Kwa wale wenye tatizo la kusikia tupeane ushauri mbinu za matibabu na changamoto tunazokabiliana nazo

Aug 21, 2019
17
17
Ndugu zangu natanguliza salamu kwenu ni matumaini yangu mko salama na mnaendelea na majukumu yenu. Kwa wale wenye changamoto za kiafya Mungu awapiganie mrudi katika hali zenu za hawali sijajua bado kama mada hii iko jukwaa husika au la.

Kama mada inavyosema huu uzi ni kwa ajili ya watu walio na tatizo la kusikia pamoja na wote wenye ndugu marafiki na majirani wenye tatizo hili tukutane hapa tupeane matibabu kwa wale waliopona hili tatizo, changamoto tunazokumbana nazo pamoja na mbinu au njia mbalimbali za kuweza kukalibiana nazo.

Nianzie kwangu, mimi ni kijana niliyebahatika kuzaliwa bila changamoto yoyote ya kiafya. Tangu mdogo nilikuwa nasikia vizuri kabisa mpaka namaliza kidato cha nne nilikuwa nasikia vizuri tu. Kipindi cha kusubiri matokeo ndio hali ilianza kubadilika na mimi sikutambua nilikuwa najua naskia vizuri tu lakini kuna rafiki yangu ndio aliyegundua na kuniuliza characteristics umekuwaje masikio siku hizi?

Kwanza nilikuwa najisikia vizuri tu baada ya siku kupita ndipo hali ilianza kubadilika kabisa; kelele masikioni zilianza. Nilikosa amani kabisa, nilikosa raha mara moja nikaanza matibabu. Nilienda Hindu Mandal hospital na Aghakhan lakini sikupata nafuu. Niliishia kupewa dozi nyingi ambazo ukimaliza unafata tena mpaka dawa zikaanza kujirudia tena yani ile ulizopewa miezi miwili iliyopita ndizo unazopewa tena mwezi huu.

Mzazi akasema twende Muhimbili lakini kabla hatujaenda Muhimbili mzazi wangu akahamishwa kituo cha kazi na kupelekwa Mwanza hivyo tukahamia Mwanza huku tukiacha makazi yetu Dar. Matibabu yakaanza Bugando nikapimwa uwezo wa kusikia (nitaweka hapa matokeo yake), dozi nimekunywa zisizo na idadi inafika kipindi mpaka mzani unakuonea huruma.

Nikaambiwa ninunue mashine yaani hearing aid tukanunua mashine hizo laki saba kinachosikitisha ni kwamba haikusaidia chochote bali zinazidisha kelele. Kuna mtu alitwambia huwa zinatofautiana ubora tununue zingine bora zaidi. Katika harakati kabla hatujanunua zingine tukapata taarifa shirika moja linagawa hizo mashine bure. Nikaenda tarehe tajwa pale Nyanza primary nikapewa hizo mashine, nazo hazikufanya chochote. Tukumbuke hapo nilisitisha kwenda form five kwa mwaka huo ili nifuatilie matibabu muda ulizidi kwenda bila matokeo yoyote kuonekana. Mwaka jana ilibidi niende tu kusoma.

Changamoto ni kubwa sana ndugu zangu lakini nashukuru Mungu nimeingia form six bila tabu yoyote na nimeanza kuzoea hali hii japo changamoto zake ni nyingi. Namisi sana kupiga story, kucheka na kujichanganya lakini Mungu ni mwema naamini ipo siku atasema neno moja tu juu yetu nasi tutapata kupona. Nilisikitika sana niliposoma uzi wa Mpauko katika harakati za kugoogle ndipo nilipoona uzi wake na kuamua kujiunga JamiiForums.

Katika harakati za kutafuta matibabu niliingia pia mtandaoni nikagundua hii hali kitaaram inaitwa tinnitus na ni watu wengi sana wanasumbuliwa na hii hali kuna mahali nilisoma wanasema wa Americans million hamsini wanasumbuliwa na hii hali.

maajabu ni kwamba watu wanapona kwa njia tofauti tofauti wengine wanapona baada ya kuanza kulala na kupata usingizi kwa masaa manane wengine baada ya kufanya mazoezi ya yoga na wengine wamepona baada ya kunya maji mengi kwa siku na kuna forum kabisa inaitwa ya watu wenye tatizo hili Web result with site links.

Tinnitus Talk
Watu wametoa shuhuda mbalimbali.

Karibuni sana.

Screenshot_2019-09-09-14-47-58.png
 
Mimi nina changamoto ya sikio moja la kulia. Nligundua mwenyewe nikiwa kidato cha 2. Lakini ninahisi ni tatizo nililozaliwa nalo ama nililolipata utotoni. Nimezunguka hospitali zote kubwa bila mafanikio. Dawa unazopewa ni Vitamin B complex tu. Niliamua kujisomea vitabu vya udaktari na internet. Niligundua kuwa tatizo ni mishipa ya fahamu yaani nirves. Shida ni kwamba hii kitu hairekebishiki.

Kutokana na maelezo yako chanzo cha tatizo lako ni ugonjwa unaoitwa tinnitus. Na hii inasabishwa na kujiweka ktk mazingira ya sauti kubwa. Mfano. Kuvaa earphones ni hatari na janga kubwa ambalo vijana wengi hawajui. Zoea tu hiyo hali hakuna dawa. Kuna doctor bingwa aliniambia nizoee tu na hii hali.

Kwa hiyo mimi nikiwa ktk maongezi nafanya timing nakaa upande ambao sikio zima linafanya kazi.
Tumuombe Mungu atatuponya!
 
thales, afadhali wewe mkuu sikio moja ni zima kabisa pole sana ila Mimi naamini matibabu yapo changamoto nahisi ni gharama kwa upande wangu sijawahi kutumia air phone kabisa naamini pia siku moja nitarudi kwenye hali yangu ya zamani
 
Mimi nina changamoto ya sikio moja la kulia. Nligundua mwenyewe nikiwa kidato cha 2. Lakini ninahisi ni tatizo nililozaliwa nalo ama nililolipata utotoni. Nimezunguka hospitali zote kubwa bila mafanikio. Dawa unazopewa ni Vitamin B complex tu. Niliamua kujisomea vitabu vya udaktari na internet. Niligundua kuwa tatizo ni mishipa ya fahamu yaani nirves. Shida ni kwamba hii kitu hairekebishiki.
Kutokana na maelezo yako chanzo cha tatizo lako ni ugonjwa unaoitwa tinnitus. Na hii inasabishwa na kujiweka ktk mazingira ya sauti kubwa. Mfano. Kuvaa earphones ni hatari na janga kubwa ambalo vijana wengi hawajui.
Zoea tu hiyo hali hakuna dawa. Kuna doctor bingwa aliniambia nizoee tu na hii hali.
Kwa hiyo mimi nikiwa ktk maongezi nafanya timing nakaa upande ambao sikio zima linafanya kazi.
Tumuombe Mungu atatuponya!
Tatizo lako copyright na langu.
Hata ninavokaa kwenye gari safari ndefu nakaa upande wa sikio zima kumwelekea jirani LA sivo atanisemesha njia nzima nitaishia ku smile tu.
Langu lilianza ghafla, wewe ilikuaje?
 
thales, Same here mimi ilinianza baada ya kuchoma sindano za quinine kutibu maralia kipindi niko shule ya msingi yakawa yanaziba yanazibuka mpaka naingia sec wazazi wangu sio watu wa kujali nilivyofika form2 ndio wakanipeleka muhimbili nikapimwa usikivu ikaonekana sikio la kulia halisikii kabisa na la kushoto linasikia ila limeanza kuaffectiwa kama anavyosema mkuu hapa nilipewa Bcomplex tu nikaambiwa Mungu akijaalia litazibuka lenyewe niache kukaa kwenye makelele, nisile kisamvu wala mihogo.

nikaendelea tu na shule aisee mkuu asikwambie mtu nimesoma kwa shida nmeishi kwa shida sana unapitia manyanyaso/wakati wmingine unakua kama kichekesho, hio hali imenibadilisha mentality yangu kabisa hadi leo mimi sipendi kukaa na watu nakaa na mtu ambae hajagundua kama nina ilo tatizo akishajua tu anaanza kunitreat tofauti na mm huwa sipendi kabisa kama ni urafiki utaisha na hata kama nilikua nasikilizana nae basi nitakua ndio simuelewi kabisa kwakifupi tatizo liko zaidi kwenye mishipa ya fahamu kadri unavyokata tamaa ndivyo unazidi kuwa husikii.

Nikikaa kwenye maspika makubwa nakua kama nataka kupoteza fahamu wakati meingine navaa earphone isiyokuwa na mziki ili tu kujiepusha kupeana Hi na watu mana inakua kero saa ingine .wakati mwingi sio kwamba sisikii unakuta nasikia ila sielewi mtu anaweza niambia kitu nikamsikia ila sijamuelewa inabidi aongee herufi kwa herufi.

Yotekwa yote nmeshaizoea hali yangu,pia hali ya kuwa sichangamani sana na watu nishaizoea hali ya kupenda kuwa kwenye mazingira ya utulivu sana huwa sipendi kukaa mahala kuna sauti nyingi zinanidisturb ila ili ujue Mungu analipa kuna watu wawili walikuaga wananinyanyasa zamani mmoja shule mwingine om wameumwa sasa wao sio half_deaf ni hawasikii kabisa.mpaka kuizoea hii hali ilinigarimu miaka 6
 
Tatizo lako copyright na langu.
Hata ninavokaa kwenye gari safari ndefu nakaa upande wa sikio zima kumwelekea jirani LA sivo atanisemesha njia nzima nitaishia ku smile tu.
Langu lilianza ghafla, wewe ilikuaje?
Pole sana kiongozi yangu pia yalianza gafla tu nashindwa kuekewa tatizo ni nini nakubaliana na hali tu nikikumbuka siku zangu za nyuma ama kweli hujafa hujaumbika Mimi huwa nacheza na mdomo ukikwepesha tu mdomo umeshanipoteza yote kwa yote Mungu ni mwwma kwa watu wake
 
Leyt Castle,
Pole sana mkuu natambua maumivi unayopitia hali hii imenifanya kuwa na marafiki wachache rafiki mkubwa ni simu yangu sipendi mazungumzo marefu.

Iyo njia ya kuvaa air phone nimeitumia sana mpaka leo nikiwa safari huwa natumia sometimes huwa tunachukuliwa kama innocent people unaweza fanya kosa ukatetewa na watu wote ningekuwa sina uhakika na kazi mimi nisingesoma ningeenda kijijini nikajikita kwenye kilimo.

lugha za arama pasipo kuongea huwa sizipendi na huwa sizijibu mpaka MTU aongee nashukuru Mungu maisha yanaendelea macho yanatumika kama masikio
 
Tatizo kubwa ni unyanyapaa linauma sana
Pole sana mkuu natambua maumivi unayopitia hali hii imenifanya kuwa na marafiki wachache rafiki mkubwa ni simu yangu sipendi mazungumzo marefu
Iyo njia ya kuvaa air phone nimeitumia sana mpaka leo nikiwa safari huwa natumia sometimes huwa tunachukuliwa kama innocent people unaweza fanya kosa ukatetewa na watu wote ningekuwa sina uhakika na kazi mimi nisingesoma ningeenda kijijini nikajikita kwenye kilimo
lugha za arama pasipo kuongea huwa sizipendi na huwa sizijibu mpaka MTU aongee nashukuru Mungu maisha yanaendelea macho yanatumika kama masikio
 
Back
Top Bottom