Masanilo
Platinum Member
- Oct 2, 2007
- 22,286
- 4,493
Nina lazimika kuweka bayana nia yangu ya kukomboa jimbo uchaguzi mkuu ujao. Nina amini raisi bora atatoka chama cha upinzani. Ni muda mrefu CCM wamekuwa madarakani lakini maendeleo ya nchi yazidi kushuka. Ufisadi usio na kina unazidi kushamiri, rushwa na kupotea kwa utaifa vinazidi kushika kasi. Mikakati yangu ni kuimarisha CHADEMA kwa ngazi ya Kaya kwa kaya. Jimbo langu lina kata 17, Sekondari za Kata 4, seminary secondary school 1, shule 2 za serikali za sekondari. Hizi shule nitazitembelea na kuwapa misaada ya hali na mali ikiwa ni pamoja kujitolea kufundisha ili nifahamike zaidi kwa wanafunzi ambao ndiyo wapiga kura 2015 hasa elimu ya uraia.
Nitaanzisha mashina ya chama kwenye kata zote 17, nitawezesha wapatikane watendaji kwenye kila kata na kufungua ofisi pamoja na kununulia baiskeli viongozi wote 17. Nitatoa ujira walau kila mwezi wa Shs 10,000 kwa kila kiongozi. Ni hela ndogo ila uwezo wangu si mkubwa na mimi si fisadi. Kila mwaka kutakuwa na mashindano ya kugombea Ng'ombe na jezi kwa vijana football na Netball. Mashindano ya mbio riadha na baiskeli. Ninaandaa manifeso ya uchaguzi ujao nikilenga matatizo ya wananchi wangu na sulihisho zake, sitoweka hapa JF maana najua itanakiliwa na CCM na kurudifiwa.
Ninampango wa kuwasiliana na Makao Makuu ili kadi na viongozi wa juu wa chama waanze kampeni mapema kuandaa wananchi wangu kulinda kura zitoshe 2015.
Pipozi powa! Peoples Power ! Tanzania is for Changes
Rev Masa K
Nitaanzisha mashina ya chama kwenye kata zote 17, nitawezesha wapatikane watendaji kwenye kila kata na kufungua ofisi pamoja na kununulia baiskeli viongozi wote 17. Nitatoa ujira walau kila mwezi wa Shs 10,000 kwa kila kiongozi. Ni hela ndogo ila uwezo wangu si mkubwa na mimi si fisadi. Kila mwaka kutakuwa na mashindano ya kugombea Ng'ombe na jezi kwa vijana football na Netball. Mashindano ya mbio riadha na baiskeli. Ninaandaa manifeso ya uchaguzi ujao nikilenga matatizo ya wananchi wangu na sulihisho zake, sitoweka hapa JF maana najua itanakiliwa na CCM na kurudifiwa.
Ninampango wa kuwasiliana na Makao Makuu ili kadi na viongozi wa juu wa chama waanze kampeni mapema kuandaa wananchi wangu kulinda kura zitoshe 2015.
Pipozi powa! Peoples Power ! Tanzania is for Changes
Rev Masa K