Kwa wajuzi wa Sheria. Naomba ufafanuzi kuhusu hili suala la mke kumfungulia kesi mume wake

goodhearted

JF-Expert Member
Feb 15, 2015
943
1,107
Kuna rafiki yangu wa karibu sana amezinguana na mkewe kama wiki 2 zimepita. Kwa influence ya wazazi wa binti imefunguliwa kesi ya kuwa jamaa kampiga mkewe na kumuumiza hivyo kwa madai ya jamaa baada yakuitwa polisi aliambiwa mkewe alifika pale kuchukua PF3 na akaenda hosptal akiwa na kaka zake.

Baadae mkewe aliondoka akamuaga mumewe kuwa anaenda nyumbani kwao na atarudi. Japo aliondoka na kaka zake ila hakusema kuwa ameenda kumshtaki jamaa polisi au hospital.

Jamaa ndo jana kapigiwa simu polisi akaripoti na baada ya kumchukua maelezo jamaa alikana kuwa hajampiga. Mshtaki ambae ni mke wa jamaa hakuwepo ila ajabu jamaa kawekwa mahabusu ndo bosi wake kazini akaenda kumdhamini.

Na ameambiwa arudi polisi wiki ijayo

Sasa wadau na wanasheria hii kitu imekaaje nimshauri nn jamaa yangu
 
Piga chini huyo si mwanamke. Mimi hata mzazi wangu au ndugu wa tumbo akanipeleka polisi na bahati mbaya nikalala mahabusu. Undugu na uhusiano umehitimishiwa hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hilo la kumpiga chini halina mjadala ila tu jamaa anachowaza ni namna gani au ni kwa vipi hio kesi ilivyo kaa polisi na namna ya kuimaliza.
 
nahitaji tofauti ya kugombana na kupigana?
Katafute kamusi ndo urudi hapa alafu ww kasichana usipende kushobokea shobokea mada zinazokuzidi umri. Wakubwa zako wakiwa wanaongea ww kimbia kacheze mbali. Shwaiiiiiiiìini
 
Katafute kamusi ndo urudi hapa alafu ww kasichana usipende kushobokea shobokea mada zinazokuzidi umri. Wakubwa zako wakiwa wanaongea ww kimbia kacheze mbali. Shwaiiiiiiiìini
Nelson(Nelly) unakalia wewe
 
Kwanini ulimpiga mkeo? mwanamke apigwi mzee hilo ni kosa kubwa sana, huyo mwanamke kama ana akili timamu asingeweza kwenda polisi na hao ndugu zake kama kungelikuwa hakuna tatizo kati yenu, kosa lako ni kumpiga mkeo ni unyanyasaji wa kijinsia na endapo hii kesi ingekuja kwangu basi wewe ungekuwa mfano kwa wengine wenye tabia ya kupiga wake zao, mwanamke anapigwa kwa maneno tu na siyo ngumu.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ajiandae kutumikia kifungo kama mke wake ataendelea na kesi.
 
Kwanini ulimpiga mkeo? mwanamke apigwi mzee hilo ni kosa kubwa sana, huyo mwanamke kama ana akili timamu asingeweza kwenda polisi na hao ndugu zake kama kungelikuwa hakuna tatizo kati yenu, kosa lako ni kumpiga mkeo ni unyanyasaji wa kijinsia na endapo hii kesi ingekuja kwangu basi wewe ungekuwa mfano kwa wengine wenye tabia ya kupiga wake zao, mwanamke anapigwa kwa maneno tu na siyo ngumu.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Kwa iyo ingekuja kwako ungejitahidi ununue mashahidi wa uongo ili tu unikomoe si ndio?

Alafu ukisha niweka mfano umwoe mke wangu na watoto wangu uwalee eti bwana hakimu. Kama kweli ww una uwezo huo basi wateja wako wanashida kuu

Mwisho naomba unifafanulie kwa nn unasema " huyo mwanamke kama ana akili timamu asingeweza kwenda polisi na hao ndugu zake "
 
Kwanini ulimpiga mkeo? mwanamke apigwi mzee hilo ni kosa kubwa sana, huyo mwanamke kama ana akili timamu asingeweza kwenda polisi na hao ndugu zake kama kungelikuwa hakuna tatizo kati yenu, kosa lako ni kumpiga mkeo ni unyanyasaji wa kijinsia na endapo hii kesi ingekuja kwangu basi wewe ungekuwa mfano kwa wengine wenye tabia ya kupiga wake zao, mwanamke anapigwa kwa maneno tu na siyo ngumu.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Kwa hiyo kwa maelezo mafupi tu haya umekamilisha ushahidi kua alimpiga mke wake?

Tuna watafsiri sheria wa hovyo Sana nchi Hii hamuishi kuamua Mambo kwa hisia na kuweka taaluma pembeni tangu muamue kua watetezi wa haki za kijinsia basi lengo kuu limekua kumsapoti mwanamke kwa kumkandamiza mwanaume hamuhitaji ushahidi wa kutosha kuamua kesi mnakurupuka tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom