Kwa upinzani huu, wale 80% waliokataa mfumo wa vyama vingi walikuwa sahihi?

Martin George

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,695
1,470
Kwa namna upinzani unavyoenenda hapa Tanzania inatia shaka kama wale wananchi 20% waliutaka upinzani was sina hii. Yaani upinzani wamekosa uzalendo kabisa, wamekuwa waropokaji kiasi cha kuweza kumsaidia adui kitaarifa bila kujijua. Kwakweli upinzani aina ya huu wa akina Chadema ktk issue ya makanikia haukubaliki kabisa, tushindane kwa hoja na si kwa kwa kuliangamiza taifa!
 
Kwa namna upinzani unavyoenenda hapa Tanzania inatia shaka kama wale wananchi 20% waliutaka upinzani was sina hii. Yaani upinzani wamekosa uzalendo kabisa, wamekuwa waropokaji kiasi cha kuweza kumsaidia adui kitaarifa bila kujijua. Kwakweli upinzani aina ya huu wa akina Chadema ktk issue ya makanikia haukubaliki kabisa, tushindane kwa hoja na si kwa kwa kuliangamiza taifa!
Walioliangamiza taifa kwa kuligawa kwa wawekezaji bure na kutunga sheria mbovu za uwekezaji ni Chadema au CCM?!

Unajitoa ufahamu wewe na haikusaidii kitu, huyo unaemwona mzalendo amekuemo kwenye baraza la Mawaziri kipindi chote cha kuwapa wawekezaji madini na mafuta & Gas bure , je alitoa mchango gani?!
 
Walioliangamiza taifa kwa kuligawa kwa wawekezaji bure na kutunga sheria mbovu za uwekezaji ni Chadema au CCM?!

Unajitoa ufahamu wewe na haikusaidii kitu, huyo unaemwona mzalendo amekuemo kwenye baraza la Mawaziri kipindi chote cha kuwapa wawekezaji madini na mafuta & Gas bure , je alitoa mchango gani?!
Kwa zama za Leo Magufuli ni mzalendo namba 1 hapa Tanzania, hutaki kaa pembeni!
 
nadhani hata chama tawala tulichokitaka kiendelee kubaki ni cha namna hii kamwe. unafiki mtupu
 
Siku acacia wakideposit trillion 108 pale BOT tunawafuta chadema!
Mbaya zaidi unajitoa fahamu wakati ccm wanamfukuza zitto kuhusu hiyo mikataba unajifanya hujui na unaona wakifanya kitu sahihi!

unafiki huu watanzania sijui tutaacha lini!
 
Siku acacia wakideposit trillion 108 pale BOT tunawafuta chadema!
Mbaya zaidi unajitoa fahamu wakati ccm wanamfukuza zitto kuhusu hiyo mikataba unajifanya hujui na unaona wakifanya kitu sahihi!

unafiki huu watanzania sijui tutaacha lini!
Hivi kwanini mnalinganisha mapato ya madini,faida na kodi iliyokwepwa? hapa ndipo mnathibitisha ujinga wenu, hiyo trilioni 108 ni thamani ya madini na si faida wala kodi. Jitahidi kusikiliza uelewe na si kujibu.
 
Hivi kwanini mnalinganisha mapato ya madini,faida na kodi iliyokwepwa? hapa ndipo mnathibitisha ujinga wenu, hiyo trilioni 108 ni thamani ya madini na si faida wala kodi. Jitahidi kusikiliza uelewe na si kujibu.
Kasome Yale mambo ambayo kamati ya prof.osoro ilitumwa kutafuta! Halafu urudi hapa!
Sio kuleta ujuaji wako uchwara hapa
 
Hivi kwanini mnalinganisha mapato ya madini,faida na kodi iliyokwepwa? hapa ndipo mnathibitisha ujinga wenu, hiyo trilioni 108 ni thamani ya madini na si faida wala kodi. Jitahidi kusikiliza uelewe na si kujibu.
Wengi wa wanaharakati wa CHADEMA wanajua trilioni 108 ndio tunawadai ACACIA. Bora unavyowapa darasa mkuu
 
Lengo kuu la vyama vingi ni kuruhusu mawazo mbadala katika kuongoza nchi. Badala yake limezaliwa janga kubwa la "divisions". Sasa vyama vinafanya maamuzi hata kama ni upuuzi kwa maslahi ya vyama vyao. Mfano ni hili la mikataba mibovu na hili wengine kutetea maslahi ya wazungu bila hata aibu. Matokeo yake kizazi cha sasa hakielewi lipi la vyama, lipi la serikali na lipi ni la kitaifa.

Ndio maana kuna baadhi ya nchi hata wazo lako binafsi kama liko tofauti na msimamo wa nchi ni kosa.
Mfano: Ni kosa kisheria kutoamini Holocaust haikutokea (Mauaji ya kimbari ya wayahudi) nchini Israel na baadhi ya nchi Ulaya kama Austria, Hungary, Romania and so on.

Inaweza isieleweke ila kwa wenzetu utaifa hauna mjadala wa kijinga. Na hili ndio matumizi mabaya ya vyama vingi.
 
Lengo kuu la vyama vingi ni kuruhusu mawazo mbadala katika kuongoza nchi. Badala yake limezaliwa janga kubwa la "divisions". Sasa vyama vinafanya maamuzi hata kama ni upuuzi kwa maslahi ya vyama vyao. Mfano ni hili la mikataba mibovu na hili wengine kutetea maslahi ya wazungu bila hata aibu. Matokeo yake kizazi cha sasa hakielewi lipi la vyama, lipi la serikali na lipi ni la kitaifa.

Ndio maana kuna baadhi ya nchi hata wazo lako binafsi kama liko tofauti na msimamo wa nchi ni kosa.
Mfano: Ni kosa kisheria kutoamini Holocaust haikutokea (Mauaji ya kimbari ya wayahudi) nchini Israel na baadhi ya nchi Ulaya kama Austria, Hungary, Romania and so on.

Inaweza isieleweke ila kwa wenzetu utaifa hauna mjadala wa kijinga. Na hili ndio matumizi mabaya ya vyama vingi.
Mkuu umenena vema kabisa!
 
Kwa namna upinzani unavyoenenda hapa Tanzania inatia shaka kama wale wananchi 20% waliutaka upinzani was sina hii. Yaani upinzani wamekosa uzalendo kabisa, wamekuwa waropokaji kiasi cha kuweza kumsaidia adui kitaarifa bila kujijua. Kwakweli upinzani aina ya huu wa akina Chadema ktk issue ya makanikia haukubaliki kabisa, tushindane kwa hoja na si kwa kwa kuliangamiza taifa!

Wapinzani wamekosa uzalendo, lakini nani wenye uzalendo??? Waliopitisha na kusaini mikataba mibovu ndio wanakuwaga wazalendo kwako? Mkuu, what has gotten into your head, and where is your common sense???
 
Back
Top Bottom