GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,052
- 107,537
Poleni na Kazi pamoja na Majukumu yenu makubwa ya kila Siku na hakika tunaona jitihada zenu hasa katika Kumsaidia na Kumuongoza vyema Mheshimiwa Rais hasa katika Utendaji wake wa kila Siku ambao najua unahitaji umakini mkubwa sana.
Naomba nikiri waziwazi hapa kuwa GENTAMYCINE siyo ‘ Muumini ‘ wa Kupenda kuona kila mara / mara kwa mara Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli anafanya ‘ Mabadiliko ‘ kwa Watendaji wake ambao hapo awali Yeye mwenyewe ndiye aliwateua huku akiwaamini kuwa watamsaidia.
Mnaweza kuona labda ni Kitu cha kawaida na mkakichukulia ‘ poa ‘ ila kwa wenye kujua ‘ Kufikiri ‘ zaidi hapa kunaonekana kuna ‘ tatizo ‘ mahala ama kwa Mheshimiwa Rais mwenyewe juu ya hao anaowateua au basi Taasisi yake ‘ Nyeti ‘ yenye Jukumu Kubwa la Kumsaidia kuwafanyia ‘ thorough vetting ‘ hao aliowapendekeza basi nayo haifanyi Kazi yake vizuri.
Ombi langu Kwenu naomba kwa Muhula ujao wa Urais basi Rais akishapendekeza tu Watu wake basi awape Kazi hiyo Watu ‘ Maalum ‘ ili wamfanyie ‘ Uchunguzi ‘ wa Kutosha wa Kimaadili na Kiuwezo wa hao Watu wake ili basi tuanze ‘ Kupumzika ‘ na hizi ‘ Breaking News ‘ za Kutumbua / Kubatilisha Uteuzi kwani zinamdhalilisha mno Rais kwa namna moja au nyingine.
Nasisitiza tena kwamba GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE sipingi kuwa na ' Mabadiliko ' ya Kiutendaji hasa ya Kiserikalini kutoka Kwake Mheshimiwa Rais ila ' Kinachonikwaza ' ni kuona haya ' Mabadiliko ' huwa yanakuwa ya mara kwa mara tofauti na Marais wengine wa nchi zingine au hata tu ' Watangulizi ' wake. Na hofu yangu Kubwa pia hali hii ya Kubadili badili Watendaji kila wakati isije pia ikampa Mheshimiwa Jina Jipya la ' Ubatizo ' la Rais Mtumbuaji na Mbadilishaji mara kwa mara.
Kwani kuna tatizo gani labda pale Mtu fulani akishajulikana kuwa ndiyo atakuwa Rais wa Tanzania basi asiombwe tu ' List ' yake ya Watendaji anaowataka katika Serikali yake ili Idara yake / Taasisi yake ' Nyeti ' iyapitie na iyakague ' Kiufundi ' kabisa hasa kwa Kuzingatia Kigezo cha Maadili na Utendaji Kazi wake ili wakishamaliza basi wanampelekea Mheshimiwa Majina ya wale waliowapitisha, waliowakataa na pengine ambao Wao ( Idara ) wanayapendekeza?
Kwa mfano katika Awamu hii hii ya Tano kuna baadhi ya Watendaji ambao wanajulikana kabisa kuwa hawawezi, hawana Sifa, wamejaa Uhuni na Utapeli mtupu huku hata tu Utendaji Wao huku walikokuwa ulikuwa ni mbaya lakini cha Kusikitisha kabisa Mheshimiwa Rais amewaamini na Kuwatea na kuna wengine alishawabadilisha ( alishawaondoa ) Uongozini mpaka Jana.
Ni ushauri tu mkiona unawafaa uchukueni mkiona hauwafai basi niachieni nao tu mwenyewe labda wengine watauchukua.
Nawasilisha.
Naomba nikiri waziwazi hapa kuwa GENTAMYCINE siyo ‘ Muumini ‘ wa Kupenda kuona kila mara / mara kwa mara Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli anafanya ‘ Mabadiliko ‘ kwa Watendaji wake ambao hapo awali Yeye mwenyewe ndiye aliwateua huku akiwaamini kuwa watamsaidia.
Mnaweza kuona labda ni Kitu cha kawaida na mkakichukulia ‘ poa ‘ ila kwa wenye kujua ‘ Kufikiri ‘ zaidi hapa kunaonekana kuna ‘ tatizo ‘ mahala ama kwa Mheshimiwa Rais mwenyewe juu ya hao anaowateua au basi Taasisi yake ‘ Nyeti ‘ yenye Jukumu Kubwa la Kumsaidia kuwafanyia ‘ thorough vetting ‘ hao aliowapendekeza basi nayo haifanyi Kazi yake vizuri.
Ombi langu Kwenu naomba kwa Muhula ujao wa Urais basi Rais akishapendekeza tu Watu wake basi awape Kazi hiyo Watu ‘ Maalum ‘ ili wamfanyie ‘ Uchunguzi ‘ wa Kutosha wa Kimaadili na Kiuwezo wa hao Watu wake ili basi tuanze ‘ Kupumzika ‘ na hizi ‘ Breaking News ‘ za Kutumbua / Kubatilisha Uteuzi kwani zinamdhalilisha mno Rais kwa namna moja au nyingine.
Nasisitiza tena kwamba GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE sipingi kuwa na ' Mabadiliko ' ya Kiutendaji hasa ya Kiserikalini kutoka Kwake Mheshimiwa Rais ila ' Kinachonikwaza ' ni kuona haya ' Mabadiliko ' huwa yanakuwa ya mara kwa mara tofauti na Marais wengine wa nchi zingine au hata tu ' Watangulizi ' wake. Na hofu yangu Kubwa pia hali hii ya Kubadili badili Watendaji kila wakati isije pia ikampa Mheshimiwa Jina Jipya la ' Ubatizo ' la Rais Mtumbuaji na Mbadilishaji mara kwa mara.
Kwani kuna tatizo gani labda pale Mtu fulani akishajulikana kuwa ndiyo atakuwa Rais wa Tanzania basi asiombwe tu ' List ' yake ya Watendaji anaowataka katika Serikali yake ili Idara yake / Taasisi yake ' Nyeti ' iyapitie na iyakague ' Kiufundi ' kabisa hasa kwa Kuzingatia Kigezo cha Maadili na Utendaji Kazi wake ili wakishamaliza basi wanampelekea Mheshimiwa Majina ya wale waliowapitisha, waliowakataa na pengine ambao Wao ( Idara ) wanayapendekeza?
Kwa mfano katika Awamu hii hii ya Tano kuna baadhi ya Watendaji ambao wanajulikana kabisa kuwa hawawezi, hawana Sifa, wamejaa Uhuni na Utapeli mtupu huku hata tu Utendaji Wao huku walikokuwa ulikuwa ni mbaya lakini cha Kusikitisha kabisa Mheshimiwa Rais amewaamini na Kuwatea na kuna wengine alishawabadilisha ( alishawaondoa ) Uongozini mpaka Jana.
Ni ushauri tu mkiona unawafaa uchukueni mkiona hauwafai basi niachieni nao tu mwenyewe labda wengine watauchukua.
Nawasilisha.