Mphamvu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 10,702
- 3,285
Pamoja na mambo mengine, mimi hupenda kula. Sio mvivu wa kula na wakati mwingine huwa nashiba vitu vidogodogo vidogo vya kula njiani, mradi tu visiwe vyakula ----- (vyenye masukari mengi na visivyo na faida mwilini.
Majuzi katika pitapita zangu nikatokea Msikiti wa Kiblatan (au Qiblahtein) ulioko maeneo ya Kariakoo (jina la mtaa sijui) lakini si mbali sana kutoka sokoni ukiwa unaelekea Kongo. Hapo nikakuta meza nyingi za kuuza mapochopocho, ukiwemo urojo ambao naupenda saanah. Pia kuna mishkaki, mihogo ya kuchoma, ndizi choma, juisi ya miwa, tende, matunda, chipsi, kuku choma, supu ya pweza, ngizi, samaki wa kukaanga na vingine vingi.
Nikaweka kituo kwa muda, nikapata nilichokipata.
Karibuni....
CC: vanmedy
Majuzi katika pitapita zangu nikatokea Msikiti wa Kiblatan (au Qiblahtein) ulioko maeneo ya Kariakoo (jina la mtaa sijui) lakini si mbali sana kutoka sokoni ukiwa unaelekea Kongo. Hapo nikakuta meza nyingi za kuuza mapochopocho, ukiwemo urojo ambao naupenda saanah. Pia kuna mishkaki, mihogo ya kuchoma, ndizi choma, juisi ya miwa, tende, matunda, chipsi, kuku choma, supu ya pweza, ngizi, samaki wa kukaanga na vingine vingi.
Nikaweka kituo kwa muda, nikapata nilichokipata.
Karibuni....
CC: vanmedy
Last edited by a moderator: