Kinyonyoke
JF-Expert Member
- Oct 4, 2016
- 3,495
- 13,132
Hii hadithi imetungwa na Deo ni hadithi nzuri sana aisee
BASI LA SHETANI-01
Deo Massawe.
0653195298.
Ulikua usiku wa kiza kinene, katika jiji la Dar es salam, kutokana na uchache wa magari barabarani basi yale machache yaliendeshwa kwa kasi.
“Tumuache hapa hapa”
“Jomba angalia hapa wanajeshi wakitunasa, tutatafuta samaki nchi kavu”
“Hakuna kukamatwa tutafanya kazi kwa sekunde”
“Haina tabu basi achia mafuta kidogo”
“Sikilizeni vijana, mnaona pale kwenye yale matuta, gari itapunguza mwendo na hapo mtamtupa kupitia mlango wa kushoto, hakikisheni umakini unazingatiwa”.
Yalikua mazungumzo ndani ya gari aina ya Toyota Land cruiser, gari hiyo ilikua inatembea kwa kasi ndani ikiwa imembeba mwanamke mmoja aliyefungwa mikono na miguu kisha kuzibwa mdomo kwa gundi, macho yake yalikua mekundu kwa kutoa machozi, alikua akisali na kutupatupa mikono huku na huko lakini hakuonewa huruma hata kidogo, mipango iliyokua ikifanyika ya kumtupa barabarani alikua akiisikia lakini hakuwa na namna ya kujiokoa.
Gari ilianza kupunguza mwendo, hapo mwanamke huyo alizidi kujitahid angalau kuongea ili awaambaie viajna waliotaka kumtupa bvasi wasimtupe kwa kishindo lakini hakuweza kutoa neno lolote.
Lilikua eneo hatari kwa kufanyia tukio lolote la kihalifu kwani kama ingetokea wanajeshi kukukuta katika eneo hilo maisha yako yangeweza kuwa hatarini ,
“Mwache hapo hapo karibu na geti” iikua sauti ya kiongozi wa kikundi hicho aliyeitwa Ribeto, na baada ya kutamka maneno hayo mwanamke huyo alitupwa mita chache kutoka lango kuu lakuingilia kambi kuu ya Lugalo, baada ya hapo gari iliongeza mwendo mara tano zaidi ya ilivyokua mwanzo.
Baada ya mwanamke huyo kutupwa alibingirika na kutumbukia katika bonde dogo lililokua pembeni ya barabara , licha mwili wake kufungwa kwa kamba ulitoa harufu kali ya muozo, harufu hiyo ili[elekea mbwa kusogelea eneo hilo na kuzama shimoni, alijitahidi kurusha mikono lakini bado mbwa walizidi kumzingira wakidhani ni mzoga wa kitu,
“Mungu naamini utanisaidia na nitatoka nikiwa hai, naomba tuma malaika mlinzi wako aje kuniokoa mahali hapa” mwanamke huyo alijisemea moyoni, huku akiendelea kuwakemea kwa vitendo mbwa waliotaka kumvamia ndani ya bonde dogo.
Mbwa wenye mafunzo maalumu, walihisi hali ya hewa kuwa tofauti na ilivyozoeleka, haraka walianza kubweka, huku wakizunguka ovyo. Wanajeshi waliokua zamu ya kulinda usiku walichukua tahadhari, kila mmoja alikaa katika nafasi yake huku baadhi ya mbwa kuachiwa na moja kwa moja walitoka haraka hadi katika lango kuu, walisogea kidogo na kuzama ndani ya shimo.
Mwanamke alizidiwa na hofu baada ya kusiki vishindo vya mbwa wakubwa wakija huku wakibweka kwa nguvu, mbwa koko mwaliokua pembeni walikimbia,
“Mungu naomba unisamehe dhambi zangu na unipokee katika ufalme wa mbinguni” mwanamke huyo alikata tama na kujikuta anatulia baaa ya mbwa mwenye ukubwa wa ndama kumdondokea kifuani, mbwa huyo alimnusanusa na ndipo mbwa huyo aliruka juu na haraka akarudi hadi alipo askari kiongozi na kumpa taarifa ya kuwa mtu aliyepo ndani ya shimo ana bomu la mkono.
Taarifa kutoka kwa mbwa huyo ilisababisha hali ya taharuki ndani ya kambi, hawakujua lengo la mtu huyo na hawakujua kama kuna wengine ambao wamewazunguka, haraka taarifa ilitumwa kwa mkuu wamajeshi kuhusu tukio hilo, huku mbwa mwingine akitumwa akiwa amefungwa kamera lengo likiwa kurudi na picha za mtu huyo na jinsi alivyojipanga.
Wanajeshi wote walipatwa na mshtuko, kuona ni mwaname aliyefungwa mikono na miguuu huku bomu likifungwa mkononii ili atakapofunguliwa bomu lilipuke.
Bila kuchelewa wanajeshi maalumu wenye uzoefu wa kutegua mabomu waliitwa na kuenda kumtoa mwanamke huyo hapo bondeni,
“Wewe ni nani ?”
“naitwa Winny naomba msinue”
“Umekujaje hapa?”
“Nimetupwa na watu ambao hata siwajui”
“Kwa nini umefungwa hivi kwani wewe ni mhalifu na kwa nini utupwe hapa”
“Japo sikumbuki vyote ila watu walionitupa hapa walikua na lengo la kuniua, hapa naomba mniokoe kuna bomu limetegwa hapa na pindi hii mikono yangu itakapoungulia bai litalipuka, naombeni niko chini ya miguu yenu niokoen”.
Yalikua majibizano baina ya mwanajeshi mkuu wa zamu ya kulinda usiku na mwanamke huyo aliyejitambulisha kwa jina Winny baada ya kufikishwa katika hospitali ya kijeshi ya Lugalo na kuondolewa gundi iliyomziba mdomo.
Winny alitetemeka kwa hofu, huku akizidi kuumia mkono kutokana na maumivu ya kamba iliyokua imekaza mikono yake, alianza kupewa matibabu ya haraka ikiwemo kuongezewa maji na chakula bomu likiwa mkononi na kitibiwa katika chumba cha pekee.
***
FIFTEEN YEARS AGO (miaka kumi na tano iliyopita)
Zilikua zimepita siku kumi na tano tangu Winny ahitimu elimu yake ya msingi akiwa na miaka kumi na nne, licha ya umri wake kuwa mdogo umbo lake liliwapagawisha wanaume, sura yake ilikua nyeupe ya kung’aa alikua mweupe na mwembamba wa wastani. Makazi yao yalikua mitaa ya Survey karibu na chuo cha Ardhi, ili kujiandaa na masomo ya kidato cha kwanza alilazimika kujiunga na masomo ya kabla (Pre-form one) baba yake mzee Mazengo alihakikisha mwanaye anapata elimu iliyo bora akawa anahudhuria masomo katika kituo kilichofunguliwa karibu na soko la Mwenge, hivyo hakuona sababu ya kupanda usafiri kutokana na ukaribu uliokuwepo kutoka nyumbani hadi shuleni.
“Hi baby girl your so beautiful (mambo binti wewe ni mzuri sana)”, ilikua sauti nzito iliyotokea ndani ya gari dogo aina ya Toyota Mark II, alikua mwanaume mweusi na mnene kiasi, baada ya sauti hiyo kumfikia Winny alilazimika kugeuka na kumuona aliyetamka maneno hayo, Winny alipogeuka alikutana nna tabasamu zitokutoka kwa mwanaume huyo na haraka mwanaume huyo alimuita wka mkono , Winny aligeuka na kurudi,
“Mambo mrembo”,
“Powa shkamoo baba”
“Nawewe shikamoo mama”
“Hahaha marahaba baba”
“Unafika wapi nikusogeze”
“Wala usijali mimi naenda shule nakaribia kufika asante”
“Naomba nitafute kwa mawasiliano haya”.
Maongezi kati ya Winny na mwanaume hayo yalikatishwa na taa za barabani kuwaka kija ni kuashiria kupita, lakini Winny alipokea kadi ya biashara (Busness Card) yenye nambari za simu.
Moyo wa Winny ulidunda kwa kasi kwani katika maisha yake yote hajawahi kukutana na mwanaume asiyemjua na atokee kumzoea hadi kuongea nae tena barabarani.
“Dr. Martin” ndilo jina lililokua katika kadi ya biashara ambayo lipokea Winny, aliificha mfukoni na kuongeza mwendo kwa lengo la kufika na kumuomba rafiki yake simu ili aweze kumpigia Dr Martin,
“Shoga leo nimepata na mimi wakwangu naona hapo nitapiga pesa kama wewe” lilikua neno la kwanza la Winny kabla ya salamu huku akipeana mkono na rafiki yake waliyekutana katika masomo ya Pre-Form one,
“Sasa ulikua unazubaa nini wewe mtoto wa kike Mungu akupe nini, hapo utapiga hela tena daktari huyu wa Muhimbili, hapa utapiga hela shosti wangu”, baada ya maongezi hayo waliingia darasani na masomo yakaanza.
Winny alikaa kiti cha nyuma mwisho, kichwa chake kikitawaliwa na mawazo juu ya mwanaume aliyeonekana kuwa na hela, alivuta picha ya maisha yatakavyokuwa pale atakapoanza kumiliki simu za kisasa pamoja na kutolewa out za mara kwa mara, maneno ya wazazi wake yalimtoka kabisa, hakujali utu wake zaidi aliwaza ni kwa jinsi gani ataweza kuwa sawa na wasichana wenzake aliowaona wakimiliki simu na vitu vya bei gali wka kutumi uzuri ambao hata yeye alikua nao.
***
Dr.Martin alikua akiishi na virusi vya ukimwi kwa mda mrefu, aliishi kwa kukomoa wanawake, hakutaka kufa peke yake, kwani wakati anatoa mawasiliano kwa Winny alikau akielekea Sinza katika hotel ya Lantana, akienda kukutana na mwaname mwingine aliyekua akimsubiria chumbani.
“Mpenzi umechelewa sana, au umepitia kwa mwanamke mwingine jamani”,
“No (hapana) mpenzi foleni kidogo imenibana”
“Twende zetu basi dear, nilikua nakusubiri kwa hamu”.
Maongezi kati ya Dr.Martin na mwanamke mwingine aitwaye Dorice, waliingia chumbani kwa ajili ya kuenda kula raha,
“Mpenzi tutumie kinga basi” sauti ya kubembeleza kutoka wka Dorice ilisikika,
“Dah jamani, kwani huniamini, au unaogopa mimba?” Dr.Martin alimuuliza taratibu
“Naogopa mimba kwa sababu sijajipanga kuzaa kwa sasa”, Dorice alijibu ingawa ukweli ni kwamba alikua akihofia kupata ukimwi ila ujasiri wa kumwambia mtu anayekupa hela kuwa naogopa ukimwi ukawa haupo,
“Ukiupata mimba mimi nitalea usijali, kwanza nakuoa kabisa” Dr. martin aliongea kwa sauti ya chini iliyopenya sikioni mwa Dorice. Dr.Martin hakuwa tayari kutumia kinga kwa mwanamke yeyote ili lengo lake litimie la kufa na wengi.
Huku wakiendelea kufanya mapenzi simu ya Martin iliita, na kwa kutumia mkono wa kushoto aliikamata na kupokea,
“Halo, mimi umenipa Busness Card asubuhi, nimetumia simu ya rafiki yangu maana mimi sina simu”
“Ahaa sasa kama huna simu basi subiri hapo hapo kwa rafiki yako namtumia hela ukanunue simu alafu unitafute na namba zako”
“Sawa asante sana”.
Yalikua maneno machache lakini yalimfanya Winny aamini kweli amepata mwanaume wa ukweli,
“Haaa! shosti unapewa simu hata hujatumika, usimuache huyo atakua amekupenda kweli”
“Ila shosti nikipata mimba baba ataniua”
“Wee thubutu kwani kondomu zimeisha dukani, yaani ukienda kwa mwanaume hakikisha unakua nan kondomu zako maana hawa wanaume some time hawana maana, waanweza kukumbia hana kondomu sasa kumkomesha unatoa zako”,
“Kweli shogaa hapo umenena”, maongezi yao yalikatika baada ya ujumbe wa fedha kuingia katika simu, haraka walikimbia duka la simu hapo hapo mwenge na kununua simu ndogo. Baada ya dakika tano Dr.Martin alipiga simu na kuongea na Winny,
“Winny tumia tu hiyo, tukionana nakupa simu kubwa, tuwasiliana hata kwa WhatsApp”,
“Waoooo, asante basi ngoja nisajili laini nitakutafuta”.
Je nini kitatokea .? tukutane sehemu ijayo.
BASI LA SHETANI-01
Deo Massawe.
0653195298.
Ulikua usiku wa kiza kinene, katika jiji la Dar es salam, kutokana na uchache wa magari barabarani basi yale machache yaliendeshwa kwa kasi.
“Tumuache hapa hapa”
“Jomba angalia hapa wanajeshi wakitunasa, tutatafuta samaki nchi kavu”
“Hakuna kukamatwa tutafanya kazi kwa sekunde”
“Haina tabu basi achia mafuta kidogo”
“Sikilizeni vijana, mnaona pale kwenye yale matuta, gari itapunguza mwendo na hapo mtamtupa kupitia mlango wa kushoto, hakikisheni umakini unazingatiwa”.
Yalikua mazungumzo ndani ya gari aina ya Toyota Land cruiser, gari hiyo ilikua inatembea kwa kasi ndani ikiwa imembeba mwanamke mmoja aliyefungwa mikono na miguu kisha kuzibwa mdomo kwa gundi, macho yake yalikua mekundu kwa kutoa machozi, alikua akisali na kutupatupa mikono huku na huko lakini hakuonewa huruma hata kidogo, mipango iliyokua ikifanyika ya kumtupa barabarani alikua akiisikia lakini hakuwa na namna ya kujiokoa.
Gari ilianza kupunguza mwendo, hapo mwanamke huyo alizidi kujitahid angalau kuongea ili awaambaie viajna waliotaka kumtupa bvasi wasimtupe kwa kishindo lakini hakuweza kutoa neno lolote.
Lilikua eneo hatari kwa kufanyia tukio lolote la kihalifu kwani kama ingetokea wanajeshi kukukuta katika eneo hilo maisha yako yangeweza kuwa hatarini ,
“Mwache hapo hapo karibu na geti” iikua sauti ya kiongozi wa kikundi hicho aliyeitwa Ribeto, na baada ya kutamka maneno hayo mwanamke huyo alitupwa mita chache kutoka lango kuu lakuingilia kambi kuu ya Lugalo, baada ya hapo gari iliongeza mwendo mara tano zaidi ya ilivyokua mwanzo.
Baada ya mwanamke huyo kutupwa alibingirika na kutumbukia katika bonde dogo lililokua pembeni ya barabara , licha mwili wake kufungwa kwa kamba ulitoa harufu kali ya muozo, harufu hiyo ili[elekea mbwa kusogelea eneo hilo na kuzama shimoni, alijitahidi kurusha mikono lakini bado mbwa walizidi kumzingira wakidhani ni mzoga wa kitu,
“Mungu naamini utanisaidia na nitatoka nikiwa hai, naomba tuma malaika mlinzi wako aje kuniokoa mahali hapa” mwanamke huyo alijisemea moyoni, huku akiendelea kuwakemea kwa vitendo mbwa waliotaka kumvamia ndani ya bonde dogo.
Mbwa wenye mafunzo maalumu, walihisi hali ya hewa kuwa tofauti na ilivyozoeleka, haraka walianza kubweka, huku wakizunguka ovyo. Wanajeshi waliokua zamu ya kulinda usiku walichukua tahadhari, kila mmoja alikaa katika nafasi yake huku baadhi ya mbwa kuachiwa na moja kwa moja walitoka haraka hadi katika lango kuu, walisogea kidogo na kuzama ndani ya shimo.
Mwanamke alizidiwa na hofu baada ya kusiki vishindo vya mbwa wakubwa wakija huku wakibweka kwa nguvu, mbwa koko mwaliokua pembeni walikimbia,
“Mungu naomba unisamehe dhambi zangu na unipokee katika ufalme wa mbinguni” mwanamke huyo alikata tama na kujikuta anatulia baaa ya mbwa mwenye ukubwa wa ndama kumdondokea kifuani, mbwa huyo alimnusanusa na ndipo mbwa huyo aliruka juu na haraka akarudi hadi alipo askari kiongozi na kumpa taarifa ya kuwa mtu aliyepo ndani ya shimo ana bomu la mkono.
Taarifa kutoka kwa mbwa huyo ilisababisha hali ya taharuki ndani ya kambi, hawakujua lengo la mtu huyo na hawakujua kama kuna wengine ambao wamewazunguka, haraka taarifa ilitumwa kwa mkuu wamajeshi kuhusu tukio hilo, huku mbwa mwingine akitumwa akiwa amefungwa kamera lengo likiwa kurudi na picha za mtu huyo na jinsi alivyojipanga.
Wanajeshi wote walipatwa na mshtuko, kuona ni mwaname aliyefungwa mikono na miguuu huku bomu likifungwa mkononii ili atakapofunguliwa bomu lilipuke.
Bila kuchelewa wanajeshi maalumu wenye uzoefu wa kutegua mabomu waliitwa na kuenda kumtoa mwanamke huyo hapo bondeni,
“Wewe ni nani ?”
“naitwa Winny naomba msinue”
“Umekujaje hapa?”
“Nimetupwa na watu ambao hata siwajui”
“Kwa nini umefungwa hivi kwani wewe ni mhalifu na kwa nini utupwe hapa”
“Japo sikumbuki vyote ila watu walionitupa hapa walikua na lengo la kuniua, hapa naomba mniokoe kuna bomu limetegwa hapa na pindi hii mikono yangu itakapoungulia bai litalipuka, naombeni niko chini ya miguu yenu niokoen”.
Yalikua majibizano baina ya mwanajeshi mkuu wa zamu ya kulinda usiku na mwanamke huyo aliyejitambulisha kwa jina Winny baada ya kufikishwa katika hospitali ya kijeshi ya Lugalo na kuondolewa gundi iliyomziba mdomo.
Winny alitetemeka kwa hofu, huku akizidi kuumia mkono kutokana na maumivu ya kamba iliyokua imekaza mikono yake, alianza kupewa matibabu ya haraka ikiwemo kuongezewa maji na chakula bomu likiwa mkononi na kitibiwa katika chumba cha pekee.
***
FIFTEEN YEARS AGO (miaka kumi na tano iliyopita)
Zilikua zimepita siku kumi na tano tangu Winny ahitimu elimu yake ya msingi akiwa na miaka kumi na nne, licha ya umri wake kuwa mdogo umbo lake liliwapagawisha wanaume, sura yake ilikua nyeupe ya kung’aa alikua mweupe na mwembamba wa wastani. Makazi yao yalikua mitaa ya Survey karibu na chuo cha Ardhi, ili kujiandaa na masomo ya kidato cha kwanza alilazimika kujiunga na masomo ya kabla (Pre-form one) baba yake mzee Mazengo alihakikisha mwanaye anapata elimu iliyo bora akawa anahudhuria masomo katika kituo kilichofunguliwa karibu na soko la Mwenge, hivyo hakuona sababu ya kupanda usafiri kutokana na ukaribu uliokuwepo kutoka nyumbani hadi shuleni.
“Hi baby girl your so beautiful (mambo binti wewe ni mzuri sana)”, ilikua sauti nzito iliyotokea ndani ya gari dogo aina ya Toyota Mark II, alikua mwanaume mweusi na mnene kiasi, baada ya sauti hiyo kumfikia Winny alilazimika kugeuka na kumuona aliyetamka maneno hayo, Winny alipogeuka alikutana nna tabasamu zitokutoka kwa mwanaume huyo na haraka mwanaume huyo alimuita wka mkono , Winny aligeuka na kurudi,
“Mambo mrembo”,
“Powa shkamoo baba”
“Nawewe shikamoo mama”
“Hahaha marahaba baba”
“Unafika wapi nikusogeze”
“Wala usijali mimi naenda shule nakaribia kufika asante”
“Naomba nitafute kwa mawasiliano haya”.
Maongezi kati ya Winny na mwanaume hayo yalikatishwa na taa za barabani kuwaka kija ni kuashiria kupita, lakini Winny alipokea kadi ya biashara (Busness Card) yenye nambari za simu.
Moyo wa Winny ulidunda kwa kasi kwani katika maisha yake yote hajawahi kukutana na mwanaume asiyemjua na atokee kumzoea hadi kuongea nae tena barabarani.
“Dr. Martin” ndilo jina lililokua katika kadi ya biashara ambayo lipokea Winny, aliificha mfukoni na kuongeza mwendo kwa lengo la kufika na kumuomba rafiki yake simu ili aweze kumpigia Dr Martin,
“Shoga leo nimepata na mimi wakwangu naona hapo nitapiga pesa kama wewe” lilikua neno la kwanza la Winny kabla ya salamu huku akipeana mkono na rafiki yake waliyekutana katika masomo ya Pre-Form one,
“Sasa ulikua unazubaa nini wewe mtoto wa kike Mungu akupe nini, hapo utapiga hela tena daktari huyu wa Muhimbili, hapa utapiga hela shosti wangu”, baada ya maongezi hayo waliingia darasani na masomo yakaanza.
Winny alikaa kiti cha nyuma mwisho, kichwa chake kikitawaliwa na mawazo juu ya mwanaume aliyeonekana kuwa na hela, alivuta picha ya maisha yatakavyokuwa pale atakapoanza kumiliki simu za kisasa pamoja na kutolewa out za mara kwa mara, maneno ya wazazi wake yalimtoka kabisa, hakujali utu wake zaidi aliwaza ni kwa jinsi gani ataweza kuwa sawa na wasichana wenzake aliowaona wakimiliki simu na vitu vya bei gali wka kutumi uzuri ambao hata yeye alikua nao.
***
Dr.Martin alikua akiishi na virusi vya ukimwi kwa mda mrefu, aliishi kwa kukomoa wanawake, hakutaka kufa peke yake, kwani wakati anatoa mawasiliano kwa Winny alikau akielekea Sinza katika hotel ya Lantana, akienda kukutana na mwaname mwingine aliyekua akimsubiria chumbani.
“Mpenzi umechelewa sana, au umepitia kwa mwanamke mwingine jamani”,
“No (hapana) mpenzi foleni kidogo imenibana”
“Twende zetu basi dear, nilikua nakusubiri kwa hamu”.
Maongezi kati ya Dr.Martin na mwanamke mwingine aitwaye Dorice, waliingia chumbani kwa ajili ya kuenda kula raha,
“Mpenzi tutumie kinga basi” sauti ya kubembeleza kutoka wka Dorice ilisikika,
“Dah jamani, kwani huniamini, au unaogopa mimba?” Dr.Martin alimuuliza taratibu
“Naogopa mimba kwa sababu sijajipanga kuzaa kwa sasa”, Dorice alijibu ingawa ukweli ni kwamba alikua akihofia kupata ukimwi ila ujasiri wa kumwambia mtu anayekupa hela kuwa naogopa ukimwi ukawa haupo,
“Ukiupata mimba mimi nitalea usijali, kwanza nakuoa kabisa” Dr. martin aliongea kwa sauti ya chini iliyopenya sikioni mwa Dorice. Dr.Martin hakuwa tayari kutumia kinga kwa mwanamke yeyote ili lengo lake litimie la kufa na wengi.
Huku wakiendelea kufanya mapenzi simu ya Martin iliita, na kwa kutumia mkono wa kushoto aliikamata na kupokea,
“Halo, mimi umenipa Busness Card asubuhi, nimetumia simu ya rafiki yangu maana mimi sina simu”
“Ahaa sasa kama huna simu basi subiri hapo hapo kwa rafiki yako namtumia hela ukanunue simu alafu unitafute na namba zako”
“Sawa asante sana”.
Yalikua maneno machache lakini yalimfanya Winny aamini kweli amepata mwanaume wa ukweli,
“Haaa! shosti unapewa simu hata hujatumika, usimuache huyo atakua amekupenda kweli”
“Ila shosti nikipata mimba baba ataniua”
“Wee thubutu kwani kondomu zimeisha dukani, yaani ukienda kwa mwanaume hakikisha unakua nan kondomu zako maana hawa wanaume some time hawana maana, waanweza kukumbia hana kondomu sasa kumkomesha unatoa zako”,
“Kweli shogaa hapo umenena”, maongezi yao yalikatika baada ya ujumbe wa fedha kuingia katika simu, haraka walikimbia duka la simu hapo hapo mwenge na kununua simu ndogo. Baada ya dakika tano Dr.Martin alipiga simu na kuongea na Winny,
“Winny tumia tu hiyo, tukionana nakupa simu kubwa, tuwasiliana hata kwa WhatsApp”,
“Waoooo, asante basi ngoja nisajili laini nitakutafuta”.
Je nini kitatokea .? tukutane sehemu ijayo.