Kwa waliokosa mkopo

hizo private ni zip kwan wengne tulisoma private ila ada ilikua laki 1 tuu tunavyoanza na tumepata au mmasemea za sasa hz?!!
 
Uliemnukuu aidha wivu unamsumbua au anawaza anavyoweza. Anadhani fedha ziko kama kitu kisichobadilika ukikiacha leo kesho utakikuta vilevile. fedha hunyumbuka (elastic) kwa kuongezeka na kupungua.
Mtu kwa mfano kasomesha mwanae kwa hela za BMK au kwa kukopa wakati afya na umri unamruhusu - kesho karudi alikotoka (back to square one) na mtoto au watoto ndo hao wanaingia chuo kikuu - ataomba mkopo in anticipation watoto wenyewe watakujaurejesha.

Hiyo sio sababu - waangalie kipato cha sasa cha mzazi na sio historia ya kipato cha mzazi.

kipato cha sasa cha mzazi wako watakipataje??....hawawezi kumjua kila mtu....na watu hudanganya sana kwenye zile fomu...ndio maana wanaegemea kwenye facts kwasababu huwez kudanganya shule ulizosoma.....
 
Sitaki kusikia upuuzi wa kuzungumzia suala la elimu ya juu ifikapo 2015 wakati wa kampeni kisa mnatuomba ajira. W,a.p.uzi wakubwa, watu tumekosa mkopo siku ya siku mnakurupuka eti fyofyofyofyo......................... Sitaki kusikia. Kama mnaweza fanyeni leo wakati wa shida zetu siyo mtuletee upuuzi, wa.p.mba.vu na wa: pu.uz wakubwa

duh pole sana mkuu, alaf umepanic sana mkuu kwa serikali yetu ya sasa hata useme vp hawakuelewi wakisha hakikisha kwamba watoto wao tayar wamepata nafas nje ya nchi na hata wale wanaosomea nchini wamepata mkopo wala hawajali, one week before tahliso walilisema hli lakn ndo hata hawana mpango wao, lakn ucjali mkuu mwisho wa serikali ya kizandiki unakaribia
 
Yaan am an orphan sina baba wala mama nimeomba mkopo hii mara ya pili nimenyimwa sijui vigezo vyakupata mkopo ni nin ,seariously am hurting...am staying with my aunt anasomesha watu wa nne wote vyuo vikuu...hii ni fair kwel nime wapa 60000....na12000,yakutumia hii sikutuibia....kama vipi wawe wana list watu wao wanaotakiwa kuomba nakupewa mkopo

Pole sana.
 
Mi nilisoma mwaka mzima bila loan. Ila mwaka wa pili niliomba nikapata. Ila nchi hii n ya kiboya sana asee. Watoto wa maskin ndo wakunyanyasika daily
 
Wkati mwingine najiuliza maswali ambayo nadhani majibu yake yananiweka njia panda
KUKOSA MIKOPO MPAKA KWA PRIORITY FACULTY .
SWALI NI JE INAWEZEKANA EMS HAWAKUFIKISHA MAOMBI NA KAMA WAMEFIKISHA NI JE ILIKUA NJE YA MUDA.?
 
Habarini za leo... kwanza tujipe hongera kwa sisi tulio pata mkopo na tuwape pole kwa walio kosa mkopo coz mm naamini kuna kupata na kukosa na yote ni matokeo..

Naamini kuwa kila alie kosa mkopo atasema kuwa yeye ni mtoto wa mkulima au yeye ni mtoto ww ma`ntilie coz hakuna ambaye ata thubutu kusema kuwa hata kama kakosa mkopo ni ana uwezo wa kulipa ada....

Tuelewe kitu kimoja kwamba sisi binadamu hatujaumbwa na ule moyo wa kuridhika lakini tuna laumu sana na kulaani bila kujua kile tunacho laani.....kwa kipindi hiki naamini kutakuwa na malalamiko mengi sana juu ya mkopo...laana nyingi kwa serikali iliyopo madarakani na hata kwa bodi ya mikopo pamoja na kejeli nyingi hasa hz znatoka kwa wale ambao wamekosa mkopo kwa sababu mbali mbali

Lakin kwa wale wote ambao wana lalamika kuhusu mkopo wasi sahau kuwa kuna wengine wana ipongeza serikali na bodi ya mikopo kwa kusikia kilo chao na kuona serikali ipo fair...so hapo tujiulize malalamiko,kejeli na laana zetu zitafanya kazii? Au sifa na pongezi zetu zinafanya kazi?

Tusi sahau haya tunafanyayo leo hasa malalamiko kwa walio kosa mkopo kwamba haya yapo tangu bodi ilipo anzishwa na yataendelea kuwepo.hadi hapo...and mm naamini hakuna siku ambayo bodi tutaisifia kuwa iko fair hata kama bodi itakuja kumpa KILA MMOJA WETU KIASI FULANI CHA PESA wapo watakao sema wamepewa kidogo...

Kwa mm nijuavyo malalamiko yetu tuyafanyayo sahizi hayawezi KAMWE KUTUPATIA MKOPO wala kutuongezea asilimia za mkopo......tukubali kwamba wakati tuna tuma maombi hakuna alie ambiwa kuwa ukituma tuu maombi ndo umeshapata mkopo....Rahasha ni wazi kila mmoja alijua kuwa suala la kupata mkopo ni probability kama tulielewa hivyo na kuamini hvyo kwa nn tutoe malalamiko ambayo kwa sasa hayatasaidia chochote kozi hayo yapo na yata kuwepo.....

Pia tukubali kuwa bodi itatoa mkopo kwa kozi zenye priority kwa sababu hii inatokana na uhitaji wa nchi na njia gani rahisi ya kuadai pesa zao ndo maana wana weka priority na non priority.....coz kuna kozi nyingne tukubali kupata ajira si kitu rahisiii je chukua

MFANO ume lalamika sana kuhusu mkopo na kozi yako ambayo ni non priority bodi ikakupa mkopo ukasoma ukamaliza kazi hujapata ukasota kazi kwa mda wa miaka 3 ukamuaa kujiajili ukapata pesa nyingi tuu SWALI je utakumbuka kuchukua millioni 15 ambazo bodi ilikukopesha kwenda kulipa deni lako ili huo mkopo wadogo zako.waje faidi na kuto lalamika kama ww utaweza kwenda kujipeleka ww kulipa deni? Nahisi hio ni ngumu kama kwa kibaka kuomba lifti kwenye gari la defenders...

Nacho hitaji hapa mm tujadili kwa walio kosa mkopo nn kifanyike ili twende chuo wote na masomo yaendelee na rujaribu kuendelea kila mwaka kuomba mkopo huenda tutakuja pata na sio kulalamika eti mm mtoto wa mkulima nimekosa sa ulitaka nani akoseeeeee jamani...unakaa na kuchagua kozi ambayao unanua kabisa hii haina mkopo unasubiri uthibitishiwe kuwa mkopo umekosa uje hapa kulalamika ....

Hta wale wa education bodi ilisema kabisa kuwa itatoa kwa wale watu wa education lakink wa masomo mawili na sio kila education

Sasa mwisho nn kifanyike kwa walio kosa mkopo tuache kulalamika?

Nakaribisha mawazo
 
Woi.....hii bodi ya mikopo ishakuwa ya wasanii
Mtu ka apply education amefiwa na mzazi mmoja
Kasoma government school

Then kanyimwa mkopo
 
kipato cha sasa cha mzazi wako watakipataje??....hawawezi kumjua kila mtu....na watu hudanganya sana kwenye zile fomu...ndio maana wanaegemea kwenye facts kwasababu huwez kudanganya shule ulizosoma.....

wachache wanaweza danganya sikatai - lakini fomu walizoanza nazo miaka 2 au 3 iliyopita zilikua zinaainisha kipato cha wazazi cha sasa na ili kuondoa kama sio kupunguza udanganyifu fomu ilibidi zipitishwe kwa serikali ya mtaa na kuendelea hadi kulishwa kiapo mahakamani. tukubali kuwa kuweka msingi kwa kipato cha zamani cha mzazi pia sio haki au tuseme sio fair
 
Back
Top Bottom