Kwa vitendo vilivyokuwa vikifanywa na kile kikosi cha Task Force cha TRA, Je Serikali ilikuwa na tofauti gani na majambazi?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Kwa kweli kwa kila mtu aliyemsikiliza Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akilihutubia Taifa kupitia social media, kuhusu madhira aliyopitia kwa miaka 5 mfululizo ya kunyanyaswa na kuteswa hadi kufungiwa akaunti zake za benki na hicho kinachoitwa Task Force ya TRA, hakika atakuwa amelengwa lengwa na machozi.

Nifahamuvyo Mimi ni kuwa kwa nchi inayoendeshwa kwa utaratibu wa utawala bora unaozingatia Katiba ya nchi, ambayo viongozi walioko madarakani waliapa kuitii, chombo pekee kilichopewa mamlaka hayo ni mhimili wa mahakama.

Ninachijiuliza ilikuwaje viongozi Wa utawala wa awamu ya 5 waamue kuivunja na kuisigina sigina Katiba hiyo ya nchi, waliyoapa kuitii na kuiheshimu?

Hivi hii serikali inawezaje kuendesha mambo yake bila kufuata Katiba ya nchi na taratibu za kisheria na kujifanyia tu mambo yake kienyeji ili mradi tu wameagizwa na yule mwendazake, ambaye ndiye aliyekuwa Mkuu wa mhimili wa Serikali?

Hivi utawezaje kutofautisha vitendo hivyo vya Task Force na vitendo vya majambazi kuwapora mali zao raia wasio na hatia?

Hakika Mungu amelipenda Taifa hili kwa kulinusuru kwa mengi, kwa kumpenda zaidi yeye na kumtwaa mbele za haki, alikodai kuwa atatuma "application" kwa Mungu ili kuomba nafasi ya kiwaongoza malaika.

Kila la kheri huko alikokwenda, tinamuombea kila aina ya baraka ili afanikishe azma yake ya kuwa Mkuu wa malaika.
 
Jamaa alikuwa akiwa kwenye mikutano yake anawaambia TRA kaeni chini na wafanyabiashara muongee nao, wakikutana vichochoroni anawaambia kamatieni hapo hapo msiwaachie.
 
Mungu aliona ni Bora amtoe fala mmoja ili Watu wake wengi waishi vizuri kwa amani na limetimia hilo
 
Jamaa alikuwa akiwa kwenye mikutano yake anawaambia TRA kaeni chini na wafanyabiashara muongee nao, wakikutana vichochoroni anawaambia kamatieni hapo hapo msiwaachie.
Umenikumbusha nilipokuwa JKT Makutupora. Tukiwa makuruta kuna wakati tulilalamikia suala la kulazimishwa kuleta kuni za mtunduru bila kupewa mashoka na mapanga wakati yapo stoo. Nakumbuka afande alitujibu kuwa kuanzia leo mambo hayo ni mwisho wake na akawakemea makamanda mbele yetu kuwa watumie akili siyo mitulinga tu. Baada ya kikao aliwaita makamanda na kunong'ona nao na yeye kuondoka,mara tukaamrishwa - haya nusu saa kila mtu alete vipande 20 vya kuni za mtunduru!!
 
Bila katiba mpya haya yataendelea kushuudiwa
... Katiba ambayo kila mtu atawajibika kwa matendo yake. Huu upuuzi wa kutoshtakiwa kwa "aliyoyafanya akiwa madarakani" ndio umepelekea hadi wajinga wajinga wengine kujiongeza kwenye hiyo list ya kutoshtakiwa ili waendeleze ufirauni wao kwa taifa hili!
 
Kwa kweli kwa kila mtu aliyemsikiliza Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akilihutubia Taifa kupitia social media, kuhusu madhira aliyopitia kwa miaka 5 mfululizo ya kunyanyaswa na kuteswa hadi kufungiwa akaunti zake za benki na hicho kinachoitwa Task Force ya TRA, hakika atakuwa amelengwa lengwa na machozi.

Nifahamuvyo Mimi ni kuwa kwa nchi inayoendeshwa kwa utaratibu wa utawala bora unaozingatia Katiba ya nchi, ambayo viongozi walioko madarakani waliapa kuitii, chombo pekee kilichopewa mamlaka hayo ni mhimili wa mahakama.

Ninachijiuliza ilikuwaje viongozi Wa utawala wa awamu ya 5 waamue kuivunja na kuisigina sigina Katiba hiyo ya nchi, waliyoapa kuitii na kuiheshimu?

Hivi hii serikali inawezaje kuendesha mambo yake bila kufuata Katiba ya nchi na taratibu za kisheria na kujifanyia tu mambo yake kienyeji ili mradi tu wameagizwa na yule mwendazake, ambaye ndiye aliyekuwa Mkuu wa mhimili wa Serikali?

Hivi utawezaje kutofautisha vitendo hivyo vya Task Force na vitendo vya majambazi kuwapora mali zao raia wasio na hatia?

Hakika Mungu amelipenda Taifa hili kwa kulinusuru kwa mengi, kwa kumpenda zaidi yeye na kumtwaa mbele za haki, alikodai kuwa atatuma "application" kwa Mungu ili kuomba nafasi ya kiwaongoza malaika.

Kila la kheri huko alikokwenda, tinamuombea kila aina ya baraka ili afanikishe azma yake ya kuwa Mkuu wa malaika.
Asante sana kwa hili ila ukweli ni kwamba Magufuli hapendwa na Mungu, bali Ghambosh ndiko aliko sasa hivi akitendewa kama misukule mingine.
 
Kwa kweli kwa kila mtu aliyemsikiliza Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akilihutubia Taifa kupitia social media, kuhusu madhira aliyopitia kwa miaka 5 mfululizo ya kunyanyaswa na kuteswa hadi kufungiwa akaunti zake za benki na hicho kinachoitwa Task Force ya TRA, hakika atakuwa amelengwa lengwa na machozi.

Nifahamuvyo Mimi ni kuwa kwa nchi inayoendeshwa kwa utaratibu wa utawala bora unaozingatia Katiba ya nchi, ambayo viongozi walioko madarakani waliapa kuitii, chombo pekee kilichopewa mamlaka hayo ni mhimili wa mahakama.

Ninachijiuliza ilikuwaje viongozi Wa utawala wa awamu ya 5 waamue kuivunja na kuisigina sigina Katiba hiyo ya nchi, waliyoapa kuitii na kuiheshimu?

Hivi hii serikali inawezaje kuendesha mambo yake bila kufuata Katiba ya nchi na taratibu za kisheria na kujifanyia tu mambo yake kienyeji ili mradi tu wameagizwa na yule mwendazake, ambaye ndiye aliyekuwa Mkuu wa mhimili wa Serikali?

Hivi utawezaje kutofautisha vitendo hivyo vya Task Force na vitendo vya majambazi kuwapora mali zao raia wasio na hatia?

Hakika Mungu amelipenda Taifa hili kwa kulinusuru kwa mengi, kwa kumpenda zaidi yeye na kumtwaa mbele za haki, alikodai kuwa atatuma "application" kwa Mungu ili kuomba nafasi ya kiwaongoza malaika.

Kila la kheri huko alikokwenda, tinamuombea kila aina ya baraka ili afanikishe azma yake ya kuwa Mkuu wa malaika.
Huyo marehemu alikuwa jambazi na fisadi mpenda sifa. Alipora hela za watu ili ajenge Chato miradi ya kipuuzii huku alisababisha mateso kwa rais wasio na hatia
 
Mbowe na wa aini yake washauriwe wa muone Mh Rais SSH ambaye kasema hadharani hataki kodi za dhuluma, mabavu na miguvu. Waende na nyaraka zao na amini atawarudishia fedha yao waliodhulumiwa na mwendazake.

Wafanyabiashara wasio wa aminifu wakidhulumu kodi hiyo haina shida. Ila wao wakiambiwa rudisha ulichochukua isivyo halali wanadhulumiwa, wana onewa. Hii ndio Tanzania ya leo.
 
Back
Top Bottom