Kwa uozo huu, hakuna budi tuchague lugha moja ya kufundishia

Kulupango

JF-Expert Member
Mar 19, 2020
288
534
Dogo yuko fm1 shule zetu za kata. Jana nikawa nambananisha maswali ya hapa na pale ya fm 1, kichwani hamna kitu.

Basi nikamwambia anitajie majina ya Topics za hesabu, akataja topic 1 tu inaitwa Real number. Nikamwambia taja topics za History, akataja Chimpanzee, taja topics za chemi hajaweza hata 1, taja topics za geography kataja Earth, taja topics za English kataja tenses, taja topics za physics kataja Matter. Kwa kweli nikachoka.

Baada ya hayo majibu nikaishiwa pose, huu ni mwezi wa 10 na anasema wameshamaliza kusoma topic zote za masomo yote, wamebakisha topic moja au mbili mbili kwa baadhi ya masomo. Masomo mengine wamemaliza kabisa.

Nikamuuliza dogo shida ni nini hadi unakuwa hivi? Akajibu hajui kiingereza, nikamuuliza somo gani wewe unaliweza vizuri akajibu kiswahili, nikamuuliza Nomino ni nini? akajibu Nomino ni maneno ambayo ni majina ya watu, vitu na hali, pia kajibu Nomino ni aina ya neno linalotaja jina la kitu, mahali, mnyama, mtu, sifa au wazo. Nika muuliza kuna aina ngapi za Nomino akajibu Kuna nomino za kawaida na nomino za kipekee, nikamuuliza taja topics za kiswahili akazitaja.

Nikaona isiwe shida huwenda huyu ni kichwa maji kwa hayo masomo mengine, kesho yake nikaenda shuleni kwao. Nikatulia sehemu pembeni karibu na wauza visheti, muda wa break nikawa natafuta vijana wa fm1. Nikawapata kama 10 hivi,

Nikawauliza maswali yale yale katika masomo yao, wote 10 hawakuweza, nikawaambia wanitajie majina ya topics za kila somo.

Kwakweli ni msiba, wale madogo 10 hakuna aliyeweza kutaja topic zaidi ya tatu. Nikawauliza shida ni nini, wakajibu shida ni kiingereza.

Maana tunakariri kiingereza bila kuelewa masomo. Kwa hiyo tunakuwa tunasahau sana kwasababu masomo ya kiingereza ni mengi.

Kesho yake nikaja tena pale shuleni, nikafanikiwa kuzungumza na vijana 20 wa form1. Majibu yakawa ni yale yale, maswali hawakuweza kujibu kiusaha, majina ya topics hawakuweza kunitajia zaidi ya topic tano kwa kila somo, lakini somo la kiswahili kila mtu yuko vizuri.

Sasa, siku ya 3 nikarudi tena pale shuleni, maana dogo nilimuuliza ni nani anatokaga wa kwanza form1. Akanitajia jina lake, nikaenda shule nikamtafuta nikampata.

Ndugu zangu inasikitisha sana kwa kweli, huyu dogo nikamuuliza maswali akawa anayajibu vizuri tu, maswali mbalimbali ya form1 akawa anayajibu safi kabisa, nikamuuliza majina ya topics akataja topics zote za masomo yote ambazo wameshafundishwa.

Nikamuuliza nipe siri ya mafanikio yako mpaka kuwazidi wenzako, akajibu ni juhudi tu na kumuomba MUNGU, nikamuuliza kwani wewe unadhania hawa wenzako wote karibu miatatu wao hawamuombi MUNGU na kufanya juhudi?

Dogo akajibu, Shida wengi wao ni tofauti na mimi, mimi nilisoma English medium shule ya msingi, kwa hiyo masomo ni kama nina yarudia yale yale ya shule ya msingi hakuna utofauti mkubwa.

Nikamuuliza kwanini hukwenda private secondary,? Akajibu kwasababu napenda kusoma shule niliyochaguliwa na serekali.

Sasa ombi langu, naona bora kubadili lugha iwe kiingireza tangu wakiwa shule ya msingi au waendelee kusoma kwa kiswahili hadi secondary, yamkini tunapoteza vipaji vingi sana kwa kigezo cha lugha.

523896_155214338014928_1544258310_n.jpg
HIV NDVYO WATOTO WA SHULE ZA KATA WANAVYOSISITZWA KUJFUNZA KIINGREZA, JAPO BADO NI TATZO :
AU serekali iweke mwaka mzima kwa watoto kujifunza lugha wanapotoka Darasa la 7, Kabla ya kuanza masomo ya kidato cha kwanza.
 
"Sisi watoto wa shule za kata sio kwamba hatupendi kuongea hio lugha ya kigeni, la hasha!

changamoto tunazopitia ni nyingi sana katika elimu, tunafundishwa kwa kiswahili kwa muda mrefu, kiingereza ni somo tu kati ya masomo 9.

Wengine kuna mashule tunafundishwa hadi kwa lugha zetu za makabila, mfano huku usukumani hata kiswahili hatukijui. Unadhani tutakiweza kiingeleza?

Kama serikali inataka na sisi tuwe washindani na tuelewe kiingeleza vizuri, basi ipige chini kiswahili toka chekechea mpaka darasa la saba, Kisw. Kiwe somo la kawaida. Utaona tutakavyowaka!

hatupendi kuwa hivi tulivyo"

Nawasilisha
 
Hii mijadara ya lugha imeisha zungumziwa sana ila ufumbuzi ndio hvyo tena haujulikani
 
Walimu wenyewe huwa wanaunganisha topics. Kagua madaftari ya wanafunzi uone jinsi wanavyoandika notes.

Mwenyewe nilimaliza form 4 nikiwa sijui kitu hiki na kile vinapatikana kwenye topics zipi, ila mwisho wa siku nilifaulu.
 
Nakupongeza sana mkuu kwa kufanya hiyo research na kupata majibu sahihi pasipo kumuonea huyo dogo.... haya ndio mambo ambayo wooooote kila mahala tuyapazie sauti kuanzia JF, Inst, Facebook, whatsap huko kwenye manyimbo ya Bongo flavor koote tupige makelele....wazazi mashuleni, mitaani kote tupaze sauti ili kufanyike mabadiriko kwenye mfumo wa elimu...

Mpaka sasa mfumo wa elimu ni mbovu, halafu huo huo mbovu umeelemewa, walimu wachache, wanafunzi wengi, madarasa machache, vitabu hakuna, nk...
 
Dogo yuko fm1 shule zetu za kata. Jana nikawa nambananisha maswali ya hapa na pale ya fm 1, kichwani hamna kitu.

Basi nikamwambia anitajie majina ya Topics za hesabu, akataja topic 1 tu inaitwa Real number. Nikamwambia taja topics za History, akataja Chimpanzee, taja topics za chemi hajaweza hata 1, taja topics za geography kataja Earth, taja topics za English kataja tenses, taja topics za physics kataja Matter. Kwa kweli nikachoka.

Baada ya hayo majibu nikaishiwa pose, huu ni mwezi wa 10 na anasema wameshamaliza kusoma topic zote za masomo yote, wamebakisha topic moja au mbili mbili kwa baadhi ya masomo. Masomo mengine wamemaliza kabisa.

Nikamuuliza dogo shida ni nini hadi unakuwa hivi? Akajibu hajui kiingereza, nikamuuliza somo gani wewe unaliweza vizuri akajibu kiswahili, nikamuuliza Nomino ni nini? akajibu Nomino ni maneno ambayo ni majina ya watu, vitu na hali, pia kajibu Nomino ni aina ya neno linalotaja jina la kitu, mahali, mnyama, mtu, sifa au wazo. Nika muuliza kuna aina ngapi za Nomino akajibu Kuna nomino za kawaida na nomino za kipekee, nikamuuliza taja topics za kiswahili akazitaja.

Nikaona isiwe shida huwenda huyu ni kichwa maji kwa hayo masomo mengine, kesho yake nikaenda shuleni kwao. Nikatulia sehemu pembeni karibu na wauza visheti, muda wa break nikawa natafuta vijana wa fm1. Nikawapata kama 10 hivi,

Nikawauliza maswali yale yale katika masomo yao, wote 10 hawakuweza, nikawaambia wanitajie majina ya topics za kila somo.

Kwakweli ni msiba, wale madogo 10 hakuna aliyeweza kutaja topic zaidi ya tatu. Nikawauliza shida ni nini, wakajibu shida ni kiingereza.

Maana tunakariri kiingereza bila kuelewa masomo. Kwa hiyo tunakuwa tunasahau sana kwasababu masomo ya kiingereza ni mengi.

Kesho yake nikaja tena pale shuleni, nikafanikiwa kuzungumza na vijana 20 wa form1. Majibu yakawa ni yale yale, maswali hawakuweza kujibu kiusaha, majina ya topics hawakuweza kunitajia zaidi ya topic tano kwa kila somo, lakini somo la kiswahili kila mtu yuko vizuri.

Sasa, siku ya 3 nikarudi tena pale shuleni, maana dogo nilimuuliza ni nani anatokaga wa kwanza form1. Akanitajia jina lake, nikaenda shule nikamtafuta nikampata.

Ndugu zangu inasikitisha sana kwa kweli, huyu dogo nikamuuliza maswali akawa anayajibu vizuri tu, maswali mbalimbali ya form1 akawa anayajibu safi kabisa, nikamuuliza majina ya topics akataja topics zote za masomo yote ambazo wameshafundishwa.

Nikamuuliza nipe siri ya mafanikio yako mpaka kuwazidi wenzako, akajibu ni juhudi tu na kumuomba MUNGU, nikamuuliza kwani wewe unadhania hawa wenzako wote karibu miatatu wao hawamuombi MUNGU na kufanya juhudi?

Dogo akajibu, Shida wengi wao ni tofauti na mimi, mimi nilisoma English medium shule ya msingi, kwa hiyo masomo ni kama nina yarudia yale yale ya shule ya msingi hakuna utofauti mkubwa.

Nikamuuliza kwanini hukwenda private secondary,? Akajibu kwasababu napenda kusoma shule niliyochaguliwa na serekali.

Sasa ombi langu, naona bora kubadili lugha iwe kiingireza tangu wakiwa shule ya msingi au waendelee kusoma kwa kiswahili hadi secondary, yamkini tunapoteza vipaji vingi sana kwa kigezo cha lugha.

HIV NDVYO WATOTO WA SHULE ZA KATA WANAVYOSISITZWA KUJFUNZA KIINGREZA, JAPO BADO NI TATZO :
AU serekali iweke mwaka mzima kwa watoto kujifunza lugha wanapotoka Darasa la 7, Kabla ya kuanza masomo ya kidato cha kwanza.
Inauma sana,imenikumbusha nilipoanza form 1,Mwalimu anafundisha,akiuliza maswali,wote kimya,waliokuwa wanajibu ni vijana waliotoka shule za mpakani Uganda,maana huko kizungu tu,
Ikabidi masomo yasitishwe tupigwe kozi ya kizungu kwa wiki 6,ilitusaidia sana.
Hapa kwetu tunatumia kizungu kila Idara,lazima tujifunze kizungu,
Wachina nyanja zote za maisha ni kichina,vitabu,shule,viwanda,wanatumia lugha yao,kizungu wanajifunza tu kama nyenzo ya kuuzia bidhaa zao.
 
Sasa mtoto unamuuliza akutajie topics za masomo kwani yeye ni mwalimu? Mtoto afundishwa contents za topic husika na ndizo utahiniwa kwazo. Hii ni sawasawa na kumfuata muumini wa dhehebu la kikristo akutajie vitabu vya agano jipya baada ya kumwambia ukwambie ujumbe uliopata katika agano jipya. Mbona kwenye Kiswahili, umehoji maudhuhi ya mada husika. Usitake kuhalalisha Kiswahili, kwa mbinu haramu, za kukinanga Kiingereza. Hiyo haikubaliki kwa mwanataaluma yeyoyote aliye makini.
 
Back
Top Bottom