Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Jifunze taratibu kwa kuanzia na wachache

Angalizo, wachache huwa hawalipi Bali wa nakupa uzoefu ambao utakufaidisha pale ukianza kufuga wengi ili kukupa faida

Inahitaji
1. Concentration (muda na Nia thabiti) wanakatisha tamaa sana.

2. Resilience (ustahimilivu na uvumilivu wa kiwango cha juu), wengi wanakurupuka nakuishia pa hovyo

3. Moyo wa kupenda .... Maana wengi huishia kususa nakufilisika hasara hujitokeza Mara kwa Mara hususani unapoanza
-vifaranga wanakufa.....uzoefu wa matunzo
-magonjwa kuvamia na kuua Kuku wako...uzoefu wa matunzo nk

Ndio maana unashauriwa kuanza taratibu. Ukifaulu na kupata udhoefu ndio unafanya shughuli halisi...kufuga wengi kwa faida

Nayafahamu haya maana wife nimfugaji wakuku ameanza kama miaka tatu hivi sasa hivi amefaulu kufaham mbinu na mahitajio yote na anao wengi.

Kila raheri mkuu.

.........................................................
 
Jifunze taratibu kwa kuanzia na wachache

Angalizo, wachache huwa hawalipi Bali wa nakupa uzoefu ambao utakufaidisha pale ukianza kufuga wengi ili kukupa faida

Inahitaji
1. Concentration (muda na Nia thabiti) wanakatisha tamaa sana.

2. Resilience (ustahimilivu na uvumilivu wa kiwango cha juu), wengi wanakurupuka nakuishia pa hovyo

3. Moyo wa kupenda .... Maana wengi huishia kususa nakufilisika hasara hujitokeza Mara kwa Mara hususani unapoanza
-vifaranga wanakufa.....uzoefu wa matunzo
-magonjwa kuvamia na kuua Kuku wako...uzoefu wa matunzo nk

Ndio maana unashauriwa kuanza taratibu. Ukifaulu na kupata udhoefu ndio unafanya shughuli halisi...kufuga wengi kwa faida

Nayafahamu haya maana wife nimfugaji wakuku ameanza kama miaka tatu hivi sasa hivi amefaulu kufaham mbinu na mahitajio yote na anao wengi.

Kila raheri mkuu.

.........................................................
Umenipa kitu hapo, Napenda kweli na muda ninao wa kutosha tuu kuhudumia, ninapotaka kuanzishia majiran wafugaji wapo na nimeanza kuwahoji na kupata elimu kidogo kidogo,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu vp kuhusu changamoto ya soko. Na je vp kuku wa mayai na wa nyama wapi wanausumbufu zaidi?
Ukisema ujipange, hutafanikiwa. Utanikuta umekula hiyo fedha kizembe

1. Anza kwa Kuku wachache kabisa 60 hivi
-watakufundisha
I) mahitaji yao
-dawa
-vyakula
-vyombo
-magonjwa nk

2. Washirika wako wa kukupa msaada
-wafugaji, majirani
-wataalamu wa mifugo nk

3. Uzoefu wa kushughulika na kero mbali mbali

Ukisha pata uzoefu kamili utaanza kuongeza idadi kadri ya mtaji na nafasi yako

Muhimu ni kwamba mambo ya ufugaji yanahitaji moyo, na uvumilivu maana faida hupatika baada ya muda kupita

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu vp kuhusu changamoto ya soko. Na je vp kuku wa mayai na wa nyama wapi wanausumbufu zaidi?

Sent using Jamii Forums mobile app

Changamoto sizielewi kwakweli kwa undani, ufatao mtazamo wangu.

1. Kuku wa nyama sio profitable
Nimekuwa mshauri mkuu kwa wife, maana Mimi Nina majukum tofauti ya kiofisi lakini ndiye ninaye focust na foreseen wa project yake

Kuku wa nyama unawanunua nakuwakuza kwa shida vifanga, yet unawauza siku moja wote na kuanza round mpya ya vifaranga wageni kwa usumbufu uleule na wengine wanajifiawa (matunzo ya vifaranga yanashabihiana kwa wote na hapo ndio kuna changamoto ya ufugaji wa Kuku, madawa, chakula, joto nk)

Kuku wa mayai ukiwatunza vifaranga kuanzia miezi tano au sita unaanza kuokota mayai mwendelezo wa zaidi ya mwaka unauza.....cash flow IPO kila siku unaokota unauza mayai, usumbufu wa kupambana na vifanga wageni itakuchukuwa muda mrefu (una nafasi yakutumia mapato yatokanayo na mauzo ya mayai kila siku kupanua idadi ya Kuku wako kwa kununua nakutunzia vifaranga wageni sambamba...fedha IPO kutoka mauzo ya mayai kila siku)

Soko la biashara za Kuku
1. Mayai lipo la uhakika

2. Nyama lipo la uhakika

Changamoto, mayai bei zake zinaeleweka hazina mijadala kwenye kuuza huhitaji saana kushawishi wanunuzi

Changamoto, kuku wa nyama kila wakati utahitaji kupambana katika bei maana kila ukuzaji hauendi sawa sawa naukubwa wa Kuku, mahitaji ya nyama na ushawishi wa mnunuzi katika siko

Thanks
 
Kwa wale mnaotaka kuingia ubia

Kuweni makini sana, hii biashara sio rahisi kivile na nimesema tangu Jana

1. Uzoefu ni lazima

2. Uvumilivu ni lazima

3. Inachukuwa muda kukulipa, ukisha ijuwa nakuimudu inalipa kweli kweli....uhakika

4. Haitaji kukurupuka, harakaharaka lazima utapiga mzinga wa hasara

5. Kama ilivyo biashara zote za shamba zinahitaji utulivu, long time plans na concentration. ( Sayansi yakilimo haitaji siasa au blabla, ni vitendo na facts )
 
Nimekupaa vyema mkuu wng
Kwa wale mnaotaka kuingia ubia

Kuweni makini sana, hii biashara sio rahisi kivile na nimesema tangu Jana

1. Uzoefu ni lazima

2. Uvumilivu ni lazima

3. Inachukuwa muda kukulipa, ukisha ijuwa nakuimudu inalipa kweli kweli....uhakika

4. Haitaji kukurupuka, harakaharaka lazima utapiga mzinga wa hasara

5. Kama ilivyo biashara zote za shamba zinahitaji utulivu, long time plans na concentration. ( Sayansi yakilimo haitaji siasa au blabla, ni vitendo na facts )

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jaribu Hao chotara mkuu anza Na wachache!
Kuna mtu anajiita mkulima _smart naona bei zake za vifaranga sio gharama kivile!
Afu yupo huko huko dar
Yeye niliona kuloiler anauza 1200 wakati huku Iringa ni balaa
 
Kama upo tayari njoo tushirikiane, mimi nina banda la kuku 1500 hivi na la kisasa kabisa,
Ndi ilikuwa nianze kufuga lakini nikapata matatizo, karibu naishi hapa Ukonga 77
Kwa mawasiliano zaidi 0738929380

1549101568395.jpeg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jaribu Hao chotara mkuu anza Na wachache!
Kuna mtu anajiita mkulima _smart naona bei zake za vifaranga sio gharama kivile!
Afu yupo huko huko dar
Yeye niliona kuloiler anauza 1200 wakati huku Iringa ni balaa

Kuwa makini utauziwa vifaranga wa kizazi cha 3 hadi 4 kwa bei hiyo
 
Hellow, naombeni ushauri natamani kufuga kuku chotara eneo ninalo ila Nina balance ya mil moja tuu, je inawezatosha kwa ufugaji wa aina hiyo ya kuku??nipo Dar es salaam Tabata

Sent using Jamii Forums mobile app
Anza kidogo kidogo sio lazima uanze na Kuku 500, kuhusu banda unaweza ukajenga banda la mbao na wavu sio lazima utumie tofali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

30 Reactions
Reply
Back
Top Bottom