GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,544
- 108,871
Mtakaonichukia kwa Hoja yangu hii nichukieni tu ila nitabaki kuwa Mkweli daima na Unafiki Kwangu GENTAMYCINE ni Mwiko. Leo kila Mwafrika anajifanya Kulalamika na Kulaani ' Mauwaji ' ya Mmarekani Mweusi George Floyd yaliyofanywa na Askari Mzungu wa Kimarekani kwa ' Ubishi ' wa Kujitakia wa huyu Mwafrika Mwenzetu wakati huku Kwetu Afrika ' tunauwana ' zaidi ya yaliyomkuta Yeye.
Waafrika ( ukiniondoa Mimi tu GENTAMYCINE ) labda na Watu wachache baadhi ni ' Wanafiki ' hakuna mfano linapokuja Suala la ama Ubaguzi au Mauwaji anayofanyiwa Mwafrika Mwenzetu wakati kama kuna Watu ambao tunauwana na kubaguana Sisi kwa Sisi basi ni Waafrika ila Wazungu wakitufundisha kuwa ' Civilized ' and ' to obey the rule of law ' tunawaona ' Wanatuchukia ' ile mbaya.
Hivi bila ' Unafiki ' na ' Chuki ' za Waafrika kama akina Joseph Kasavubu na ' Mpuuzi ' Mwenzie Mobutu Seseseko Afrika ingempoteza ' Jembe ' kama Hayati Patrice Emery Lumumba ambaye ' Kiuhalisia ' ndiyo inasemaka alikuwa Kiongozi wa Afrika aliyekuwa akiwapenda Kidhati kabisa Waafrika ambao hao hao baadae ndiyo walikuwa kufanya ' Collaboration ' na Wazungu na Kumuua?
Siungi mkono kabisa na kilichofanywa na Askari Mzungu wa Kimarekani ila sitaki pia Kuunga mkono ' Unafiki ' uliopitiliza wa Sisi Waafrika wa Kujifanya eti ' tumeumia ' na ' kuguswa ' kivile na Kifo chake wakati huku huku Afrika wengine tunawauwa Wazazi wetu, Ndugu zetu, Wanetu na hata Kuwatoa Kafara na Kuwachuna Ngozi Wenzetu ili ' tutajirike ' hasa Kimaisha na tutambe.
Hivi huyu Marehemu George Floyd angetii ' Amri ' ya wale Mapolisi ihusuyo mazingira halisi ya nyakati hizi za Janga hili baya na hatari la CORONA yangemkuta yaliyomkuta? Na wengi ' tumeshadadia ' tu Kusikitika kwa ' Kuuwawa ' Kwake lakini tumesahau kuwa hata Yeye pia kabla ya ' Kubinywa ' vile Sakafuni hadi akarudisha Chenji Mbinguni nae ' aliwatusi ' sana tu Askari wale.
Mpaka leo sijaona Serikali ya Tanzania yenyewe kama yenyewe ' ikilaani ' hiki Kitendo na naipongeza kwa hilo. Na kama Waafrika tumepata ' Uchungu ' nalo sana basi hii iwe ni sehemu yetu ya Kuanzia ya Sisi ' Kutojipendekeza ' kabisa kuhangaika kwenda Kwao huko ' Mamtoni ' na badala yake Waafrika wote tubaki ' Makwetu ' na tuzitengeneze nchi zetu ziwe nzuri kama za Marekani / Ulaya.
Sijajua kama Marehemu George Floyd ameshazikwa au bado ila kama tayari Kazikwa namuombea tu Makazi mema na mapya huko aendako Ahera!
Waafrika ( ukiniondoa Mimi tu GENTAMYCINE ) labda na Watu wachache baadhi ni ' Wanafiki ' hakuna mfano linapokuja Suala la ama Ubaguzi au Mauwaji anayofanyiwa Mwafrika Mwenzetu wakati kama kuna Watu ambao tunauwana na kubaguana Sisi kwa Sisi basi ni Waafrika ila Wazungu wakitufundisha kuwa ' Civilized ' and ' to obey the rule of law ' tunawaona ' Wanatuchukia ' ile mbaya.
Hivi bila ' Unafiki ' na ' Chuki ' za Waafrika kama akina Joseph Kasavubu na ' Mpuuzi ' Mwenzie Mobutu Seseseko Afrika ingempoteza ' Jembe ' kama Hayati Patrice Emery Lumumba ambaye ' Kiuhalisia ' ndiyo inasemaka alikuwa Kiongozi wa Afrika aliyekuwa akiwapenda Kidhati kabisa Waafrika ambao hao hao baadae ndiyo walikuwa kufanya ' Collaboration ' na Wazungu na Kumuua?
Siungi mkono kabisa na kilichofanywa na Askari Mzungu wa Kimarekani ila sitaki pia Kuunga mkono ' Unafiki ' uliopitiliza wa Sisi Waafrika wa Kujifanya eti ' tumeumia ' na ' kuguswa ' kivile na Kifo chake wakati huku huku Afrika wengine tunawauwa Wazazi wetu, Ndugu zetu, Wanetu na hata Kuwatoa Kafara na Kuwachuna Ngozi Wenzetu ili ' tutajirike ' hasa Kimaisha na tutambe.
Hivi huyu Marehemu George Floyd angetii ' Amri ' ya wale Mapolisi ihusuyo mazingira halisi ya nyakati hizi za Janga hili baya na hatari la CORONA yangemkuta yaliyomkuta? Na wengi ' tumeshadadia ' tu Kusikitika kwa ' Kuuwawa ' Kwake lakini tumesahau kuwa hata Yeye pia kabla ya ' Kubinywa ' vile Sakafuni hadi akarudisha Chenji Mbinguni nae ' aliwatusi ' sana tu Askari wale.
Mpaka leo sijaona Serikali ya Tanzania yenyewe kama yenyewe ' ikilaani ' hiki Kitendo na naipongeza kwa hilo. Na kama Waafrika tumepata ' Uchungu ' nalo sana basi hii iwe ni sehemu yetu ya Kuanzia ya Sisi ' Kutojipendekeza ' kabisa kuhangaika kwenda Kwao huko ' Mamtoni ' na badala yake Waafrika wote tubaki ' Makwetu ' na tuzitengeneze nchi zetu ziwe nzuri kama za Marekani / Ulaya.
Sijajua kama Marehemu George Floyd ameshazikwa au bado ila kama tayari Kazikwa namuombea tu Makazi mema na mapya huko aendako Ahera!