sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 645
MEI 2 5, 1963, mjini Addis Ababa, Viongozi wa nchi 31 za Afrika walioanzisha Umoja wa nchi huru za Afrika [OAU] siku hiyo, walikuwa na kazi ngumu kucha gua kipi kipewe kipaumbele na umoja huo, kati ya vita vya ukombozi wa kisiasa dhidi ya ukoloni mkongwe, na vita vya ukombozi dhidi ya ubeberu wa kiuchumi wa nchi za Magharibi.
Ni Rais wa kwanza wa Ghana na mwanaharakati wa mapambano barani Afrika, Kwame Nkrumah, aliyetegua kitendawili hiki kwa tamko lake maarufu kwamba, Utafuteni kwanza ufalme wa kisiasa na mengine yote mtazidishiwa.
Kwa kibwagizo hicho, OAU ilianza harakati kwa kujikita zaidi katika vita vya ukombozi wa kisiasa barani Afrika badala ya ukombozi wa kiuchumi. Nkrumah akasema, Ghana iongoze harakati hizo na Makao Makuu ya ukombozi yawe Accra, Ghana; lakini Julius K. Nyerere wa Tanzania akapinga, akasema, Makao Makuu yawe Dar es Salaam, karibu na kichwa cha udhalimu Afrika Kusini ya Makaburu, ili iwe rahisi kuutokomeza ubaguzi wa rangi. Nyerere akashinda, Makao Makuu ya harakati za kupigania uhuru barani yakawa Dar es Salaam.
Ile dhana ya Nkrumah kwamba ukijikomboa kisiasa utakuwa pia umejikomboa kiuchumi haikufanya kazi, wala haijafanya kazi hadi leo. Afrika sasa yote ni huru, lakini hakuna hata nchi moja ya Kiafrika iliyo huru kiuchumi; zote ni masikini, zinazidi kuwa masikini kuliko hata kabla ya enzi za uhuru.
Kati ya nchi 42 masikini sana duniani [LDCs], 28 zinatoka bara la Afrika ambazo zimebebeshwa na nchi tajiri deni la zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 40 ambalo halilipiki. Tanzania pekee ina deni linalozidi dola bilioni nane. Hali hii ya umasikini imezidi kuongezeka kutokana kwamba, viongozi wengi walioongoza harakati za kuleta uhuru hawakufanya hivyo kwa lengo kamili la kuondoa ukoloni na utegemezi; walichotaka ni kuchukua nafasi ya wakoloni na kubakia ndani ya mfumo wa kikoloni.
Ni Rais wa kwanza wa Ghana na mwanaharakati wa mapambano barani Afrika, Kwame Nkrumah, aliyetegua kitendawili hiki kwa tamko lake maarufu kwamba, Utafuteni kwanza ufalme wa kisiasa na mengine yote mtazidishiwa.
Kwa kibwagizo hicho, OAU ilianza harakati kwa kujikita zaidi katika vita vya ukombozi wa kisiasa barani Afrika badala ya ukombozi wa kiuchumi. Nkrumah akasema, Ghana iongoze harakati hizo na Makao Makuu ya ukombozi yawe Accra, Ghana; lakini Julius K. Nyerere wa Tanzania akapinga, akasema, Makao Makuu yawe Dar es Salaam, karibu na kichwa cha udhalimu Afrika Kusini ya Makaburu, ili iwe rahisi kuutokomeza ubaguzi wa rangi. Nyerere akashinda, Makao Makuu ya harakati za kupigania uhuru barani yakawa Dar es Salaam.
Ile dhana ya Nkrumah kwamba ukijikomboa kisiasa utakuwa pia umejikomboa kiuchumi haikufanya kazi, wala haijafanya kazi hadi leo. Afrika sasa yote ni huru, lakini hakuna hata nchi moja ya Kiafrika iliyo huru kiuchumi; zote ni masikini, zinazidi kuwa masikini kuliko hata kabla ya enzi za uhuru.
Kati ya nchi 42 masikini sana duniani [LDCs], 28 zinatoka bara la Afrika ambazo zimebebeshwa na nchi tajiri deni la zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 40 ambalo halilipiki. Tanzania pekee ina deni linalozidi dola bilioni nane. Hali hii ya umasikini imezidi kuongezeka kutokana kwamba, viongozi wengi walioongoza harakati za kuleta uhuru hawakufanya hivyo kwa lengo kamili la kuondoa ukoloni na utegemezi; walichotaka ni kuchukua nafasi ya wakoloni na kubakia ndani ya mfumo wa kikoloni.