Gwanggaeto the Great
JF-Expert Member
- Apr 14, 2018
- 817
- 1,772
Hivi kuna drama inayomuhusu Dangun Wanggeom?!, Nasikia alikuwa si Binadamu.Arthdal chronicles ep 7
Tagon ni mwanadamu mwenye tabia na mipango ya kishetani ndio maana si ajabu kukuta baba yake alitamani kumuua ili jinamizi la kumzaa muhuni atakayeleta mtafaruku kwenye ardhi ya arthdal limuondokee, kinyume chake tagon kwa mara nyengine alimaliza uhai wa mzee wake mwengine baada ya kumuua mama yake hapo mwanzoni.
moja kati ya sifa kubwa ya igutu ni uwezo wao wa kujifunza kwa haraka sana pamoja na kuyazoea mazingira mageni kwa muda mfupi ndio maana si ajabu kumuona eunseom (song joong ki) anaweza kupigana kwa kutumia zana zilizotengenezwa kwa chuma eg panga, shoka haliyakuwa kwa miaka 20 ya kuzaliwa kwake hajawahi kuzishuhudia machoni mwake, si hivyo tu eunseom pia ana uwezo mkubwa wa kuendesha farasi haliyakuwa watu wa kabila la wahan kiupande wao wanamchukulia farasi kama ni kiumbe mfano wa kuku (hawamtumii kwa usafiri).
View attachment 1136289
ndio maana pia si ajabu kumshuhudia saya (song joong ki) na yeye akiwa na chembe chembe za ukatili ambazo amejifunzia kutoka kwa Tagon anayemchukulia kama ni baba yake pamoja na Tanya ambaye anamchukulia ni kama mlezi wake (mama)
wote wawili hawaoni tabia kutoa uhai wa mtu anayewaekea kikwazo kwenye njia zao za kuyatafuta mafanikio yao ya kuitawala ardhi ya arthdal.
ninachokiona ni kitendo cha sanya kutaka kumtumia mwanadada tanya ili atimize malengo yake kama ilivyo tagon anavyomtumia taelha, na wakati huo huo tanya atataka kumtumia sanya kwa sababu tanya anamfahamu sanya kupitia ndoto alizokuwa anaziota eunseom (sijajua kama sanya na yeye ana uwezo wa kuona matukio ya mbeleni kwa njia ya ndoto kama ilivyo kwa mdogo wake eunseom)
sanya ndio kikoo kilichotabiriwa so that sijui kioo hicho kitatumika vipi:
je atakuwa kioo kwa kumsaidia tagon atimize ndoto yake ya kuiendesha dunia atakavyo huku akimsubiria baba yake amrithishe madaraka pindi tagon atakapochoka au kioo hicho kitabeba sifa ya mapinduzi ya kumuondoa nguvuni tagon na hatimaye sanya kujimilikisha madaraka ya arthdal.
si tunafahamu karma is bitch,kama ilivyo tagon alivyomtoa uhai baba yake je na sanya atamtoa uhai bwana tagon?
tusisahau tagon ndiye aliongoza kampeni ya kumuua ragaz ambaye ni baba mzazi wa eunseom na sanya pamoja na mauaji ya kizazi kizima cha neandthal species.
sifikirii kama mapacha eunseom na sanya wataungana kwa pamoja kwa sababu ni watu waliokuzwa mazingira tofauti ya kitabia, mmoja anawajali wananchi wanaonyanyaswa na mmoja amekulia nyumba ya shetani mwenye kupenda harufu ya damu ya wanaonyanyaswa.
kongole kwa song joong ki kwa kutuonyesha sura mbili zenye kutofautiana kimatendo kwenye kiwiliwili kimoja.
View attachment 1136291