Kwa ujinga huu ni ndoto Tanzania kuwa 'Super Power' kwenye ukanda wa EAC

Feedback

JF-Expert Member
Mar 14, 2011
7,988
4,507
No wonder kwanini Tanzania tunaendelea kuburuzwa na kutengwa kwenye EAC, kama tutaendelea kupeleka wawakilishi EALA kwa mihemko ya kisiasa, yaani unampeleka Fancy kutetea taifa kufanya lobbying mbele ya wanasheria nguli kutoka Kenya, Uganda unawaacha wanasheria wazoefu kina Taslima, Macha kwa vile tu ni wapinzani, unamwacha memba mzoefu Zainabu Kawawa? Unamwacha Wenje kwa vile tu chama chake hakikuleta mwanamke? Unamwacha Makongoro aliyefanya lobbying hadi bomba la mafuta toka Uganda likapita Tanzania? Kweli?

Kwenye suala la ku serve national interests wanaCCM wenzetu hebu tuwe serious kidogo tuondoe uvyama, kule hawaendi kuwakilisha CCM wala Chadema wanakwenda kuwakilisha nchi.

Wenzetu huko Wakenya kwa mfano when comes issue ya kutetea nchi yao wako very serious and strong wanaleta competent representatives ndio maana labda wana maendeleo kutuzidi, sidhani kwenye bunge kama hili huwa wanaleta vitoto vitoto vya kuuza sura kama tunavyofanya sisi, that is why may be Kenya is becoming the super power among member states of the community, wengine tutabaki kulialia tu Kenya wanautumia mlima Kilimanjaro wanachukua watalii wetu kumbe tatizo ni sisi hatuna watu wa ku-defend our national interests. Tubadilike.
 
Nimekuelewa una maanisha wabunge wa CCM wangeiga mfano wa JPM ambaye kamteua Prof Mkumbo wa ACT kuwa Katibu Mkuu.
Ndio mkuu, wabunge wa CCM wangekuwa na mantiki kama kina Macha na Wenje wangekuwa wanakwenda kufanya kampeni ya Chadema lakini wanakwenda kutetea mlima Kilimanjaro usitumike hovyo, kulinda heshima ya Mtanzania awe Chadema au CCM, kutetea aridhi isitumiwe hovyo na wageni. Sasa unapopeleka mtu ambaye hata kujieleza hawezi unamkomoa nani.
 
Makonda au Bashite alisema kweli, wabunge wengi ni wachekeshaji hawana LA maana hata kidogo. Unamuacha Taslima kwa vile unamchukia Maalim na kumpa Mnyaa kwa vile unampenda Lipumba?
Mnyaa hakustahili kuchaguliwa. Taslima yuko vizuri kisiasa, hivi kweli Mnyaa Engineer ana uwakilishi gani kwa EAC paliposheheneni Wanasheria nguli Na Business professionals? English yenyewe 13%.
 
Makonda au Bashite alisema kweli, wabunge wengi ni wachekeshaji hawana LA maana hata kidogo. Unamuacha Taslima kwa vile unamchukia Maalim na kumpa Mnyaa kwa vile unampenda Lipumba?
Siasa zetu za ndani zimetupumbaza hadi zimeanza kuvuka mipaka, ni ujinga.

Kwa kitendo hiki CCM wamefaidika nini kwa vile nafasi bado ni za Chadema na inawezekana wakarudishwa wale wale wakaongezewa mwanamke mmoja tu CCM wakalazimishwa kuchagua wawili kati ya watatu.
 
Mnyaa hakustahili kuchaguliwa. Taslima yuko vizuri kisiasa, hivi kweli Mnyaa Engineer ana uwakilishi gani kwa EAC paliposheheneni Wanasheria nguli Na Business professionals? English yenyewe 13%.

Nimesikitika sana.CCM wanapindisha hata ukweli wanataka usome kadiri ya wingi wao.

Nina imani bado CDM INA nafasi ya kuwarudisha Wenje na Masha.Wagombea wa CDM CCM inawauma.kama.wao ndiyo CDM. Kuna moja naliona Mkullu ana taka watu wake naona imeshindikana.

Issue ya radhi EAC bado ni tete unampeleka Mnyaa au Fancy unawaacha akina Shyrise Bhanji duh!

CCM kweli chama Cha Majangili.
 
Nia yao iliku
Nimesikitika sana.CCM wanapindisha hata ukweli wanataka usome kadiri ya wingi wao.

Nina imani bado CDM INA nafasi ya kuwarudisha Wenje na Masha.Wagombea wa CDM CCM inawauma.kama.wao ndiyo CDM. Kuna moja naliona Mkullu ana taka watu wake naona imeshindikana.

Issue ya radhi EAC bado ni tete unampeleka Mnyaa au Fancy unawaacha akina Shyrise Bhanji duh!

CCM kweli chama Cha Majangili.
Nia yao ilikuwa kuwaliza CDM. Kwa kumpa Mnyaa wa Cuf ya Lipumba! Anyway Masha alistahili kwa CV yake siyo Fancy Nkuhi! Wanajidai kutetea wanawake mbona hawakumchagua Mama Rose awe Rais?
 
Nimesikitika sana.CCM wanapindisha hata ukweli wanataka usome kadiri ya wingi wao.

Nina imani bado CDM INA nafasi ya kuwarudisha Wenje na Masha.Wagombea wa CDM CCM inawauma.kama.wao ndiyo CDM. Kuna moja naliona Mkullu ana taka watu wake naona imeshindikana.

Issue ya radhi EAC bado ni tete unampeleka Mnyaa au Fancy unawaacha akina Shyrise Bhanji duh!

CCM kweli chama Cha Majangili.
Huyo Nancy sijui kama anajua hata maana ya common market protocol achilia mbali kujua faida na hasara zake na jinsi itakavyotunufaisha.
 
Juzi hadi leo mnakazania yawe na mnawashangilia na kuwasifia kwa kumuita Mhe. Makonda kuhojiwa, leo mnawageuka, nyie vipeeeeee!?

Ha ha haaaaaaaaaaaaa
 
Nia yao ilikuwa kuwaliza CDM. Kwa kumpa Mnyaa wa Cuf ya Lipumba! Anyway Masha alistahili kwa CV yake siyo Fancy Nkuhi! Wanajidai kutetea wanawake mbona hawakumchagua Mama Rose awe Rais?
Mbona nafasi za Chadema bado zipo palepale, nafikiri nia yao kuu ilikuwa kuwachagulia Chadema wagombea wanaowataka.

Kama ingewezekana Chadema wangemuongeza mtu kama Halima Mdee awe mgombea mwanamke pamoja na kina Masha ili CCM wachague.
 
Mnyaa hakustahili kuchaguliwa. Taslima yuko vizuri kisiasa, hivi kweli Mnyaa Engineer ana uwakilishi gani kwa EAC paliposheheneni Wanasheria nguli Na Business professionals? English yenyewe 13%.
Life is not all about laws guys
 
Mlishangiria Ubinafsi
mkaona kama ACT itapata si chama cha Tanzania
leo mmeanza kulialia
hahaha nabado
mtulie dawa iwaingie

Dawa ya moto ni moto
Safi sana wabunge
Chadema wameambulia ZERO
 
Back
Top Bottom