya YES.

Piga picha kwa hayo machache hapo juu, na toa maoni yako. Kisha changanua nini kitatokea na watanzania itakuwa vipi wakati wa jumuiya ya Afrika mashariki watakapounganisha Nchi.

QED
 
sisi tutafaudu tu totoz za Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi, maana wabongo nawaheshimu kwa UKWARE, tehe! kwenye hayo ya juu bado saaaaana mkuuu!.si unaona Mkwere anavyjitahidi ku spread teritorry, mara kaoa huku mara kuleeeee sasa hivi na yeye atabamba kitu cha Kenya kisingizio itakuwa EAC.
 
sisi tutafaudu tu totoz za Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi, maana wabongo nawaheshimu kwa UKWARE, tehe! kwenye hayo ya juu bado saaaaana mkuuu!.si unaona Mkwere anavyjitahidi ku spread teritorry, mara kaoa huku mara kuleeeee sasa hivi na yeye atabamba kitu cha Kenya kisingizio itakuwa EAC.

Mkuu, we acha tu. Wakati jamaa airline yao Kenya Airways KQ inaongaza Africa na KQ ina 49% Precision Air sisi hatujui ATCL itaamka lini.

Kuhusu totos, Mkuu kwa sekta hiyo tumewapita ndo maana wakenya wanapenda totozi wa Kitanzania. Mimi nina distant sisters wangu wawili, jamaa wakipenda wanapenda kweli. Sisters wamemwagiwa nyumba, usafiri, elimu kwa watoto. Jamaa wamekabidhi hadi benk account na hawafanyi expenditure bila kuwashirikisha sisters. Kwa hili nimeshangaa sana.

Wadada wa Kenya nao wanapenda wa TZ wakidai ni wapole na gentlemen.

Yote tisa mkuu. Totos wako Rwanda achana na TZ au KE.

Kiuchumi, itakuwa ni maumivu tu. Jamaa uchumi wao ni much stronger more than 10 times based on excahnge rate. Tusubiri tuone . .
 
Ni kweli, wakenya wako step ahead, mfano Superman umejaribu kuongelea machinga hapo juu, hapa kwetu machinga kwa kweli ni kero, wanalazimisha watu kununua bidhaa hata kama ulikuwa hauhitaji, mfano ukiulizia bei na ukashindwa kununua itakuwa kesi, kwamba ulikuwa unamtania, Wamachinga wa Kenya wapo straight, hafuati na kusumbua mtu, kama una shida utakuja mwenyewe, Suala la Jinsia katika ujasiliamali kwa hilo nalo Kenya wametupiga fimbo, hapa kwetu binti akijihusisha na Umachinga ama Ukondakta utasikia wanamwita malaya ama mtu aliyeshindikana, tena wanawake wenzao hao hao ndio wa kwanza kumcheka, penye ukweli uongo hujitenga! tunatakiwa tujifunze mazuri kutoka kwa majirani zetu.
 
Wenzetu wako mbele dunia nzima ukiondoa ukabila ambao ni complex, mengine wanatuzidi sana!
 
Superman, watani wametuzidi kila kitu; na usiku ukiingia usijicheleweshe mitaani kwani wazee wa kazi (majambazi) ndio wanatawala. Ukiwa na bahati mbaya kukutana nao, ukiita msaada hakuna atakayetoka.
 
Ni kweli, wakenya wako step ahead, mfano Superman umejaribu kuongelea machinga hapo juu, hapa kwetu machinga kwa kweli ni kero, wanalazimisha watu kununua bidhaa hata kama ulikuwa hauhitaji, mfano ukiulizia bei na ukashindwa kununua itakuwa kesi, kwamba ulikuwa unamtania, Wamachinga wa Kenya wapo straight, hafuati na kusumbua mtu, kama una shida utakuja mwenyewe, Suala la Jinsia katika ujasiliamali kwa hilo nalo Kenya wametupiga fimbo, hapa kwetu binti akijihusisha na Umachinga ama Ukondakta utasikia wanamwita malaya ama mtu aliyeshindikana, tena wanawake wenzao hao hao ndio wa kwanza kumcheka, penye ukweli uongo hujitenga! tunatakiwa tujifunze mazuri kutoka kwa majirani zetu.

Shomari nakubaliana na wewe. Maana mabinti wako ngangari huku wanakomaa sambamba na vijana wa kiume.

Unafikiri nini kifanyike ili tuweze kucompete nao hasa zama hizi za common market.
 
Wenzetu wako mbele dunia nzima ukiondoa ukabila ambao ni complex, mengine wanatuzidi sana!

Genekai, ni kweli kabisa kamanda.

Kinachotia uchungu, sisi Watanzania ama katika personal level au National Level hatuko serious na Maendeleo kwa ujumla. wakati wenzetu maendeleo ni kama wako vitani.

Nini kifanyike hasa kubadili hali hii wadau?
 
Superman, watani wametuzidi kila kitu; na usiku ukiingia usijicheleweshe mitaani kwani wazee wa kazi (majambazi) ndio wanatawala. Ukiwa na bahati mbaya kukutana nao, ukiita msaada hakuna atakayetoka.

Mkuu,

Kwa hili ni kweli. Maana hata ujambazi mkubwa wa kutumia silaha TZ katika mabenki nk tumeshuhudia wakitajwa.

Huku kuna hao jamaa wanaitwa Mungiki ni balaa. Nasikia hata Serikali imenywea maana ni network kubwa sana na wakubwa wako involved na wana mgao wao.

Wakati mwingine ukitaka usalama, targets wao wanawapelekea pesa regular. Usipofanya hivyo, wakikutokea "Utajuuuta kuwafahamu".

Mimi mkuu, nikirudi home saa 12 nimeshafunga milango, naendelea na maisha yangu unless kama nina official function sehemu zinazoeleweka.

Hili nalo limekaaje la ujambazi zama hizi za towards EA federation?
 
Genekai, ni kweli kabisa kamanda.

Kinachotia uchungu, sisi Watanzania ama katika personal level au National Level hatuko serious na Maendeleo kwa ujumla. wakati wenzetu maendeleo ni kama wako vitani.

Nini kifanyike hasa kubadili hali hii wadau?[/QUOTE]

MKUU NAOMBA UMUULIZE "MKWERE"...MAANA ALISHAWAHI KUULIZWA SWALI KAMA HILO PALE MLIMANI CITY WAKATI WA ECONOMIC FORUM MOJA...JIBU ALILOTOA HATA MIE SIHITAJI KUIONA TANZANIA INAFIKA ROBO YA KENYA...KAMA HATA BABAKO HAJUI KWANINI FAMILIA YAKE MASIKINI... NI AIBU SANA KUANZA KUFIKIRIA KUIFIKIA FAMILIA TAJIRI...tafakari..chukua hatua...kwa msaada wa watu wa merikaniiii
 
kenya hamna uswahili ,dar longolongo nyingi na uswahili wa kutosha . nairobi inafanana na arusha karibu vitu vingi sababu arusha hamna waswahilina. imekula kwetu . tuamishe makao makuu yasiwe karibu na costal areas labda itasaidia
 
kenya hamna uswahili ,dar longolongo nyingi na uswahili wa kutosha . nairobi inafanana na arusha karibu vitu vingi sababu arusha hamna waswahilina. imekula kwetu . tuamishe makao makuu yasiwe karibu na costal areas labda itasaidia

so na nji isiongozwe na mtu wa haya maeneo...maana ndio chanzo cha longolongo..ahahahahahaaaaa... mkwereeeeeeeeee kazi unayo
 
Wasiwasi wangu EAC ikiingia wabongo wengi tutakosa ajira kwa maana jamaa kama anafanya kazi msaa nane basi yote ni productive sio sisi unafanya masaa nane nusu upo kwenye JF. Kuhusu swala la totoz bila ya kupinga Rwanda kuna totoz kuliko sehemu yoyote EAC ila hata hapo kenya pengine sio nairobi kuna totoz ni balaa nimepata kutembelea sehemu moja ya milima ya tao la africa maeneo ya voi kuna totoz balaa bila kusahau watoto wa kilenjin usipime.....

ATCL imebaki story sasa hivi uganda inakuja juu kwenye secta ya usafiri wa anga. Kenya ni moja ya nchi ambayo wananchi hawakunyimwa elimu ndio maana unaona hata chokoraa anaongea kizungu!
 
Genekai, ni kweli kabisa kamanda.

Kinachotia uchungu, sisi Watanzania ama katika personal level au National Level hatuko serious na Maendeleo kwa ujumla. wakati wenzetu maendeleo ni kama wako vitani.

Nini kifanyike hasa kubadili hali hii wadau?[/QUOTE]

Duh, ukweli unauma lakini ndo hivyo tena.

Sasa, ni nini maoni yako Mkuu?

MKUU NAOMBA UMUULIZE "MKWERE"...MAANA ALISHAWAHI KUULIZWA SWALI KAMA HILO PALE MLIMANI CITY WAKATI WA ECONOMIC FORUM MOJA...JIBU ALILOTOA HATA MIE SIHITAJI KUIONA TANZANIA INAFIKA ROBO YA KENYA...KAMA HATA BABAKO HAJUI KWANINI FAMILIA YAKE MASIKINI... NI AIBU SANA KUANZA KUFIKIRIA KUIFIKIA FAMILIA TAJIRI...tafakari..chukua hatua...kwa msaada wa watu wa merikaniiii
 
kenya hamna uswahili ,dar longolongo nyingi na uswahili wa kutosha . nairobi inafanana na arusha karibu vitu vingi sababu arusha hamna waswahilina. imekula kwetu . tuamishe makao makuu yasiwe karibu na costal areas labda itasaidia

Mkuu, labda ungefafanua NRB inafanana na ARS katika nynaja zipi maana umeongea kijumla sana.

Halafu sijui kwa nini unasema Arusha hakuna Uswahilina wakati Idara za Serikali ziko Kibao na ulisikia hoja za mapungufu ya arusha wakati wa Uchaguzi.

FYI: Kenya haiifikii Tanzania kwa vivutio vya Utalii ambavyo majority viko arusha. Yet pato letu la utalii linasikitisha ukilinganisha na Kenya.

Kata issue Mkuu, tuambie nini kifanyike?
 
so na nji isiongozwe na mtu wa haya maeneo...maana ndio chanzo cha longolongo..ahahahahahaaaaa... mkwereeeeeeeeee kazi unayo

Mkuu, ina maana kweli Tanzania bila kumhusisha Mkwere haitaendelea?

Kuna vijana nawafahamu wa Kibongo, tulimaliza nao chuo kikuu manzese (UDSM) miaka ya nyuma 1992 wako 4. Walikuwa Engineering. Vijana wakaanzisha ofisi yao ya Electrical Contractors na Structured Cabling. Wakaanzio Mtongani, kisha Magomeni katika mazingira duni sana.

Leo hii ninayo furaha kukwambia vijana hawa wanamapato yanayopita $ 10 Million kwa Mwaka na bado wanagonga mzigo kama hawana pesa.

Lakini hili si kwa watanzania wote wakati Kenya ni kwa majority.

Ama tumelogwa (kama uchawi upo), au bongo zetu zina kasoro, au attitude zetu zina mushkeli?
 
Wasiwasi wangu EAC ikiingia wabongo wengi tutakosa ajira kwa maana jamaa kama anafanya kazi msaa nane basi yote ni productive sio sisi unafanya masaa nane nusu upo kwenye JF. Kuhusu swala la totoz bila ya kupinga Rwanda kuna totoz kuliko sehemu yoyote EAC ila hata hapo kenya pengine sio nairobi kuna totoz ni balaa nimepata kutembelea sehemu moja ya milima ya tao la africa maeneo ya voi kuna totoz balaa bila kusahau watoto wa kilenjin usipime.....

ATCL imebaki story sasa hivi uganda inakuja juu kwenye secta ya usafiri wa anga. Kenya ni moja ya nchi ambayo wananchi hawakunyimwa elimu ndio maana unaona hata chokoraa anaongea kizungu!

We acha tu Mkuu, maana sasa na mimi imenibidi nifanye kazi kama wao. Maambukizi ya longolongo za Bongo yaliishia airport maana jamaa hawaelewi hizo.

Si hivyo tu, hata ukigonga mzigo jamaa wanaangalia results tu na si longolongo.

Kufukuzwa kazi hapa ni jambo la kawida kama performance yako ni below standard both in government and private. Bongo je?

Kuhusu Totoz, kwa kweli mimi sina uzoefu sana.

Ili kuna kijiwe kikubwa kina Businesses Complexes nyingi sana kuna restaurant . . . sasa kaka wakati wa lunch usipime. ukija wewe nadhani utataka kuwa pale kila wakati.

Aiseee kuna totozi halafu wanajua kuvaa halafu wameenda shule, unabaki kujiuliza tu ingekuwa vipi ingekuwa vipi kama ningezaliwa Kenya sehemu hii. ila wengi ni international.

Hata hivyo bado Totoz za bongo kwa ujumla wako juu, maana hizi za huku nyingi ni black sana halafu zimekaa kama ndume usoni (LOL).

Rawnda kwa Kagame,mambo makubwa huko. and Guess what, lazima Rwanda watakuwa kidume cha EA maana kila mtu atataka kuoa huko.

Uliza kwa nini Brazili uchumi wao unakuwa haraka. Totoz za huko ni balaa. dunia nzima inaenda kuoa na kujichanganya huko.

Au vipi bana. Au wewe una maoni gani?
 
By the way, kuhusu Elimu, huku Elimu yote basic ni Bure toka Baba Kibaki aingie Madarakani . . . a point to note.
 
Bora hiyo EA Federation ije tu, tutajua huko huko mbele. Kama ni sasa au baadaye it wont make any difference. Ingawa Kenya na wao wana Matatizo mengi lakini wanapiga hatua. Bajeti yao wanajitegemea. Si kama sisi akina Matonya. Viongozi wote wa juu wanafanya siasa zaidi badala ya kuleta maendeleo "ya kweli".

Inaniuma sana, nikifikiria huwaga ninalia, inaniuma sana.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom