Kwa wana wakike na wakiume tu

Dr Louis

JF-Expert Member
Nov 12, 2017
442
421
Baada ya kufanya utafiti na kuridhika nao. Sasa tumeamua kuutoa mbele ya Watanzania! Kama hujui hesabu hasa Probability sasa iko hivi, probability ni uwezekano wa kitu fulani kutokea sasa leo tunaenda kuzungumzia uwezekano wa mtu kuolewa au kuoa hasahasa nchini Tanzania.

*WANAWAKE*

1. Ukiwa una tabia nzuri ila shape na sura haujafinikiwa uwezekano wa kuolewa ni asilimia 30%.

2. Ukiwa una tabia nzuri shape nzuri ila sura haukufanikiwa uwezekano wa kuolewa ni asilimia 75%.

3.Ukiwa na sura nzuri shape nzuri na tabia nzuri uwezekano wa kuolewa ni asilimia 80% kama hauna mtoto. Na kama una mtoto ila haukai naye ni asilimia 56%.

4. Kama umezaa mtoto na uko unaishi naye yaani hana pa kwenda basi uwezekano wa wewe kuolewa na mtu ambaye sie baba wa mtoto ni 15% .

5. Ikijulikana wewe ni kicheche mtaani kwenu haujatulia basi uwezekano wa kuolewa ni asilimia 3% tu, ila uwezekano wa kupewa mimba zile zisizofahamika na kupata watoto wasio na Baba ni asilimia 97%.

6. Ikijulikana wewe ni bikra mbele ya watu na wakajua wakawa na uhakika basi uwezekano wa kuolewa ni asilimia 67.5%, na hizi zaweza kuongezeka kufikia hata 89% ikiwa una shape ya uhakika.

Kwa wanawake ikumbukwe kila ngazi ya elimu unayoongeza kwenye maisha yako inapunguza uwezekano wa kuolewa kwa kiasi fulani:

7. Kama una degree moja uwezekano wa kuolewa ni asilimia 62%.

8. Kama una masters basi uwezekano wa kuolewa ni asilimia 41%.

9. Kama una PHD basi uwezekano wa kuolewa ni asilimia 24%.

10. Kama umekuwa Profesa basi dada yangu uwezekano wa wewe kuolewa ni asilimia 2% hadi 8%.

11. Kama una matege na ndo changamoto yako basi dada ukivaa sketi siku zote uwezekano wa kuolewa unakuwa asilimia 70%. Lakini kama unavaa suruali kuonyesha matege yako miguu inazunguka zunguka kama feni basi uwezekano wa kuolewa ni asilimia 3%. Na hawa wanaume watakaokuoa ni wale vipofu!

12. Kama umezalishwa watoto kama watatu na hujaolewa basi wewe uwezekano wa kuolewa ni asilimia 0.05%.

13. Kama unashinda online kazi kupost picha insta, whatsapp, facebook, panyabuku na countabuku basi uwezekano wa wewe kuolewa ni asilimia 1%.Yaani kila mwanamume anahisi wewe ni mali ya umma.

14. Kama wewe ni kibonge sana basi uwezekano wa kuolewa ni asilimia 35%. Punguza kula dada yangu. Ukishaolewa kula nenepa mpaka upasuke.

15. Kama wewe ni mwembamba sana basi uwezekano wa kuolewa ni asilimia 35%. Nenepa kidogo bana.!

16. Kama unatumia simu ya TECNO uwezekano wa kuolewa ni asilimia 68%.

17. Kama unatumia iPhone basi uwezekano wa kuolewa ni asilimia 8%.

18. Kama una marafiki wengi wa kiume kuliko wa kike. Basi uwezekano wa kuolewa ni asilimia 28%. Utasema hao ni marafiki ila kumbuka wanaume hawaaminianagi. Wewe pia utaonekana ni mali ya umma hata kama sio!

19. Kama unanuka mdomo. Dagaa sijui wa juzi ulikula basi uwezekano wa kuolewa na wewe ni asilimia 20%. Hamna mwanamume ambaye yuko radhi atapike siku akiambiwa *"You can now kiss the bride!"*

Naona mpaka hapo mtakuwa mmeelewa maana ya probability na mnaweza kucalculate za kwenu. Haya tuamie kwa upande wa pili

*WANAUME*
1. Kama hauna hela, narudia tena yaani kama *hauna hela* kwa wakati huu na ule ujao tunaouelekea, uwezekano wa kuoa wewe ni asilimia 0.00000000001%.
2. Kama una hela basi uwezekano wa wewe kuoa, tena kuoa mwanamke umtakaye wewe mwenyewe kwa wakati huu na ujao ni asilimia 100000%.

*Simple sana kwa mwanaume*

*MWISHO*
 
Safi sana ila kuna kimoja ukiwa unanuka uchi na unasifa zoote hizo kuolewa ni asilimia 0000000.0
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom