Kwa uongo huu unaosambaza Zitto Kabwe dhidi ya Rais, hakika inadhihirisha kuwa umetekwa na Mafisadi

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Kwanza nioneshe masikitiko yangu kwa kijana mwenzetu, Zitto Kabwe ambaye hapo awali tulimuamini kwa kujenga hoja madhubuti kwenye mapambano dhidi ya ufisadi. Hakika mara kadhaa Zitto Kabwe aliibuka shujaa na hoja zake zilikuwa na mashiko.

Ila kwa sasa sijaelewa nini kimemkumba ndugu Zitto Kabwe. Kwa sasa amegeuka kuwa mtetezi wa Ufisadi na Mafisadi. Nimejiuliza sana nini kinaendelea nyuma ya pazia.

Awali alizusha kuwa Ndege Mpya zilizonunuliwa na Serikali kwa ajili ya ATCL ni Mtumba kutoka shirika la Ndege la Kazakhstan. Tena Zitto akaenda mbali kwa kusema kuwa ndege hizo zilipaswa kununuliwa kwa dola za kimarekani milioni 9 kwa kila moja lakini Serikali imenunua kwa Dola milioni 61. Waandishi wa habari waliopata fursa ya kujionea ndege ya kwanza iliyowasili hakika wamestaajabu sana baada ya kubaini kuwa Zitto Kabwe kasema uongo. Baadhi ya waandishi ambao nilikuwa nao karibu wamehoji sababu hasa ya Zitto Kabwe kutunga uongo ule.

Leo amekuja na kihoja kingine kuwa eti Habinder Seth, mmiliki wa IPTL aligharamia mkutano wa CCM uliomchagua Rais Magufuli kuwa Mwenyekiti wa chama hicho na ndio maana Rais hachukui hatua dhidi yake. Lengo la Zitto Kabwe kutunga uongo huu ni kumpaka matope Rais na kumhusisha na matendo ya kifisadi ambayo hana.

Hapa ndipo ninapokumbuka maneno ya Zitto Kabwe kuwa Usimwamini Mwanasiasa. Kwa hili nimemdharau sana Zitto Kabwe
 
Kama kutetea maslahi ya Taifa hila hasa wizi wa fedha za Escro ni Kutetea ufisadi acha iwe,Kama kupigania demokrasia iliyobakwa na kikundi chenye maslahi yao binafsi ni kutetea Ufisadi acha iwe. ZZK usivunjwe moyo na mifisadi kama hili lililoandika huu ujinga.
 
Kwanza yani mi hata niviite vindege kwanza vya hovyo mi nashangaa kuona baadhi ya watanzania eti wanafurahia hizo ndege mbili duh! Kweli huu ni msiba Atleast kwa sasa tungekuwa na ndege 20, Hivi kweli Nchi yetu ina ndege mbili jaman hebu tuweni serious kwanza hata mataifa ya wenzatu wanashangaa kwa Nchi kama hii
 
Si mlimshangilia Zitto na ACT yake mkijua wako upande wenu. Sasa ndo mtajua rangi halisi ya Zitto. Atamshambulia baba Jesca mpaka aombe po. Mtajuta kuwafahamu Waha wa Kigoma. Mimi binafsi namwamini Zitto kwamba Magufuli katuletea mtumba toka Kazakhstan na sio brand new toka Canada.
 
Upinzan wa tz hovyo tu, kwanini wasfate mbinu aluowaambia prof mkumbo?wabafl namna ya kufanya siasa hii ya sahz n ya zaman na haiwez kuzaa matunda
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Kwanza nioneshe masikitiko yangu kwa kijana mwenzetu, Zitto Kabwe ambaye hapo awali tulimuamini kwa kujenga hoja madhubuti kwenye mapambano dhidi ya ufisadi. Hakika mara kadhaa Zitto Kabwe aliibuka shujaa na hoja zake zilikuwa na mashiko.

Ila kwa sasa sijaelewa nini kimemkumba ndugu Zitto Kabwe. Kwa sasa amegeuka kuwa mtetezi wa Ufisadi na Mafisadi. Nimejiuliza sana nini kinaendelea nyuma ya pazia.

Awali alizusha kuwa Ndege Mpya zilizonunuliwa na Serikali kwa ajili ya ATCL ni Mtumba kutoka shirika la Ndege la Kazakhstan. Tena Zitto akaenda mbali kwa kusema kuwa ndege hizo zilipaswa kununuliwa kwa dola za kimarekani milioni 9 kwa kila moja lakini Serikali imenunua kwa Dola milioni 61. Waandishi wa habari waliopata fursa ya kujionea ndege ya kwanza iliyowasili hakika wamestaajabu sana baada ya kubaini kuwa Zitto Kabwe kasema uongo. Baadhi ya waandishi ambao nilikuwa nao karibu wamehoji sababu hasa ya Zitto Kabwe kutunga uongo ule.

Leo amekuja na kihoja kingine kuwa eti Habinder Seth, mmiliki wa IPTL aligharamia mkutano wa CCM uliomchagua Rais Magufuli kuwa Mwenyekiti wa chama hicho na ndio maana Rais hachukui hatua dhidi yake. Lengo la Zitto Kabwe kutunga uongo huu ni kumpaka matope Rais na kumhusisha na matendo ya kifisadi ambayo hana.

Hapa ndipo ninapokumbuka maneno ya Zitto Kabwe kuwa Usimwamini Mwanasiasa. Kwa hili nimemdharau sana Zitto Kabwe

Nonsense, waandishi hawakuziona. Acha kudanganya, kusema uongo ni dhambi
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Kwanza nioneshe masikitiko yangu kwa kijana mwenzetu, Zitto Kabwe ambaye hapo awali tulimuamini kwa kujenga hoja madhubuti kwenye mapambano dhidi ya ufisadi. Hakika mara kadhaa Zitto Kabwe aliibuka shujaa na hoja zake zilikuwa na mashiko.

Ila kwa sasa sijaelewa nini kimemkumba ndugu Zitto Kabwe. Kwa sasa amegeuka kuwa mtetezi wa Ufisadi na Mafisadi. Nimejiuliza sana nini kinaendelea nyuma ya pazia.

Awali alizusha kuwa Ndege Mpya zilizonunuliwa na Serikali kwa ajili ya ATCL ni Mtumba kutoka shirika la Ndege la Kazakhstan. Tena Zitto akaenda mbali kwa kusema kuwa ndege hizo zilipaswa kununuliwa kwa dola za kimarekani milioni 9 kwa kila moja lakini Serikali imenunua kwa Dola milioni 61. Waandishi wa habari waliopata fursa ya kujionea ndege ya kwanza iliyowasili hakika wamestaajabu sana baada ya kubaini kuwa Zitto Kabwe kasema uongo. Baadhi ya waandishi ambao nilikuwa nao karibu wamehoji sababu hasa ya Zitto Kabwe kutunga uongo ule.

Leo amekuja na kihoja kingine kuwa eti Habinder Seth, mmiliki wa IPTL aligharamia mkutano wa CCM uliomchagua Rais Magufuli kuwa Mwenyekiti wa chama hicho na ndio maana Rais hachukui hatua dhidi yake. Lengo la Zitto Kabwe kutunga uongo huu ni kumpaka matope Rais na kumhusisha na matendo ya kifisadi ambayo hana.

Hapa ndipo ninapokumbuka maneno ya Zitto Kabwe kuwa Usimwamini Mwanasiasa. Kwa hili nimemdharau sana Zitto Kabwe
Wengine bado tunasubiri majina ya walioficha fedha Uswis!!
 
Oposition tunawapenda sana ila kwa sasa kila tawi wanaloparamia linakatika.Tutamuomba baadae aje kuthibitisha. Heko kwa mh Magu kukaa kimya
Sijapata kuona Oposition wanakuwa kwenye wakati mgumu kama utawala huu wa Magufuli. Hakika kawashika kwenye nyeti
 
Binafsi nilivyo ona ile habari ya Ndege eti si mpya imetoka kwa Zitto niliamini kuna kiwanda cha uongo kilikuwa kazini, jina la Zitto labda linatumika tu ila ujumbe si wake. Nashangaa mpaka sasa sijaona habari ya kanusho toka kwa Zitto kukana habari ile.

Inasikitisha sana kuona vijana wachache wa upinzani wenye bongo zilizo vizuri wakipotea kijinga hivi. Matamko ya upotoshaji wa maksudi kutoka kwa Zitto yanazidi kuongezeka kila kukicha, tuliona post ya Zitto kuhusu VAT kwenye miamala ya kibenki, akaja na post ya Ndege zilizonunuliwa si mpya sasa ni hii ya singa singa, uaminifu ni kitu chenye thamani kubwa Zitto.
 
Hauna jipya wala sio mzalendo.
Kazi kutetea tuu ccm kila kukicha ata wakikuchukulia mke utatea tuu.
Punguza njaa.
Mambo mengi ya msingi huwa hujadili unakujaga na vihoja vya umbea umbea.
Zito kawakamata kooni unasema katumwa na ma fisadi. Siuseme katumwa na ccm. Unaweza kutenganisha ufisadi na ccm?

Ufisadi na ccm ni sawa uunganishe moto ya mishumaa miwili utoke moto mmoja.
 
Back
Top Bottom