Kwa wale ambao wakiingia kwenye swimming pool wanatembea

Bornagan

Member
Oct 7, 2018
94
95
Huwa najisikia vibaya sana ninapoenda hoteli yenye swimming pool naishia kutembea kwenye maji na kucheki wengine wakiogelea.

Natamani kujifunza kuogelea maana naweza zama siku yoyote kwenye pantoni nikashinda kujitetea maana pia napandaga panton karibu kila wiki mara mbili na kuogelea sijui.

Hebu tupeane uzoefu ni wapi naweza jifunza ogelea kwa Dar.
 
Hili ni jukwaa la mapenzi sasa uliposema kutembea nikadhani ile 'kutembea' ya mtaani....... 'anatembea na mke wa Mtu'

Kwa hiyo kwa sentensi yako nikafikiri unawananga wale wanaoingia kwenye swimming pool na 'kubanjuana' mumo mumo.
 
Hili ni jukwaa la mapenzi sasa uliposema kutembea nikadhani ile 'kutembea' ya mtaani 'anatembea na mke wa Mtu'
Hahahah nimeweka humu kwa maana ni jukwaa langu pendwa na pia wadau wa swimming wengi ni kwa ajili ya wabebezi in lemutuz tone (voice)
 
Hapa najitayarisha kwenda pale tanzanite park kuangalia watt wazuri wakiogelea
Nasikia tanzanite park kuna watu wanafundisha sijui kweli?? Ebu nipe uzoefu mkuu? Na weekends panajaa sana?? Maana kwa eneo la makumbusho mpka Morocco imekuwa maarufu sana
 
Huwa najisikia vibaya sana ninapoenda hoteli yenye swimming pool naishia kutembea kwenye maji na kucheki wengine wakiogelea.. natamani kujifunza kuogelea maana naweza zama siku yoyote kwenye pantoni nikashinda kujitetea maana pia napandaga panton karibu kila wiki mara mbili na kuogelea sijui ebu tupeane uzoefu ni wapi naweza jifunza ogelea kwa dar.
Kama unataka kweli kujifunza kuswim kigamboni kuna mwalimu mzuri sana alinipa maujanja mpk Leo naweza kuogelea baharini umbali mrefu na kwa muda mrefu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nasikia tanzanite park kuna watu wanafundisha sijui kweli?? Ebu nipe uzoefu mkuu? Na weekends panajaa sana?? Maana kwa eneo la makumbusho mpka Morocco imekuwa maarufu sana
Kama unataka kujifunza usipende kufanyia sehemu ambazo kuna mauzo hutafanikiwa mapema interactions zitamuwa mingi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwa najisikia vibaya sana ninapoenda hoteli yenye swimming pool naishia kutembea kwenye maji na kucheki wengine wakiogelea.. natamani kujifunza kuogelea maana naweza zama siku yoyote kwenye pantoni nikashinda kujitetea maana pia napandaga panton karibu kila wiki mara mbili na kuogelea sijui ebu tupeane uzoefu ni wapi naweza jifunza ogelea kwa dar.
Kwa nini upate shida ya kujifunza kuogelea? Nunua life jacket. Ukilivaa lile, unaanza kuelea from day 1!
 
Back
Top Bottom