Kwa wakazi wa mwanza na Dar na wengine wote wenye experience naomba mnisaidie hapa....

Tasia I

JF-Expert Member
Apr 21, 2010
1,223
193
Nawasalim wote,
1. Naomba kufaham kulingana na mnavyo faham,
biashara ya haisi (hiace) kwa siku hulaza sh.ngapi kwa tajiri
na makubaliano hua yapoje kulingana na sehem yenyewe
(kama ni dar, mwanza n.k)

2. Hali ya kibiashara hii ipoje katika hilo eneo husika. yaani biashara ipo au
inafanyika kwa shida?

Mawazo yenu yatanisaidi sana kwsababu nina plan ya kuifanya biashara hii ila sijawahi before
hivy siifaham saaana.

Asanteni wote.
 
Kwa Mwanza inalipa zaidi kwa kuwa hakuna foleni, hesabu makubaliano kama umemjazia mafuta full tank akilaza gar jioni apige full tank na hesabu 40000/= Posho yake na konda wake watajijua wenyewe, no mshahara.
 
Kwa mwanza ni 40000 unapata tajiri kwasiku,mwanzo umjazie fulltank nakilasiku ajaze fulltank,poshoyao wanajilipa wenyewe,ila kuna usumbufu mkubwa kwa trafiki nahata madreva wengi ni wasanii ambao si waaminifu,ukipata dereva mwaminifu utaiweza ila kazi ngumu kidogo
 
Angalia sana madereva wanabadili tairi na kung'oa accessories kama air-conditioning system. Kwa ufupi you need to work hard to backup your dream brother. Good luck.
 
kama wewe utakuwa dreva,sawa utapata faida.otherwise achana nayo.sikukatishi tamaa ila yamenikuta
 
Kwa mwanza sawa, dar ni utumbo mtupu! niifanya kati ya 1999-2001, ku ukweli ni ugonjwa wa moyo, unaweza ng'oa mtu meno. Kwa dar tafuta zile basi kubwa za kichina zinalipa sana, ningekuwa na hea ningefanya. NOAH zinafanya kazi sana mikoani na wanapata hela nzuri sana. Kuna mtu anayo Musoma anaagiza nyingine soon. Usiangalie Hiace tu.
 
Back
Top Bottom