Djunior
Member
- Sep 28, 2010
- 45
- 1
Siku ile ya tarehe 5/5/2010. Akiwa mbele ya wazee wa Dar-es-Salam, Mh JK huku akiwaita wafanyakazi wa Tanzania mbayuwayu, alitamba na kusema "Mimi ndiyo mwajiri wa wafanyakazi wote hivyo atakayegoma nitamfukuza kazi,na kama ni kura sizihitali kura zenu, vijana wapo tayari Watatumia virungu,risasi za mpira na ikibidi za moto oa watasimama mahakamani na bandeji kichwani" mmh! Hii ndiyo kauli ya Mh JK. Wapendwa wafanyakazi hima wakati wetu wa kutamba umefika 31/10/2010 kwa nguvu zote mbele ya karatasi ya kupigia kura nenda kasitishe ajira yake. Mwajiri kiongozi atakaejali wafanyakazi na kuwafikisha Mafisadi wote mahakamani na kurudisha ardhi iliyouzwa kwa wageni kupitia migongo ya mafisadi. Hii oi oafasi ya pekee tuliyopewa na Mungu. Hima kwa pamoja.ushindi wa nguvu chagua Dr Slaa ndiyo kiongozi pekee anaefaa. MUNGU IBARIKI TANZANIA. MUNGU WABARIKI WAEANYAKAZI WOTE.Amen .