Kwa wahenga tu: Kwanini watu wengi wenye roho nzuri huwa na maisha magumu au ya kawaida tu?

Blueface

Member
May 2, 2020
46
47
Hili jambo nimekua nikilifikiria kwa miaka mingi bila majibu.Hata wewe hapo ulipo jaribu kuangalia katika familia au ukoo wenu. Unaweza kuta katika ukoo au familia ndugu yenu mwenye roho mbaya ndiye mwenye uwezo kifedha kuliko nyie wenye moyo wa kutoa. Katika jamii tunazoishi yaani wale watu wenye huruma na moyo wa kujitolea kwenye matatizo ya wenzao huwa na maisha magumu au ya kawaida sana.

Labda ungetegemea kwa kadiri mtu anavyosaidia wenzake ndo na yeye mambo yake yanyooke lakini inakua tofauti.Wapo watu wengi waliofirisika kwa kusaidia ndugu au marafiki mwisho wa siku wakajikuta wameishiwa kabisa. Mbaya zaidi wale waliosaidiwa huanza kuwacheka na kuwakejeli. Nimeona mfano huo kwa baba yangu. Tangu tukiwa wadogo ndugu wengi walikuwa wakija pale nyumbani na kusaidiwa hadi ada za shule kwa wale waliokua wanasoma. Sasa imepita miaka mingi maisha yake ni yaleyale, wale waliosaidiwa wengi wapo kimya tena baadhi wako ulaya lakini hata kupiga simu kutoa salamu ni mtihani.

Upande wa pili ukiangalia watu wenye roho mbaya na wabinafsi huwa wanafanikiwa sana pamoja na roho zao mbaya. Hawa ni wale watu ambao hawatoi msaada hata kama mtu anaumwa labda kwenye msiba ndo utawaona wanatoa misaada ya sifa.Kwa nini iko hivyo wakati tunaambiwa kwenye dini kadri unavyotoa ndivyo unapata zaidi? Kwa nini mwenye roho ngumu ndo afanikiwe kuliko mwenye roho nzuri? Majibu yenu tafadhali. Pascal Mayalla, Mshana Jr na wahenga wengine, nahitaji busara zenu huku.
 
Japo sijatajwa kwenye uhenga hapo acha nijipendekeze tu.

Mwenye roho nzuri ni sawa na tenga la nyanya hata ulipeleke baharini au ziwani kuchotea maji haliwezi kujaa. Roho nzuri yao inawadidimiza hawaweki akiba.

Mwenye roho mbaya mbinafsi ni sawa na ndoo ukikinga maji yanajaa. Hawa mara nyingi wana uwezo mkubwa wa kuweka akiba. Wahenga walishasema akiba haiozi.
 
Shujaa ni yule anaeweza kumsaidia mtu bila kujali hali anayopitia.

Usiache kumsaidia mtu kama nafasi au uwezo wa kumsaidia unao hasa ukizingatia huwezi kujua ni kwa namna gani utaibadilisha hali/nafasi ya unaemsaidia hata kama sio ndugu.

Usitegemee kusaidiwa unapotoa msaada, sababu usipofanyiwa wema kwa wema uliowapa utaumia sana. Karma is real, You are an angel. Hata kama wao watasahau ulichowasaidia lakini Mungu yupo anaona na wala hawezi kusahau.
 
Nimeona mfano huo kwa baba yangu.Tangu tukiwa wadogo ndugu wengi walikuwa wakija pale nyumbani na kusaidiwa hadi ada za shule kwa wale waliokua wanasoma.Sasa imepita miaka mingi maisha yake ni yaleyale, wale waliosaidiwa wengi wapo kimya tena baadhi wako ulaya lakini hata kupiga simu kutoa salamu ni mtihani.
Tenda wema nenda zako...
 
Hakikisha unaposaidia mtu/watu usitoe kila kitu mpaka kufikia kujiumiza sehemu ya wewe mwenyewe (saidia kwa kiasi).

Furaha, amani na utulivu upo zaidi kwa mtoaji kuliko anaepokea (hivyo basi usiache kuwasaidia).

Kutokukulipa mema kwa uliowasaidia kusikuumize kichwa sababu tabia zao na tabia yako ni tofauti (usibadili tabia sababu ya ubaya wao)
 
Nadhani ni mtazamo na nani umewaona zaidi mahali unapoishi. Binafsi nimewaona waliofanikiwa kadhaa wakiwasaidia wengine sana tu. Tena bila kinyongo wala masharti na nimewaona masikini wenye roho za sumu.

Na kinyume chake.

Wakati mwingine roho mbaya hutokana na malezi, kutendwa, kuiga, masharti ya waganga na baadhi mafunzo kutoka kwa wahamasishaji eti usipokuwa bahili hufanikiwi.

Mungu Ibariki Tz - MITz
 
Sipo kwenye "Uhenga"

Watu wenye roho nzuri si watu wa materialistic things. Haijalishi atambulike yumo kundi la wenye nacho, mwenye kipato cha kati au fukara. Makundi yote hayo watu wenye roho nzuri ukiwatizama utawaona wana kitu kinachofanana. Nacho si watu wenye kuvipa kipaombele vile vyenye kupewa thamani ya kimali na watu kwenye jamii. Kwa sababu si vitu vyenye kuwapa amani na furaha isiyokuwa na kifani kwenyw moyo.

Mtu mwenye roho nzuri kuna hali imo ndani ya moyo wake ambayo akifanya jambo zuri linampa amani, faraja na raha isiyo na kifani. Huwa haina mfano kuielezea kwa maandishi! Ila mtafute mwenye roho nzuri umuulize akifanya jambo jema huwa anajisikiaje? Hiyo hali anayojisikia ndiyo inayomfanya havikuzi wala kuvipa thamani vitu vinavyotolewa macho na wengi. Moingoni mwa sababu ni kuwa wanaamini materialistic things wanaweza wakavipata au wakavikosa.

Huwa hawajali wakiwa nacho au wakipungukiwa! Kitu pekee wanachojali ni upendo, ni roho nzuri. Ndiyo maana huwezi kumkuta mwenye roho nzuri akiwa na mwenye msongo wa mawazo hatari! Kwa sababu moyo wake bado una upendo na ndiyo tumaini linalompa faraja.
 
Sipo kwenye "Uhenga"

Watu wenye roho nzuri si watu wa materialistic things. Haijalishi atambulike yumo kundi la wenye nacho, mwenye kipato cha kati au fukara. Makundi yote hayo watu wenye roho nzuri ukiwatizama utawaona wana kitu kinachofanana. Nacho si watu wenye kuvipa kipaombele vile vyenye kupewa thamani ya kimali na watu kwenye jamii. Kwa sababu si vitu vyenye kuwapa amani na furaha isiyokuwa na kifani kwenyw moyo.

Mtu mwenye roho nzuri kuna hali imo ndani ya moyo wake ambayo akifanya jambo zuri linampa amani, faraja na raha isiyo na kifani. Huwa haina mfano kuielezea kwa maandishi! Ila mtafute mwenye roho nzuri umuulize akifanya jambo jema huwa anajisikiaje? Hiyo hali anayojisikia ndiyo inayomfanya havikuzi wala kuvipa thamani vitu vinavyotolewa macho na wengi. Moingoni mwa sababu ni kuwa wanaamini materialistic things wanaweza wakavipata au wakavikosa.

Huwa hawajali wakiwa nacho au wakipungukiwa! Kitu pekee wanachojali ni upendo, ni roho nzuri. Ndiyo maana huwezi kumkuta mwenye roho nzuri akiwa na mwenye msongo wa mawazo hatari! Kwa sababu moyo wake bado una upendo na ndiyo tumaini linalompa faraja.
Nimekupata mkuu!Ila nilitaka kujua kwa kadiri ya mafundisho ya Dino na kijamii tunafundishwa unaposaidia ndo unapata baraka nyingi ila naona watoaji wengi maisha yao yapo kawaida tu nikadhani wale wenye uwezo wasiotoa watapata laana wafilisike wawe maskini lakini kadiri wanabyokuwa wabahili na roho mbaya ndo Mali zao zinaongezeka!
 
Wengi tunataka tukimsaidia mtu, naye aje atusaidie baadae badala ya kufanya kama kupanda mbegu kwa Mungu ambaye yeye ndio atatafuta mtu mwingine/namna nyingine kabisa wa kutusaidia matatizo yetu, wakati mwingine ikawa akiba kwa vizazi vyetu wakati tukiwa hatupo duniani. Tenda wema nenda zako!
 
Yesu alivyosema ni Rahisi kwa ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko tajiri kuona ufalme wa Mungu Ulielewaje mkuu?
Hakumaanisha utajiri wa fedha alimaanisha kujihesabia haki, soma biblia tangu Mwanzo hadi ufunuo utangundua Yesu hakufanya Kazi na maskini hata mmoja, pia kwenye agano la kale yeyote alieandikwa hakua maskini wote walijitosheleza kiuchumi ila walikua na kiu ya kumtumikia Mungu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Roho mbaya (Protestant ethics):

Postpone enjoyments, be selfish, be frugal, invest, make more profits. Give good education to children. Focus on yourself na usitapanye pesa.

Roho nzuri (Christian values):

Toa ndugu, toa ndugu, toa ulicho nacho, kwani bwana ana kuona mpaka moyoni mwako. Usiwe na wasiwasi, kwamba utakula nn mezani kwa bwana Kuna chakula Cha uzima.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Matajiri wote wanaroho nzuri japo hawawezi kukidhidhi mahitaji ya kila mhitaji, sijawahi kuona mtu anafilisika kwa kula yeye na familia yake, tunatakiwa kusaidia ikiwa tu unauwezo wa kutoa msaada kwa wakati huo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom