kwa wanaCDM tu! chadema dodoma wapata ofisi mpya-tuwasaidie!

kweleakwelea

JF-Expert Member
Nov 29, 2010
3,065
1,535
Wandugu wapendwa!

kwa kiasi fulani kile kilio cha ofisi ya chama cha demokrasia na maendeleo kuwa na ofisi ya mkoa yenye kufikika kwa urahisi (strategic location) na watu wengi (busy street) na yenye uwalau kidogo kwa maana ya space imepatikana. Hii ina maana kuwa ile ofisi iliyokuwa inatumika awali na chadema mkoa (sokoni majengo imepakana na market view barguest house & canna lodge annex) itabakia kuwa ya chadema wilaya dodoma. Point ya kwanza hapa ni kuwa ongezeko la ofisi katika eneo hili inaimarisha pumzi ya chama.

Kazi ya utafutaji wa ofisi imekuwa si rahisi sana kwani ni wenye nyumba wachache wanaokubali kuwa ofisi zao zikodishwe na vyama vya siasa na hasa vya upinzani. tunawapongeza katibu wa mkoa Bw. Faustine Masawe 0659 086673 (mwenye light green shirt) na katibu wa vijana mkoa bwana Iddi Kizota (mwenye dark clothes) 0787 303015 au 0715 303015 kwa jitihada zao za dhati kukijenga chama kwenye mkoa ambao umekuwa mgumu kama huu na hivyo hadi leo hii chadema dodoma inajivunia.

ofisi hii iko barabara ya tisa ( 9 ) nyumba ya tatu kutoka barabara ya lami. inatazamana kabisa na uwanja wa barafu pahala ambapo tipa huwa zinapaki na mikutano ya hadhara huwa inafanyika. ni katika barabara hii ndipo inapopatikana kidia vision hotel.... inaonekana kwa mbaali katika picha iliyo attached. kwa ufupi ni mahala panapofikika kirahisi sana.

kwa muda huu ambapo chadema dodoma inaendelea kutafuta ofisi kubwa zaidi yenye hadhi ya mji wa dodoma ambao huwakutanisha wabunge woote na mara nyingine viongozi wote wa chama hiki kutoka kila pembe ya nchi yetu, chama mkoani dodoma kina jukumu la kuikarabati na kuiwekea samani ofisi hii ili ifanane na makusudio yake na kuweza kutekeleza majukumu yake. ofisi hii hapo awali ilikuwa ni salon ya kunyoa nywele.

kwa sasa hivi changamoto ni kama zifuatazo

1. kama inavyoonekana kuna haja ya kumwaga kifusi mbele ya jengo.

2. kupata samani zinazoendana na chama kwa ajili ya ofisi.. at least kiti ya mwenyekiti, meza mbili za ofisi, viti kadhaa vya wajumbe,

3. hapo nje limetolewa wazo kuwa pazungushiwe mbao ili kuwa na baraza kwa ajili ya kusubiria au wageni wengine. eneo hilo linatakiwa kuwa na tea table na viti kadhaa / bench kwa ajili ya wageni wengine wa chama.

mwenye maoni au support please contact katibu wa mkoa Bw. Faustine Masawe 0659 086673 na 0766 297418 au katibu wa vijana mkoa bwana Iddi Kizota 0787 303015 au 0715 303015. makamanda hawa wamekaa katika kochi wakitafakari mkakati wa kuifanya ofisi iwe kwenye chati....(however, kochi hilo ni mali ya mmiliki aliyepita wa ofisi)

kwa yeyote aliye tayari kuchangia samani na marekebisho ofisi ya mkoa dodoma kwa kutumia mpesa tafadhali tumia

0766 297418 Bwana Faustine Massawe, katibu wa mkoa. kuhakikisha hili tafadhali cheki na Bw. Komu, mkurugenzi wa fedha wa chama, 0713 615603 Dar es salaam.

karibuni tujenge chama! changamoto hii imekuwa ikitolewa sana hapa JF. Mh. Regia upo?

welcome ALL!
 

Attachments

  • IMAG0387.jpg
    IMAG0387.jpg
    216.4 KB · Views: 93
  • IMAG0386.jpg
    IMAG0386.jpg
    229.5 KB · Views: 113
  • IMAG0406.jpg
    IMAG0406.jpg
    195.6 KB · Views: 126
  • IMAG0407.jpg
    IMAG0407.jpg
    192.2 KB · Views: 97
  • IMAG0402.jpg
    IMAG0402.jpg
    130.1 KB · Views: 111
pepo mbili itawauma sana! hamna ujanja! ndio maana siku moja kijiweni mtu mmoja alichangia maoni kuwa wale woote walio chini ya darasa la saba ndio hawaelewi Chadema wakitembea nje ya bunge.woote waliosoma wanaona wako sahihi. huyu pepo mbili pepo moja ni la ujinga. lingine la umasikini.
 
Weka akaunti namba au namba ya Mpesa iliyohalalishwa na chama makao makuu tuchangie mahela hapo kuifanya ofisi iendane na hadhi ya mkoa. Ukombozi haupatikani kwa kutumia hela ya mafisadi bali kwa hiki kidogo tulichonacho kuchangia chama.
 
kimilidzo...point taken.. nitawaona wakuu wa mkoa kwa ajili ya namba ya mpesa
 
Tuchangie topic jamani tusitolewe kwenye reli na hawa mapepo!Inashangaza tumeshamjua lakini ana2win kwa kututoa kwenye mijadala.Binafsi napongeza juhudi za cdm mkoa dodoma.Hili jimbo la dom mjini cdm tujipange tulichukue uchaguzi ujao hivyo nawapa changamoto uongozi wa cdm mkoa kuanza kuandaa mgombea mwenye ushawishi mkubwa mbele ya wanadodoma ambaye atamgalagaza huyu malole ambaye najua atataka tena!
 
Tuchangie topic jamani tusitolewe kwenye reli na hawa mapepo!Inashangaza tumeshamjua lakini ana2win kwa kututoa kwenye mijadala.Binafsi napongeza juhudi za cdm mkoa dodoma.Hili jimbo la dom mjini cdm tujipange tulichukue uchaguzi ujao hivyo nawapa changamoto uongozi wa cdm mkoa kuanza kuandaa mgombea mwenye ushawishi mkubwa mbele ya wanadodoma ambaye atamgalagaza huyu malole ambaye najua atataka tena!

aise we una akili mno
 
Thanks, kwa yeyote aliye tayari kuchangia samani na marekebisho ofisi ya mkoa dodoma kwa kutumia mpesa tafadhali tumia

0766 297418 Bwana Faustine Massawe, katibu wa mkoa. kuhakikisha hili tafadhali cheki na Bw. Komu, mkurugenzi wa fedha wa chama, 0713 615603 Dar es salaam.

Malole the current mp must go!

binafsi ninaahidi laki moja. nitaiwakilisha baada ya wiki moja!

karibuni na wengine tuchangie.
 
hongera cdm dodoma kwa kuwa na ofisi ya mkoa, nami nawaomba viongozi wa cdm Iringa nao wafungue ofisi ya mkoa badala ya kutegemea ofisi ya manispaa, naamini hili litawezekana sooon kwa uwepo wa wabunge Msigwa na Chiku Abwao
 
Thanks, kwa yeyote aliye tayari kuchangia samani na marekebisho ofisi ya mkoa dodoma kwa kutumia mpesa tafadhali tumia

0766 297418 Bwana Faustine Massawe, katibu wa mkoa. kuhakikisha hili tafadhali cheki na Bw. Komu, mkurugenzi wa fedha wa chama, 0713 615603 Dar es salaam.

Malole the current mp must go!

binafsi ninaahidi laki moja. nitaiwakilisha baada ya wiki moja!

karibuni na wengine tuchangie.

A note of thanks and will I do the same in the end of the month (Laki moja kwa office hiyo ya Dodoma na niliaidi some amount for Jamii Forum (20,000) ila hizi sijui naziwakilishaje?)
 
Nitakuja kutembelea ofisi hizo......................................
 
akhsanteni Mutakyamirwa na wenzako kwa ahadi hizi. chama kitajengwa na sisi wenyewe ambao tumesema INATOSHA! tujenge tanzania ambayo tunataka kuwaachia watoto wetu, sio hii Tanzania inayoongozwa na waganga wa kienyeji! tuseme HAPANA IMETOSHA!! tukijenge chama chetu CHADEMA!! ndio jukwaa letu lililobaki! tukishindwa sasa hadi hapo 2015 amini usiamini HAITAWEZEKANA TEEEEENNNNNNNAAAAAAAAA!!!

karibuni ofisini, au pigeni namba za simu hizo!! mchango waweza kuwa hata wa ushauri sio tu mali...utathaminiwa sana........hatuna namna....namna ni hii moja tu!karibuni sana hata kutembelea.....

tusiogope kujionyesha mbele za wenzetu, juu ya tunachokiamini na kukipigania...hatuna namna...wandugu THERE IS NO FUTURE KWA MWENDO HUU WA UTAWALA ULIOKO SASA!!! hatukuwahi kusikia habari za udini....hatukuwahi kusikia malimbikizo ya mali tena nje ya nchi kwa kiasi hiki..eti wana vizima vya mafuta yemen, eti ni wawekezaji wakubwa huko komoro....eti wanaleta al shabaab wauwe makamanda wetu katika vita dhidi ya ufisadi!!! tukiwashtaki kwa umma wanadai eti kuangusha serekali ni mwiko na kwamba siku zote mtawala halali atapatikana kupitia sanduku la kura...wanasema hivyo kwa sababu wanajua kuwa TUME NI ZA KWAO, NA UWEZO WA KUIBA KURA WANAO..... NA HAWAKO TAYARI KUBADILISHA KATIBA ILI TANZANIA AJIPATIE VIONGOZI BORA!!!ni lazima tuseme HAPANA!!

na tena haisaidii sana kukaa kwenye kompyuta na lap top kutiliana hasira... ni mwanzo mzuri kuhamasishana... lakini ni lazima pia sasa tuwafuate wananchi huko waliko tuwaelezee waelewe......ni lazima tuwe na jukwaa.....tumelipata na kamwe tusiliache liyeyuke na matumaini yetu!!

kama unauchukia UDINI....kama unauchukia UFISADI....kama kweli wewe ni mwanatanzania, mtoto wa Tanzania, shime tuungane tuirejeshe treni kwenye reli mara moja tuu mara hii tena......TUIJENGE CHADEMA.....

hata kama wewe ni mwanaCCM... lakini unavichukia hivyo vilivyoainishwa hapo juu..basi iadabishe CCM, isaidie chadema. kama anavyofanya Sitta, Sumaye na wanaCCM wengine wenye akili.....iadabishe CCM mara moja tuu mara hii tuu...ili kitapojipanga kurudi mara nyingine pale 2020 kirudi kikiwa na akili timamu!!

naomba kuwakilisha!
 
Wandugu wapendwa!

kwa kiasi fulani kile kilio cha ofisi ya chama cha demokrasia na maendeleo kuwa na ofisi ya mkoa yenye kufikika kwa urahisi (strategic location) na watu wengi (busy street) na yenye uwalau kidogo kwa maana ya space imepatikana. Hii ina maana kuwa ile ofisi iliyokuwa inatumika awali na chadema mkoa (sokoni majengo imepakana na market view barguest house & canna lodge annex) itabakia kuwa ya chadema wilaya dodoma. Point ya kwanza hapa ni kuwa ongezeko la ofisi katika eneo hili inaimarisha pumzi ya chama.

Kazi ya utafutaji wa ofisi imekuwa si rahisi sana kwani ni wenye nyumba wachache wanaokubali kuwa ofisi zao zikodishwe na vyama vya siasa na hasa vya upinzani. tunawapongeza katibu wa mkoa Bw. Faustine Masawe 065 908673 na katibu wa vijana mkoa bwana Iddi Kizota 0787 303015 au 0715 303015 kwa jitihada zao za dhati kukijenga chama kwenye mkoa ambao umekuwa mgumu kama huu na hivyo hadi leo hii chadema dodoma inajivunia.

ofisi hii iko barabara ya tisa ( 9 ) nyumba ya tatu kutoka barabara ya lami. inatazamana kabisa na uwanja wa barafu pahala ambapo tipa huwa zinapaki na mikutano ya hadhara huwa inafanyika. ni katika barabara hii ndipo inapopatikana kidia vision hotel.... inaonekana kwa mbaali katika picha iliyo attached. kwa ufupi ni mahala panapofikika kirahisi sana.

kwa muda huu ambapo chadema dodoma inaendelea kutafuta ofisi kubwa zaidi yenye hadhi ya mji wa dodoma ambao huwakutanisha wabunge woote na mara nyingine viongozi wote wa chama hiki kutoka kila pembe ya nchi yetu, chama mkoani dodoma kina jukumu la kuikarabati na kuiwekea samani ofisi hii ili ifanane na makusudio yake na kuweza kutekeleza majukumu yake. ofisi hii hapo awali ilikuwa ni salon ya kunyoa nywele.

kwa sasa hivi changamoto ni kama zifuatazo

1. kama inavyoonekana kuna haja ya kumwaga kifusi mbele ya jengo.

2. kupata samani zinazoendana na chama kwa ajili ya ofisi.. at least kiti ya mwenyekiti, meza mbili za ofisi, viti kadhaa vya wajumbe,

3. hapo nje limetolewa wazo kuwa pazungushiwe mbao ili kuwa na baraza kwa ajili ya kusubiria au wageni wengine. eneo hilo linatakiwa kuwa na tea table na viti kadhaa / bench kwa ajili ya wageni wengine wa chama.

mwenye maoni au support please contact katibu wa mkoa Bw. Faustine Masawe 065 908673 au katibu wa vijana mkoa bwana Iddi Kizota 0787 303015 au 0715 303015. makamanda hawa wamekaa katika kochi wakitafakari mkakati wa kuifanya ofisi iwe kwenye chati....(however, kochi hilo ni mali ya mmiliki aliyepita wa ofisi)

karibuni tujenge chama! changamoto hii imekuwa ikitolewa sana hapa JF. Mh. Regia upo?


welcome ALL!

No ya simu hapo Mr.Massawe haijakamilika naomba ukiweza uweke kisahii. nimemtumia ujumbe bwana Kizota wa kumpongeza baada ya sekunde 30 akanipigia kushukuru pia. Kilichonifurahisha ni uwajibikaji wake wa haraka sana pale aliponipigia.
 
No ya simu hapo Mr.Massawe haijakamilika naomba ukiweza uweke kisahii. nimemtumia ujumbe bwana Kizota wa kumpongeza baada ya sekunde 30 akanipigia kushukuru pia. Kilichonifurahisha ni uwajibikaji wake wa haraka sana pale aliponipigia.

Sorry kaka! kweli. namba ya bwana massawe ni 0659 086673 hii ni tigo! pia 0766 297418 kwa ajili ya michango au ushauri pia mawazo....

narudia pia katibu wa mkoa vijana Bw. Iddi Kizota Iddi Kizota 0787 303015 au 0715 303015

pongezi zako ni za ukweli na si za utani... hawa makamanda wanafanya kazi inavyopasika na ni kutoka damuni.... wanatutia moyo sana na ni mfano wa kuigwa. kama sio hawa hadi sasa hivi chadema ilikuwa haipo dodoma...kumbuka ni ngome kongwe wa ccm.... walitoka nayo zama za kweuzi ambapio kwa kiasi kikubwa dodoma ilikuwa imejaa wanasiasa wa ccm na wafanyakazi wa serekali ambao wengi ni waoga kujiionyesha japo sheria ya utumishi inawaruhusu kuwa wanachama...

pamoja nao tunatumia sayansi ya hali ya juu kukijenga chama mkoani hapa...tunakiri mafanikia ni makubwa sana pia of recent!

asante kwa kucall...hutia moyo sana wenzetu walio mstari wa mbele hasa wanapojua wana watu nyuma yao.....

chadema vema!
 
Hongera sana viongozi wa CDM-Dom, niwavumilivu sana! Hongera pia bwana Idd kizota kwani jitihada zako binafsi nazijua. Keep it up! CDM NI VEMA!
 
Nitajitolea mali yangu kwa ajili ya CHADEMA, hapa UDOM tunaendelea kuhamasishana. Mimi ninaleta laki moja mara nitakapo rudi dodoma kutoka safari
 
Back
Top Bottom