Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

kwangu mimi huwezi kuizungumzia nchi ya Joseon bila ya jeong do jeon(sambong). nikiangalia harakati zake za kupigania usawa kwenye taifa la Goryeo kwa kupambana na waziri mkuu lee I-Nim mpaka akaamua kuwa muasi na kufanya mapinduzi, kutafautiana na rafiki yake kipenzi Jeong mong ju (poeun) great thinker wa kipindi hicho ambaye alikuwa akiamini wao kwa pamoja wana uwezo wa kurudisha heshima ya taifa la goryeo ila bahati mbaya sambong hakuwa tena na mawazo ya goryeo, kwangu mimi urafiki wa sambong na poeun ulikuwa ni zaidi ya urafiki wa lipumba na seif.

ukiangalia drama hii ya jeong do jeon ndipo utapata kufahamu zaidi jinsi walivyokutana kwa mara ya kwanza kati ya sambong na general yi seong ye mnamo mwaka 1383 kwenye kambi za hamgyong wakati ambao yi seong ye alikuwa anaongoza vita dhidi ya wavamizi wa japan.

mwaka 1388 wakati ambao taifa la mongols lilipoivamia taifa la goryeo ndipo yi seong ye akaamrishwa kuivamia kaskazini mwa liaodong ila cha kushangaza lee seong ye akakataa oda ya mfalme na ya general choi young na akatoa sababu zifuatazo kwa ushauri wa mwanamipango sambong
  1. taifa la goryeo ni dogo hivyo halina uwezo wa kuvamia taifa kubwa
  2. hali ya hewa ilikuwa ni ya mvua hivyo basi msafara wa kuelekea kaskazini utakumbana na dhoruba nyingi
  3. kama nchi itaelekea vitani upande wa kaskazini basi wajapan watavamia upande wa kusini
  4. kwa kuwa ni wakati wa mvua basi wananchi wanapaswa kulima na si kwenda vitani baada ya majibizano ya muda mrefu yi seong ye akaamua kurudi mji mkuu wa gaegyeong pamoja na jeshi lake na kutokezea vita ya wenye kwa wenyewe jambo lililopelekea general choi young kushindwa vita na ukawa ni mwisho wake wa kuwa na nguvu.
View attachment 1057742
huyu choi young alijitabiria kabla ya kifo chake ya kwamba kaburi lake halitaota majani, ilichukua miaka mingi mnooo kaburi lake kuota majani.


kukosa nguvu kwa choi young kulipelekea kambi inayopigania goryeo ipoteze nguvu kubwa na kubaki jeong mong jo peke yake na upinzani dhidi ya rafiki yake kipenzi sambong ulizidi hadi kupelekea kutoa amri ya sambong anyongwe.

ila siku chache kabla ya kunyongwa kwa sambong lee bang won ambaye alikuwa ni mtoto wa tano wa general yi seong ye alimuua jeong mong jo (poeun) kwenye daraja la sonjukkyo na ukawa ndio mwisho wa harakati zake za kuipigania goryeo.
kabla ya kifo chake aliandika shairi na kumtumia yi bangwon ampelekee baba yake ambalo nimeliweka post ya juu.

Though I die and die again a hundred times,
That my bones turn to dust, whether my soul remains or not,
Ever loyal to my Lord, how can this red heart ever fade away?
jamaa alikuwa mzalendo aliyepitiliza, alikuwa akimaanisha ya kwamba kwenye maisha yake hawezi kuitumikia GORYEO halafu baadae aitumikie JOSEON hata kama atakufa mara 100.

yi seong ye akawa mfalme wa joseon na ukawa ndio mwisho wa utawala wa wang clan ulioasisiwa na mfalme wang gun na kuanza kwa utawala wa lee (yi) clan sambong akawa waziri mkuu wa joseon na ndiye aliyesimamia ujenzi wa ikulu ya joseon na akaipa jina la Gyeongbokgung palace ambayo mpaka leo inatumika kwa ajili ya kuigizia drama na pia kuwa ni kivutio cha utalii.

hii ikulu wananchi waliwahi kuichoma moto kwenye vita ya imjin baada ya mfalme seonjo kukimbia ikulu
View attachment 1057743
vita ya madaraka ikaingia tena kwenye taifa la joseon baada ya yi bang won kutokuchaguliwa kuwa ni mrithi wa kiti cha mfalme ambapo nafasi yake alipewa mtoto wa kwanza wa mke wa pili wa general yiseongye (yi bangseok) na aliamini aliyesababisha yeye kukosa nafasi ni sambong kutokana na bifu la kumuua rafiki yake poeun.

kosa lile lile alolifanya general choi young la kutaka goryeo ivamie nchi ya china kwa ajili ya kuurudisha mji wa liaodong ambao kihistoria ilikuwa ni ngome ya goguryeo kabla utawala wake haujaanguka naye sambong alilirejea tena kwani naye aliamini joseon ina uwezo wa kuipiga china. siku chache baada ya kufa kwa malikia sindeok naye yi bangwon aliitumia nafasi hii kufanya mapinduzi kwa kuwaua ndugu zake ambao walizaliwa na mama wa kambo na pia kumuua sambong na wafuasi wake na akabeba ufalme.
View attachment 1057744
yi bangwon akamtangaza sambong kama ni muasi wa taifa na mwili wake utupwe na pia akamtangaza jeong mong jo kama ni shujaa wa goryeo.
cha ajabu yi bang won bado aliendelea kutumia baadhi ya mifumo ilioanzishwa na sambong chini ya utawala wake.
  1. sambong aliamini ya kwamba nchi bora ni ile ambayo ina good connections kati ya kiongozi mkuu na wafuasi wake, it means yeye aliamini ya kwamba mfalme hapaswi kuwa na nguvu kubwa ya kimaamuzi kwa sababu itakuwa ni hatari hususani itakapotokezea siku ambayo taifa litatawaliwa na mwendawazimu wa matendo na si akili.
  2. yi bang won na wafuasi wake waliamini ya kwamba nchi bora ni ile ambayo itajengwa kwa nguvu na maamuzi ya mfalme au raisi kwa nyakati hizi kama ilivyo katiba ya TANZANIA ukiangalia kwa jicho la tatu.
  3. nilichopenda ni kwamba wote walikuwa wanawapigania raia na si maslahi yao tofauti na viongozi wa kileo, huyu yi bang won licha ya kujenga misingi imara ya joseon lakini alikuwa ni muuaji aliyevuka mipaka, inamaana sambong alikuwa sahihi kiupande fulani
ukimaliza hii itafute the great king sejong drama, imeelezea kiundani maisha ya lee bang won na utawala wake pamoja na utawala wa mtoto wake yi do (sejong the great).
raha ya drama za joseon uzifuatilie kwa mtiririko wa wafalme zinavutia sana​

best drama kwa mwaka 2014, humu ndani muna veterani watupu wanaofahamu maana halisi ya sanaa.

Aiseeee wewe jamaa ni noma sana
Kwa wengine wasiojua hizi mambo zetu za Korea mimi huwa naonekana najuaaaa ila hapa najiona kabisa sijui.

Sasa jana baada ya kumaliza kuangalia King Gwanggaeto nikajikuta namuuliza swali mtu ambaye hajui mambo ya Korea baada ya kugundua Houyan ndio Beijing ya leo China.

Swali nililomuuliza ni kwamba “Ni wazi Korea, Japan na China zilikuwa ktk muunganiko. Ilikuwaje zimejitenga kama ilivyo leo hii?”

Nimengalia drama nyingi ila sio ktk mtiririko, na ili upate kulifahamu hili vyema basi uweze kuunganisha drama hizo ktk mtiririko...

Naomba unipe mtiririko mzuri/sahihi wa hizo drama ambazo zinaelezea/kuonesha mgawanyiko huo.
Hata ukielezea kwa maandishi pamoja na hizo drama itakuwa vizuri zaidi, asante.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
yi bang win poem

This won’t matter, that won’t matter.
The walls behind the temple of the city's deity* has fallen - shall it be this
Let us mingle together like this and enjoy it for a hundred years.
(Yi Bang-won is declaring the death of the era - the Goryeo Dynasty)

great thinker jeong mong jo poem: anamjibu
Though I die and die again a hundred times,
That my bones turn to dust, whether my soul remains or not,
Ever loyal to my Lord, how can this red heart ever fade away?

  1. kwenye siasa hakuna makubaliano ndio maana kila siku kuna umwagaji wa damu unaoweza kuepukika, tafsiri halisi ya neno siasa ni kitendo cha kulipiza kisasi kwa mpinzani wako haijalishi ametenda jambo jema, kwenye siasa umwagaji wa damu na ulipizaji kisasi hautakwisha, hiyo ndio maana halisi ya siasa.
  2. kwenye siasa sote tunaishi kwenye kilele cha mlima na wala haichukui muda mkubwa sana kwa mmoja wetu kudondoka kwenye kilima cha siasa,
  3. kwenye siasa yeyote aliyepoteza nguvu hana utofauti wowote na marehemu na hata nguo ya ndani pia atapangiwa kuvaa.
nisikuchoshe itafute hii drama haijalishi umeshaangalia six flying dragons pamoja na the greet seer drama.
ila usisahau ni wachache sana wanaoua kwa upanga na wao wakafa kwa upanga isipokuwa yule ambaye ataweka udhaifu kwenye ngome yake kama alivyofanya mwanaharakati jung do jeon a.k.a sambong.

nimetembelea kissassian.sh bahati mbaya sijakutana na link ya hii drama​

Nilikuwa nakumbuka hiyo ‘Sambong’ ila sikuwa na uhakika sana, asante.

Ujue Six flying dragons nimekuona mara nyingi ukiisifia hapa ila huwa hainivutii sababu imekaa kichina china hivi, na mimi ukitaka kunichefua niletee drama ya kichina, sizipendi kabisa maana zina mambo ya kichawi ambayo siyaamini, sipendi drama za mambo ya kufikirika.

Vipi ktk hii Sambong na six flying dragons nianze na ipi? Nimewahi kuona ukisema kuna kama muendelezo fulani baina ya hizo drama mbili.

Hiyo The Great Seer ipo ktk list yangu kitambo tu, Jin Jin Hee yupo tena? Hiyo ni lazima


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
siku 3 zilizopita:
Girls’ Generation’s Taeyeon took No. 1 on global iTunes charts and more:
Taeyeon’s b-side “Blue” has also been a hit elsewhere in the world. It came in at No. 1 on the iTunes Top Songs chart in 11 regions: Saudi Arabia, United Arab Emirates, Singapore, Thailand, Cambodia, Malaysia, Philippines, Taiwan, Hong Kong, Macao, and Vietnam.

kama waarabu kanzu wapenda dini kwa maslahi yao tu wanapenda muziki wa korea kwa nini mimi mlala hoi nisiyemiliki hata kisima cha maji machafu nisiwapende wakorea.
korea forever mpaka nifanikiwe kumiliki apartment yangu maeneo ya BUSAN.

sidhani kama mwanadamu asiyevutiwa na rangi blue, ndio asili ya mawingu, bahari na ndio rangi inayo onyesha creativity pamoja na intelligency.
ndio rangi inayowakilisha loyalty,wisdom na hata uaminifu, ukiangalia rangi ya blue stress zote za umasikini zinakimbia lakini jaribu kuangalia rangi ya ...................................., unaweza kujikuta upo ICU kwa stress.
hata marehemu wote wanapenda rangi blue huko waliko kwa sababu wamechoshwa na giza.
wajinga wataitaja rangi kijani na manjano kwenye nafasi tupu nilioiwacha hapo juu​

kuna mtumishi mmoja kwa jinsi nilivyoshindwa kupata usingizi muda huu nina wasiwasi ananinyemelea achukue roho yake lakini nishamwambia kama ndio lengo lake basi silali, tutakesha pamoja kama mbuzi mzazi.


Tunatofautiana ktk hili. Mimi hii miziki ya Kikorea ambayo naipenda sana ni mpaka niusikie ktk drama as OST ndio niutafute na kuudownload kabisa.

Ila hivihivi sifuatilii kabisa miziki yao. Huwezi amini wale madogo waliotikisa Dunia ktk charts za Billboard sijui wimbo wao hata mmoja! Kila mara huwa nasema nitafuatilia ila nasahau, mwisho nimeona niache tu.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
my queen hata huku kwetu tunatembelewa na misimu minne kila mwaka lakini cha ajabu msimu wa jua kali ndio hutaka sifa kama za bwana yule mvaa suti za bendera.
laiti kama nisingelikuwa ni mfuasi wa buddha basi usiku huu ningelikwenda kwa mchumba wa zamani nikamshushia mapovu kama ya lee jun ki, bahati nzuri sana ndio hivyo mimi ni mwendo wa kukesha kwenye hekalu za dini pendwa.

aminas japokuwa muda huu unaota ndoto za panya anamshinda paka kwa ujanja, nikupe taarifa my queen taeyeon amerudi.

four seasons, nadhani huu wimbo unakuhusu japokuwa maisha yako ya mahusiano siyafahamu (nimegeuka mtabiri).
we missed each other we are sick of each other
you were my world but ill let you go.


ninavyowapenda waimbaji wakorea asilimia 95 wanaweza kuperform live bila ya mashabiki kuchoshwa na mikono juu kama tunamuomba mungu atushushie fedha na dhahabu huko aliko.
wenzetu halafu wanawajenga waimbaji wao kupitia show tofauti zinazoendeshwa na vyombo vya habari na chengine hawajisikii pindi wanapoalikwa kuperform labda wazongwe na ratiba.
unakuta vyombo vya habari vingi vinavyoendesha variety show za muziki wana kumbi na studio zao kubwa sana.
wakorea wametuacha mbali sana utafikiri wamepata uhuru miaka 300 iliopita.

Kwani Siku Izi Hulali!??
 
Hurrayyyyyyyyy
Hatimaye nimemaliza kuangalia King Gwanggaeto The Great. Nimechokaaaaa
emoji31.png
emoji31.png
emoji31.png

Ilikuwa safari ndefu ya episodes 92 ila ya kuvutia na kusikitisha.
Ni nzuri, nimeikubali.

Asante @Great Conqueror kwa pendekezo, lilikuwa pendekezo bora.
Bado naangalia na Yi San pia japo sijafika mbali sana, nipo episode ya 28 nataka niangalie mpya nichangamke kidogo.
Umeona Jinsi Territory ya Gogryeo ilivyokuwa Kubwa Chini ya Mfalme Gwanggaetto the Great, Ilikuwa inafika Korea Kusini,Korea Kaskazini(Chimbuko lake),China,Mongolia na Urusi. Ramani ya Sasa ya Korea ni ndogo sababu ya watu wapuuuzi toka Shilla waliungana na Tang dynasty ( China) wakaiangusha Gogryeo,Baekje na Gaya. Katika Suala la Kugawana Territory Nchi inayochukua eneo kubwa ni ile yenye jeshi Imara na iliyoombwa msaada hivyo Tang(China) wakachukua Eneo kubwa Shilla wakaachiwa hako karamani Baadae Shilla dynasty inaangushwa Ikaja Goryeo,Joseon,Korea Empire kisha North na South.

Humo kwenye hiyo King Gwanggaetto kuna wanatumia akili sana Ukimtoa the North Gost( Dam doek) kuna1 Murong Un na 2 Ha muji( the Military Advisor) yupi aliyekukosha kwa weledi wake?!, miye Ha Muji.

Nakumbuka tulianza wote Yi san miye nishaimaliza,Nikaja Jewel in the Palace tayari,nikaanza Joseon Gunman tayari, Emperor of the Sea tayari,Nikaenda kwa Princess Jammyung Go tayari na sasa niko likizo maana nilikuwa natazama episode 6-7 kwa siku nilikuwa nalewa, japo naenda mdogo mdogo Jang yeong Sil nafikiria Kuianza Sambong na the Great seer.
 
Vipi ktk hii Sambong na six flying dragons nianze na ipi? Nimewahi kuona ukisema kuna kama muendelezo fulani baina ya hizo drama mbili.
  1. jeong do jeon drama ni project ya mwaka 2014 kupitia shirika la KBS na six flying dragons ni project ya mwaka 2015 kupitia shirika la SBS na chakuvutia zaidi zote zimejengwa na takribani episode 50.
  2. zote zinazungumzia harakati za mwishoni za kuanguka tawala iliojaa rushwa ya goryeo na kuanzishwa joseon dynasty.
  3. six flying dragons kwa kiasi kikubwa imejaribu kuonyesha umuhimu wa lee bang won kwenye hizi harakati za kuiangusha goryeo akishirikiana na wanadamu wengine watano ambao ni lee seong gye, jung do jeon (sambong), lee bang ji, muhyul, na mwanadada boon yi.
  4. ukija kwenye jung do jeon ndio imeelezea kiuazi harakati za huyu jamaa kutoka kuwa mwanasiasa wa chini mpaka kuitikisa goryeo, ndani ya jung do jeon hutokuta uhusika wa lee bang ji, boon yi na muhyul, just ni wahusika wasiokuwa na rekodi yoyote muhimu kwenye harakati za kuiangusha goryeo kihistoria.
  5. kama ilivyokuwa kwa jing birok na admiral yi soon shin drama na hapa ndio hivyo hivyo ni marejeo ya matukio kwa kiasi kikubwa na kwa kuwa project ya jung do jeon ndio ya mwanzo kivyovyote itakuwa ni bora hata kibajeti.
  6. wengi wao wanaovutiwa na six flying dragons ni wale wapenzi wa mapigano lakini kwa wale wapenzi wa siasa za kibabe nakushauri itafute jung do jeon drama.
 
Umeona Jinsi Territory ya Gogryeo ilivyokuwa Kubwa Chini ya Mfalme Gwanggaetto the Great, Ilikuwa inafika Korea Kusini,Korea Kaskazini(Chimbuko lake),China,Mongolia na Urusi. Ramani ya Sasa ya Korea ni ndogo sababu ya watu wapuuuzi toka Shilla waliungana na Tang dynasty ( China) wakaiangusha Gogryeo,Baekje na Gaya. Katika Suala la Kugawana Territory Nchi inayochukua eneo kubwa ni ile yenye jeshi Imara na iliyoombwa msaada hivyo Tang(China) wakachukua Eneo kubwa Shilla wakaachiwa hako karamani Baadae Shilla dynasty inaangushwa Ikaja Goryeo,Joseon,Korea Empire kisha North na South.
kutoka mwaka 391 chini ya go damdeok hadi 668 chini ya bojang ilipoangushwa goguryeo ni miaka takribani 270 imepita, uhusiano wa shilla na Tang ulianza miaka 660 hivyo ukisema shilla ndio imechangia goguryeo/ korea kupoteza eneo kubwa sidhani kama ni sahihi kiupande fulani.
 
Umeona Jinsi Territory ya Gogryeo ilivyokuwa Kubwa Chini ya Mfalme Gwanggaetto the Great, Ilikuwa inafika Korea Kusini,Korea Kaskazini(Chimbuko lake),China,Mongolia na Urusi. Ramani ya Sasa ya Korea ni ndogo sababu ya watu wapuuuzi toka Shilla waliungana na Tang dynasty ( China) wakaiangusha Gogryeo,Baekje na Gaya. Katika Suala la Kugawana Territory Nchi inayochukua eneo kubwa ni ile yenye jeshi Imara na iliyoombwa msaada hivyo Tang(China) wakachukua Eneo kubwa Shilla wakaachiwa hako karamani Baadae Shilla dynasty inaangushwa Ikaja Goryeo,Joseon,Korea Empire kisha North na South.

Humo kwenye hiyo King Gwanggaetto kuna wanatumia akili sana Ukimtoa the North Gost( Dam doek) kuna1 Murong Un na 2 Ha muji( the Military Advisor) yupi aliyekukosha kwa weledi wake?!, miye Ha Muji.

Nakumbuka tulianza wote Yi san miye nishaimaliza,Nikaja Jewel in the Palace tayari,nikaanza Joseon Gunman tayari, Emperor of the Sea tayari,Nikaenda kwa Princess Jammyung Go tayari na sasa niko likizo maana nilikuwa natazama episode 6-7 kwa siku nilikuwa nalewa, japo naenda mdogo mdogo Jang yeong Sil nafikiria Kuianza Sambong na the Great seer.

Nimeiona Chief
Damdeok nimemkubali sana hasa kwa kupendelea kwake kusikiliza maoni ya washauri wake tofauti na wafalme wengine ambao wako kama ‘jiwe’ letu.

Hakuna shaka Ha Muji ndio alikuwa genius kuliko hao wengine wote sababu mipango yake asilimia kubwa ilifanikiwa. Director amefanya kazi nzuri sana kumteua mhusika wa Ha Muji, amevaa uhusika kwa namna iliyovutia sana.
Jana machozi yamenitoka alipouawa ktk episode 89, ilikuwa episode chungu sana kwangu.

Watu ambao niliumia kwa vifo vyao ktk series hii ni Sagal Hyeon na Ha Muji.

Vilevile nimevutiwa sana na swordsmanship ya Damdeok, vile anavyorusha sword na kuidaka katikati ya mapambano alinivutia.
Mtu niliyekubali mapigo yake humo ni Sagal Hyeon, jamaa alikuwa anapigana kitaalam sana. Alinikumbusha Gukseon Munno wa kwenye Queen Seondeok.

Yi San nachechemea nayo kama unavyoenda mdogomdogo na Jang Yeong Sil, na hizo zote ambazo umeziangalia ikiwemo hiyo Jang Yeong Sil nimeshaziona zote.
Utanipiga gape ukianza kuangalia Sambong na Great Seer pekee.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
kutoka mwaka 391 chini ya go damdeok hadi 668 chini ya bojang ilipoangushwa goguryeo ni miaka takribani 270 imepita, uhusiano wa shilla na Tang ulianza miaka 660 hivyo ukisema shilla ndio imechangia goguryeo/ korea kupoteza eneo kubwa sidhani kama ni sahihi kiupande fulani.

Kuna siku uliwahi kusema ktk King Gwanggaeto kuna mapungufu mengi ikiwemo kutokuoneshwa uhalisia wa maisha ya wananchi wake kwa nyakati zote alizokuwa vitani maana drama yote imetawaliwa na vita mwanzo mwisho...

Well, nafikiri walitumia eneo lile la bar pamoja na wale jamaa wafua vyuma (iron smiths) kama kuelezea hilo. Nadhani unakumbuka kuwa majadiliano mengi ya ‘kijiwe’ kile yalibase kwenye namna ambavyo maisha yanavyoendelea mitaani.

Ile drama ina matukio mengi sana, mengine Director amejaribu kuyaondoa ili kupunguza wingi wa episodes kama harusi n.k


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kuna siku uliwahi kusema ktk King Gwanggaeto kuna mapungufu mengi ikiwemo kutokuoneshwa uhalisia wa maisha ya wananchi wake kwa nyakati zote alizokuwa vitani maana drama yote imetawaliwa na vita mwanzo mwisho...

Well, nafikiri walitumia eneo lile la bar pamoja na wale jamaa wafua vyuma (iron smiths) kama kuelezea hilo. Nadhani unakumbuka kuwa majadiliano mengi ya ‘kijiwe’ kile yalibase kwenye namna ambavyo maisha yanavyoendelea mitaani.

Ile drama ina matukio mengi sana, mengine Director amejaribu kuyaondoa ili kupunguza wingi wa episodes kama harusi n.k


Sent from my iPhone using JamiiForums
yes niliwahi kusoma taarifa kupitia special thread ya soompi kwa mujibu wa KBS ilitakiwa kuwa na episode 100 lakini ikapunguzwa hadi 92.
 
Kuna siku uliwahi kusema ktk King Gwanggaeto kuna mapungufu mengi ikiwemo kutokuoneshwa uhalisia wa maisha ya wananchi wake kwa nyakati zote alizokuwa vitani maana drama yote imetawaliwa na vita mwanzo mwisho...

Well, nafikiri walitumia eneo lile la bar pamoja na wale jamaa wafua vyuma (iron smiths) kama kuelezea hilo. Nadhani unakumbuka kuwa majadiliano mengi ya ‘kijiwe’ kile yalibase kwenye namna ambavyo maisha yanavyoendelea mitaani.

Ile drama ina matukio mengi sana, mengine Director amejaribu kuyaondoa ili kupunguza wingi wa episodes kama harusi n.k


Sent from my iPhone using JamiiForums
maisha yote muathirika wa vita vya mara kwa mara ni fukara, na kwa mfumo wa korea ulivyokuwa ni walalahoi ndio walimaji wakuu huku ujira wao ni mdogo.

ardhi ya goguryeo kwa kiasi kikubwa ilikuwa ni ya milima na baridi kali hivyo basi kilimo nacho ilikuwa ni shida, kivyovyote licha ya goguryeo kujitanua sidhani kama wananchi walikuwa na maisha bora ya kujivunia.
 
Umeona Jinsi Territory ya Gogryeo ilivyokuwa Kubwa Chini ya Mfalme Gwanggaetto the Great, Ilikuwa inafika Korea Kusini,Korea Kaskazini(Chimbuko lake),China,Mongolia na Urusi. Ramani ya Sasa ya Korea ni ndogo sababu ya watu wapuuuzi toka Shilla waliungana na Tang dynasty ( China) wakaiangusha Gogryeo,Baekje na Gaya. Katika Suala la Kugawana Territory Nchi inayochukua eneo kubwa ni ile yenye jeshi Imara na iliyoombwa msaada hivyo Tang(China) wakachukua Eneo kubwa Shilla wakaachiwa hako karamani Baadae Shilla dynasty inaangushwa Ikaja Goryeo,Joseon,Korea Empire kisha North na South.
halafu mkuu si kila muda unatakiwa uonyeshe ubabe wako mbele ya jamii, jaribu kujishusha zaidi na zaidi kwa dhumuni la kufikia lengo lako na hiyo ndio silaha walioitumia shilla.

Kim Chun-Chu alikuwa ni zaidi ya mwanadiplomasia anayejua kutumia ulimi wake ipasavyo kwa dhumuni la kuyafikia malengo yake, alishaona kwa nguvu ya shilla hawakuwa na uwezo wa kusimama na goguryeo na hata Baekje hivyo solution ni bora tuwe mbwa wa Tang china kuliko kuvamiwa na ndugu zetu.

hatimaye alifanikiwa malengo yake kwa sababu baekje iliangushwa, ikafuata goguryeo baadae shilla na tang wakageukiana na hatimaye tang akachapwa kwa ushirikiano wa wanajeshi waliokuwa wa goguryeo, baekje na shilla.

shilla wakafanikiwa kuziunganisha kingdom 3 kwa mara ya kwanza kwenye historia, ndipo takribani miaka mingi kupita ikawa ni zamu ya goryeo kuziunganssha tena kingdom 3 baada ya shilla kuanguka pamoja na balhae kuchapwa na KHITAN.
 
maisha yote muathirika wa vita vya mara kwa mara ni fukara, na kwa mfumo wa korea ulivyokuwa ni walalahoi ndio walimaji wakuu huku ujira wao ni mdogo.

ardhi ya goguryeo kwa kiasi kikubwa ilikuwa ni ya milima na baridi kali hivyo basi kilimo nacho ilikuwa ni shida, kivyovyote licha ya goguryeo kujitanua sidhani kama wananchi walikuwa na maisha bora ya kujivunia.

Ni kweli kabisa, zaidi ya amani na imani iliyotokana na kuwa na mfalme ambaye ni mwamba wa vita ni wazi maisha yalikuwa ya taabu.

Hata wafanyabiashara wakubwa na wakulima wakubwa nadhani nao walionja makali ya vita maana lazima walikuwa wanatoa vipande na rations kulingana na namna wanavyozalisha.

Hapa nawaza tu ndio sisi tungekuwa ktk nchi ile ya Goryeo yenye milima na baridi kali + vita visivyoisha kwa aina ya viongozi wetu sijui ingekuwaje! Mungu Mkubwa


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nimengalia drama nyingi ila sio ktk mtiririko, na ili upate kulifahamu hili vyema basi uweze kuunganisha drama hizo ktk mtiririko...

Naomba unipe mtiririko mzuri/sahihi wa hizo drama ambazo zinaelezea/kuonesha mgawanyiko huo.
Hata ukielezea kwa maandishi pamoja na hizo drama itakuwa vizuri zaidi, asante.
drama zinazozungumzia taifa la joseon zipo nyingi sana dada yangu kwa makadirio zinafika 100, kwa kuwa hatujibii mtihani wa fasihi nyengine nyingi sijaziangalia.

  1. jung do jeon + six flying dragons :(kuanzishwa kwa joseon kuanzia mfalme taejo hadi taejong) the greet seer sikuifuatilia kwa sababu haipo kiuhalisia wa matukio. Ni sawa na kuangalia king gwaggaeto drama baadae ukafuatilia the legend drama japokuwa zote zimemzungumzia go damdeok.
  2. the great king sejong + tree with deep roots + jang yeong sil drama:(ukiiangalia sejong the great drama basi utakuwa umeshajirahisishia kila kitu, utayafahamu maisha yake taejong na utawala wake, maisha ya sejong, maisha ya jang young sil na ushirikiano wake mkubwa na sejong katika kuifanya joseon kuwa ni nchi ya sayansi, harakati za sejong kuanzisha herufi za korea(hangul) na mengine mengi sana) + (Jang yeong sil umesema umeshaiangalia, + tree with deep roots ndani yake kuna kikundi fulani kinaitwa milbon kama nipo sahihi ambao walitaka kulipiza kisasi cha mauaji ya sambong, pia imezungumzia harakati za sejong kuanzisha hangul letter) Cha kuvutia aliyeigiza uhusika wa mfalme sejong na taejo ndani ya sejong drama ndio hao hao waliyoigiza uhusika wa sejong na taejong ndani ya jang yeong sil drama.
  3. the princess man drama: romeo and juliett kutoka korea, love story kati ya mtoto wa mfalme na kijana ambaye baba yake alihukumiwa kwa usaliti
  4. queen for seven days drama : malikia aliyekaa madarakani kwa siku saba, sijui kama itakuvutia kwa sababu ni love story kwa kiwango kikubwa inayombatana na uchoyo wa madaraka, wivu kati ya ndugu wawili.
  5. ukiangalia jingbirok + admiral yi soon shin utakuwa ushamfahamu seonjo na vita ya imjin, zipo nyengine lakini ndio hivyo hatujibii mtihani wa fasihi
  6. heo jun drama: maisha ya daktari wa mfalme seonjo na familia yake nzima aliyeitwa heo jun, mtaalamu wa tiba aliyebobea nyakati hizo.
  7. the crowned clown, goddess of fire, the kings face, hong gil dong (maisha ya gwanghae ambayo pia utayapata kwenye no 5 na no 6) hii jung yi goddess of fire inazungumzia maisha ya mwandada fulani aliekuwa ni genius kwa utengenezaji wa vyombo vya kigae huku kwetu tunaita kaure, cha ajabu wenzetu wametengeneza miaka karne ya 16 ila sisi mpaka leo tunashindwa.
  8. dong yi, yi san, haechi, jang ok jung, jackpot (maisha ya mfalme sukjong, mfalme yi san, yeong jo), ongezea warrior baek dong soo, secret door
  9. joseon gun man, mr sunshine :nyakati za mwisho wa utawala wa joseon kabla ya kutawaliwa rasmi na japan.
  10. comrade, seoul 1945 : vita ya korea
 
The main objective of an audit is to enable the auditor to report on the truth and fairness of the financial position shown by the statement of financial position, of the profit or loss shown by the income statement, statement of cash flows, statement of changes in equity and of any other information required to be disclosed in the financial statements, in accordance with an identified financial reporting framework, legislation or relevant professional board.

kwa msaada wa mr google jamani:
nimemaliza kuziangalia episde 2 za drama inayoitwa the banker, haikuwa na rate kubwa lakini ni best drama kutokana na mtiririko wake.
veterani katika ubora wao
1553952715446.png
 
The main objective of an audit is to enable the auditor to report on the truth and fairness of the financial position shown by the statement of financial position, of the profit or loss shown by the income statement, statement of cash flows, statement of changes in equity and of any other information required to be disclosed in the financial statements, in accordance with an identified financial reporting framework, legislation or relevant professional board.

kwa msaada wa mr google jamani:
nimemaliza kuziangalia episde 2 za drama inayoitwa the banker, haikuwa na rate kubwa lakini ni best drama kutokana na mtiririko wake.
veterani katika ubora wao
View attachment 1058094

Jana nimejaribu kuangalia Waikiki 2 maana sio kwa sifa mnazoimwagia hapa lakini inanisumbua, Memories of Alhambra ndio kabisaaaaa inazingua kinoma.

Naendelea kujikongoja na Yi San, ngoja nijaribu na hii maana jana nimeiona pia KissAsian ila sikushawishika japo nilimuona mzee wangu.
Ngoja niicheki inibust kuangalia drama nyingine maana nakosa hamasa.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom