Kwa ulimwengu huu wa sasa Fani ya Procurement bado inafundishwa vyuoni kwa sababu gani?

Subiri majizi ya umma yaje yakufokee.
Hii kada ndio kada ya upigaji sasa hivi baada ya Magu kuwapiga wahasibu na kitu kizito kichwani
 
Kwanini iwe kawaida kwa graduate kujiajiri kwa kazi sawa na mhitimu wa kidato cha sita? Kuna umuhimu gani wa yeye kusoma kwa ngazi mpaka ya huko juu?
Hiyo ni problem ya mifumo iliyopo na umasikini wa nchi afu jobless ni tatizo la dunia nzima. Kuhusu graduate kufanya kazi sawa na wa kidato cha sita ina depend na utundu na ujanja wa mtu. Kama unashangaa hilo ungeanza kushangaa kwa nini kwenye list ya matajiri wa Tanzania mbona hamna maprofessa.
 
Mkuu, kama hizo SWOT na strategic management hazimuwezeshi fresh graduate kujiajiri, it's nothing.
Hapo ni swala la kijana mwenyewe sasa, mtu unafundishwa ili umanage biashara yako lazima ujue swot
S-strength
W-weakness
O-opportunities
T-threats

Sasa yote hayo utayasoma ndani ya hiyo procurement, ukizitumia hizo skills mbona waweza kujiajiri bila shida
 
Mkuu mbona Kuna mkunga ambaye hajui kusoma Wala kuandika na anazalisha vizuri je taaluma ya ukunga ifutwe?
Hoja ya msingi sana.

Watu wanachokosea ni kupima uhalali wa kitu kulingana na soko la ajira, which is totally wrong.

Example, Kwa sababu graduates wengi wa Economics hawana ajira, ndo tufute somo la economics? No.

Mjadala ili uwe na tija ni lazima tujikite kwenye fundamental questions.
 
Hapo ni swala la kijana mwenyewe sasa, mtu unafundishwa ili umanage biashara yako lazima ujue swot
S-strength
W-weakness
O-opportunities
T-threats

Sasa yote hayo utayasoma ndani ya hiyo procurement, ukizitumia hizo skills mbona waweza kujiajiri bila shida
Mkuu, let's make a long story short ni kwamba, mitaala ya Tanzania ipo irrelevant kabisa na mazingira yetu.
 
At least hiyo entrepreneurship mngeiondoka kutoka ndani ya procurement kisha ikawa bachelor degree ya kujitegemea hapo ingekuwa na mantiki kidogo. Kwa mfano bachelor degree in Agriculture and Entrepreneurship au Bachelor Degree in mobile device repair and Entrepreneurship.
procurement ni zaidi ya kununua, yani hata mafuta ya gari lako mpaka yakufikie ni matokeo ya Procurement and supply chain
 
Hivi kweli kabisa haujaona umuhimu wa mgavi?, mahospitali, mashule, mahoteli, majeshi, ofisi za umma na binafsi n.k anahitajika huyu mtaalamu.
 
Baadhi ya vyuo Duniani vimekuwa vikifanya mabadiliko ya mitaala na kufuta ama kuachana na fani ambazo haziendani na wakati.

Bado najiuliza, kwa Dunia ya sasa fani ya Procurement inafundishwa vyuoni kwa sababu gani? Ni fani ambayo haina umuhimu wowote kwa karne hii ya 21.

Mtoto akisoma Procurement basi umuhimu wake ni aajiriwe Serikalini zaidi ya hapo fani haina umuhimu wowote,na haina msaada wowote kwa mhitimu. kwanini iendelee kufunishwa vyuoni?

Hii fani ilipaswa kuwa sehemu ya course za watu wanaosoma finance/accounts lakini sio kuwa independent course.

Wakati tunafanya mabadiliko ya mitaala ya elimu, tusisahau ya vyuo vikuu. Vyuo wao wanachotaka ni hela tu kwa kuanzisha fani sizizo na maana yoyote ambazo hazina msaada kwa wahitimu.

Fani ya Procurement inapaswa kufutwa. Mzee Kishimba aliwahi kuuliza, mtu anasoma fani ya manunuzi ananunua nini?
Kwa kifupi ni kwamba wewe haujui umuhimu wa procurement ndio maana umeandika hoja zisizo na mashiko
 
procurement anasoma vitu kama tender, strategic mnagment, store, logistics, warehouse mng, enterprenuership, marketing, financial mangement mambo ya economic order quantinty pia accounting and finance usisahau commerce pia wanasoma, kimsingi mradi wowote wa serikari haufanywi bira dhabuni ya watu procurement (PMU), HIZO barbra, madaraji, majengo vyote zpo processing na procurement. ani ni fanj pana sana braza

Inshort busness yeyote lazma iusishe negotian na contract mqnqgent, handling, issues, dispatchin, inspection na receiving and recept of material ndo.maana wagqvi na manunuzi wqnafanya kazi sehemu yeyote
 
Hivi unajua hata mkandarasi wa SGR na Stigler gorge amepatikana kwa mchakato tuliofanya watu wa procurement?
mwana haelewi uyu, moja ya fani nyeti sana ani ata sbule unayoona inajenvwa ni proceessing na procurement, mgavi akisema sikupi tenda ndo imeisha iyo. uyu PMU katika taasis hingne anaeza kuwa mtu wa marketing, avvountant kwamaana acounting analysis wanazisoma, awa ni.watu wa bandari pia😁, awa jamaa warespect aisee
 
procurement anasoma vitu kama tender, strategic mnagment, store, logistics, warehouse mng, enterprenuership, marketing, financial mangement mambo ya economic order quantinty pia accounting and finance usisahau commerce pia wanasoma, kimsingi mradi wowote wa serikari haufanywi bira dhabuni ya watu procurement (PMU), HIZO barbra, madaraji, majengo vyote zpo processing na procurement. ani ni fanj pana sana braza

Inshort busness yeyote lazma iusishe negotian na contract mqnqgent, handling, issues, dispatchin, inspection na receiving and recept of material ndo.maana wagqvi na manunuzi wqnafanya kazi sehemu yeyote
Huyo mgavi "fresh graduate" anajiajiri vp?
 
Inshort busness yeyote lazma iusishe negotian na contract mqnqgent, handling, issues, dispatchin, inspection na receiving and recept of material ndo.maana wagqvi na manunuzi wqnafanya kazi sehemu yeyote
Umeongea fact zamani hizo mambo ulizogusia hapo za procurement zilikuwa chini ya ofisi ya mhasibu

Ila baada ya kuona upana na umuhimu wake ndio maana taaluma ya procurement and logistics management zikaongezwa kwenye vyuo vingi duniani lengo wapatikane watu wenye taaluma za ugavi(manunuzi, utunzaji na usambazaji) na ili mhasibu adeal tu na kutunza hesabu katika kampuni

Sasa mleta mada anaposema kuwa procurement katika karne hii ya 21 haina faida basi akae akijua hiyo ni mojawapo kozi ambayo inaendana na karne ya 21 na ndio maana vyuo vingi procurement imeanza kufundishwa miaka ya karibuni
 
Back
Top Bottom