Francis12
JF-Expert Member
- Sep 30, 2016
- 7,533
- 22,276
Kwa wanamabadiliko wote,
Najua mmeumia sana lakini nawashauri mpunguze munkari. Najua hasira zenu, majuto yenu, na maumivu yenu maana mmekuwa disappointed na mtu mliyejitolea kumpigania kwa nguvu zenu zote. Mlijitoa kufa na kupona mwaka 2015, na kusacrifice mambo mengi kwa ajili yake. Lakini msipaniki. Time is our best teacher. Letz wait muda utasema.
Kupaniki kwetu ndio furaha ya CCM, ndio ajenda yao, ndio plan yao. Kuzodoana kwetu, kushukiana, kuraruana huku mitandaoni ndio azma yao. If you can't convince them, confuse them. Ndicho CCM wanachofaya. Lengo lao ni kuona sisi tunabaki na taharuki kila uchao, tukose concentration kwenye mambo ya msingi. Ushindi wao ni kuona tunahukumiana kwa kunyosheana vidole. Tusiwape ii hiyo nafasi.
Mzee Lowassa kasema ameongea mengi na JPM lakini ametaja moja tu la kumpongeza. Hatujui hayo mengine ni yapi. Ni wazi kauli yake haijaridhisha wengi (mimi nikiwemo) but letz give him benefit of doubts. Tusianze kushikana mashati. Lowassa kumpongeza JPM akufanyi maisha kuwa rahisi huku mtaani, hakufanyi bank ziache kufilisika, hakufanyi ajira zipatikane, hakufanyi madawa yawepo hospitalini. So tusitoke kwenye mstari.
Nachojua ni kwamba upinzani ni harakati za kupigania social and economic welfare ya mwananchi. Kutoa mawazo mbadala ya kusaidia serikali kuona pale iliposhindwa kuona. Upinzani ni spirit. Na spirit hiyo haifi, haifutiki, haiharibiki, haipotei. Ni safari ambayo ipo na itakuwepo hadi mwisho wa nyakati. Hata Lowassa aondoke leo, au Chadema ife leo, siasa za mageuzi hazitakwisha. It will never happen for any society to live without opposing and competing ideologies! Never ever.!
Kwahiyo let us relax na tuendelee kupigania nchi yetu kwa maslahi ya vizazi vyetu. Lowassa awepo au asiwepo isituzuie kupigania yale tunayoamini ni sahihi. Kabla hajaja opposition tulikuwepo na tulipigana sana. So hata akiamua kurudi huko alikokuwa ni sawa tu. Kuvunjika kwa koleo hakuwezi kuwa mwisho wa uhunzi.!
Malisa GJ
Najua mmeumia sana lakini nawashauri mpunguze munkari. Najua hasira zenu, majuto yenu, na maumivu yenu maana mmekuwa disappointed na mtu mliyejitolea kumpigania kwa nguvu zenu zote. Mlijitoa kufa na kupona mwaka 2015, na kusacrifice mambo mengi kwa ajili yake. Lakini msipaniki. Time is our best teacher. Letz wait muda utasema.
Kupaniki kwetu ndio furaha ya CCM, ndio ajenda yao, ndio plan yao. Kuzodoana kwetu, kushukiana, kuraruana huku mitandaoni ndio azma yao. If you can't convince them, confuse them. Ndicho CCM wanachofaya. Lengo lao ni kuona sisi tunabaki na taharuki kila uchao, tukose concentration kwenye mambo ya msingi. Ushindi wao ni kuona tunahukumiana kwa kunyosheana vidole. Tusiwape ii hiyo nafasi.
Mzee Lowassa kasema ameongea mengi na JPM lakini ametaja moja tu la kumpongeza. Hatujui hayo mengine ni yapi. Ni wazi kauli yake haijaridhisha wengi (mimi nikiwemo) but letz give him benefit of doubts. Tusianze kushikana mashati. Lowassa kumpongeza JPM akufanyi maisha kuwa rahisi huku mtaani, hakufanyi bank ziache kufilisika, hakufanyi ajira zipatikane, hakufanyi madawa yawepo hospitalini. So tusitoke kwenye mstari.
Nachojua ni kwamba upinzani ni harakati za kupigania social and economic welfare ya mwananchi. Kutoa mawazo mbadala ya kusaidia serikali kuona pale iliposhindwa kuona. Upinzani ni spirit. Na spirit hiyo haifi, haifutiki, haiharibiki, haipotei. Ni safari ambayo ipo na itakuwepo hadi mwisho wa nyakati. Hata Lowassa aondoke leo, au Chadema ife leo, siasa za mageuzi hazitakwisha. It will never happen for any society to live without opposing and competing ideologies! Never ever.!
Kwahiyo let us relax na tuendelee kupigania nchi yetu kwa maslahi ya vizazi vyetu. Lowassa awepo au asiwepo isituzuie kupigania yale tunayoamini ni sahihi. Kabla hajaja opposition tulikuwepo na tulipigana sana. So hata akiamua kurudi huko alikokuwa ni sawa tu. Kuvunjika kwa koleo hakuwezi kuwa mwisho wa uhunzi.!
Malisa GJ