Kwa unafiki na ubinafsi huu kamwe sitoacha kuwachana Waziri Mwakyembe na Msemaji wa Serikali, Dkt. Abbas huku nikimweka kiporo Naibu Spika

Mzukulu

JF-Expert Member
Feb 14, 2020
1,401
2,631
Wiki iliyopita wakati Klabu ya JKT Tanzania ikicheza dhidi ya Yanga SC katika Uwanja wa Jamhuri katika Mji Mkuu wa Tanzania Dodoma mara baada ya Mchezo huo haraka sana Katibu wa Wizara husika ya Michezo ambaye pia ni Msemaji wa Serikali Dkt. Abbas pamoja na Waziri wake Dkt. Mwakyembe waliamua Kuzuia Watazamaji Kuingia tena kwa kile walichosema Kukiukwa kwa taratibu za Kujikinga dhidi ya Ugonjwa wa COVID-19 (CORONA) kwakuwa Uwanja ulijaa kupita Kiasi na Kuhatarisha Afya za Wahudhuriaji.

Katika hali isiyokuwa ya Kawaida ambayo Mzukulu bila Uwoga wala Unafiki au Aibu alisema ni kwamba jana katika Mchezo baina ya Mbeya City na Simba SC katika Uwanja wa Sokoine Uwanja huo ulijaza kupita Kiasi na hata Picha zilionekana kwa tulioutazama huo Mpira lakini pia hapakuwa na kinachoitwa Social Distancing kama ilivyokuwa ikisisitizwa na mpaka hivi sasa Uwanja huo haujazuiwa Kuingiza Mashabiki na Wahusika Katibu wa Wizara Dkt. Abbas na Waziri wake Dkt. Mwakyembe wamenyamaza kama si Kuuchuna.

Najua fika kuwa hakuna hatua yoyote ile ya Kinidhamu ambayo itachukuliwa na Wahusika ( hasa Waziri Dkt. Mwakyembe ) dhidi ya Uwanja huo wa Sokoine Mkoani Mbeya kwakuwa Tukio zima la jana Waziri Dkt. Mwakyembe alilitumia kama Ngazi yake ya Kupandia katika Kujipatia Umaarufu zaidi wa Kisiasa, Kueneza Ukabila wake ambao kwa huko Mbeya umeota Mizizi. Na najua hata Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson ambaye anautaka Ubunge wa Mbeya Mjini kwa Udi na Uvumba na alikuwepo lilimsaidia pia.

Mzukulu ninamalizia kwa kusema kama Uwanja wa Jamhuri Dodoma ulipewa adhabu basi na wa Sokoine Mbeya nao uadhibiwe pia tena haraka.
 
Upumbavu imewajaa viongozi wetu hao kuanzia kwa Boss adi wasaidizi wote. Kweli ujinga ni mtaji wa umaskini.
 
Upumbavu umewajaa viongozi wetu hao kuanzia kwa Boss adi wasaidizi wote. Kweli ujinga ni mtaji wa umaskini.
 
Ni kama vile molinga anafunga goli la pili ndio anapewa hela, wakati huo huo anadai hela zake miezi karibu 4 hajapewa utopolo Ni shida.
 
Haya Uwanja umefungiwa kwa Mbeya City na pia Yanga na Simba zikienda Mikoani kucheza mashabiki hawaruhusiwi.
 
huyu aliyempa hii wizara naye hakufikiria vizuri huyu waziri akili zilishaondoka utazuiaje washabiki wasishabikie timu zao au unatafuta ujiko baada ya timu ya mkoa wake kufungwa waziri kila siku anatema pumba halafu mnadai wabunge wawe wasomi kama usomi ndio huu Mungu anisamehe
 
Wiki iliyopita wakati Klabu ya JKT Tanzania ikicheza dhidi ya Yanga SC katika Uwanja wa Jamhuri katika Mji Mkuu wa Tanzania Dodoma mara baada ya Mchezo huo haraka sana Katibu wa Wizara husika ya Michezo ambaye pia ni Msemaji wa Serikali Dkt. Abbas pamoja na Waziri wake Dkt. Mwakyembe waliamua Kuzuia Watazamaji Kuingia tena kwa kile walichosema Kukiukwa kwa taratibu za Kujikinga dhidi ya Ugonjwa wa COVID-19 (CORONA) kwakuwa Uwanja ulijaa kupita Kiasi na Kuhatarisha Afya za Wahudhuriaji.

Katika hali isiyokuwa ya Kawaida ambayo Mzukulu bila Uwoga wala Unafiki au Aibu alisema ni kwamba jana katika Mchezo baina ya Mbeya City na Simba SC katika Uwanja wa Sokoine Uwanja huo ulijaza kupita Kiasi na hata Picha zilionekana kwa tulioutazama huo Mpira lakini pia hapakuwa na kinachoitwa Social Distancing kama ilivyokuwa ikisisitizwa na mpaka hivi sasa Uwanja huo haujazuiwa Kuingiza Mashabiki na Wahusika Katibu wa Wizara Dkt. Abbas na Waziri wake Dkt. Mwakyembe wamenyamaza kama si Kuuchuna.

Najua fika kuwa hakuna hatua yoyote ile ya Kinidhamu ambayo itachukuliwa na Wahusika ( hasa Waziri Dkt. Mwakyembe ) dhidi ya Uwanja huo wa Sokoine Mkoani Mbeya kwakuwa Tukio zima la jana Waziri Dkt. Mwakyembe alilitumia kama Ngazi yake ya Kupandia katika Kujipatia Umaarufu zaidi wa Kisiasa, Kueneza Ukabila wake ambao kwa huko Mbeya umeota Mizizi. Na najua hata Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson ambaye anautaka Ubunge wa Mbeya Mjini kwa Udi na Uvumba na alikuwepo lilimsaidia pia.

Mzukulu ninamalizia kwa kusema kama Uwanja wa Jamhuri Dodoma ulipewa adhabu basi na wa Sokoine Mbeya nao uadhibiwe pia tena haraka.
Kihere here sio kizuri
 
Back
Top Bottom