Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,987
Sasa, kura ya kutokuwa na imani na waziri Mkuu ni nzuri sana kwani inamaanisha kuwa watu hawana imani na serikali yao na moja kwa moja inaonesha kuwa hawana imani na Rais. Huwezi kupiga kura ya kutokuwa na imani na "Waziri Mkuu" halafu ukabakia na imani na Rais. Kwa sababu, hata Waziri Mkuu akiondoka bado utakuwa na rais yule yule na itakuwa ni rekodi tu kuwa mawaziri wakuu "wawili" wameshindwa kufanya kazi. Yawezekana kabisa hoja ikajengwa vizuri kuwa tatizo kubwa ni Rais mwenyewe kama mkuu wa serikali na utumishi wote wa umma nchini. Hivyo, kumwajibisha Waziri Mkuu ni njia moja tu nyuma ya kumwajibisha rais - kwani Rais anaweza kuwajibishwa na bunge kwa mashtaka ya kibunge (impeachment) chini ya Ibara ya 46.
Lakini ukiondoa la kumwondoa rais tatizo kubwa la msingi linakabili utawala wa Tanzania ni CCM. Kumwondoa Waziri Mkuu wa CCM hakutaondoa tatizo la msingi kwani Waziri Mkuu atakayekuja atakuwa ni miongoni mwa wabunge hawa hawa na kwa hakika kabisa atakuwa ni mwana CCM. Sasa, je kumwondoa Pinda na serikali ya sasa na kuingiza serikali nyingine kutakuwa kumetatua tatizo la msingi yaani CCM yenyewe?
Ushahidi uko wazi; baada ya kuondolewa Lowassa na mawaziri wengine aliteuliwa WM mwingine na baraza jingine lakini matokeo yake yamekuwa yale yale. Je, itakuwa ni ajabu sana kufikiria kwamba Pinda akiondoka ataingia Waziri Mkuu mwingine ambaye naye hatoukwa tofauti na hawa wengine kwa sababu na yeye kama waliomtangulia nao ni wana CCM? Au kwa namna moja tunapenda drama ya serikali kuangushwa, na mazingaombwe yote yanayotokana na hilo ili tuweze kusema serikali imeanguka? Vipi kama ikianguka na bado ikaja serikali nyingine?
Binafsi naamini, njia pekee ya kuokoa nchi yetu na hasa utendaji serikalini siyo kuwaacha wana CCM waendelee kuteuliana na kuteuliwa kushika nafasi mbalimbali; njia pekee ni kubadilisha chama tawala. Sasa hapa bila ya shaka ninatofautiana na wengine wengi ambao bado wana matumaini kuwa CCM bado inaweza "kutawala vizuri" kama Waziri Mkuu akiondolewa. Kuondolewa kwa Waziri Mkuu na baraza la sasa itakuwa ni kwa ajili ya kuwawajibisha wao tu kwa yaliyotokea na kwa haki hoja inaweza kutolewa kuwa wanastahili. Lakini, kudhania kuwa hawa wakiondoka tutakuwa tumegusa tatizo la msingi ni kujidanganya.
Kwa kadiri ya kwamba CCM bado iko madarakani basi tatizo la msingi BADO lipo!
Hivyo hoja inayotakiwa kutolewa kwa usahihi kabisa chini ya Ibara ya 90 ya Katiba ni Rais kuamua kuvunja Bunge. Ili hili lifanyike badala ya kutoa hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Azimio la Bunge litolewe kumtaka Rais avunje Bunge ili watu wote warudi madarakani na Chama cha Mapinduzi kitafute ridhaa mpya kwa wananchi! Hoja ya Zitto naikubali kwa asilimia 100 lakini pia naamini haitagusa msingi wa tatizo lenyewe; ningependa viongozi wa upinzani waende mbali zaidi ili wananchi warudi kwenye uchaguzi ndani ya miezi mitatu ijayo!
Faida za kuvunja Bunge:
a. Kila chama kitatengeneza hoja mpya ya kwenda kwa wananchi na kutafura ridhaa yao
b. Kundi la wabunge wachovu wataondolewa na wananchi
c. Wabunge wapya ambao wanakubalika na wananchii watapatikana
d. Rais ajaye atapewa nafasi ya kuunda serikali kutoka katika wabunge wapya
e. Rais mwenyewe naye atatafuta ridhaa na kushindanishwa na wengi
f.
Lakini ukiondoa la kumwondoa rais tatizo kubwa la msingi linakabili utawala wa Tanzania ni CCM. Kumwondoa Waziri Mkuu wa CCM hakutaondoa tatizo la msingi kwani Waziri Mkuu atakayekuja atakuwa ni miongoni mwa wabunge hawa hawa na kwa hakika kabisa atakuwa ni mwana CCM. Sasa, je kumwondoa Pinda na serikali ya sasa na kuingiza serikali nyingine kutakuwa kumetatua tatizo la msingi yaani CCM yenyewe?
Ushahidi uko wazi; baada ya kuondolewa Lowassa na mawaziri wengine aliteuliwa WM mwingine na baraza jingine lakini matokeo yake yamekuwa yale yale. Je, itakuwa ni ajabu sana kufikiria kwamba Pinda akiondoka ataingia Waziri Mkuu mwingine ambaye naye hatoukwa tofauti na hawa wengine kwa sababu na yeye kama waliomtangulia nao ni wana CCM? Au kwa namna moja tunapenda drama ya serikali kuangushwa, na mazingaombwe yote yanayotokana na hilo ili tuweze kusema serikali imeanguka? Vipi kama ikianguka na bado ikaja serikali nyingine?
Binafsi naamini, njia pekee ya kuokoa nchi yetu na hasa utendaji serikalini siyo kuwaacha wana CCM waendelee kuteuliana na kuteuliwa kushika nafasi mbalimbali; njia pekee ni kubadilisha chama tawala. Sasa hapa bila ya shaka ninatofautiana na wengine wengi ambao bado wana matumaini kuwa CCM bado inaweza "kutawala vizuri" kama Waziri Mkuu akiondolewa. Kuondolewa kwa Waziri Mkuu na baraza la sasa itakuwa ni kwa ajili ya kuwawajibisha wao tu kwa yaliyotokea na kwa haki hoja inaweza kutolewa kuwa wanastahili. Lakini, kudhania kuwa hawa wakiondoka tutakuwa tumegusa tatizo la msingi ni kujidanganya.
Kwa kadiri ya kwamba CCM bado iko madarakani basi tatizo la msingi BADO lipo!
Hivyo hoja inayotakiwa kutolewa kwa usahihi kabisa chini ya Ibara ya 90 ya Katiba ni Rais kuamua kuvunja Bunge. Ili hili lifanyike badala ya kutoa hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Azimio la Bunge litolewe kumtaka Rais avunje Bunge ili watu wote warudi madarakani na Chama cha Mapinduzi kitafute ridhaa mpya kwa wananchi! Hoja ya Zitto naikubali kwa asilimia 100 lakini pia naamini haitagusa msingi wa tatizo lenyewe; ningependa viongozi wa upinzani waende mbali zaidi ili wananchi warudi kwenye uchaguzi ndani ya miezi mitatu ijayo!
Faida za kuvunja Bunge:
a. Kila chama kitatengeneza hoja mpya ya kwenda kwa wananchi na kutafura ridhaa yao
b. Kundi la wabunge wachovu wataondolewa na wananchi
c. Wabunge wapya ambao wanakubalika na wananchii watapatikana
d. Rais ajaye atapewa nafasi ya kuunda serikali kutoka katika wabunge wapya
e. Rais mwenyewe naye atatafuta ridhaa na kushindanishwa na wengi
f.