Kwa utaratibu huu hata ajira za Ualimu, Unesi, Uaskari zitatolewa kivyama

maramia

JF-Expert Member
Jul 17, 2015
2,030
1,344
Nina wasi wasi mkubwa suala hili la uteuzi wa viongozi likiachwa likaendelea kama linavyoonekana litaipeleka nchi hii pabaya sana.

Kwa mfano, kuteuliwa kwa maDAS kwa namna walivyoteuliwa ni hatari sana tena zaidi ya hatari, watu wanateuliwa halafu ndiyo vinaitishwa vyeti kuona cv zao, kweli Rais anaweza kuteua watendaji wa serikali kwa kuangalia utendaji wa kisiasa?
Naomba wanasheria wetu waliangalie suala hili kama halikukiuka misingi ya utawala bora au kukiuka katiba?

Nijuavyo mimi ofisi ya DAS ni ya kiutawala zaidi inayosimamia sheria na taratibu za utumishi katika wilaya, kwa hiyo isingefaa wakateuliwa wapiga debe wa chama katika chaguzi kwa kazi kama hiyo, kazi ambayo tangu huko nyuma imekuwa ikihitaji elimu ya utawala ya kiwango cha juu toka toka vyuo kama Mzumbe n.k

Inawezekana huu ni mkakati wa mapema wa mheshimiwa Rais kuanza kujipanga mapema kwa uchaguzi wa 2020 akizingatia msemo wa mwisho wa uchaguzi mmoja ndiyo mwanzo wa uchaguzi mwingine.

Naamini pia kwamba uteuzi huu haukuzingatia uwezo wala tija kwa taifa uliojikita zaidi katika ushabiki wa kichama ambao haukufanywa kisayansi na menejimenti ya utumishi na kama umefanywa ni kwa njia ya shinikizo fulani la chama ili kujipanga.

Hivi kama mambo yatafanywa kwa namna hii hawa wasomi wetu wenye vyeti na taaluma zao za utawala na uongozi lakini wenye itikadi tofauti tofauti za vyama watafanya kazi gani?
Nasema hivyo kwa sababu kwa mujibu wa ufukunyuku wangu maDAS wote walioteuliwa ni makada na wakereketwa wa CCM.

Hali hii inatoa picha kwamba tusipoangalia huko mbele tuendako tunaweza kujikuta hata waalimu, waganga, askari n.k wanaajiriwa kwa vigezo vya uanachama wa vyama vya siasa ili kujihakikishia uhakika wa ushindi katika chaguzi nyingine zijazo.
SIASA NI UJANJA NA USHINDI NI MIKAKATI.
 
Nina wasi wasi mkubwa suala hili la uteuzi wa viongozi likiachwa likaendelea kama linavyoonekana litaipeleka nchi hii pabaya sana.

Kwa mfano, kuteuliwa kwa maDAS kwa namna walivyoteuliwa ni hatari sana tena zaidi ya hatari, watu wanateuliwa halafu ndiyo vinaitishwa vyeti kuona cv zao, kweli Rais anaweza kuteua watendaji wa serikali kwa kuangalia utendaji wa kisiasa?
Naomba wanasheria wetu waliangalie suala hili kama halikukiuka misingi ya utawala bora au kukiuka katiba?

Nijuavyo mimi ofisi ya DAS ni ya kiutawala zaidi inayosimamia sheria na taratibu za utumishi katika wilaya, kwa hiyo isingefaa wakateuliwa wapiga debe wa chama katika chaguzi kwa kazi kama hiyo, kazi ambayo tangu huko nyuma imekuwa ikihitaji elimu ya utawala ya kiwango cha juu toka toka vyuo kama Mzumbe n.k

Inawezekana huu ni mkakati wa mapema wa mheshimiwa Rais kuanza kujipanga mapema kwa uchaguzi wa 2020 akizingatia msemo wa mwisho wa uchaguzi mmoja ndiyo mwanzo wa uchaguzi mwingine.

Naamini pia kwamba uteuzi huu haukuzingatia uwezo wala tija kwa taifa uliojikita zaidi katika ushabiki wa kichama ambao haukufanywa kisayansi na menejimenti ya utumishi na kama umefanywa ni kwa njia ya shinikizo fulani la chama ili kujipanga.

Hivi kama mambo yatafanywa kwa namna hii hawa wasomi wetu wenye vyeti na taaluma zao za utawala na uongozi lakini wenye itikadi tofauti tofauti za vyama watafanya kazi gani?
Nasema hivyo kwa sababu kwa mujibu wa ufukunyuku wangu maDAS wote walioteuliwa ni makada na wakereketwa wa CCM.

Hali hii inatoa picha kwamba tusipoangalia huko mbele tuendako tunaweza kujikuta hata waalimu, waganga, askari n.k wanaajiriwa kwa vigezo vya uanachama wa vyama vya siasa ili kujihakikishia uhakika wa ushindi katika chaguzi nyingine zijazo.
SIASA NI UJANJA NA USHINDI NI MIKAKATI.
Ndio utatolewa ki vyama na wote watakuwa CCM! Mna kingine?
 
Nina wasi wasi mkubwa suala hili la uteuzi wa viongozi likiachwa likaendelea kama linavyoonekana litaipeleka nchi hii pabaya sana.

Kwa mfano, kuteuliwa kwa maDAS kwa namna walivyoteuliwa ni hatari sana tena zaidi ya hatari, watu wanateuliwa halafu ndiyo vinaitishwa vyeti kuona cv zao, kweli Rais anaweza kuteua watendaji wa serikali kwa kuangalia utendaji wa kisiasa?
Naomba wanasheria wetu waliangalie suala hili kama halikukiuka misingi ya utawala bora au kukiuka katiba?

Nijuavyo mimi ofisi ya DAS ni ya kiutawala zaidi inayosimamia sheria na taratibu za utumishi katika wilaya, kwa hiyo isingefaa wakateuliwa wapiga debe wa chama katika chaguzi kwa kazi kama hiyo, kazi ambayo tangu huko nyuma imekuwa ikihitaji elimu ya utawala ya kiwango cha juu toka toka vyuo kama Mzumbe n.k

Inawezekana huu ni mkakati wa mapema wa mheshimiwa Rais kuanza kujipanga mapema kwa uchaguzi wa 2020 akizingatia msemo wa mwisho wa uchaguzi mmoja ndiyo mwanzo wa uchaguzi mwingine.

Naamini pia kwamba uteuzi huu haukuzingatia uwezo wala tija kwa taifa uliojikita zaidi katika ushabiki wa kichama ambao haukufanywa kisayansi na menejimenti ya utumishi na kama umefanywa ni kwa njia ya shinikizo fulani la chama ili kujipanga.

Hivi kama mambo yatafanywa kwa namna hii hawa wasomi wetu wenye vyeti na taaluma zao za utawala na uongozi lakini wenye itikadi tofauti tofauti za vyama watafanya kazi gani?
Nasema hivyo kwa sababu kwa mujibu wa ufukunyuku wangu maDAS wote walioteuliwa ni makada na wakereketwa wa CCM.

Hali hii inatoa picha kwamba tusipoangalia huko mbele tuendako tunaweza kujikuta hata waalimu, waganga, askari n.k wanaajiriwa kwa vigezo vya uanachama wa vyama vya siasa ili kujihakikishia uhakika wa ushindi katika chaguzi nyingine zijazo.
SIASA NI UJANJA NA USHINDI NI MIKAKATI.
Umenikumbusha enzi za chama kimoja ukitaka ajira lazima uwe na kadi ya umoja wa vijana
 
Tunakoelekea msishangae mkasikia uteuzi wa maafisa elimu wa kisiasa kama ilivyokuwa kwenye DAS

Zaid pia naamin tutafika kwenye uteuzi wa mahead master wa kisiasa

Maana sasa lazima tulipe fadhira
Mambo haya siyo ya kawaida na nafikiri limefanyika ili mkubwa aweke watu wake serikalini.Haiwezekani nafasi ambayo inahitaji watu waliosomea lakini pia wawe na uzoefu mkubwa wa kiutendaji serikalini lakini leo hii mtu anaamua kuweka watu wake kwa kisingizio cha kuirekebisha Nchi. kinacho nishangaza mimi nikuona hata marais wastaafu wanamwangalia tu afanye atakavyo, kwanini hawamwambii hapa sasa umekosea! mwisho wa udikiteta ni dhiki kuu kwa kila mtu! sitashangaa kuona hata nafasi zingine za kiutumishi atafanya uteuzi yeye.Watanzania lazima tusimame na tuseme hapana inatosha.
 
Kasungura kenyewe kadogo, kwahiyo hawa wapigania matumbo kama akina #Lizabon & Co' tutawatupia huko kwenye wizara za elimu na afya.
 
Ndio utatolewa ki vyama na wote watakuwa CCM! Mna kingine?
Mimi huwa siwashangai watu kama nyie kwasababu hata Hitller alikuwa nao, musolin alikuwa nao,Idd Amini alikuwa nao, wapambe nyie ni hatari kuliko mshika madaraka! mpo tayari kumwambia watoto wote wanao zaliwa sasa wanaitwa jina lake.Ninyi mnataka pesa tu basi. hamfikiri kingine chochote
 
Mi mtoa mada ni mwanachama wa CCM na kabla nilikuwa mwanaTANU tangu 1976 yeyote asidhani mimi ni mwanachama wa chama chochote cha upinzani, kwa hiyo nisishambuliwe kwa mtazamo kwamba nimeandika kwa chuki kuishambulia serikali kama mpinzani.

Lakini watanzania wenzangu, kama kuna anayedhani utaratibu huu wa kulimbikiza ajira kwenye mgongo wa chama kimoja utazaa matunda mazuri atakuwa anakosea sana tena sana si kidogo, mkuu wa nchi hawezi kugeuza ajira za kitaalamu kuwa za kisiasa na bado tukafikiri anatuweka nchi kwenye hali ya matumaini chanya.

Mifano iko mingi, aslani hakuna mtawala aliyetumia mtindo huu akafanikiwa, sijui serikali yetu imeuiga kutoka wapi huu.
Marais kama Saddam wa Iraq, Nicolae Ceassescou wa iliyokuwa Romania, Mobutu wa Zaire na wengine walioujaribu mtindo huu hakuna aliyefanikiwa ila walijenga chuki kubwa miongoni mwa wananchi, maana hii haitofautiani sana na udini.
YANGU MACHO!
 
Haya ni moja kati ya matukio mengi ya hovyo hovyo ambayo yatatokea...
Unapo kua na washauri toka nchi jirani unategemea nini!?!?
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom