Mwendabure
JF-Expert Member
- Mar 10, 2011
- 2,138
- 1,040
Habari Wakuu!
Ni hivi karibuni serekali yetu imekiri kwamba wazamiaji wa kukodi kutoka Afrika Kusini wameshindwa kuifikia Meli iliyozama baharini na kusababisha vifo vya ndg zetu huko Zanzibar. Mimi binafsi kwa uelewa wangu mdogo kuhusu masuala ya bahari ningependa kueleweshwa vema haya yafuatayo.
1. Ni umbali (kina) gani unaweza kufikika kiurahisi na kwa kutumia vifaa gani?
2. Kuna tofauti gani ya hali ya bahari kati ya kina kidogo na kina kirefu?
3. Nimekuwa mara nyingi nikiona ktk sinema au hata baadhi ya vipindi vya TV wazamiaji au watafiti na wapiga picha za bahari wakifika hadi ktk sakafu ya bahari kwa kutumia vifaa kama vile mitungi ya gesi huwa wanaweza kufikia kina gani cha bahari kwa vifaa kama hivyo?
Natumaini nimeeleweka vema na nitapata majibu murua kwa faida yangu na wengine pia. Binafsi naamini hadi sasa serikali yetu haina mpango wa kutoa elimu au ufafanuzi wa kutosha hasa kwa Mtanzania wa kiwango cha uelewa kama wangu kuhusu kinachoendelea juu ya sakata hili na hatma ya miili ya wapendwa wetu waliopotelea baharini.
Nawasilisha!
Ni hivi karibuni serekali yetu imekiri kwamba wazamiaji wa kukodi kutoka Afrika Kusini wameshindwa kuifikia Meli iliyozama baharini na kusababisha vifo vya ndg zetu huko Zanzibar. Mimi binafsi kwa uelewa wangu mdogo kuhusu masuala ya bahari ningependa kueleweshwa vema haya yafuatayo.
1. Ni umbali (kina) gani unaweza kufikika kiurahisi na kwa kutumia vifaa gani?
2. Kuna tofauti gani ya hali ya bahari kati ya kina kidogo na kina kirefu?
3. Nimekuwa mara nyingi nikiona ktk sinema au hata baadhi ya vipindi vya TV wazamiaji au watafiti na wapiga picha za bahari wakifika hadi ktk sakafu ya bahari kwa kutumia vifaa kama vile mitungi ya gesi huwa wanaweza kufikia kina gani cha bahari kwa vifaa kama hivyo?
Natumaini nimeeleweka vema na nitapata majibu murua kwa faida yangu na wengine pia. Binafsi naamini hadi sasa serikali yetu haina mpango wa kutoa elimu au ufafanuzi wa kutosha hasa kwa Mtanzania wa kiwango cha uelewa kama wangu kuhusu kinachoendelea juu ya sakata hili na hatma ya miili ya wapendwa wetu waliopotelea baharini.
Nawasilisha!