1000 digits
JF-Expert Member
- Oct 16, 2012
- 6,252
- 7,930
Ni kweli itatucost sana.Nawaza KIJANA KAMA SABAYA kwa madaraka ya uDC na kutegemea kinga kutoka kwa aliyemteua lakini sio kinga ya Kikatiba anayafanya anayoyafanya kwa mkono wa Chuma ,Itakuaje apewe Urais kwa katiba hii tuliyonayo ambayo rais yupo juu ya kila kitu na hana sheria wala mtu wa kumzuia jambo lolote alimradi linampendeza machoni pale?? Mtu kama yule anaweza akaamka asunuhi akasema nileteeni Nyama ya Fulani ikiwa imeshachomwa na kuiva niile kama kiti moto na hakuna wa kumpinga mana atachagua kamati ya Roho Mbaya nchi nzima.
Hapana Vijana tumewaona walivyo na keep hemko kwa madaraka waliyopewa ya Ukuu wa Wilaya na Mikoa.
Kama wanaUwezo wajitokeze wenyewe kwa uwezo wao kuanzia huku chini na waonyeshe uwezo wa kuongoza ,kushawishi ,kuunganisha watu, kutumikia watu , upendo ,uvumilivu,uwezo wa kujenga hoja bila jaziba ,uadilifu wa kuzaliwa sio wa kujipendekeza,ukweli,ubunifu n.k.
Sio hawa vijana wa CCM na Chadema wanaounga mkono kuminywa kwa Demokrasia ili wao pekee ndio waendelee kuuaminisha umma kuwa hakuna wenye uwezo kuliko wao.
Tunachopenda kuona kwenye Taifa letu ni fursa sawa za Kisiasa ,kiuchumi, kijamii n.k. Wataonekana tu vijana na wazee na wale wa umri wa Kati wenye uwezo mkubwa wa kuongoza . Uongozi ni kipaji lakini kutawala ni kujikweza kupitia mabavu.
Hapana Vijana tumewaona walivyo na keep hemko kwa madaraka waliyopewa ya Ukuu wa Wilaya na Mikoa.
Kama wanaUwezo wajitokeze wenyewe kwa uwezo wao kuanzia huku chini na waonyeshe uwezo wa kuongoza ,kushawishi ,kuunganisha watu, kutumikia watu , upendo ,uvumilivu,uwezo wa kujenga hoja bila jaziba ,uadilifu wa kuzaliwa sio wa kujipendekeza,ukweli,ubunifu n.k.
Sio hawa vijana wa CCM na Chadema wanaounga mkono kuminywa kwa Demokrasia ili wao pekee ndio waendelee kuuaminisha umma kuwa hakuna wenye uwezo kuliko wao.
Tunachopenda kuona kwenye Taifa letu ni fursa sawa za Kisiasa ,kiuchumi, kijamii n.k. Wataonekana tu vijana na wazee na wale wa umri wa Kati wenye uwezo mkubwa wa kuongoza . Uongozi ni kipaji lakini kutawala ni kujikweza kupitia mabavu.