Kwa Wasomi Wetu wa Sayansi & Engineering: Unajua Nanotechnology, Njoo Tuungane

Ufipa-Kinondoni

JF-Expert Member
Jan 3, 2012
4,582
2,783
Kwa watu wadadisi wa mambo wa maendeleo ya Sayansi na Uhandisi wanasema "Nanotechnology" ndo taaluma ya juu kabisa kwa wakati huu duniani. Imeweza kubadiri sura ya tafiti za dunia ya kwanza na baadhi ya nchi zilizojizatiti kuwekeza katika tafiti. Imeweza kuzalisha bidhaa mpya nyingi na za kisasa kabisa duniani na kufanya mapinduzi ya viwanda hasa katika mawasiliano na elektroniki, tiba na kilimo.

Katika siku za hivi karibuni Chuo cha Nelson Mandela cha pale Arusha kimejikita katika tafiti mbalimbali zinazolenga kuendeleza taaluma hii hapa nchini. Pia wanafunzi na wanataaluma mbalimbali wa vyuo vya hapa nchini wemeungana na kuanzisha chama cha watu wanaotaka kuendeleza tafiti za taaluma hizi injulikanayo kama "Tanzania Nanotechnology Initiatives-TANi" tanzaniananotech.org ikijumuisha wataalam katika masomo ya chemistry, biology, physics, engineering na computer.

Kwa wale wenye nia thabiti ya kufanya tafiti na kusimamia maendeleo ya nchi yetu kisayansi. Karibu tuungane.
 
Mkuu tuna equipments za ku back up research in such an advanced field kweli.
Wakati basic researches tu on a tissue level zinatushinda ije kuwa at a molecular level.
Na financial support inatoka wapi? Nchi ya nje gani iko tayari kutoa hela bongo na kuacha wanasayansi wake, kwa scientific credibility gani tuliyonayo?
Serikali inashindwa kutoa funds kwa very basic and simple research itakuja kuwa kwenye nano technology ambayo wanasiasa wataona kama ndoto za alinacha!
Ngoja ni visit kwanza.
 
Its a good start ila na doubt sana sustainability yake.
Ila ngoja na mimi nikajiunge nisiwe pessimist sana.
 
Mkuu tuna equipments za ku back up research in such an advanced field kweli.
Wakati basic researches tu on a tissue level zinatushinda ije kuwa at a molecular level.
Na financial support inatoka wapi? Nchi ya nje gani iko tayari kutoa hela bongo na kuacha wanasayansi wake, kwa scientific credibility gani tuliyonayo?
Serikali inashindwa kutoa funds kwa very basic and simple research itakuja kuwa kwenye nano technology ambayo wanasiasa wataona kama ndoto za alinacha!
Ngoja ni visit kwanza.
Sorry! Tab yangu naona haikuwa active eneo la kuandikia nikashindwa kujibu.
Nadhani hata lengo la kuanzisha chuo cha mandela ni kuinua kiwango cha tafiti za kisanyasi hapa nchini. Kwa hali niliyoona tunaweza kufanya kwa kuanzia na collaborative research. Mfano, kuanzia mwaka jana Nelson Mandela wanapeleka wanafunzi wao Africa Kusini kufanya dissertation zao hasa kwa vile hakuna vifaa muhimu kwetu.

Hii, inaongeza wataalam wa kuweza kutumia vifaa vya kisasa kabisa ambavyo wezetu wanatumia katika tafiti zao. Angalia profile mbalimbali za wanachama wa TANi.

Its a good start ila na doubt sana sustainability yake.
Ila ngoja na mimi nikajiunge nisiwe pessimist sana.
Kupanga ni kuchagua. Mpaka sasa, imesemekana Chuo cha mandela kama chuo kinachotazamiwa kuwa kitovu cha utafiti wa sayansi nchini, kina vifaa vingi sana vya nyana mbalimbali za kisayansi. Juzi juzi tu, kimeweza kuangiza SEM (Scanning Electron Microscope) X-Ray diffraction kwa ajili ya ku-analyze aina mbalimbali za materials katika maabara zake.

Hivyo, tujue mwanzo mgumu ila tutafika.

Ngoja nijishauri kdogo!! ntakuja!!
Bwana mzee, unahaki ya kujishauri katika kila kitu unachofanya. Ila ni bora usiwe mbali na wengine. Nimewahi kujifunza kitu kinachofanya waweze kudhubutu katika maisha.

Twende mkuu.
 
Kwa watu wadadisi wa mambo wa maendeleo ya Sayansi na Uhandisi wanasema "Nanotechnology" ndo taaluma ya juu kabisa kwa wakati huu duniani. Imeweza kubadiri sura ya tafiti za dunia ya kwanza na baadhi ya nchi zilizojizatiti kuwekeza katika tafiti. Imeweza kuzalisha bidhaa mpya nyingi na za kisasa kabisa duniani na kufanya mapinduzi ya viwanda hasa katika mawasiliano na elektroniki, tiba na kilimo.

Katika siku za hivi karibuni Chuo cha Nelson Mandela cha pale Arusha kimejikita katika tafiti mbalimbali zinazolenga kuendeleza taaluma hii hapa nchini. Pia wanafunzi na wanataaluma mbalimbali wa vyuo vya hapa nchini wemeungana na kuanzisha chama cha watu wanaotaka kuendeleza tafiti za taaluma hizi injulikanayo kama "Tanzania Nanotechnology Initiatives-TANi" tanzaniananotech.org ikijumuisha wataalam katika masomo ya chemistry, biology, physics, engineering na computer.

Kwa wale wenye nia thabiti ya kufanya tafiti na kusimamia maendeleo ya nchi yetu kisayansi. Karibu tuungane.
Ninaikubali sana hii kitu aise, jinsi ya kujiunga sasa, hebu nidokezee mkuu, safi sanaaa kwa hii information, niliwahi kusomoma juu ya hii kitu kwenye mtandao but sikujua kama Tz kuna hii ,TANi
 
What's TANi, Wasiliana na hawa jamaa hata kwa email. You can get full info. Uzinduzi utafanyika hivi karibuni. Pia angalia katiba yake online utaona hapohapo kwenye web.
Ninaikubali sana hii kitu aise, jinsi ya kujiunga sasa, hebu nidokezee mkuu, safi sanaaa kwa hii information, niliwahi kusomoma juu ya hii kitu kwenye mtandao but sikujua kama Tz kuna hii ,TANi
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom