Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Hawa kuku wa kisasa mwenzenu kuwala naogopa kuwafuga mie nitaweza?

FL usiogope utaweza tu, yaani mie ninawafuga muda tu, ila inataka moyo usile hela ya chakula chao na dawa, pia usiwe mtu mkarimu sana, uwachukulie kama biashara na sio chakula: kila mgeni akija apikiwe, unaingia bandani na kumfungia mwingine akapike kwake! hapo faida hamna kabisa!

Unajua kuna wengine wala hatauwali sana ila tunawafuga ni business, kuna watu hawali uyoga lakini wanalima, hii ni biashara.

Mie kwakweli hawa wa kienyeji ndio huwa nawaona kama pets kiasi unakuwa mmeishamzoea sana hata kumchinja mnamuonea huruma, kama ni watoto wanaweza lia kabisa!:D
 
UFUGAJI BORA WA KUKU WA NYAMA NA MAYAI:
WIKI YA KWANZA:SIKU YA 1 - 6 WAPE:GLUCOSEBROILER BOOST AU AMINOVIT AU SUPERVITVIGOSTART KWENYE CHAKULA (KILO 1 KWA MFUKO 1 WA KG 50) KUANZIA WIKI YA KWANZA HADI YA 4
SIKU YA 7CHANJO YA NEWCASTLE - MASAA 2 TU, WEKA MAJI NA VITAMIN MARA BAADA YA KUTOA MAJI YA CHANJO
WIKI YA PILICHANJO YA GUMBORO - MASAA 2 TU, HALAFU ENDELEA NA MAJI YA VITAMIN
WIKI YA TATUDOXICOL AU CTC20% NA AMPROLIUM, VITAMIN NA MOLASSES KWA SIKU 5 - 7
WIKI YA NNEHAKIKISHA KUKU WA NYAMA WANAKUWA KATIKA DOSE KUBWA YA VITAMIN
WIKI YA SITAWAPE KUKU WA NYAMA MAJI YA VITAMIN ASUBUHI NA MATUPU JIONI
WIKI YA NANEWAPE KUKU WA MAYAI CHANJO YA NDUIDAWA ZA MINYOO (PIPERAZINE AU LEKIWORM)VITAMIN AU SUPERVIT LAYERSWALISHE GROWERS MASH AU FARMERS CONCENTRATE HADI MIEZI 3 NA 1/2 TUMIA LAYERS MASH WAKIFIKA MIEZI 4 KAMILI AU WAPE MAJANI
WIKI YA KUMI NA MBILIWAPE CHANJO YA NEWCASTLE ( RUDIA KILA BAADA YA MIEZI 3) MASAA 2 KISHA WAPE MAJI YA VITAMIN
WIKI YA KUMI NA SITAKATA MIDOMO KISHA WAPE NEOXYVITAL KWA SIKU 3-5 ANDAA VIOTA
WIKI YA 54WAPE VIRUTUBISHO VYENYE KUONGEZA WINGI WA MAYAI MFANO GLP ( KILO 1 KWA KILA KILO 50 ZA CHAKULA, WIKI YA KWANZA NA NUSU KWA WIKI ZINAZOFUATA NA VITAMIN
WIKI YA 72TUMIA V RID KUSAFISHA MABANDA ILI KUUA VIJIDUDU PIA WEKA MAJI YA DAWA HII KWENYE DISH YA KUSAFISHIA MIGUU (FOOTBATH) ILI KUHAKIKISHA UDHIBITI WA VIJIDUDU (BIOSECURITY) NA KWAMBA VIFARANGA WANAOWEKWA HAWAATHIRIWI NA VIJIDUDU HIVYO.
WIKI YA 96ONDOA KUKU WOTE WALIOZEEKA

All the Best

This is the reason why I love JF! where else could someone get such a productive staaff!! Nashukuru sana mama Joe. Thanks alot
 
FL usiogope utaweza tu, yaani mie ninawafuga muda tu, ila inataka moyo usile hela ya chakula chao na dawa, pia usiwe mtu mkarimu sana, uwachukulie kama biashara na sio chakula: kila mgeni akija apikiwe, unaingia bandani na kumfungia mwingine akapike kwake! hapo faida hamna kabisa!
Unajua kuna wengine wala hatauwali sana ila tunawafuga ni business, kuna watu hawali uyoga lakini wanalima, hii ni biashara.
Mie kwakweli hawa wa kienyeji ndio huwa nawaona kama pets kiasi unakuwa mmeishamzoea sana hata kumchinja mnamuonea huruma, kama ni watoto wanaweza lia kabisa!:D

Asante mama Joe, kuna wakati mfugaji anajikuta amekuwa rafiki wa wanyama wake kiasi kwamba kumuuza yule mnyama/wanyama anapata huruma. Siku nilipouza dume la kondoo home kwetu, madogo waligoma kula na dume limeshakwenda. Umenikumbusha mbali.

nitaku-pm siku nikianza kuwafuga kibiashara.
 
Ni biashara nzuri to think of, ila ina high risk - kuku hata mia tano wanaweza kufa just for 24 hrs, so someone has to study the risk first before jumping into this business, unaweza kupata presha.
 
Kuku ni biashara nzuri sana lakini inabidi uwe mjanja,
kwanza jifunze kutengeneza chakula cha kuku mwenyewe usiwe unanunua. Pili usiwe mbahili...hakikisha wanakula vizuri na madawa ya kupulizia kwenye mabanda unatumia anza na kuku 2000.

Good luck.
Biashara ya kuku kama unataka kufa mapema basi anza na kuku 2,000 wakati hujajenga uzeofu wa shughuli hizi.
Ushauri wangu ni kuwa.

a) Fanya utafiti wa kina kuhusu soko la uhakika ili wasikudodee baada ya kukua [wanakula kama nzige]
b) anza na idadi ndogo ujenge uzoefu na hata ikitokea hasara basi inakuwa manageable'
c) Nenda kwa afisa mifugo yoyote uliyekaribu nae aangalie eneo ulilonalo halafu akushauri aina ya banda la kujenga pamoja na mambo mengine yanayohusu ufugaji wa kuku wa kisasa.
 
Then tusaidiane hapa;

tupeni in black and white pros na cons za kuku wa kienyeji v/s kuku wa kisasa!

Na yule mtu anayeanza leo; aanzie wapi on both types, Mama Joe?
 
Unaweza usimpate kirahisi kwa sababu anaweza asijue kuwa unahitaji material zaidi,pili anaweza asipitie hapa leo,cha kufanya M-PM.

Ni mawazo yangu.
 
Wakuu hii bishara naona kama kwa sasa imefikia next level. namaanisha invention ya matumizi ya ARV'S kuwakuza kuku haraka.juzi nimeingia Iringa baa moja inaitwa sterio maarufu kwa uchomaji wa kuku, nikaagiza nusu kuku!! believe you me, sahani ilijaa utafikiri mpaka nikashtuka. Jamani you guys you are killing us softly!
 
Weka wazi zaidi unataka kufuga kuku wa kienyeji au wa kisasa? Maana mbinu za kufuga ni tofauti kati ya aina hizimbili za kuku.
 
Wakuu hii bishara naona kama kwa sasa imefikia next level. namaanisha invention ya matumizi ya ARV'S kuwakuza kuku haraka.juzi nimeingia Iringa baa moja inaitwa sterio maarufu kwa uchomaji wa kuku, nikaagiza nusu kuku!! believe you me, sahani ilijaa utafikiri mpaka nikashtuka. Jamani you guys you are killing us softly!!!

Sisi tunaongelea ufugaji wa kuku, hayo mambo yako yaliyokukuta huko iringa na kuku wako wa ARV's sisi hatuyahitaji kwa sasa. kama huna comments za ufugaji basi tuache sisi tuendelee ku discuss ki-vyetu.
 
Weka wazi zaidi unataka kufuga kuku wa kienyeji au wa kisasa???? maana mbinu za kufuga ni tofauti kati ya aina hizimbili za kuku.

This will benefits all. ukiwa na nondo za kufuga kuku wa kienyeji mwaga. wa kisasa mwaga pia. What I have discovered is that This topic has been a real benefit to most of us! Thanks again
 
Asante mama Joe, kuna wakati mfugaji anajikuta amekuwa rafiki wa wanyama wake kiasi kwamba kumuuza yule mnyama/wanyama anapata huruma. Siku nilipouza dume la kondoo home kwetu,madogo waligoma kula na dume limeshakwenda. umenikumbusha mbali.

nitaku-pm siku nikianza kuwafuga kibiashara.
Karibu mkuu
 
Weka wazi zaidi unataka kufuga kuku wa kienyeji au wa kisasa? Maana mbinu za kufuga ni tofauti kati ya aina hizimbili za kuku.

Kwanza tujifunze faida na hasara za za aina zote; then ndi tuta specialize!

Nimesikia Ruvu JKT wanauza vifaranga wa kuku wa kienyeji; mwenye taarifa zaidi atuhabarishe ; huyu aliyenambia naye amesikia!
 
Kuku wa kienyeji
Faida
  • Ni gharama ndogo kuwatunza: chakula chao ni rahisi, pia wanaweza kujitafutia wenyewe, maji yao pia sio lazima yawe maji salama.
  • Hawahitaji umeme au taa usiku au wakati wa baridi kwa vifaranga, labda uwe umenunua vifaranga na hawakuzalishwa na majike wa kuwafunika usiku
  • Nyumba zao ni rahisi zinaweza kuwa za mabanzi/ mbao au mabati / tofali kutegemeana na uwezo wa mtu
  • wanastahimili magonjwa, hivyo hawahitaji kuwatibia mara kwa mara au kuwapa vitamin (Newcastle tu au chanjo ya mdondo ndio inahitajika)
  • Ni chakula bora ambacho mlaji anaweza kula kila siku bila kuhofia madhara ya madawa au vitamin
  • Ni kama pets katika familia kwasababu wanakua taratibu
Hasara
  • Wanahitaji nafasi kubwa, kwa ajili ya kujitafutia chakula pia kukuwezesha kuhamisha nyumba zao kuzuia vinyesi vyao visiwaletee magonjwa
  • Vifo vingi wakiwa vifaranga (ajali, mwewe, vicheche) magonjwa na ukubwani wezi pia (maana hawafungwi sana pia wanaweza toka nje bila wewe kujua wakaibiwa)
  • Wanachukua muda mrefu hadi kuwatayari kuuzwa, hivyo sio biashara ya haraka haraka. Soko lao linategemea na eneo na bei yake haitabiriki (unaweza kufuga kuchi/jogoo na majike kwa gharama sawa ila kuuza bei tofauti kwani uzito wao hautabiriki hivyo unapokuwa na vifaranga hujui utavuna kiasi gani)
  • Hawatabiriki kuhusu kuongezeka au kuzaliana mfano anaweza atage mayai mengi ukamwacha alalie, kisha siku chache kabla ya kutotoa akayaacha, pia wanakunywa mayai maana hawakatwi midomo.

Kuku wa kisasa
Faida
  • Wanaweza kufugwa hata kwenye eneo dogo la uani, mradi uwe msafi mfano kuku 200 kwa banda la mita 3 kwa 5 /6
  • Wakitunzwa vizuri kwa kufuata masharti ya chakula chao hadi kufikia kuuzwa au kutaga wanakufa wachache sana (<5 kwa banda la kuku 200)
  • Wanachukua muda mfupi hadi kuuzwa mfano wa mayai utawalisha miezi 6 wanaanza kutaga na kuku wa nyama ni mwezi na nusu (wiki 6 au 7) kutegemea na uzito utakaotaka. Hivyo ukipishanisha kuku wa nyama kwa wiki mbili kila mwisho wa mwezi una kuku wa kuuza. Na kuku wa mayai kila siku una mayai unauza hadi miezi 18 unawauza kuku wenyewe pia. Hii ni faida kubwa na inaweza kukuwezesha usihitaji mshahara wako. Soko la kuku wa nyama na mayai ni kubwa na linatabirika (bei mara nyingi inajulikana toka unachukua vifaranga)
  • Very tamed... labda ukosee masharti ya dawa na chakula, lakini wa mayai wakianza kutaga ni moja kwa moja, pia ukiwakata midomo mayai yapo salama. Kama nyumba zao ni salama na hakuna wezi wanaoingia sio rahisi kutoka nje na kuibiwa au kutaga mayai nje.
Hasara
  • Inahitaji mtaji: hela ya chakula na dawa bila kukosa, ukiwakosesha chakula au dawa kwa wakati wao utapata hasara kubwa (wanaweza kufa, wakawa viwete, kudumaa wasikue au kutotaga mayai), chakula chao pia ni bei kubwa kama huchanganyi mwenyewe, maji lazima uweke waterguard au chemsha hasa wiki za mwanzo.
  • Wanahitaji umeme au taa ili waweze kula masaa 24 (hata mkaa wakiwa wadogo kama kuna baridi)
  • Nyumba zao ziwe za bati au tofali ili kuzuia unyevu wa ardhini pia sakafu ipigwe plasta, wanahitaji hewa safi hivyo madirisha makubwa hewa itembee. Ziba mianya yote ya mwewe, kunguru, vicheche kuingia kwa kuweka wavu madirishani
  • Kama hufuati masharti ya chanjo na dawa unaweza hatarisha afya za walaji kwakuwa utahitajika kuwatibu wakiugua wiki za mwisho ambapo unawauza. Vitamini pia zinatakiwa zipunguzwe wiki za kuuza kuku wa nyama.
  • Wanahitaji usafi kwenye banda: randa za mbao (saw dusts) zinahitajika ili kuzuia vinyesi visilete ubichi na ubaridi wa floor wanapolala. Kubadilisha hizi randa kila zikilowa ili kuzuia ugonjwa wa mafua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom