Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Jamani si ndio kama hivi nimekukumbuka Unnie? Of course ninazo ktk PC, kwa sasa ninazo drama 5 na movie moja.
Ngoja nikifikisha walau 10 nikucheki nikupatie...
Hii strong woman ni nzuri comedy kibao na ina crime pia.
Make sure huangalii hizi ninazokuambia, nakuhifadhia...
Unnie amesmile niko mkao nasubiria kwa hamu ila nahisi zitafika 10 Dec😎..
 
30 days left arthdal chronicles episode 13 itoke
mwezi august umekuwa mrefu sana bila ya shaka kuna mjinga itakuwa ameuwekea super glue ili siku zake zisogee kwa taratibu kama kinyonga.
upanga
kioo
kengele.

ushirikiano wa mwanamama Kim Young-Hyun pamoja na ahjussi Park Sang-Yeon umekuwa ni chachu ya kuzalishwa kwa project zinazokidhi kiwango cha juu kama standard gauge ya kolomijee country.
 
Hahaaaaa yani kama ubalozi wa Korea ungetoa ofa kwa wanaoipenda Korea Wallah nisingeikosa nafasi ya kwenda kutalii kisiwani Jeju na jijini Seoul.

Nawapenda kitambo na mpaka nimeiambukiza familia yangu, mdogo wangu nae kawa mlevi wa drama za Kikorea siku hizi sihangaiki kudownload drama kila weekend naletewa mzigo wa wiki nzima.
Viva Korean Drama
Una stahiki. Heshima.
 
mjinga wewe kutoka pyongyang ndio nini kunipa heshima ya ufalme haliyakuwa sina hata kibanda cha udongo nitakachokitumia kama ikulu?

bridal mask hadithi yake inatokana na simulizi zinazotumia lugha ya katuni a.k.a manhwa kwa lugha ya korea au comics book kwa lugha ya beberu mweupe.

hata a man called a god drama nayo pia ni manhwa.
chukua hadithi za kipepe na rungu lake kama senga zitengenezee drama au movie.​
Komas minda.
 
Jaman hii season ya kingdom inanimalizia mb msaada maana nimevutiwa nayo balaa
kingdom wameishia season 1 na ilicontained episode 6.
season 2 mpaka mwakani inshallah ndio itaonyeshwa tena kupitia netflix

mwanzoni nilikuwa mshabiki mkubwa sana wa kazi za mwanamama kim eun seok lakini tokea nimfahamu shoga yake anayeitwa kim eun hee nimejikuta nahamishia majeshi yangu yote upande wake.

wote ni waandishi wazuri wa script ila ninachompendea kim eun hee ni uwezo wake wa kuandika hadithi zinazobeba mandhari tofauti ya matukio anayotaka kutufikishia wana hadhira kuanizia signal, ghost, sign drama pamoja na 3 days drama.

alichokifanya mwanamama kim eun hee ni kuigeuza webtoon inayoitwa Land of the Gods ambayo ameiandika mwenyewe kuwa drama.
1565725850094.png
 
teh teh teh gwanggaeto alikuwa hana utofauti na stering wa kihindi muda wote anapiga yeye tu.
yule fala kama angeliendelea kuishi kwa miaka 10 zaidi nadhani angelitembeza kipigo mpaka akafika maeneo ya chato.
alikufa akiwa na miaka 39 ya kuzaliwa.​
Chato wangalikuwa Ukoo wa Dam
teh teh teh gwanggaeto alikuwa hana utofauti na stering wa kihindi muda wote anapiga yeye tu.
yule fala kama angeliendelea kuishi kwa miaka 10 zaidi nadhani angelitembeza kipigo mpaka akafika maeneo ya chato.
alikufa akiwa na miaka 39 ya kuzaliwa.​
images.jpeg


King Gwanggaeto alikuwa moto hata chato wangekuwa ukoo wa Dam
 
DESIGNATED SURVIVOR 60 DAYS DRAMA:
ni mimi peke yangu ndiye ninayeifuatilia hii drama inayotokanwa na series ya kimarekani?
sijabahatika kuangalia episode ya jana na leo (13, 14) ila nimeanza kuwa na wasiwasi huenda hata mshauri mkuu wa raisi bwana han naye ni sehemu ya wahusika wa mkakati wa kufanya uasi either kwa kufahamu au kwa kutumiwa bila ya kujifahamu. huenda advisor han ndiye aliyempa amri secretary cha yong jin ampigie simu waziri wa ulinzi kwa ajili ya kusitisha ule mpango.
  • han ndiye aliyetengeneza mpango wa kumfanya bwana park mu jin awe waziri wa mazingira haliyakuwa anafahamu fika jamaa hana uzoefu wowote wa kiuongozi
  • yeye ndiye aliyemtuma PMJ kwenye mkutano uliokuwa ukijadili ajenda ya mazingira uliohudhuriwa na wanadiplomasia kutoka marekani, kwa kuwa alikuwa anafahamu fika jamaa hana uzoefu wa siasa muda wowote ataleta majanga yatakayopelekea kufukuzwa kwake.
  • hata Oh Young-Seok naye alishawahi kusema ya kwamba Park mu jin naye pia ni sehemu ya wahusika wa mpango wa kuripua bunge, hii inaonyesha dhihiri mastermind wa huu mpango tayari alishakwisha waandaa designated survivors wawili wa tukio hilo kwa wakati mmoja, mmoja kati yao watamtumia kwa siku 60 baadae watamuweka raisi wanayemtaka kwa njia ya kura.
1565727961246.png
 
Hapana aiseee Empress Ki imenishinda kwa kweli Togon kanivunja moyo was kuiangalulia ni boya sana
empress ki nilifika episode ya 11 ikanishinda kuiendeleza mpaka leo hii licha ya kusifiwa kote na wadau mbali mbali ulimwenguni.

drama nyengine inayoniwia vigumu kuiangalia ni jewel in the palace pamoja na dong yi.
halafu nimejishtukizia ya kwamba sina mapenzi makubwa sana na project za ji chang wook, nimeangalia project zake mbili tu nazo ni K2 na warrior baek dong soo drama
 
empress ki nilifika episode ya 11 ikanishinda kuiendeleza mpaka leo hii licha ya kusifiwa kote na wadau mbali mbali ulimwenguni.

drama nyengine inayoniwia vigumu kuiangalia ni jewel in the palace pamoja na dong yi.
halafu nimejishtukizia ya kwamba sina mapenzi makubwa sana na project za ji chang wook, nimeangalia project zake mbili tu nazo ni K2 na warrior baek dong soo drama
Healer hujaangalia? Ningekutambulisha mchumba mwingine
 
Kim Eun Sook’s New Drama Starring Kim Go Eun And Lee Min Ho Shares Broadcasting Details
On August 12, Hwa&Dam Pictures and Studio Dragon announced, “Kim Eun Sook’s new drama ‘The King: The Eternal Monarch’ is set to premiere in the first half of 2020 and we have decided to air the drama on SBS.” With the televising rights being sold to SBS, “The King: The Eternal Monarch” will air first on the broadcasting channel and will then be distributed across various platforms through Hwa&Dam Pictures and Studio Dragon.

Kim Eun Sook has penned numerous hits such as “Descendants of the Sun,” “Heirs,” “Goblin,” and “Mr. Sunshine.” The upcoming drama will reunite her with “Heirs” lead Lee Min Ho and “Goblin” lead Kim Go Eun.

“The King: The Eternal Monarch” will be a fantasy drama about two parallel universes of a monarchy and a democracy. Lee Min Ho will play Emperor Lee Gon, who tries to close the door between the two worlds, while Kim Go Eun will take on the role of detective Jung Tae Eul, who works with the emperor to protect people’s lives.

1565731701380.png
 
Hapana aiseee Empress Ki imenishinda kwa kweli Togon kanivunja moyo was kuiangalulia ni boya sana
Hahaha! Huyo Togon unavyomuona "boya" kiasi hicho ni sababu tu ana maadui kila kona na hana mtu wa kumwamini na kila anayeonekana yuko karibu yake kwa namna moja au nyingine ni mnafiki wa kutupwa.

Ukifuatilia hata watu walioko karibu yake sana hususan hata Queen Dowager naye anamtumia tu kwa maslahi yake licha ya kuwa ni mama yake mzazi. Vita kali sana ya madaraka hiyo!

Kwahiyo katika hali kama hiyo inamlazimu kuwa mpole mpaka pale atakapopata mahala pa kusimamia na kujenga ushawishi wa kutosha ili kuweza kuzivunja-vunja ng'ome za maadui zake wa kisiasa.

Isitoshe hiyo hali yake ya "uzembe" unayoiona ndiyo kwa namna moja ama nyingine iliwafanya hata wale maadui zake wakuu wampuuze bila kujua kuwa jamaa naye ana "mishe" zake za siri na anajipanga kimyakimya ili kulipa kisasi kwa wabaya wake.
 
Back
Top Bottom